<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<?xml-stylesheet type="text/css" href="../styles/defaut.css"?>
<book value="PSA">
<id>PSA 19PSASWU60.PTX Swahili - Union Version June 2003 </id>
<intro>
<ide>CP-1252 </ide>
<rem>For any non-Paratext use of this text, permission must be obtained from the copyright holder </rem>
<h>ZABURI </h>
<mt1>ZABURI </mt1>
<d>KITABU CHA KWANZA </d>
</intro>

<c><cn>1</cn>
<q1><vn>1 </vn>Heri mtu yule asiyekwenda </q1>
<q2>Katika shauri la wasio haki; </q2>
<q1>Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; </q1>
<q2>Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>1:1</xo>
<xt>Mwa 5:24; Ayu 31:5; Zab 81:12; Mit 4:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Bali sheria ya 
<nd>Bwana</nd> ndiyo impendezayo, </q1>
<q2>Na sheria yake huitafakari mchana na usiku. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Naye atakuwa kama mti uliopandwa </q1>
<q2>Kandokando ya vijito vya maji, </q2>
<q1>Uzaao matunda yake kwa majira yake, </q1>
<q1>Wala jani lake halinyauki; </q1>
<q2>Na kila alitendalo litafanikiwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>1:3</xo>
<xt>Yer 17:8; Mwa 39:3; Zab 128:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Sivyo walivyo wasio haki; </q1>
<q2>Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni, </q1>
<q2>Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> anaijua njia ya wenye haki, </q1>
<q2>Bali njia ya wasio haki itapotea. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>1:6</xo>
<xt>Nah 1:7; Yn 10:14</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>2</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mbona mataifa wanafanya ghasia, </q1>
<q2>Na makabila wanatafakari ubatili? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>2:1-2</xo>
<xt>Mdo 4:25-26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Wafalme wa dunia wanajipanga, </q1>
<q2>Na wakuu wanafanya shauri pamoja, </q2>
<q1>Juu ya 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Na juu ya masihi<f> <fn>a</fn><note>
<fr>2:2</fr>
<ft> Au, mtiwa mafuta.</ft></note></f> wake, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>2:2</xo>
<xt>Zab 45:7; Yn 1:41</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Na tuvipasue vifungo vyao, </q1>
<q2>Na kuzitupia mbali nasi kamba zao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>2:3</xo>
<xt>Lk 19:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Yeye aketiye mbinguni anacheka, </q1>
<q2>Bwana anawafanyia dhihaka. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>2:4</xo>
<xt>Zab 11:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Ndipo atakaposema nao kwa hasira yake, </q1>
<q2>Na kuwafadhaisha kwa ghadhabu yake. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nami nimemweka mfalme wangu </q1>
<q2>Juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Nitaihubiri amri; 
<nd>Bwana</nd> aliniambia, </q1>
<q2>Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>2:7</xo>
<xt>Mdo 13:33; Ebr 1:5; 5:5; Mt 8:29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Uniombe, nami nitakupa mataifa kuwa urithi wako, </q1>
<q2>Na miisho ya dunia kuwa milki yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>2:8</xo>
<xt>Dan 7:13,14; Yn 17:4,5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Utawaponda kwa fimbo ya chuma, </q1>
<q2>Na kuwavunja kama chombo cha mfinyanzi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>2:9</xo>
<xt>Ufu 2:26-27; 12:5; 19:15; Mt 21:44</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Na sasa, enyi wafalme, fanyeni akili, </q1>
<q2>Enyi waamuzi wa dunia, mwadibiwe. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Mtumikieni 
<nd>Bwana</nd> kwa kicho, </q1>
<q2>Shangilieni kwa kutetemeka. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Shikeni yaliyo bora<f> <fn>b</fn><note>
<fr>2:12</fr>
<ft> Au, Pokeeni mafundisho au, Mbu suni Mwana.</ft></note></f>, asije akafanya hasira </q1>
<q2>Nanyi mkapotea njiani, </q2>
<q1>Kwa kuwa hasira yake itawaka upesi; </q1>
<q2>Heri wote wanaomkimbilia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>2:12</xo>
<xt>Yn 5:22,23; Yer 17:7</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>3</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd>, watesi wangu wamezidi kuwa wengi, </q1>
<q2>Ni wengi wanaonishambulia, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>3:1</xo>
<xt>2 Sam 15:13--17:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ni wengi wanaoiambia nafsi yangu, </q1>
<q2>Hana wokovu huyu kwa Mungu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>3:2</xo>
<xt>2 Sam 16:8; Zab 22:7,8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Na Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, U ngao yangu pande zote, </q1>
<q2>Utukufu wangu na mwinua kichwa changu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>3:3</xo>
<xt>2 Fal 25:27; Zab 27:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Kwa sauti yangu namwita 
<nd>Bwana</nd> </q1>
<q2>Naye aniitikia toka mlima wake mtakatifu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Nalijilaza nikalala usingizi, nikaamka, </q1>
<q2>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> ananitegemeza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>3:5</xo>
<xt>Zab 4:8; Mit 3:24; Mdo 12:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Sitayaogopa makumi elfu ya watu, </q1>
<q2>Waliojipanga juu yangu pande zote. </q2>
<q1><vn>7 </vn>
<nd>Bwana</nd>, uinuke, Mungu wangu, uniokoe, </q1>
<q2>Maana umewapiga taya adui zangu wote; </q2>
<q2>Umewavunja meno wasio haki. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Wokovu una 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Baraka yako na iwe juu ya watu wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>3:8</xo>
<xt>Zab 37:39,40; Mit 21:31; Hes 13:4</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>4</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu wa haki yangu, uniitikie niitapo; </q1>
<q2>Umenifanyizia nafasi wakati wa shida; </q2>
<q2>Unifadhili na kuisikia sala yangu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Enyi wanadamu, hata lini utukufu wangu utafedheheka? </q1>
<q2>Je! Mtapenda ubatili na kutafuta uongo? </q2>
<q1><vn>3 </vn>Bali jueni ya kuwa 
<nd>Bwana</nd> amejiteulia mtauwa; </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> atasikia nimwitapo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>4:3</xo>
<xt>Kut 33:16; 2 Pet 2:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Mwe na hofu wala msitende dhambi, </q1>
<q2>Tafakarini vitandani mwenu na kutulia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>4:4</xo>
<xt>Efe 4:26; Mit 3:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Toeni dhabihu za haki, </q1>
<q2>Na kumtumaini 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>4:5</xo>
<xt>Kum 33:19; Zab 37:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Wengi husema, Nani atakayetuonyesha mema? </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd>, utuinulie nuru ya uso wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>4:6</xo>
<xt>Zab 80:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Umenitia furaha moyoni mwangu, </q1>
<q2>Kupita yao wanapozidishiwa nafaka na divai. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara, </q1>
<q2>Maana Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, peke yako, </q2>
<q2>Ndiwe unijaliaye kukaa salama. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>4:8</xo>
<xt>Law 26:5; Kum 12:10; Yn 14:27; Flp 4:7</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>5</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uyasikilize maneno yangu, </q1>
<q2>Ukuangalie kutafakari kwangu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Uisikie sauti ya kilio changu, </q1>
<q2>Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, </q2>
<q2>Kwa maana Wewe ndiwe nikuombaye. </q2>
<q1><vn>3 </vn>
<nd>Bwana</nd>, asubuhi utaisikia sauti yangu, </q1>
<q2>Asubuhi nitakupangia dua yangu na kutazamia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>5:3</xo>
<xt>Zab 30:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Maana huwi Mungu apendezwaye na ubaya; </q1>
<q2>Mtu mwovu hatakaa kwako; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>5:4</xo>
<xt>Mal 2:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Wajivunao hawatasimama mbele za macho yako; </q1>
<q2>Unawachukia wote watendao ubatili. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>5:5</xo>
<xt>Zab 14:1; Hab 1:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Utawaharibu wasemao uongo; </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> humzira mwuaji na mwenye hila </q2>
<q1><vn>7 </vn>Bali mimi, kwa wingi wa fadhili zako, </q1>
<q2>Nitaingia nyumbani mwako; </q2>
<q1>Na kusujudu kwa kicho, </q1>
<q2>Nikilielekea hekalu lako takatifu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>5:7</xo>
<xt>1 Fal 8:29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>
<nd>Bwana</nd>, uniongoze kwa haki yako, </q1>
<q2>Kwa sababu yao wanaoniotea. </q2>
<q1>Uisawazishe njia yako mbele ya uso wangu, </q1>
<q2><vn>9 </vn>Maana vinywani mwao hamna uaminifu; </q2>
<q1>Mtima wao ni shimo tupu, koo lao ni kaburi wazi, </q1>
<q2>Ulimi wao hujipendekeza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>5:9</xo>
<xt>Rum 3:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Wewe, Mungu, uwapatilize, </q1>
<q2>Na waanguke kwa mashauri yao. </q2>
<q1>Uwatoe nje kwa ajili ya wingi wa makosa yao, </q1>
<q2>Kwa maana wamekuasi Wewe. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Nao wote wanaokukimbilia watafurahi; </q1>
<q2>Watapiga daima kelele za furaha. </q2>
<q1>Kwa kuwa Wewe unawahifadhi, </q1>
<q2>Walipendao jina lako watakufurahia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>5:11</xo>
<xt>1 Kor 2:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Kwa maana Wewe utambariki mwenye haki; </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd>, utamzungushia radhi kama ngao. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>6</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd>, usinikemee kwa hasira yako, </q1>
<q2>Wala usinirudi kwa ghadhabu yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>6:1</xo>
<xt>Zab 38:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>
<nd>Bwana</nd>, unifadhili, maana ninanyauka; </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd>, uniponye, mifupa yangu imefadhaika. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>6:2</xo>
<xt>Hos 6:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Na nafsi yangu imefadhaika sana; </q1>
<q2>Na Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, hata lini? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>6:3</xo>
<xt>Mit 18:14; Mt 26:38</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>
<nd>Bwana</nd> urudi, uniopoe nafsi yangu, </q1>
<q2>Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Maana mautini hapana kumbukumbu lako; </q1>
<q2>Katika kuzimu ni nani atakayekushukuru? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>6:5</xo>
<xt>Zab 30:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nimechoka kwa kuugua kwangu; </q1>
<q2>Kila usiku nakieleza kitanda changu; </q2>
<q2>Nalilowesha godoro langu kwa machozi yangu. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Jicho langu limeharibika kwa masumbufu, </q1>
<q2>Na kuchakaa kwa sababu yao wanaoniudhi. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ondokeni kwangu, ninyi nyote mtendao uovu; </q1>
<q2>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> ameisikia sauti ya kilio changu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>6:8</xo>
<xt>Mt 7:23; Lk 13:27</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>
<nd>Bwana</nd> ameisikia dua yangu; </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> atayatakabali maombi yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>6:9</xo>
<xt>Zab 3:4; 31:22; 40:1,2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, </q1>
<q2>Watarudi nyuma, kwa ghafula wataaibika. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>7</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd>, Mungu wangu, nimekukimbilia Wewe, </q1>
<q2>Uniokoe na wote wanaonifuatia, uniponye. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Asije akaipapura nafsi yangu kama simba, </q1>
<q2>Akiivunja-vunja pasipokuwa na wa kuponya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>7:2</xo>
<xt>1 Pet 5:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>
<nd>Bwana</nd>, Mungu wangu, ikiwa nimetenda haya, </q1>
<q2>Ikiwa mna uovu mikononi mwangu, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>7:3</xo>
<xt>2 Sam 16:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Ikiwa nimemlipa mabaya </q1>
<q2>Yeye aliyekaa kwangu salama; </q2>
<q1>(Hasha! Nimemponya yeye </q1>
<q2>Aliyekuwa mtesi wangu bila sababu;) <f> <fn>-</fn><note>
<xo>7:4</xo>
<xt>1 Sam 24:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Basi adui na anifuatie, </q1>
<q2>Na kuikamata nafsi yangu; </q2>
<q1>Naam, aukanyage uzima wangu, </q1>
<q2>Na kuulaza utukufu wangu mavumbini. </q2>
<q1><vn>6 </vn>
<nd>Bwana</nd> uondoke kwa hasira yako; </q1>
<q2>Ujiinue juu ya jeuri ya watesi wangu; </q2>
<q1>Uamke kwa ajili yangu; </q1>
<q2>Umeamuru hukumu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>7:6</xo>
<xt>Zab 94:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Kusanyiko la mataifa na likuzunguke, </q1>
<q2>Na juu yake uketi utawale. </q2>
<q1><vn>8 </vn>
<nd>Bwana</nd> atawaamua mataifa, </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd>, unihukumu mimi, </q2>
<q1>Kwa kadiri ya haki yangu, </q1>
<q2>Sawasawa na unyofu nilio nao. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Ubaya wao wasio haki na ukome, </q1>
<q2>Lakini umthibitishe mwenye haki. </q2>
<q1>Kwa maana mjaribu mioyo na viuno </q1>
<q2>Ndiye Mungu aliye mwenye haki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>7:9</xo>
<xt>Ufu 2:23; 1 Sam 16:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Ngao yangu ina Mungu, </q1>
<q2>Awaokoaye wanyofu wa moyo. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Mungu ni mwamuzi mwenye haki, </q1>
<q2>Naam, Mungu aghadhibikaye kila siku. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Mtu asiporejea ataunoa upanga wake; </q1>
<q2>Ameupinda uta wake na kuuweka tayari; </q2>
<q1><vn>13 </vn>Naye amemtengenezea silaha za kufisha, </q1>
<q2>Akifanya mishale yake kuwa ya moto. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Tazama, huyu ana utungu wa uovu, </q1>
<q2>Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Amechimba shimo, amelichimba chini sana, </q1>
<q2>Akatumbukia katika handaki aliyoifanya! <f> <fn>-</fn><note>
<xo>7:15</xo>
<xt>Est 7:10; Mit 5:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Madhara yake yatamrejea kichwani pake, </q1>
<q2>Na dhuluma yake itamshukia utosini. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>7:16</xo>
<xt>1 Fal 2:32</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Nitamshukuru 
<nd>Bwana</nd> kwa kadiri ya haki yake; </q1>
<q2>Nitaliimbia jina la 
<nd>Bwana</nd> aliye juu. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>8</cn>
<q1><vn>1 </vn>Wewe, MUNGU, Bwana wetu </q1>
<q2>Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote! </q2>
<q1>Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni; </q1>
<q1><vn>2 </vn>Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao </q1>
<q2>Umeiweka misingi ya nguvu; </q2>
<q1>Kwa sababu yao wanaoshindana nawe; </q1>
<q2>Uwakomeshe adui na mijilipiza kisasi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>8:2</xo>
<xt>Mt 21:16; 11:25; 1 Kor 1:27</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, </q1>
<q2>Mwezi na nyota ulizoziratibisha; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>8:3</xo>
<xt>Zab 44:16; 19:1; Ayu 22:12; Rum 1:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, </q1>
<q2>Na binadamu hata umwangalie? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>8:4</xo>
<xt>Ayu 7:17-18; Zab 144:3; Ebr 2:6-8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; </q1>
<q2>Umemvika taji ya utukufu na heshima; </q2>
<q1><vn>6 </vn>Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; </q1>
<q2>Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>8:6</xo>
<xt>1 Kor 15:27; Efe 1:22; Ebr 2:8; Mwa 1:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Kondoo, na ng'ombe wote pia; </q1>
<q2>Naam, na wanyama wa kondeni; </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ndege wa angani, na samaki wa baharini; </q1>
<q2>Na kila kipitacho njia za baharini. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Wewe, MUNGU, Bwana wetu, </q1>
<q2>Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote! <f> <fn>-</fn><note>
<xo>8:9</xo>
<xt>Ayu 11:7; Zab 35:10</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>9</cn>
<q1><vn>1 </vn>Nitamshukuru 
<nd>Bwana</nd> kwa moyo wangu wote; </q1>
<q2>Nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu; </q2>
<q1><vn>2 </vn>Nitafurahi na kukushangilia Wewe; </q1>
<q2>Nitaliimbia jina lako, Wewe Uliye juu. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Kwa sababu adui zangu hurudi nyuma; </q1>
<q2>Hujikwaa na kuangamia mbele zako. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Kwa maana umenifanyia hukumu na haki </q1>
<q2>Umeketi kitini pa enzi ukihukumu kwa haki. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Umewakemea mataifa; </q1>
<q2>Na kumwangamiza mdhalimu; </q2>
<q1>Umelifuta jina lao milele na milele; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>9:5</xo>
<xt>Kum 9:14</xt></note></f> </q1>
<q2><vn>6 </vn>Adui wamekoma na kuachwa ukiwa milele. </q2>
<q1>Nayo miji yao uliing'oa; </q1>
<q2>Hata kumbukumbu lao limepotea. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Bali 
<nd>Bwana</nd> atakaa milele, </q1>
<q2>Ameweka kiti chake tayari kwa hukumu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>9:7</xo>
<xt>Zab 90:2; Mik 5:2; Hab 1:12; Ebr 1:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Naye atauhukumu ulimwengu kwa haki; </q1>
<q2>Atawaamua watu kwa adili. </q2>
<q1><vn>9 </vn>
<nd>Bwana</nd> atakuwa ngome kwake aliyeonewa, </q1>
<q2>Naam, ngome kwa nyakati za shida. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Nao wakujuao jina lako wakutumaini Wewe, </q1>
<q2>Maana Wewe, 
<nd>Bwana</nd> hukuwaacha wakutafutao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>9:10</xo>
<xt>Zab 91:14; Yn 17:3; 2 Kor 4:6; 2 Tim 1:12; 1 Yoh 2:3,4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Mwimbieni 
<nd>Bwana</nd> akaaye Sayuni, </q1>
<q2>Yatangazeni kati ya watu matendo yake. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Maana mlipiza kisasi cha damu awakumbuka, </q1>
<q2>Hakukisahau kilio cha wanyonge. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, unifadhili, </q1>
<q2>Tazama mateso niteswayo na wanaonichukia; </q2>
<q1>Wewe uniinuaye katika malango ya mauti, </q1>
<q2><vn>14 </vn>Ili nizisimulie sifa zako zote; </q2>
<q1>Katika malango ya binti Sayuni </q1>
<q2>Nitaufurahia wokovu wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>9:14</xo>
<xt>Zab 13:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Mataifa wamezama katika shimo walilolifanya; </q1>
<q2>Kwa wavu waliouficha imenaswa miguu yao. </q2>
<q1><vn>16 </vn>
<nd>Bwana</nd> amejidhihirisha na kutekeleza hukumu; </q1>
<q2>Amemnasa mdhalimu kwa kazi ya mikono yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>9:16</xo>
<xt>Kut 7:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Wadhalimu watarejea kuzimu, </q1>
<q2>Naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>9:17</xo>
<xt>Ayu 8:13; Zab 50:22; Yer 2:32; Hos 2:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>Kwa maana mhitaji hatasahauliwa daima; </q1>
<q2>Matumaini ya wanyonge hayatapotea milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>9:18</xo>
<xt>Zab 12:5; Flp 1:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>
<nd>Bwana</nd>, usimame, mwanadamu asipate nguvu, </q1>
<q2>Mataifa wahukumiwe mbele zako. </q2>
<q1><vn>20 </vn>
<nd>Bwana</nd>, uwawekee kitisho, </q1>
<q2>Mataifa na wajijue kuwa ni binadamu. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>10</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, kwa nini wasimama mbali? </q1>
<q2>Kwani kujificha nyakati za shida? </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kwa kiburi chake asiye haki mnyonge anafuatiwa kwa ukali; </q1>
<q2>Na wanaswe kwa hila zizo hizo walizoziwaza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>10:2</xo>
<xt>Mit 5:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake, </q1>
<q2>Na mwenye choyo humkana 
<nd>Bwana</nd> na kumdharau. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Mdhalimu kwa kiburi cha uso wake </q1>
<q2>Asema, Hatapatiliza. </q2>
<q1>Jumla ya mawazo yake ni, Hakuna Mungu; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>10:4</xo>
<xt>2 Fal 18:35; Ayu 21:15; Zab 12:3-5</xt></note></f> </q1>
<q2><vn>5 </vn>Njia zake ni thabiti kila wakati. </q2>
<q1>Hukumu zako ziko juu asizione, </q1>
<q2>Adui zake wote awafyonya. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Asema moyoni mwake, Sitaondoshwa, </q1>
<q2>Kizazi baada ya kizazi sitakuwamo taabuni. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Kinywa chake kimejaa laana, </q1>
<q2>Na hila na dhuluma. </q2>
<q1>Chini ya ulimi wake kuna madhara na uovu, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>10:7</xo>
<xt>Rum 3:14</xt></note></f> </q1>
<q2><vn>8 </vn>Hukaa katika maoteo ya vijiji. </q2>
<q1>Mahali pa siri humwua asiye na hatia, </q1>
<q2>Macho yake humvizia mtu duni. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Huotea faraghani kama simba pangoni, </q1>
<q2>Huotea amkamate mtu mnyonge. </q2>
<q1>Naam, humkamata mtu mnyonge, </q1>
<q2>Akimkokota wavuni mwake. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Hujikunyata na kuinama; </q1>
<q2>Watu duni huanguka kwa nguvu zake. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Asema moyoni mwake, Mungu amesahau, </q1>
<q2>Auficha uso wake, haoni kamwe. </q2>
<q1><vn>12 </vn>
<nd>Bwana</nd>, uondoke, Ee Mungu, uuinue mkono wako, </q1>
<q2>Usiwasahau wanyonge. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Kwani mdhalimu kumdharau Mungu. </q1>
<q2>Akisema moyoni mwake, Hutapatiliza? </q2>
<q1><vn>14 </vn>Umeona, maana unaangalia madhara na jeuri, </q1>
<q2>Uyatwae mkononi mwako. </q2>
<q1>Mtu duni hukuachia nafsi yake, </q1>
<q2>Maana umekuwa msaidizi wa yatima. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Uuvunje mkono wake mdhalimu, </q1>
<q2>Na mbaya, uipatilize dhuluma yake, hata usiione. </q2>
<q1><vn>16 </vn>
<nd>Bwana</nd> ndiye Mfalme milele na milele; </q1>
<q2>Mataifa wamepotea kutoka nchi yake. </q2>
<q1><vn>17 </vn>
<nd>Bwana</nd>, umeisikia tamaa ya wanyonge, </q1>
<q2>Utaitengeneza mioyo yao, utalitega sikio lako. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Ili kumhukumu yatima naye aliyeonewa, </q1>
<q2>Binadamu aliye udongo asizidi kudhulumu. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>11</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd> ndiye niliyemkimbilia. </q1>
<q2>Mbona mnaiambia nafsi yangu, </q2>
<q2>Kimbia kama ndege mlimani kwenu? </q2>
<q1><vn>2 </vn>Maana, tazama, wasio haki wanaupinda uta, </q1>
<q2>Wanaitia mishale yao katika upote, </q2>
<q2>Ili kuwapiga gizani wanyofu wa moyo. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Kama misingi ikiharibika, </q1>
<q2>Mwenye haki atafanya nini? </q2>
<q2><vn>4 </vn>
<nd>Bwana</nd> yu katika hekalu lake takatifu. </q2>
<q1>
<nd>Bwana</nd> ambaye kiti chake kiko mbinguni, </q1>
<q2>Macho yake yanaangalia; </q2>
<q2>Kope zake zinawajaribu wanadamu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>11:4</xo>
<xt>Hab 2:20; Efe 5:13; Ebr 4:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>
<nd>Bwana</nd> humjaribu mwenye haki; </q1>
<q2>Bali nafsi yake humchukia asiye haki, </q2>
<q2>Na mwenye kupenda udhalimu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>11:5</xo>
<xt>Ayu 5:17; Zab 94:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Awanyeshee wasio haki mitego, </q1>
<q2>Moto na kiberiti na upepo wa hari, </q2>
<q2>Na viwe fungu la kikombe chao. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> ndiye mwenye haki, </q1>
<q2>Apenda matendo ya haki, </q2>
<q2>Wanyofu wa moyo watamwona uso wake. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>12</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd>, uokoe, maana mcha Mungu amekoma, </q1>
<q2>Maana waaminifu wametoweka katika wanadamu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>12:1</xo>
<xt>Isa 57:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Husemezana yasiyofaa kila mtu na mwenziwe, </q1>
<q2>Wenye midomo ya kujipendekeza; </q2>
<q2>Husemezana kwa mioyo ya unafiki; </q2>
<q1><vn>3 </vn>
<nd>Bwana</nd> ataikata midomo yote ya kujipendekeza, </q1>
<q2>Nao ulimi unenao maneno ya kiburi; </q2>
<q1><vn>4 </vn>Waliosema, Kwa ndimi zetu tutashinda; </q1>
<q2>Midomo yetu ni yetu wenyewe, </q2>
<q2>Ni nani aliye bwana juu yetu? </q2>
<q1><vn>5 </vn>Kwa ajili ya kuonewa kwao wanyonge, </q1>
<q2>Kwa ajili ya kuugua kwao wahitaji, </q2>
<q1>Sasa nitasimama, asema 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Nitamweka salama yeye wanayemfyonya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>12:5</xo>
<xt>Kut 3:7,8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Maneno ya 
<nd>Bwana</nd> ni maneno safi, </q1>
<q2>Ni fedha iliyojaribiwa kalibuni juu ya nchi; </q2>
<q2>Iliyosafishwa mara saba. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>12:6</xo>
<xt>2 Sam 22:31; Zab 18:30; Mit 30:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, ndiwe utakayetuhifadhi, </q1>
<q2>Utatulinda na kizazi hiki milele. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Wasio haki hutembea pande zote, </q1>
<q2>Ufisadi ukitukuka kati ya wanadamu. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>13</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, hata lini utanisahau, hata milele? </q1>
<q2>Hata lini utanificha uso wako? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>13:1</xo>
<xt>Kum 31:17; Ayu 13:24; Zab 22:1; Isa 59:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Hata lini nifanye mashauri nafsini mwangu, </q1>
<q1>Nikihuzunika moyoni mchana kutwa? </q1>
<q2>Hata lini adui yangu atukuke juu yangu? </q2>
<q1><vn>3 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wangu, uangalie, uniitikie; </q1>
<q2>Uyatie nuru macho yangu, </q2>
<q2>Nisije nikalala usingizi wa mauti. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>13:3</xo>
<xt>Ezr 9:8; Zab 18:28; Lk 2:32; Ufu 21:23; Zab 76:5,6; Isa 37:36; Yer 51:39; Efe 5:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Adui yangu asije akasema, Nimemshinda; </q1>
<q2>Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Nami nimezitumainia fadhili zako; </q1>
<q2>Moyo wangu na uufurahie wokovu wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>13:5</xo>
<xt>2 Nya 20:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Naam, nimwimbie 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>14</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu; </q1>
<q2>Wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo, </q2>
<q2>Hakuna atendaye mema. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>14:1-3</xo>
<xt>Rum 3:10-12; Zab 10:4; Mit 1:7,22; Mwa 6:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Toka mbinguni 
<nd>Bwana</nd> aliwachungulia wanadamu, </q1>
<q2>Aone kama yuko mtu mwenye akili, </q2>
<q2>Amtafutaye Mungu. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Wote wamepotoka, wameoza wote pamoja, </q1>
<q2>Hakuna atendaye mema, </q2>
<q2>La! Hata mmoja. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Je! Wote wafanyao maovu hawajui? </q1>
<q2>Walao watu wangu kama walavyo mkate, </q2>
<q2>Hawamwiti 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Hapo ndipo walipoingiwa na hofu nyingi, </q1>
<q2>Maana Mungu yupo pamoja na kizazi cha haki. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Mnalitia aibu shauri la mtu mnyonge, </q1>
<q2>Bali 
<nd>Bwana</nd> ndiye aliye kimbilio lake. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Laiti wokovu wa Israeli utoke katika Sayuni! </q1>
<q1>
<nd>Bwana</nd> awarudishapo wafungwa wa watu wake; </q1>
<q2>Yakobo atashangilia, </q2>
<q2>Israeli atafurahi. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>15</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd>, ni nani atakayekaa </q1>
<q2>Katika hema yako? </q2>
<q1>Ni nani atakayefanya maskani yake </q1>
<q2>Katika kilima chako kitakatifu? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>15:1</xo>
<xt>Zab 2:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ni mtu aendaye kwa ukamilifu, </q1>
<q2>Na kutenda haki. </q2>
<q1>Asemaye kweli kwa moyo wake, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>15:2</xo>
<xt>Zab 84:11; Isa 33:15,16</xt></note></f> </q1>
<q2><vn>3 </vn>Asiyesingizia kwa ulimi wake. </q2>
<q1>Wala hakumtenda mwenziwe mabaya, </q1>
<q2>Wala hakumsengenya jirani yake. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Machoni pake mtu asiyefaa hudharauliwa, </q1>
<q2>Bali huwaheshimu wamchao 
<nd>Bwana</nd> </q2>
<q1>Ingawa ameapa kwa hasara yake, </q1>
<q2>Hayabadili maneno yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>15:4</xo>
<xt>Yos 9:18-20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Hakutoa fedha yake apate kula riba, </q1>
<q2>Hakutwaa rushwa amwangamize asiye na hatia. </q2>
<q1>Mtu atendaye mambo hayo </q1>
<q2>Hataondoshwa milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>15:5</xo>
<xt>Eze 18:8,9</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>16</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mungu, unihifadhi mimi, </q1>
<q2>Kwa maana nakukimbilia Wewe. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>16:1</xo>
<xt>Zab 25:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Nimemwambia 
<nd>Bwana</nd>, Ndiwe 
<nd>Bwana</nd> wangu; </q1>
<q2>Sina wema ila utokao kwako. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, </q1>
<q2>Hao ndio niliopendezwa nao. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Huzuni zao zitaongezeka </q1>
<q2>Wambadilio Mungu kwa mwingine; </q2>
<q1>Sitazimimina sadaka zao za damu, </q1>
<q2>Wala kuyataja majina yao midomoni mwangu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>
<nd>Bwana</nd> ndiye fungu la posho langu, </q1>
<q2>Na la kikombe changu; </q2>
<q2>Wewe unaishika kura yangu. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Kamba zangu zimeniangukia mahali pema, </q1>
<q2>Naam, nimepata urithi mzuri. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Nitamhimidi 
<nd>Bwana</nd> aliyenipa shauri, </q1>
<q2>Naam, mtima wangu umenifundisha usiku. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Nimemweka 
<nd>Bwana</nd> mbele yangu daima, </q1>
<q2>Kwa kuwa yuko kuumeni kwangu, sitaondoshwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>16:8-11</xo>
<xt>Mdo 2:25-28</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Kwa hiyo moyo wangu unafurahi, </q1>
<q2>Nao utukufu wangu unashangilia, </q2>
<q2>Naam, mwili wangu nao utakaa kwa kutumaini. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Maana hutakuachia kuzimu nafsi yangu, </q1>
<q2>Wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>16:10</xo>
<xt>Mdo 13:35; Zab 49:15; Mdo 2:27; Dan 9:24; Lk 1:35</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Utanijulisha njia ya uzima; </q1>
<q2>Mbele za uso wako ziko furaha tele; </q2>
<q1>Na katika mkono wako wa kuume </q1>
<q2>Mna mema ya milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>16:11</xo>
<xt>Mdo 2:28</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>17</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, usikie haki, ukisikilize kilio changu, </q1>
<q2>Utege sikio lako kwa maombi yangu, </q2>
<q2>Yasiyotoka katika midomo ya hila. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Hukumu yangu na itoke kwako, </q1>
<q2>Macho yako na yatazame mambo ya adili. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Umenijaribu moyo wangu, umenijilia usiku, </q1>
<q2>Umenihakikisha usione neno; </q2>
<q2>Nimenuia kinywa changu kisikose, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>17:3</xo>
<xt>Ayu 23:10; Yak 3:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Mintarafu matendo ya wanadamu; </q1>
<q2>Kwa neno la midomo yako </q2>
<q2>Nimejiepusha na njia za wenye jeuri. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>17:4</xo>
<xt>Rum 12:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Nyayo zangu zimeshikamana na njia zako, </q1>
<q2>Hatua zangu hazikuondoshwa. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Ee Mungu, nimekuita kwa maana utaitika, </q1>
<q2>Utege sikio lako ulisikie neno langu. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Dhihirisha fadhili zako za ajabu </q1>
<q2>Wewe uwaokoaye wanaokukimbilia; </q2>
<q2>Kwa mkono wako wa kuume </q2>
<q1>Uwaokoe nao wanaowaondokea. </q1>
<q1><vn>8 </vn>Unilinde kama mboni ya jicho, </q1>
<q2>Unifiche chini ya uvuli wa mbawa zako; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>17:8</xo>
<xt>Kum 32:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Wasinione wasio haki wanaonionea, </q1>
<q2>Adui za roho yangu wanaonizunguka. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Wameukaza moyo wako, </q1>
<q2>Kwa vinywa vyao hutoa majivuno. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Sasa wametuzunguka hatua zetu, </q1>
<q2>Na kuyakaza macho yao watuangushe chini. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>17:11</xo>
<xt>1 Sam 23:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Kama mfano wa simba atakaye kurarua, </q1>
<q2>Kama mwana-simba aoteaye katika maoteo yake. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, usimame, umkabili, umwinamishe, </q1>
<q2>Kwa upanga wako uniokoe nafsi na mtu mbaya. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, kwa mkono wako uniokoe na watu, </q1>
<q2>Watu wa dunia hii ambao fungu lao li katika maisha haya. </q2>
<q2>Matumbo yao wayajaza kwa hazina yako, </q2>
<q1>Hushiba wana, huwaachia watoto wao akiba zao, </q1>
<q1><vn>15 </vn>Bali mimi nikutazame uso wako katika haki, </q1>
<q2>Niamkapo nishibishwe kwa sura yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>17:15</xo>
<xt>Ayu 19:26,27; Kol 1:15</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>18</cn>
<q1><vn>1 </vn>Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, nguvu zangu, nakupenda sana; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:1</xo>
<xt>Kum 32:4; 1 Sam 2:2; Zab 91:2</xt></note></f> </q1>
<q1><vn>2 </vn>
<nd>Bwana</nd> ni jabali langu, na boma langu, na mwokozi wangu, </q1>
<q1>Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia, </q1>
<q2>Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:2</xo>
<xt>Ebr 2:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Nitamwita 
<nd>Bwana</nd> astahiliye kusifiwa, </q1>
<q2>Hivyo nitaokoka na adui zangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:3</xo>
<xt>Zab 76:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Kamba za mauti zilinizunguka, </q1>
<q2>Mafuriko ya uovu yakanitia hofu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:4</xo>
<xt>Zab 116:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Kamba za kuzimu zilinizunguka, </q1>
<q2>Mitego ya mauti ikanikabili. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Katika shida yangu nalimwita 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Na kumlalamikia Mungu wangu. </q2>
<q1>Akaisikia sauti yangu hekaluni mwake, </q1>
<q2>Kilio changu kikaingia masikioni mwake. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ndipo nchi iliyotikisika na kutetemeka, </q1>
<q2>Misingi ya milima ikasuka-suka; </q2>
<q2>Ikatikisika kwa sababu alikuwa na ghadhabu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:7</xo>
<xt>Mdo 4:31</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Kukapanda moshi kutoka puani mwake, </q1>
<q2>Moto ukatoka kinywani mwake ukala, </q2>
<q2>Makaa yakawashwa nao. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Aliziinamisha mbingu akashuka, </q1>
<q2>Kukawa na giza kuu chini ya miguu yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:9</xo>
<xt>Isa 64:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Akapanda juu ya kerubi akaruka, </q1>
<q2>Naam, aliruka upesi juu ya mabawa ya upepo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:10</xo>
<xt>Zab 99:1; 104:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Alifanya giza kuwa mahali pake pa kujificha, </q1>
<q2>Kuwa hema yake ya kumzunguka. </q2>
<q2>Giza la maji na mawingu makuu ya mbinguni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:11</xo>
<xt>Zab 97:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Toka mwangaza uliokuwa mbele zake </q1>
<q2>Kukapita mawingu yake makuu. </q2>
<q2>Mvua ya mawe na makaa ya moto. </q2>
<q1><vn>13 </vn>
<nd>Bwana</nd> alipiga radi mbinguni, </q1>
<q2>Yeye Aliye juu akaitoa sauti yake, </q2>
<q2>Mvua ya mawe na makaa ya moto. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:13</xo>
<xt>Zab 29:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Akaipiga mishale yake akawatawanya, </q1>
<q2>Naam, umeme mwingi sana, akawatapanya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:14</xo>
<xt>Hes 24:8; Kum 32:23; Ayu 6:4; Zab 21:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Ndipo ilipoonekana mikondo ya maji, </q1>
<q2>Misingi ya ulimwengu ikafichuliwa, </q2>
<q1>Ee 
<nd>Bwana</nd>, kwa kukemea kwako, </q1>
<q2>Kwa mvumo wa pumzi ya puani mwako. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Alipeleka kutoka juu akanishika, </q1>
<q2>Na kunitoa katika maji mengi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:16</xo>
<xt>Zab 144:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Akaniokoa na adui yangu mwenye nguvu, </q1>
<q1>Na wale walionichukia, </q1>
<q2>Maana walikuwa na nguvu kuliko mimi. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Walinikabili siku ya msiba wangu, </q1>
<q2>Lakini 
<nd>Bwana</nd> alikuwa tegemeo langu. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Akanitoa akanipeleka panapo nafasi, </q1>
<q2>Aliniponya kwa kuwa alipendezwa nami. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:19</xo>
<xt>Zab 118:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>
<nd>Bwana</nd> alinitendea sawasawa na haki yangu, </q1>
<q2>Sawasawa na usafi wa mikono yangu akanilipa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:20</xo>
<xt>2 Sam 22:21; Mit 18:10; Mt 6:4; 1 Kor 3:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Maana nimezishika njia za 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Wala sikumwasi Mungu wangu. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Hukumu zake zote zilikuwa mbele yangu, </q1>
<q2>Wala amri zake sikujiepusha nazo. </q2>
<q1><vn>23 </vn>Nami nalikuwa mkamilifu mbele zake, </q1>
<q2>Nikajilinda na uovu wangu. </q2>
<q1><vn>24 </vn>Mradi 
<nd>Bwana</nd> amenilipa sawasawa na haki yangu, </q1>
<q2>Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:24</xo>
<xt>Rut 2:12; Mt 10:41,42</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>25 </vn>Kwa mtu mwenye fadhili utakuwa mwenye fadhili; </q1>
<q2>Kwa mkamilifu utajionyesha kuwa mkamilifu; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:25</xo>
<xt>Mt 18:32-35</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>26 </vn>Kwake ajitakasaye utajionyesha kuwa mtakatifu; </q1>
<q2>Na kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:26</xo>
<xt>Law 26:23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>27 </vn>Maana Wewe utawaokoa watu wanaoonewa, </q1>
<q2>Na macho ya kiburi utayadhili. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:27</xo>
<xt>Mit 6:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>28 </vn>Kwa kuwa Wewe unaiwasha taa yangu; </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> Mungu wangu aniangazia giza langu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:28</xo>
<xt>Ayu 18:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>29 </vn>Maana kwa msaada wako nafuatia jeshi, </q1>
<q2>Kwa msaada wa Mungu wangu naruka ukuta. </q2>
<q1><vn>30 </vn>Mungu, njia yake ni kamilifu, </q1>
<q2>Ahadi ya 
<nd>Bwana</nd> imehakikishwa, </q2>
<q1>Yeye ndiye ngao yao. </q1>
<q2>Wote wanaomkimbilia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:30</xo>
<xt>Kum 32:4; Rum 12:3; Ufu 15:3; Zab 12:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>31 </vn>Maana ni nani aliye Mungu ila 
<nd>Bwana</nd>? </q1>
<q2>Ni nani aliye mwamba ila Mungu wetu? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:31</xo>
<xt>Kum 32:31; 2 Sam 22:32</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>32 </vn>Mungu ndiye anifungaye mshipi wa nguvu, </q1>
<q2>Naye anaifanya kamilifu njia yangu. </q2>
<q1><vn>33 </vn>Miguu yangu anaifanya kuwa ya kulungu, </q1>
<q2>Na kunisimamisha mahali pangu pa juu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:33</xo>
<xt>Hab 3:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>34 </vn>Ananifundisha mikono yangu vita, </q1>
<q2>Mikono yangu ikaupinda upinde wa shaba. </q2>
<q1><vn>35 </vn>Nawe umenipa ngao ya wokovu wako, </q1>
<q1>Mkono wako wa kuume umenitegemeza, </q1>
<q2>Na unyenyekevu wako umenikuza. </q2>
<q1><vn>36 </vn>Umezifanyizia nafasi hatua zangu, </q1>
<q2>Na miguu yangu haikuteleza. </q2>
<q1><vn>37 </vn>Nitawafuatia adui zangu na kuwapata, </q1>
<q2>Wala sitarudi nyuma hata wakomeshwe. </q2>
<q1><vn>38 </vn>Nitawapiga-piga wasiweze kusimama, </q1>
<q2>Wataanguka chini ya miguu yangu. </q2>
<q1><vn>39 </vn>Nawe hunifunga mshipi wa nguvu kwa vita, </q1>
<q2>Hunitiishia chini yangu walioniondokea. </q2>
<q1><vn>40 </vn>Naam, adui zangu umewafanya wanipe visogo, </q1>
<q2>Nao walionichukia nimewakatilia mbali. </q2>
<q1><vn>41 </vn>Walipiga yowe, lakini hakuna wa kuokoa, </q1>
<q2>Walimwita 
<nd>Bwana</nd> lakini hakuwajibu, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:41</xo>
<xt>Mit 1:28</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>42 </vn>Nikawaponda kama mavumbi mbele ya upepo, </q1>
<q2>Nikawatupa nje kama matope ya njiani. </q2>
<q1><vn>43 </vn>Umeniokoa na mashindano ya watu, </q1>
<q2>Umenifanya niwe kichwa cha mataifa. </q2>
<q2>Watu nisiowajua walinitumikia. </q2>
<q1><vn>44 </vn>Kwa kusikia tu habari zangu, </q1>
<q2>Mara wakanitii. </q2>
<q2>Wageni walinijia wakinyenyekea. </q2>
<q1><vn>45 </vn>Wageni nao walitepetea, </q1>
<q2>Walitoka katika ngome zao wakitetemeka. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:45</xo>
<xt>Mik 7:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>46 </vn>
<nd>Bwana</nd> ndiye aliye hai; </q1>
<q2>Na ahimidiwe mwamba wangu; </q2>
<q2>Na atukuzwe Mungu wa wokovu wangu; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:46</xo>
<xt>Yer 10:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>47 </vn>Ndiye Mungu anipatiaye kisasi; </q1>
<q2>Na kuwatiisha watu chini yangu. </q2>
<q1><vn>48 </vn>Huniponya na adui zangu; </q1>
<q2>Naam, waniinua juu yao walioniinukia, </q2>
<q2>Na kuniponya na mtu wa jeuri. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:48</xo>
<xt>Zab 59:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>49 </vn>Basi, 
<nd>Bwana</nd>, nitakushukuru kati ya mataifa, </q1>
<q2>Nami nitaliimbia jina lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:49</xo>
<xt>Rum 15:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>50 </vn>Ampa mfalme wake wokovu mkuu, </q1>
<q2>Amfanyia fadhili masihi<f> <fn>c</fn><note>
<fr>18:50</fr>
<ft> Au, mtiwa mafuta.</ft></note></f> wake, </q2>
<q2>Daudi na mzao wake hata milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>18:50</xo>
<xt>Zab 144:10</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>19</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, </q1>
<q2>Na anga laitangaza kazi ya mikono yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>19:1</xo>
<xt>Isa 40:22; Rum 1:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Mchana husemezana na mchana, </q1>
<q2>Usiku hutolea usiku maarifa. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Hakuna lugha wala maneno, </q1>
<q2>Sauti yao haisikilikani. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Sauti yao imeenea duniani mwote, </q1>
<q2>Na maneno yao hata miisho ya ulimwengu. </q2>
<q1>Katika hizo ameliwekea jua hema, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>19:4</xo>
<xt>Rum 10:18</xt></note></f> </q1>
<q2><vn>5 </vn>Kama bwana arusi akitoka chumbani mwake, </q2>
<q1>Lafurahi kama mtu aliye hodari </q1>
<q2>Kwenda mbio katika njia yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>19:5</xo>
<xt>Mhu 11:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Kutoka kwake lautoka mwisho wa mbingu, </q1>
<q2>Na kuzunguka kwake hata miisho yake, </q2>
<q1>Wala kwa hari yake </q1>
<q2>Hakuna kitu kilichositirika. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>19:6</xo>
<xt>Mhu 1:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Sheria ya 
<nd>Bwana</nd> ni kamilifu, </q1>
<q2>Huiburudisha nafsi. </q2>
<q1>Ushuhuda wa 
<nd>Bwana</nd> ni amini, </q1>
<q2>Humtia mjinga hekima. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Maagizo ya 
<nd>Bwana</nd> ni ya adili, </q1>
<q2>Huufurahisha moyo. </q2>
<q1>Amri ya 
<nd>Bwana</nd> ni safi, </q1>
<q2>Huyatia macho nuru. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>19:8</xo>
<xt>Neh 9:13; Rum 7:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Kicho cha 
<nd>Bwana</nd> ni kitakatifu, </q1>
<q2>Kinadumu milele. </q2>
<q1>Hukumu za 
<nd>Bwana</nd> ni kweli, </q1>
<q2>Zina haki kabisa. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Ni za kutamanika kuliko dhahabu, </q1>
<q2>Kuliko wingi wa dhahabu safi. </q2>
<q1>Nazo ni tamu kuliko asali, </q1>
<q2>Kuliko sega la asali. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Tena mtumishi wako huonywa kwazo, </q1>
<q2>Katika kuzishika kuna thawabu nyingi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>19:11</xo>
<xt>Mit 6:22,23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Ni nani awezaye kuyatambua makosa yake? </q1>
<q2>Unitakase na mambo ya siri. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Umzuie mtumishi wako asitende mambo ya kiburi, </q1>
<q2>Yasinitawale mimi. </q2>
<q1>Ndipo nitakapokuwa kamili, </q1>
<q2>Nami nitakuwa safi, sina kosa lililo kubwa. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Maneno ya kinywa changu, </q1>
<q2>Na mawazo ya moyo wangu, </q2>
<q1>Yapate kibali mbele zako, Ee 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Mwamba wangu, na mwokozi wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>19:14</xo>
<xt>Isa 44:6</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>20</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd> akujibu siku ya dhiki, </q1>
<q2>Jina la Mungu wa Yakobo likuinue. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>20:1</xo>
<xt>Isa 50:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Akupelekee msaada toka patakatifu pake, </q1>
<q2>Na kukutegemeza toka Sayuni. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Azikumbuke sadaka zako zote, </q1>
<q2>Na kuzitakabali dhabihu zako. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako, </q1>
<q2>Na kuyatimiza mashauri yako yote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>20:4</xo>
<xt>1 Yoh 5:14,15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Na tuushangilie wokovu wako, </q1>
<q2>Kwa jina la Mungu wetu tuzitweke bendera zetu. </q2>
<q2>
<nd>Bwana</nd> akutimizie matakwa yako yote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>20:5</xo>
<xt>Isa 12:1,2; 1 Sam 17:45</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Sasa najua kuwa 
<nd>Bwana</nd> amwokoa masihi<f> <fn>d</fn><note>
<fr>28:6</fr>
<ft> Au, mtiwa mafuta.</ft></note></f> wake; </q1>
<q2>Atamjibu toka mbingu zake takatifu, </q2>
<q1>Kwa matendo makuu ya wokovu </q1>
<q2>Ya mkono wake wa kuume. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Hawa wanataja magari na hawa farasi, </q1>
<q2>Bali sisi tutalitaja jina la 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wetu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>20:7</xo>
<xt>Amu 7:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Wao wameinama na kuanguka, </q1>
<q2>Bali sisi tumeinuka na kusimama. </q2>
<q1><vn>9 </vn>
<nd>Bwana</nd>, umwokoe mfalme, </q1>
<q2>Utuitikie siku tuitayo. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>21</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, mfalme atazifurahia nguvu zako, </q1>
<q2>Na wokovu wako ataufanyia shangwe nyingi sana. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Umempa haja ya moyo wake, </q1>
<q2>Wala hukumzuilia matakwa ya midomo yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>21:2</xo>
<xt>Yn 11:42</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Maana umemsogezea baraka za heri, </q1>
<q2>Umemvika taji ya dhahabu safi kichwani pake. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Alikuomba uhai, ukampa, </q1>
<q2>Muda mrefu wa siku nyingi, milele na milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>21:4</xo>
<xt>2 Sam 7:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Utukufu wake ni mkuu kwa wokovu wako, </q1>
<q2>Heshima na adhama waweka juu yake. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Maana umemfanya kuwa baraka za milele, </q1>
<q2>Wamfurahisha kwa furaha ya uso wako. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Kwa kuwa mfalme humtumaini 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Na kwa fadhili zake Aliye juu hataondoshwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>21:7</xo>
<xt>Zab 91:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Mkono wako utawapata adui zako wote, </q1>
<q2>Mkono wako wa kuume utawapata wanaokuchukia. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Utawafanya kuwa kama tanuru ya moto, </q1>
<q2>Wakati wa ghadhabu yako. </q2>
<q1>
<nd>Bwana</nd> atawameza kwa ghadhabu yake, </q1>
<q2>Na moto utawala. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>21:9</xo>
<xt>Kum 32:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Matunda yao utayaharibu na kuyaondoa katika nchi, </q1>
<q2>Na wazao wao katika wanadamu. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Madhali walinuia kukutenda mabaya, </q1>
<q2>Waliwaza hila wasipate kuitimiza. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Kwa maana utawafanya kukupa kisogo, </q1>
<q2>Kwa upote wa uta wako ukiwaelekezea mishale. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, utukuzwe kwa nguvu zako, </q1>
<q2>Nasi tutaimba na kuuhimidi uweza wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>21:13</xo>
<xt>Ufu 15:3,4</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>22</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mungu wangu, Mungu wangu, </q1>
<q2>Mbona umeniacha? </q2>
<q1>Mbona U mbali na wokovu wangu, </q1>
<q2>Na maneno ya kuugua kwangu? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>22:1</xo>
<xt>Mt 27:46; Mk 15:34; Ebr 5:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu </q1>
<q2>Na wakati wa usiku lakini sipati raha. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Na Wewe U Mtakatifu, </q1>
<q2>Uketiye juu ya sifa za Israeli. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>22:3</xo>
<xt>Isa 6:3; Ufu 4:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Baba zetu walikutumaini Wewe, </q1>
<q2>Walitumaini, na Wewe ukawaokoa. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Walikulilia Wewe wakaokoka, </q1>
<q2>Walikutumaini wasiaibike. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Lakini mimi ni mdudu wala si mtu, </q1>
<q2>Laumu ya wanadamu na mzaha wa watu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>22:6</xo>
<xt>Isa 53:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Wote wanionao hunicheka sana, </q1>
<q2>Hunifyonya, wakitikisa vichwa vyao; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>22:7</xo>
<xt>Mt 27:39; 9:24; Mk 15:20,29; Lk 23:35; 16:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Husema, Umtegemee 
<nd>Bwana</nd>; na amponye; </q1>
<q2>Na amwokoe sasa, maana apendezwa naye. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>22:8</xo>
<xt>Mt 27:43</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Naam, Wewe ndiwe uliyenitoa tumboni, </q1>
<q2>Ulinitumainisha matitini mwa mama yangu. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Kwako nalitupwa tangu tumboni, </q1>
<q2>Toka tumboni mwa mamangu ndiwe Mungu wangu. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Usiwe mbali nami maana taabu i karibu, </q1>
<q2>Kwa maana hakuna msaidizi. </q2>
<b></b>
<q1><vn>12 </vn>Mafahali wengi wamenizunguka, </q1>
<q2>Walio hodari wa Bashani wamenisonga; </q2>
<q1><vn>13 </vn>Wananifumbulia vinywa vyao, </q1>
<q2>Kama simba apapuraye na kunguruma. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>22:13</xo>
<xt>Zab 35:21; 1 Pet 5:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Nimemwagika kama maji, </q1>
<q2>Mifupa yangu yote imeteguka, </q2>
<q1>Moyo wangu umekuwa kama nta, </q1>
<q2>Na kuyeyuka ndani ya mtima wangu. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Nguvu zangu zimekauka kama gae, </q1>
<q2>Ulimi wangu waambatana na taya zangu; </q2>
<q2>Unaniweka katika mavumbi ya mauti <f> <fn>-</fn><note>
<xo>22:15</xo>
<xt>Mit 17:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Kwa maana mbwa wamenizunguka; </q1>
<q2>Kusanyiko la waovu wamenisonga; </q2>
<q2>Wamenizua mikono na miguu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>22:16</xo>
<xt>Zek 12:10; Lk 23:33; Yn 20:27</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Naweza kuihesabu mifupa yangu yote; </q1>
<q2>Wao wananitazama na kunikodolea macho. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Wanagawanya nguo zangu, </q1>
<q2>Na vazi langu wanalipigia kura. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>22:18</xo>
<xt>Mt 27:35; Mk 15:24; Luk 23:34; Yn 19:24</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Nawe, 
<nd>Bwana</nd>, usiwe mbali, </q1>
<q2>Ee Nguvu zangu, fanya haraka kunisaidia. </q2>
<q1><vn>20 </vn>Uniponye nafsi yangu na upanga, </q1>
<q2>Mpenzi wangu na nguvu za mbwa. </q2>
<q1><vn>21 </vn>Kinywani mwa simba uniokoe; </q1>
<q2>Naam, toka pembe za nyati umenijibu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>22:21</xo>
<xt>2 Tim 4:17</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>22 </vn>Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu, </q1>
<q2>Katikati ya kusanyiko nitakusifu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>22:22</xo>
<xt>Ebr 2:12; Yn 20:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>23 </vn>Ninyi mnaomcha 
<nd>Bwana</nd>, msifuni, </q1>
<q2>Enyi nyote mlio wazao wa Yakobo, mtukuzeni, </q2>
<q2>Mcheni, enyi nyote mlio wazao wa Israeli. </q2>
<q1><vn>24 </vn>Maana hakulidharau teso la mteswa, </q1>
<q2>Wala hakuchukizwa nalo; </q2>
<q1>Wala hakumficha uso wake, </q1>
<q2>Bali alipomlilia akamsikia. </q2>
<q1><vn>25 </vn>Kwako zinatoka sifa zangu </q1>
<q2>Katika kusanyiko kubwa. </q2>
<q1>Nitaziondoa nadhiri zangu </q1>
<q2>Mbele yao wamchao. </q2>
<q1><vn>26 </vn>Wapole watakula na kushiba, </q1>
<q2>Wamtafutao 
<nd>Bwana</nd> watamsifu; </q2>
<q1>Mioyo yenu na iishi milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>22:26</xo>
<xt>Yn 6:57,51</xt></note></f> </q1>
<q2><vn>27 </vn>Miisho yote ya dunia itakumbuka, </q2>
<q1>Na watu watamrejea 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Jamaa zote za mataifa watamsujudia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>22:27</xo>
<xt>Zab 2:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>28 </vn>Maana ufalme una 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Naye ndiye awatawalaye mataifa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>22:28</xo>
<xt>Zab 47:7-9; Zek 14:9; Mt 6:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>29 </vn>Wakwasi wote wa dunia watakula na kusujudu, </q1>
<q2>Humwinamia wote washukao mavumbini; </q2>
<q1>Naam, yeye asiyeweza kujihuisha nafsi yake, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>22:29</xo>
<xt>Isa 26:19</xt></note></f> </q1>
<q2><vn>30 </vn>Wazao wake watamtumikia. </q2>
<q1>Zitasimuliwa habari za 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Kwa kizazi kitakachokuja, </q2>
<q1><vn>31 </vn>Nao watawahubiri watakaozaliwa haki yake, </q1>
<q2>Ya kwamba ndiye aliyeyafanya. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>23</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd> ndiye mchungaji wangu, </q1>
<q2>Sitapungukiwa na kitu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>23:1</xo>
<xt>Yn 10:11; 1 Pet 2:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, </q1>
<q2>Kando ya maji ya utulivu huniongoza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>23:2</xo>
<xt>Ufu 7:17; Eze 34:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza </q1>
<q2>Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, </q1>
<q2>Sitaogopa mabaya; </q2>
<q1>Kwa maana Wewe upo pamoja nami, </q1>
<q2>Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>23:4</xo>
<xt>Zab 46:11; Isa 8:10; Zek 8:23; Mt 1:23; Mdo 18:9,10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Waandaa meza mbele yangu, </q1>
<q2>Machoni pa watesi wangu. </q2>
<q1>Umenipaka mafuta kichwani pangu, </q1>
<q2>Na kikombe changu kinafurika. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Hakika wema na fadhili zitanifuata </q1>
<q2>Siku zote za maisha yangu; </q2>
<q1>Nami nitakaa nyumbani mwa 
<nd>Bwana</nd> milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>23:6</xo>
<xt>2 Kor 5:1</xt></note></f> </q1>
<b></b></c>

<c><cn>24</cn>
<q1><vn>1 </vn>Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Dunia na wote wakaao ndani yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>24:1</xo>
<xt>1 Kor 10:26; Kut 9:29; Ayu 41:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Maana ameiweka misingi yake juu ya bahari, </q1>
<q2>Na juu ya mito ya maji aliithibitisha. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Ni nani atakayepanda katika mlima wa 
<nd>Bwana</nd>? </q1>
<q2>Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake? </q2>
<q1><vn>4 </vn>Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, </q1>
<q1>Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili, </q1>
<q2>Wala hakuapa kwa hila. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>24:4</xo>
<xt>Mt 5:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Atapokea baraka kwa 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Na haki kwa Mungu wa wokovu wake. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Hiki ndicho kizazi cha wamtafutao, </q1>
<q2>Wakutafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Inueni vichwa vyenu, enyi malango, </q1>
<q2>Inukeni, enyi malango ya milele, </q2>
<q2>Mfalme wa utukufu apate kuingia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>24:7</xo>
<xt>Hag 2:7; Mal 3:1; 1 Kor 2:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ni nani Mfalme wa utukufu? </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> mwenye nguvu, hodari, </q2>
<q2>
<nd>Bwana</nd> hodari wa vita. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Inueni vichwa vyenu, enyi malango, </q1>
<q2>Naam, viinueni, enyi malango ya milele, </q2>
<q2>Mfalme wa utukufu apate kuingia. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Ni nani huyu Mfalme wa utukufu? </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> wa majeshi, </q2>
<q2>Yeye ndiye Mfalme wa utukufu. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>25</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, nakuinulia nafsi yangu, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>25:1</xo>
<xt>1 Sam 1:15; Zab 86:4; Omb 3:41</xt></note></f> </q1>
<q1><vn>2 </vn>Ee Mungu wangu, </q1>
<q1>Nimekutumaini Wewe, nisiaibike, </q1>
<q2>Adui zangu wasifurahi kwa kunishinda. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>25:2</xo>
<xt>Zab 7:1; 18:2; Rum 10:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Naam, wakungojao hawataaibika hata mmoja; </q1>
<q2>Wataaibika watendao uhaini bila sababu. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unijulishe njia zako, </q1>
<q2>Unifundishe mapito yako, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>25:4</xo>
<xt>Kut 33:13; Zab 143:8; Mit 8:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Uniongoze katika kweli yako, </q1>
<q2>Na kunifundisha. </q2>
<q1>Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu, </q1>
<q2>Nakungoja Wewe mchana kutwa. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, kumbuka rehema zako na fadhili zako, </q1>
<q2>Maana zimekuwako tokea zamani. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Usiyakumbuke makosa ya ujana wangu, </q1>
<q2>Wala maasi yangu. </q2>
<q1>Unikumbuke kwa kadiri ya fadhili zako, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd> kwa ajili ya wema wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>25:7</xo>
<xt>Zab 51:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>
<nd>Bwana</nd> yu mwema, mwenye adili, </q1>
<q2>Kwa hiyo atawafundisha wenye dhambi njia. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Wenye upole atawaongoza katika hukumu, </q1>
<q2>Wenye upole atawafundisha njia yake. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Njia zote za 
<nd>Bwana</nd> ni fadhili na kweli, </q1>
<q2>Kwao walishikao agano lake na shuhuda zake. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, kwa ajili ya jina lako, </q1>
<q2>Unisamehe uovu wangu, maana ni mwingi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>25:11</xo>
<xt>Zab 31:3; 79:9; Rum 5:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Ni nani amchaye 
<nd>Bwana</nd>? </q1>
<q2>Atamfundisha katika njia anayoichagua. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>25:12</xo>
<xt>Zab 37:23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Nafsi yake itakaa hali ya kufanikiwa; </q1>
<q2>Wazao wake watairithi nchi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>25:13</xo>
<xt>Zab 37:11,22,29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Siri ya 
<nd>Bwana</nd> iko kwao wamchao, </q1>
<q2>Naye atawajulisha agano lake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>25:14</xo>
<xt>Mit 3:32; Yn 7:17; 2 Kor 4:2-6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Macho yangu humwelekea 
<nd>Bwana</nd> daima, </q1>
<q2>Naye atanitoa miguu yangu katika wavu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>25:15</xo>
<xt>Zab 141:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Uniangalie na kunifadhili, </q1>
<q2>Maana mimi ni mkiwa na mteswa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>25:16</xo>
<xt>Zab 69:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Katika shida za moyo wangu unifanyie nafasi, </q1>
<q2>Na kunitoa katika dhiki zangu. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Utazame teso langu na taabu yangu; </q1>
<q2>Unisamehe dhambi zangu zote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>25:18</xo>
<xt>2 Sam 16:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Uwatazame adui zangu, maana ni wengi, </q1>
<q2>Wananichukia kwa machukio ya ukali. </q2>
<q1><vn>20 </vn>Unilinde nafsi yangu na kuniponya, </q1>
<q2>Nisiaibike, maana nakukimbilia Wewe. </q2>
<q1><vn>21 </vn>Ukamilifu na unyofu zinihifadhi, </q1>
<q2>Maana nakungoja Wewe. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Ee Mungu, umkomboe Israeli, </q1>
<q2>Katika taabu zake zote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>25:22</xo>
<xt>Zab 130:8</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>26</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unihukumu mimi, </q1>
<q1>Maana nimekwenda kwa ukamilifu wangu, </q1>
<q2>Nami nimemtumaini 
<nd>Bwana</nd> bila wasiwasi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>26:1</xo>
<xt>Zab 7:8; 28:7; Mit 29:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unijaribu na kunipima; </q1>
<q2>Unisafishe mtima wangu na moyo wangu. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Maana fadhili zako zi mbele ya macho yangu, </q1>
<q2>Nami nimekwenda katika kweli yako. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Sikuketi pamoja na watu wa ubatili, </q1>
<q2>Wala sitaingia mnamo wanafiki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>26:4</xo>
<xt>Zab 1:1; Yer 15:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Nimelichukia kusanyiko la watenda mabaya, </q1>
<q2>Wala sitaketi pamoja na watu waovu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>26:5</xo>
<xt>Zab 5:5; 15:4; 31:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nitanawa mikono yangu kwa kutokuwa na hatia, </q1>
<q2>Na kuizunguka madhabahu yako, Ee 
<nd>Bwana</nd> <f> <fn>-</fn><note>
<xo>26:6</xo>
<xt>Kut 30:19; Zab 73:13; 1 Tim 2:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ili niitangaze sauti ya kushukuru, </q1>
<q2>Na kuzisimulia kazi zako za ajabu. </q2>
<q1><vn>8 </vn>
<nd>Bwana</nd>, nimependa makao ya nyumba yako, </q1>
<q2>Na mahali pa maskani ya utukufu wako. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Usiiondoe nafsi yangu pamoja na wakosaji, </q1>
<q2>Wala uhai wangu pamoja na watu wa damu. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Mikononi mwao mna madhara, </q1>
<q2>Na mkono wao wa kuume umejaa rushwa. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Ila mimi nitakwenda kwa ukamilifu wangu; </q1>
<q2>Unikomboe, unifanyie fadhili. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Mguu wangu umesimama palipo sawa; </q1>
<q2>Katika makusanyiko nitamhimidi 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>27</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd> ni nuru yangu na wokovu wangu, </q1>
<q2>Nimwogope nani? </q2>
<q1>
<nd>Bwana</nd> ni ngome ya uzima wangu, </q1>
<q2>Nimhofu nani? </q2>
<q1><vn>2 </vn>Watenda mabaya waliponikaribia, </q1>
<q2>Wanile nyama yangu, </q2>
<q1>Watesi wangu na adui zangu, </q1>
<q2>Walijikwaa wakaanguka. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Jeshi lijapojipanga kupigana nami, </q1>
<q2>Moyo wangu hautaogopa. </q2>
<q1>Vita vijaponitokea, </q1>
<q2>Hata hapo nitatumaini. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Neno Moja nimelitaka kwa 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Nalo ndilo nitakalolitafuta, </q2>
<q1>Nikae nyumbani mwa 
<nd>Bwana</nd> </q1>
<q2>Siku zote za maisha yangu, </q2>
<q1>Niutazame uzuri wa 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Na kutafakari hekaluni mwake. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Mradi atanisitiri bandani mwake siku ya mabaya, </q1>
<q2>Atanisitiri katika sitara ya hema yake, </q2>
<q2>Na kuniinua juu ya mwamba. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>27:5</xo>
<xt>Mit 18:10; Isa 4:6; Kol 3:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Na sasa kichwa changu kitainuka </q1>
<q2>Juu ya adui zangu wanaonizunguka. </q2>
<q1>Nami nitatoa dhabihu za shangwe hemani mwake; </q1>
<q2>Nitaimba, naam, nitamhimidi 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, usikie, kwa sauti yangu ninalia, </q1>
<q2>Unifadhili, unijibu. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Uliposema, Nitafuteni uso wangu, </q1>
<q2>Moyo wangu umekuambia, </q2>
<q2>
<nd>Bwana</nd>, uso wako nitautafuta. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Usinifiche uso wako, </q1>
<q2>Usijiepushe na mtumishi wako kwa hasira. </q2>
<q1>Umekuwa msaada wangu, usinitupe, </q1>
<q2>Wala usiniache, Ee Mungu wa wokovu wangu. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Baba yangu na mama yangu wameniacha, </q1>
<q2>Bali 
<nd>Bwana</nd> atanikaribisha kwake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>27:10</xo>
<xt>Isa 49:15; Yn 16:32; 2 Tim 4:16-18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unifundishe njia yako, </q1>
<q2>Na kuniongoza katika njia iliyonyoka; </q2>
<q1>Kwa sababu yao wanaoniotea; </q1>
<q2><vn>12 </vn>Usinitie katika nia ya watesi wangu; </q2>
<q1>Maana mashahidi wa uongo wameniondokea, </q1>
<q2>Nao watoao jeuri kama pumzi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>27:12</xo>
<xt>1 Sam 22:9; Mt 26:59,60</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Naamini ya kuwa nitauona wema wa 
<nd>Bwana</nd> </q1>
<q2>Katika nchi ya walio hai. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>27:13</xo>
<xt>Zab 112:7,8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Umngoje 
<nd>Bwana</nd>, uwe hodari, </q1>
<q2>Upige moyo konde, naam, umngoje 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>27:14</xo>
<xt>Zab 62:1,5; Isa 25:9; Hab 2:3</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>28</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, nitakuita Wewe, mwamba wangu, </q1>
<q2>Usiwe kwangu kama kiziwi. </q2>
<q1>Nisije nikafanana nao washukao shimoni, </q1>
<q2>Ikiwa umeninyamalia. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Uisikie sauti ya dua yangu nikuombapo, </q1>
<q2>Nikipainulia patakatifu pako mikono yangu. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Usinikokote pamoja na wasio haki, </q1>
<q2>Wala pamoja na watenda maovu. </q2>
<q1>Wawaambiao jirani zao maneno ya amani, </q1>
<q2>Lakini mioyoni mwao mna madhara. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Uwape sawasawa na vitendo vyao, </q1>
<q2>Na kwa kadiri ya ubaya wa kufanya kwao, </q2>
<q2>Uwape sawasawa na kazi ya mikono yao, </q2>
<q2>Uwalipe stahili zao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>28:4</xo>
<xt>Ufu 22:12; 2 Tim 4:14</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>5 </vn>Maana hawazifahamu kazi za 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Wala matendo ya mikono yake. </q2>
<q2>Atawavunja wala hatawajenga; </q2>
<q1><vn>6 </vn>Na ahimidiwe 
<nd>Bwana</nd>. </q1>
<q2>Maana ameisikia sauti ya dua yangu; </q2>
<q1><vn>7 </vn>
<nd>Bwana</nd> ni nguvu zangu na ngao yangu. </q1>
<q2>Moyo wangu umemtumaini, </q2>
<q1>Nami nimesaidiwa; </q1>
<q2>Basi, moyo wangu unashangilia, </q2>
<q2>Na kwa wimbo wangu nitamshukuru. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>28:7</xo>
<xt>Zab 18:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>
<nd>Bwana</nd> ni nguvu za watu wake, </q1>
<q2>Naye ni ngome ya wokovu kwa masihi<f> <fn>e</fn><note>
<fr>28:8</fr>
<ft> Au, mtiwa mafuta.</ft></note></f> wake. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Uwaokoe watu wako, uubariki urithi wako, </q1>
<q2>Uwachunge, uwachukue milele. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>29</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mpeni 
<nd>Bwana</nd>, enyi wana wa Mungu, </q1>
<q2>Mpeni 
<nd>Bwana</nd> utukufu na nguvu; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>29:1-2</xo>
<xt>Zab 96:7-9; 1 Nya 16:28,29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Mpeni 
<nd>Bwana</nd> utukufu wa jina lake; </q1>
<q2>Mwabuduni 
<nd>Bwana</nd> kwa uzuri wa utakatifu. </q2>
<b></b>
<q1><vn>3 </vn>Sauti ya 
<nd>Bwana</nd> i juu ya maji; </q1>
<q2>Mungu wa utukufu alipiga radi; </q2>
<q2>
<nd>Bwana</nd> yu juu ya maji mengi. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Sauti ya 
<nd>Bwana</nd> ina nguvu; </q1>
<q2>Sauti ya 
<nd>Bwana</nd> ina adhama; </q2>
<q1><vn>5 </vn>Sauti ya 
<nd>Bwana</nd> yaivunja mierezi; </q1>
<q2>Naam, 
<nd>Bwana</nd> aivunja-vunja mierezi ya Lebanoni; </q2>
<q1><vn>6 </vn>Airusha-rusha kama ndama wa ng'ombe; </q1>
<q2>Lebanoni na Sirioni kama mwana-nyati. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>29:6</xo>
<xt>Zab 114:4; Kum 3:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Sauti ya 
<nd>Bwana</nd> yaipasua miali ya moto; </q1>
<q1><vn>8 </vn>Sauti ya 
<nd>Bwana</nd> yalitetemesha jangwa; </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> alitetemesha jangwa la Kadeshi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>29:8</xo>
<xt>Hes 13:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Sauti ya 
<nd>Bwana</nd> yawazalisha ayala, </q1>
<q2>Na kuifichua misitu; </q2>
<q1>Na ndani ya hekalu lake </q1>
<q2>Wanasema wote, Utukufu. </q2>
<q1><vn>10 </vn>
<nd>Bwana</nd> aliketi juu ya Gharika; </q1>
<q2>Naam, 
<nd>Bwana</nd> ameketi hali ya mfalme milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>29:10</xo>
<xt>Zab 93:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>
<nd>Bwana</nd> atawapa watu wake nguvu; </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> atawabariki watu wake kwa amani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>29:11</xo>
<xt>Isa 40:29</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>30</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, nitakutukuza kwa maana umeniinua, </q1>
<q2>Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wangu, </q1>
<q2>Nalikulilia ukaniponya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>30:2</xo>
<xt>Zab 6:2-4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Umeniinua nafsi yangu, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, kutoka kuzimu. </q2>
<q1>Umenihuisha na kunitoa </q1>
<q2>Miongoni mwao washukao shimoni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>30:3</xo>
<xt>Zab 40:1,2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Mwimbieni 
<nd>Bwana</nd> zaburi, </q1>
<q2>Enyi watauwa wake. </q2>
<q1>Na kufanya shukrani. </q1>
<q2>Kwa kumbukumbu la utakatifu wake. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo, </q1>
<q2>Katika radhi yake mna uhai. </q2>
<q1>Huenda kilio huja kukaa usiku, </q1>
<q2>Lakini asubuhi huwa furaha. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>30:5</xo>
<xt>Zab 16:11; Ufu 22:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nami nilipofanikiwa nalisema, </q1>
<q2>Sitaondoshwa milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>30:6</xo>
<xt>Ayu 29:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>
<nd>Bwana</nd>, kwa radhi yako </q1>
<q2>Wewe uliuimarisha mlima wangu. </q2>
<q1>Uliuficha uso wako, </q1>
<q2>Nami nikafadhaika. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>30:7</xo>
<xt>Zab 104:29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, nalikulilia Wewe, </q1>
<q2>Naam, kwa 
<nd>Bwana</nd> naliomba dua. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Mna faida gani katika damu yangu </q1>
<q2>Nishukapo shimoni? </q2>
<q1>Mavumbi yatakusifu? </q1>
<q2>Yataitangaza kweli yako? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>30:9</xo>
<xt>Zab 115:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, usikie, unirehemu, </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd>, uwe msaidizi wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>30:10</xo>
<xt>Zab 4:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Uligeuza matanga yangu kuwa machezo; </q1>
<q2>Ulinivua gunia, ukanivika furaha. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>30:11</xo>
<xt>2 Sam 6:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Ili utukufu wangu ukusifu, </q1>
<q2>Wala usinyamaze. </q2>
<q1>Ee 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wangu, </q1>
<q2>Nitakushukuru milele. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>31</cn>
<q1><vn>1 </vn>Nimekukimbilia Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Nisiaibike milele. </q2>
<q2>Kwa haki yako uniponye, </q2>
<q1><vn>2 </vn>Unitegee sikio lako, uniokoe hima. </q1>
<q2>Uwe kwangu mwamba wa nguvu, </q2>
<q2>Nyumba yenye maboma ya kuniokoa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>31:2</xo>
<xt>Zab 71:2; Mit 22:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Ndiwe genge langu na ngome yangu; </q1>
<q2>Kwa ajili ya jina lako uniongoze, unichunge. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>31:3</xo>
<xt>Zab 23:3; Yer 14:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Utanitoa katika wavu walionitegea kwa siri, </q1>
<q2>Maana Wewe ndiwe ngome yangu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Mikononi mwako naiweka roho yangu; </q1>
<q2>Umenikomboa, Ee 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wa kweli. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>31:5</xo>
<xt>Lk 23:46; Mdo 7:59; 2 Tim 1:12; Ebr 6:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nawachukia wao washikao yasiyofaa yenye uongo; </q1>
<q2>Bali mimi namtumaini 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Na nishangilie, nizifurahie fadhili zako, </q1>
<q2>Kwa kuwa umeyaona mateso yangu. </q2>
<q2>Umeijua nafsi yangu taabuni, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>31:7</xo>
<xt>Yn 10:27</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Wala hukunitia mikononi mwa adui; </q1>
<q2>Miguu yangu umeisimamisha panapo nafasi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>31:8</xo>
<xt>Zab 18:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unifadhili, maana ni katika dhiki, </q1>
<q2>Jicho langu limenyauka kwa masumbufu, </q2>
<q2>Naam, mwili wangu na nafsi yangu. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Maana maisha yangu yamekoma kwa huzuni, </q1>
<q2>Na miaka yangu kwa kuugua. </q2>
<q1>Nguvu zangu zinatetemeka kwa uovu wangu, </q1>
<q2>Na mifupa yangu imekauka. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Kwa sababu ya watesi wangu nimekuwa laumu, </q1>
<q2>Naam, hasa kwa jirani zangu; </q2>
<q1>Na kitu cha kutisha kwa rafiki zangu; </q1>
<q2>Walioniona njiani walinikimbia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>31:11</xo>
<xt>Zab 88:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Nimesahauliwa kama mfu asiyekumbukwa; </q1>
<q2>Nimekuwa kama chombo kilichovunjika. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Maana nimesikia masingizio ya wengi; </q1>
<q2>Hofu ziko pande zote. </q2>
<q1>Waliposhauriana juu yangu, </q1>
<q2>Walifanya hila wauondoe uhai wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>31:13</xo>
<xt>Yer 20:3; Omb 2:22; Mt 27:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Lakini mimi nakutumaini Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Nimesema, Wewe ndiwe Mungu wangu. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Nyakati zangu zimo mikononi mwako; </q1>
<q2>Uniponye na adui zangu, nao wanaonifuatia. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Umwangaze mtumishi wako </q1>
<q2>Kwa nuru ya uso wako; </q2>
<q2>Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>31:16</xo>
<xt>Hes 6:25; Zab 4:6; Dan 9:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, nisiaibishwe, maana nimekuita; </q1>
<q2>Waaibishwe wasio haki, wanyamaze kuzimuni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>31:17</xo>
<xt>Zab 25:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>Midomo ya uongo iwe na ububu, </q1>
<q2>Imneneayo mwenye haki maneno ya kiburi, </q2>
<q2>Kwa majivuno na dharau. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>31:18</xo>
<xt>Zab 12:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Jinsi zilivyo nyingi fadhili zako </q1>
<q2>Ulizowawekea wakuchao; </q2>
<q1>Ulizowatendea wakukimbiliao </q1>
<q2>Mbele ya wanadamu! <f> <fn>-</fn><note>
<xo>31:19</xo>
<xt>Isa 64:4; 1 Kor 2:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Utawasitiri na fitina za watu </q1>
<q2>Katika sitara ya kuwapo kwako; </q2>
<q1>Utawaficha katika hema </q1>
<q2>Na mashindano ya ndimi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>31:20</xo>
<xt>Zab 27:5; Ayu 5:21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>
<nd>Bwana</nd> ahimidiwe; kwa maana amenitendea </q1>
<q2>Fadhili za ajabu katika mji wenye boma. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Nami nalisema kwa haraka yangu, </q1>
<q2>Nimekatiliwa mbali na macho yako; </q2>
<q1>Lakini ulisikia sauti ya dua yangu </q1>
<q2>Wakati nilipokulilia. </q2>
<q1><vn>23 </vn>Mpendeni 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Ninyi nyote mlio watauwa wake. </q2>
<q1>
<nd>Bwana</nd> huwahifadhi waaminifu, </q1>
<q2>Humlipa atendaye kiburi malipo tele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>31:23</xo>
<xt>1 Pet 1:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>24 </vn>Iweni hodari, mpige moyo konde, </q1>
<q2>Ninyi nyote mnaomngoja 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>32</cn>
<q1><vn>1 </vn>Heri aliyesamehewa dhambi, </q1>
<q2>Na kusitiriwa makosa yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>32:1-2</xo>
<xt>Rum 4:7-8; Zab 85:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Heri 
<nd>Bwana</nd> asiyemhesabia upotovu, </q1>
<q2>Ambaye rohoni mwake hamna hila. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>32:2</xo>
<xt>Law 17:4; Rum 5:13; Yn 1:47; 2 Kor 1:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Niliponyamaza mifupa yangu ilichakaa </q1>
<q2>Kwa kuugua kwangu mchana kutwa. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Kwa maana mchana na usiku </q1>
<q2>Mkono wako ulinilemea. </q2>
<q1>Jasho langu likakauka hata nikawa </q1>
<q2>Kama nchi kavu wakati wa kaskazi. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Nalikujulisha dhambi yangu, </q1>
<q2>Wala sikuuficha upotovu wangu. </q2>
<q1>Nalisema, Nitayakiri maasi yangu kwa 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>32:5</xo>
<xt>Mit 28:13; Isa 65:24; Lk 15:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Kwa hiyo kila mtu mtauwa </q1>
<q2>Akuombe wakati unapopatikana. </q2>
<q1>Hakika maji makuu yafurikapo, </q1>
<q2>Hayatamfikia yeye. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>32:6</xo>
<xt>1 Tim 1:16; Isa 55:6; Yn 7:34</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ndiwe sitara yangu, utanihifadhi na mateso, </q1>
<q2>Utanizungusha nyimbo za wokovu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>32:7</xo>
<xt>Zab 9:9; Mit 18:10; Isa 4:6; Mt 23:37; Kol 3:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; </q1>
<q2>Nitakushauri, jicho langu likikutazama. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>32:8</xo>
<xt>Isa 48:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Msiwe kama farasi wala nyumbu, </q1>
<q2>Walio hawana akili. </q2>
<q1>Kwa matandiko ya lijamu na hatamu </q1>
<q2>Sharti kuwazuia hao, au hawatakukaribia. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Naye mtu mwovu ana mapigo mengi, </q1>
<q2>Bali amtumainiye 
<nd>Bwana</nd> fadhili zitamzunguka. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>32:10</xo>
<xt>Mit 13:21; Zab 34:8; Mit 16:20; Yer 17:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Mfurahieni 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Shangilieni, enyi wenye haki </q2>
<q1>Pigeni vigelegele vya furaha; </q1>
<q2>Ninyi nyote mlio wanyofu wa moyo. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>33</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mpigieni 
<nd>Bwana</nd> vigelegele, enyi wenye haki, </q1>
<q2>Kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Mshukuruni 
<nd>Bwana</nd> kwa kinubi, </q1>
<q2>Kwa kinanda cha nyuzi kumi mwimbieni sifa. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Mwimbieni wimbo mpya, </q1>
<q2>Pigeni kwa ustadi kwa sauti ya shangwe. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>33:3</xo>
<xt>Isa 42:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Kwa kuwa neno la 
<nd>Bwana</nd> lina adili, </q1>
<q2>Na kazi yake yote huitenda kwa uaminifu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Huzipenda haki na hukumu, </q1>
<q2>Nchi imejaa fadhili za 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Kwa neno la 
<nd>Bwana</nd> mbingu zilifanyika, </q1>
<q2>Na jeshi lake lote kwa pumzi ya kinywa chake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>33:6</xo>
<xt>Yn 1:1-3; Ebr 11:3; Ayu 26:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Hukusanya maji ya bahari chungu chungu, </q1>
<q2>Huviweka vilindi katika ghala. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Nchi yote na imwogope 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Wote wakaao duniani na wamche. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Maana Yeye alisema, ikawa; </q1>
<q2>Na Yeye aliamuru, ikasimama. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>33:9</xo>
<xt>Mwa 1:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>
<nd>Bwana</nd> huyabatilisha mashauri ya mataifa, </q1>
<q2>Huyatangua makusudi ya watu. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Shauri la 
<nd>Bwana</nd> lasimama milele, </q1>
<q2>Makusudi ya moyo wake vizazi na vizazi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>33:11</xo>
<xt>Ayu 23:13; Mit 19:21; Eze 38:10; Mdo 4:27,28</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Heri taifa ambalo 
<nd>Bwana</nd> ni Mungu wao, </q1>
<q2>Watu aliowachagua kuwa urithi wake. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Toka mbinguni 
<nd>Bwana</nd> huchungulia, </q1>
<q2>Huwatazama wanadamu wote pia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>33:13</xo>
<xt>2 Nya 16:9; Ayu 28:24; Zab 11:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Toka mahali pake aketipo </q1>
<q2>Huwaangalia wote wakaao duniani. </q2>
<q1><vn>15 </vn>yeye aiumbaye mioyo yao wote </q1>
<q2>Huzifikiri kazi zao zote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>33:15</xo>
<xt>Isa 64:8; Ayu 11:11; Zab 44:21; Mit 24:12; Yer 32:19; Hes 7:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Hapana mfalme aokokaye kwa wingi wa uwezo, </q1>
<q2>Wala shujaa haokoki kwa wingi wa nguvu. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Farasi hafai kitu kwa wokovu, </q1>
<q2>Wala hamponyi mtu kwa wingi wa nguvu zake. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Tazama, jicho la 
<nd>Bwana</nd> li kwao wamchao, </q1>
<q2>Wazingojeao fadhili zake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>33:18</xo>
<xt>Ayu 36:7; Zab 34:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Yeye huwaponya nafsi zao na mauti, </q1>
<q2>Na kuwahuisha wakati wa njaa. </q2>
<q1><vn>20 </vn>Nafsi zetu zinamngoja 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Yeye ndiye msaada wetu na ngao yetu. </q2>
<q1><vn>21 </vn>Maana mioyo yetu itamfurahia, </q1>
<q2>Kwa kuwa tumelitumainia jina lake takatifu. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, fadhili zako zikae nasi, </q1>
<q2>Kama vile tulivyokungoja Wewe. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>34</cn>
<q1><vn>1 </vn>Nitamhimidi 
<nd>Bwana</nd> kila wakati, </q1>
<q2>Sifa zake zi kinywani mwangu daima. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>34:1</xo>
<xt>1 Sam 21:13-15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Katika 
<nd>Bwana</nd> nafsi yangu itajisifu, </q1>
<q2>Wanyenyekevu wasikie wakafurahi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>34:2</xo>
<xt>Yer 9:24; 1 Kor 1:31</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Mtukuzeni 
<nd>Bwana</nd> pamoja nami, </q1>
<q2>Na tuliadhimishe jina lake pamoja. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Nalimtafuta 
<nd>Bwana</nd> akanijibu, </q1>
<q2>Akaniponya na hofu zangu zote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>34:4</xo>
<xt>Zab 18:6; Yon 2:2; Mt 7:7; Lk 11:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Wakamwelekea macho wakatiwa nuru, </q1>
<q2>Wala nyuso zao hazitaona haya. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Maskini huyu aliita, 
<nd>Bwana</nd> akasikia, </q1>
<q2>Akamwokoa na taabu zake zote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>34:6</xo>
<xt>Zab 3:4; 2 Sam 22:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Malaika wa 
<nd>Bwana</nd> hufanya kituo, </q1>
<q2>Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>34:7</xo>
<xt>Dan 6:22; Mwa 32:1; 2 Fal 6:17; Ebr 1:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Onjeni mwone ya kuwa 
<nd>Bwana</nd> yu mwema; </q1>
<q2>Heri mtu yule anayemtumaini. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>34:8</xo>
<xt>1 Pet 2:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Mcheni 
<nd>Bwana</nd>, enyi watakatifu wake, </q1>
<q2>Yaani, wamchao hawahitaji kitu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>34:9</xo>
<xt>Flp 4:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Wana-simba hutindikiwa, huona njaa; </q1>
<q2>Bali wamtafutao 
<nd>Bwana</nd> hawatahitaji kitu cho chote kilicho chema. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Njoni, enyi wana, mnisikilize, </q1>
<q2>Nami nitawafundisha kumcha 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Ni nani mtu yule apendezwaye na uzima, </q1>
<q2>Apendaye siku nyingi apate kuona mema? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>34:12-16</xo>
<xt>1 Pet 3:10-12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Uuzuie ulimi wako na mabaya, </q1>
<q2>Na midomo yako na kusema hila. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>34:13</xo>
<xt>1 Pet 2:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Uache mabaya ukatende mema, </q1>
<q2>Utafute amani ukaifuatie. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Macho ya 
<nd>Bwana</nd> huwaelekea wenye haki, </q1>
<q2>Na masikio yake hukielekea kilio chao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>34:15</xo>
<xt>Ayu 36:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Uso wa 
<nd>Bwana</nd> ni juu ya watenda mabaya, </q1>
<q2>Aliondoe kumbukumbu lao duniani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>34:16</xo>
<xt>Law 17:10; Yer 44:11; Mit 10:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Walilia, naye 
<nd>Bwana</nd> akasikia, </q1>
<q2>Akawaponya na taabu zao zote. </q2>
<q1><vn>18 </vn>
<nd>Bwana</nd> yu karibu nao waliovunjika moyo, </q1>
<q2>Na waliopondeka roho huwaokoa. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Mateso ya mwenye haki ni mengi, </q1>
<q2>Lakini 
<nd>Bwana</nd> humponya nayo yote. </q2>
<q1><vn>20 </vn>Huihifadhi mifupa yake yote, </q1>
<q2>Haukuvunjika hata mmoja. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>34:20</xo>
<xt>Yn 19:36</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Uovu utamwua asiye haki, </q1>
<q2>Nao wamchukiao mwenye haki watahukumiwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>34:21</xo>
<xt>Zab 94:23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>22 </vn>
<nd>Bwana</nd> huzikomboa nafsi za watumishi wake, </q1>
<q2>Wala hawatahukumiwa wote wamkimbiliao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>34:22</xo>
<xt>2 Sam 4:9; Zab 103:4</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>35</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, utete nao wanaoteta nami, </q1>
<q2>Upigane nao wanaopigana nami. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Uishike ngao na kigao, </q1>
<q2>Usimame unisaidie. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Uutoe na mkuki uwapinge wanaonifuatia, </q1>
<q2>Uiambie nafsi yangu, Mimi ni wokovu wako. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Waaibishwe, wafedheheshwe, </q1>
<q2>Wanaoitafuta nafsi yangu. </q2>
<q1>Warudishwe nyuma, wafadhaishwe, </q1>
<q2>Wanaonizulia mabaya. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Wawe kama makapi mbele ya upepo, </q1>
<q2>Malaika wa 
<nd>Bwana</nd> akiwaangusha chini. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Njia yao na iwe giza na utelezi, </q1>
<q2>Malaika wa 
<nd>Bwana</nd> akiwafuatia. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Maana bila sababu wamenifichia wavu, </q1>
<q2>Bila sababu wameichimbia shimo nafsi yangu. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Uharibifu na umpate kwa ghafula, </q1>
<q1>Na wavu aliouficha umnase yeye mwenyewe; </q1>
<q2>Kwa uharibifu aanguke ndani yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>35:8</xo>
<xt>1 The 5:3; Zab 7:15; Mit 5:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Na nafsi yangu itamfurahia 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Na kuushangilia wokovu wake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>35:9</xo>
<xt>1 Sam 2:1; Zab 13:5; Isa 61:10; Ebr 3:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Mifupa yangu yote itasema, </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd>, ni nani aliye kama Wewe? </q2>
<q2>Umponyaye maskini na mtu aliye hodari kumshinda yeye, </q2>
<q2>Naam, maskini na mhitaji na mtu amtekaye. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>35:10</xo>
<xt>Zab 71:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Mashahidi wa udhalimu wanasimama, </q1>
<q2>Wananiuliza mambo nisiyoyajua. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Wananilipa mabaya badala ya mema, </q1>
<q2>Hata nafsi yangu ikaingia ukiwa. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Bali mimi, walipougua wao, </q1>
<q2>Nguo yangu ilikuwa gunia. </q2>
<q1>Nalijitesa nafsi yangu kwa kufunga; </q1>
<q2>Maombi yangu yakarejea kifuani mwangu. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Nalijifanya kama kwamba ni rafiki au ndugu yangu, </q1>
<q2>Naliinama nikilia kama aliyefiwa na mamaye. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Lakini nikijikwaa hufurahi na kukusanyana, </q1>
<q2>Walinikusanyikia watu ovyo nisiowajua, </q2>
<q2>Wananipapura wala hawakomi. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Kama wenye mzaha wakikufuru karamuni </q1>
<q2>Wananisagia meno. </q2>
<q1><vn>17 </vn>
<nd>Bwana</nd>, hata lini utatazama? </q1>
<q2>Uiokoe nafsi yangu na maharabu yao, </q2>
<q2>Na mpenzi wangu na wana-simba. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Nitakushukuru katika kusanyiko kubwa; </q1>
<q2>Nitakusifu kati ya watu wengi. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Walio adui zangu bure wasinisimange, </q1>
<q2>Wanaonichukia bila sababu wasining'ong'e. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>35:19</xo>
<xt>Zab 69:5; Yn 15:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Maana hawasemi maneno ya amani, </q1>
<q2>Na juu ya watulivu wa nchi huwaza hila. </q2>
<q1><vn>21 </vn>Nao wananifumbulia vinywa vyao, </q1>
<q2>Husema, Ewe! Ewe! Jicho letu limeona. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, umeona, usinyamaze; </q1>
<q2>Ee Bwana, usiwe mbali nami. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>35:22</xo>
<xt>Kut 3:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>23 </vn>Uamke, uwe macho ili kunipatia hukumu </q1>
<q2>Kwa ajili ya madai yangu, </q2>
<q2>Mungu wangu na Bwana wangu. </q2>
<q1><vn>24 </vn>Unihukumu kwa haki yako, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wangu, </q2>
<q2>Wala wasinisimangize. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>35:24</xo>
<xt>Zab 7:8; 26:1; 2 The 1:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>25 </vn>Wasiseme moyoni, Haya! Ndivyo tutakavyo; </q1>
<q2>Wasiseme, Tumemmeza. </q2>
<q1><vn>26 </vn>Waaibishwe, wafedheheshwe pamoja, </q1>
<q2>Wanaoifurahia hali yangu mbaya. </q2>
<q1>Wavikwe aibu na fedheha, </q1>
<q2>Wanaojikuza juu yangu. </q2>
<q1><vn>27 </vn>Washangilie na kufurahi, </q1>
<q2>Wapendezwao na haki yangu. </q2>
<q1>Naam, waseme daima, Atukuzwe 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Apendezwaye na amani ya mtumishi wake. </q2>
<q1><vn>28 </vn>Na ulimi wangu utanena haki yako, </q1>
<q2>Na sifa zako mchana kutwa. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>36</cn>
<q1><vn>1 </vn>Kuasi kwake yule mwovu hunena moyoni mwake, </q1>
<q2>Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>36:1</xo>
<xt>Rum 3:18; Mwa 20:11; Mit 8:13; Mhu 12:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kwa maana hujipendekeza machoni pake </q1>
<q2>Kuwa upotovu wake hautaonekana na kuchukiwa. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Maneno ya kinywa chake ni uovu na hila, </q1>
<q2>Ameacha kuwa na akili na kutenda mema. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>36:3</xo>
<xt>Yer 4:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Huwaza maovu kitandani pake, </q1>
<q2>Hujiweka katika njia mbaya; ubaya hauchukii. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>36:4</xo>
<xt>Mik 2:1; Isa 65:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, fadhili zako zafika hata mbinguni, </q1>
<q2>Uaminifu wako hata mawinguni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>36:5</xo>
<xt>Zab 57:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Haki yako ni kama milima ya Mungu, </q1>
<q2>Hukumu zako ni vilindi vikuu, </q2>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unawaokoa wanadamu na wanyama. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>36:6</xo>
<xt>Ayu 11:8; Rum 11:33; Ayu 7:20; Zab 145:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ee Mungu, jinsi zilivyo na thamani fadhili zako! </q1>
<q2>Wanadamu huukimbilia uvuli wa mbawa zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>36:7</xo>
<xt>Rut 2:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Watashibishwa kwa unono wa nyumba yako, </q1>
<q2>Nawe utawanywesha mto wa furaha zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>36:8</xo>
<xt>Ayu 20:17; Ufu 22:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Maana kwako Wewe iko chemchemi ya uzima, </q1>
<q2>Katika nuru yako tutaona nuru. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>36:9</xo>
<xt>Isa 12:3; Yer 2:13; Zek 13:1; Yn 4:10,14; Ufu 21:6; Mdo 26:18; Efe 5:8; Kol 1:13; 1 Pet 2:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Uwadumishie wakujuao fadhili zako, </q1>
<q2>Na wanyofu wa moyo uaminifu wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>36:10</xo>
<xt>Yer 22:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Mguu wa kiburi usinikaribie, </q1>
<q2>Wala mkono wa wasio haki usinifukuze. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Huko ndiko walikoanguka wafanyao maovu; </q1>
<q2>Wameangushwa chini wasiweze kusimama. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>37</cn>
<q1><vn>1 </vn>Usikasirike kwa sababu ya watenda mabaya, </q1>
<q2>Usiwahusudu wafanyao ubatili. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Maana kama majani watakatika mara, </q1>
<q2>Kama miche mibichi watanyauka. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Umtumaini 
<nd>Bwana</nd> ukatende mema, </q1>
<q2>Ukae katika nchi, upendezwe na uaminifu. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Nawe utajifurahisha kwa 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Naye atakupa haja za moyo wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:4</xo>
<xt>Ayu 27:10; Wim 2:3; Isa 58:14; 1 Pet 1:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Umkabidhi 
<nd>Bwana</nd> njia yako, </q1>
<q2>Pia umtumaini, naye atafanya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:5</xo>
<xt>Mt 6:25; 1 Pet 5:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Ataitokeza haki yako kama nuru, </q1>
<q2>Na hukumu yako kama adhuhuri. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:6</xo>
<xt>Mik 7:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ukae kimya mbele za 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Nawe umngojee kwa saburi; </q2>
<q1>Usimkasirikie yeye afanikiwaye katika njia yake, </q1>
<q2>Wala mtu afanyaye hila. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ukomeshe hasira, uache ghadhabu, </q1>
<q2>Usikasirike, mwisho wake ni kutenda mabaya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:8</xo>
<xt>Ayu 5:2; Zab 73:3; Mit 14:29; Efe 4:26; Yak 1:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Maana watenda mabaya wataharibiwa, </q1>
<q2>Bali wamngojao 
<nd>Bwana</nd> ndio watakaoirithi nchi. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Maana bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo, </q1>
<q2>Utapaangalia mahali pake wala hatakuwapo. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Bali wenye upole watairithi nchi, </q1>
<q2>Watajifurahisha kwa wingi wa amani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:11</xo>
<xt>Mt 5:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Asiye haki hunuia mabaya juu ya mwenye haki, </q1>
<q2>Na kumsagia meno yake. </q2>
<q1><vn>13 </vn>
<nd>Bwana</nd> atamcheka, </q1>
<q2>Maana ameona kwamba siku yake inakuja. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:13</xo>
<xt>1 Sam 26:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Wasio haki wamefuta upanga na kupinda uta, </q1>
<q2>Wamwangushe chini maskini na mhitaji, </q2>
<q2>Na kuwaua wenye mwenendo wa unyofu. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Upanga wao utaingia mioyoni mwao wenyewe, </q1>
<q2>Na nyuta zao zitavunjika. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Kidogo alicho nacho mwenye haki ni bora </q1>
<q2>Kuliko wingi wa mali wa wasio haki wengi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:16</xo>
<xt>Mit 15:16; 1 Tim 6:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Maana mikono ya wasio haki itavunjika, </q1>
<q2>Bali 
<nd>Bwana</nd> huwategemeza wenye haki. </q2>
<q1><vn>18 </vn>
<nd>Bwana</nd> anazijua siku za wakamilifu, </q1>
<q2>Na urithi wao utakuwa wa milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:18</xo>
<xt>Zab 1:6; Isa 60:21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Hawataaibika wakati wa ubaya, </q1>
<q2>Na siku za njaa watashiba. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:19</xo>
<xt>Ayu 5:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Bali wasio haki watapotea, </q1>
<q2>Nao wamchukiao 
<nd>Bwana</nd> watatoweka, </q2>
<q1>Kama uzuri wa mashamba, </q1>
<q2>Kama moshi watatoweka. </q2>
<q1><vn>21 </vn>Asiye haki hukopa wala halipi, </q1>
<q2>Bali mwenye haki hufadhili, hukirimu. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Maana waliobarikiwa na yeye watairithi nchi, </q1>
<q2>Nao waliolaaniwa na yeye wataharibiwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:22</xo>
<xt>Mit 3:33</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>23 </vn>Hatua za mtu zaimarishwa na 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Naye aipenda njia yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:23</xo>
<xt>Zab 121:3; Mit 16:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>24 </vn>Ajapojikwaa hataanguka chini, </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> humshika mkono na kumtegemeza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:24</xo>
<xt>Mik 7:8; 2 Kor 4:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>25 </vn>Nalikuwa kijana nami sasa ni mzee, </q1>
<q2>Lakini sijamwona mwenye haki ameachwa </q2>
<q2>Wala mzao wake akiomba chakula. </q2>
<q1><vn>26 </vn>Mchana kutwa hufadhili na kukopesha, </q1>
<q2>Na mzao wake hubarikiwa. </q2>
<q1><vn>27 </vn>Jiepue na uovu, utende mema, </q1>
<q2>Na kukaa hata milele. </q2>
<q1><vn>28 </vn>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> hupenda haki, </q1>
<q2>Wala hawaachi watauwa wake. </q2>
<q1>Wao hulindwa milele, </q1>
<q2>Bali mzao wa wasio haki ataharibiwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:28</xo>
<xt>Zab 11:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>29 </vn>Wenye haki watairithi nchi, </q1>
<q2>Nao watakaa humo milele. </q2>
<q1><vn>30 </vn>Kinywa chake mwenye haki hunena hekima, </q1>
<q2>Na ulimi wake husema hukumu. </q2>
<q1><vn>31 </vn>Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake. </q1>
<q2>Hatua zake hazitelezi. </q2>
<q1><vn>32 </vn>Mtu asiye haki humvizia mwenye haki, </q1>
<q2>Na kutafuta jinsi ya kumfisha. </q2>
<q1><vn>33 </vn>
<nd>Bwana</nd> hatamwacha mkononi mwake, </q1>
<q2>Wala hatamlaumu atakapohukumiwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:33</xo>
<xt>Zab 109:31</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>34 </vn>Wewe umngoje 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Uishike njia yake, </q2>
<q1>Naye atakutukuza uirithi nchi, </q1>
<q2>Wasio haki watakapoharibiwa utawaona. </q2>
<q1><vn>35 </vn>Nimemwona mtu asiye haki mkali sana, </q1>
<q2>Akijieneza kama mwerezi wa Lebanoni. </q2>
<q1><vn>36 </vn>Nikapita na kumbe! Hayuko, </q1>
<q2>Nikamtafuta wala hakuonekana. </q2>
<q1><vn>37 </vn>Umwangalie sana mtu mkamilifu, </q1>
<q2>Umtazame mtu mnyofu, </q2>
<q2>Maana mwisho wake mtu huyo ni amani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:37</xo>
<xt>Ayu 1:1; Isa 32:17; Lk 2:25-30; Mdo 7:59,60; 1 The 4:17; 2 Tim 4:6-8; 2 Pet 1:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>38 </vn>Wakosaji wataangamizwa pamoja, </q1>
<q2>Wasio haki mwisho wao wataharibiwa. </q2>
<q1><vn>39 </vn>Na wokovu wa wenye haki una 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Yeye ni ngome yao wakati wa taabu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:39</xo>
<xt>Zab 3:8; Isa 12:2; Yon 2:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>40 </vn>Naye 
<nd>Bwana</nd> huwasaidia na kuwaopoa; </q1>
<q2>Huwaopoa na wasio haki na kuwaokoa; </q2>
<q2>Kwa kuwa wamemtumaini Yeye. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>37:40</xo>
<xt>1 Nya 5:20; Dan 3:17</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>38</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, usinilaumu katika ghadhabu yako, </q1>
<q2>Wala usiniadhibu kwa ukali wa hasira yako. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kwa maana mishale yako imenichoma, </q1>
<q2>Na mkono wako umenipata. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Hamna uzima katika mwili wangu </q1>
<q2>Kwa sababu ya ghadhabu yako. </q2>
<q1>Wala hamna amani mifupani mwangu </q1>
<q2>Kwa sababu ya hatia zangu. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Maana dhambi zangu zimenifunikiza kichwa, </q1>
<q2>Kama mzigo mzito zimenilemea mno. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Jeraha zangu zinanuka, zimeoza, </q1>
<q2>Kwa sababu ya upumbavu wangu. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nimepindika na kuinama sana, </q1>
<q2>Mchana kutwa nimekwenda nikihuzunika. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Maana viuno vyangu vimejaa homa, </q1>
<q2>Wala hamna uzima katika mwili wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>38:7</xo>
<xt>Ayu 7:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Nimedhoofika na kuchubuka sana, </q1>
<q2>Nimeugua kwa fadhaa ya moyo wangu. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Bwana, haja zangu zote ziko mbele zako, </q1>
<q2>Kuugua kwangu hakukusitirika kwako. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Moyo wangu unapwita-pwita, </q1>
<q2>Nguvu zangu zimeniacha; </q2>
<q2>Nuru ya macho yangu nayo imeniondoka. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Wanipendao na rafiki zangu wanasimama mbali na pigo langu; </q1>
<q2>Naam, karibu zangu wamesimama mbali. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>38:11</xo>
<xt>Lk 10:31</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Nao wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego; </q1>
<q2>Nao wanaotaka kunidhuru hunena mabaya; </q2>
<q2>Na kufikiri hila mchana kutwa. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Lakini kama kiziwi sisikii, </q1>
<q2>Nami ni kama bubu asiyefumbua kinywa chake. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia, </q1>
<q2>Ambaye hamna hoja kinywani mwake. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Kwa kuwa nakungoja Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Wewe utajibu, Ee Bwana, Mungu wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>38:15</xo>
<xt>Yer 14:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Maana nalisema, Wasije wakanifurahia; </q1>
<q2>Mguu wangu ukiteleza wajitukuza juu yangu. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Kwa maana mimi ni karibu na kusita, </q1>
<q2>Na maumivu yangu yako mbele yangu daima. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Kwa maana nitaungama uovu wangu, </q1>
<q2>Na kusikitika kwa dhambi zangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>38:18</xo>
<xt>Ayu 31:33; Zab 32:5; Mit 28:13; 2 Kor 7:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Lakini adui zangu ni wazima wenye nguvu, </q1>
<q2>Nao wanaonichukia bure wamekuwa wengi. </q2>
<q1><vn>20 </vn>Naam, wakilipa mabaya kwa mema, </q1>
<q2>Huwa adui zangu kwa kuwa nalifuata lililo jema. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>38:20</xo>
<xt>1 Yoh 3:12; 1 Pet 3:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, usiniache, </q1>
<q2>Mungu wangu, usijitenge nami. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>38:21</xo>
<xt>Zab 22:1,11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>22 </vn>Ufanye haraka kunisaidia, </q1>
<q2>Ee Bwana, wokovu wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>38:22</xo>
<xt>Kut 15:2; Isa 12:2</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>39</cn>
<q1><vn>1 </vn>Nalisema, Nitazitunza njia zangu </q1>
<q2>Nisije nikakosa kwa ulimi wangu; </q2>
<q1>Nitajitia lijamu kinywani, </q1>
<q2>Maadamu mtu mbaya yupo mbele yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>39:1</xo>
<xt>1 Fal 2:4; Mit 4:26,27; Ebr 2:1; Kol 4:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Nalikuwa sisemi, nalinyamaa kimya, </q1>
<q2>Sina faraja, maumivu yangu yakazidi. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Moyo wangu ukawa moto ndani yangu, </q1>
<q2>Na katika kuwaza kwangu moto ukawaka; </q2>
<q2>Nalisema kwa ulimi wangu, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>39:3</xo>
<xt>Yer 20:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>
<nd>Bwana</nd>, unijulishe mwisho wangu, </q1>
<q2>Na kiasi cha siku zangu ni kiasi gani; </q2>
<q2>Nijue jinsi nilivyo dhaifu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Tazama, umefanya siku zangu kuwa mashubiri; </q1>
<q2>Maisha yangu ni kama si kitu mbele zako. </q2>
<q2>Kila mwanadamu, ingawa amesitawi, ni ubatili. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>39:5</xo>
<xt>Zab 90:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Binadamu huenda tu huko na huko kama kivuli; </q1>
<q1>Hufanya ghasia tu kwa ajili ya ubatili; </q1>
<q2>Huweka akiba wala hajui ni nani atakayeichukua. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Na sasa ninangoja nini, Ee Bwana? </q1>
<q2>Matumaini yangu ni kwako. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Uniokoe na maasi yangu yote, </q1>
<q2>Usinifanye laumu ya mpumbavu. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Nimenyamaza, sitafumbua kinywa changu, </q1>
<q2>Maana Wewe ndiwe uliyeyafanya. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Uniondolee pigo lako; </q1>
<q2>Kwa uadui wa mkono wako nimeangamia. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Ukimrudi mtu kwa kumkemea kwa uovu wake, </q1>
<q2>Watowesha uzuri wake kama nondo. </q2>
<q2>Kila mwanadamu ni ubatili. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, usikie maombi yangu, </q1>
<q2>Utege sikio lako niliapo, </q2>
<q2>Usiyanyamalie machozi yangu. </q2>
<q1>Kwa maana mimi ni mgeni wako, </q1>
<q2>Msafiri kama baba zangu wote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>39:12</xo>
<xt>Law 25:23; 1 Nya 29:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Uniachilie nikunjuke uso, </q1>
<q2>Kabla sijaondoka nisiwepo tena. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>39:13</xo>
<xt>Ayu 10:20,21</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>40</cn>
<q1><vn>1 </vn>Nalimngoja 
<nd>Bwana</nd> kwa saburi, </q1>
<q2>Akaniinamia akakisikia kilio changu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Akanipandisha toka shimo la uharibifu, </q1>
<q2>Toka udongo wa utelezi; </q2>
<q1>Akaisimamisha miguu yangu mwambani, </q1>
<q2>Akaziimarisha hatua zangu. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Akatia wimbo mpya kinywani mwangu, </q1>
<q2>Ndio sifa zake Mungu wetu. </q2>
<q1>Wengi wataona na kuogopa, </q1>
<q2>Nao watamtumaini 
<nd>Bwana</nd> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Heri aliyemfanya 
<nd>Bwana</nd> kuwa tumaini lake, </q1>
<q2>Wala hakuwaelekea wenye kiburi, </q2>
<q2>Wala hao wanaogeukia uongo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>40:4</xo>
<xt>Zab 2:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wangu, umefanya kwa wingi </q1>
<q2>Miujiza yako na mawazo yako kwetu; </q2>
<q1>Hakuna awezaye kufananishwa nawe; </q1>
<q2>Kama ningependa kuyatangaza na kuyahubiri, </q2>
<q2>Ni mengi sana hayahesabiki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>40:5</xo>
<xt>Isa 55:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo, </q1>
<q2>Masikio yangu umeyazibua, </q2>
<q2>Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>40:6-8</xo>
<xt>Ebr 10:5-7; Hos 6:6; Mt 9:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ndipo niliposema, Tazama nimekuja, </q1>
<q2>(Katika gombo la chuo nimeandikiwa,) <f> <fn>-</fn><note>
<xo>40:7</xo>
<xt>Lk 24:44; Yn 5:39; Mdo 10:43; Ebr 10:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Kuyafanya mapenzi yako, </q1>
<q1>Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; </q1>
<q2>Naam, sheria yako imo moyoni mwangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>40:8</xo>
<xt>Ayu 23:12; Yer 15:16; Yn 4:34; Rum 7:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko kubwa. </q1>
<q2>Sikuizuia midomo yangu; Ee 
<nd>Bwana</nd>, unajua. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>40:9</xo>
<xt>Zab 139:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Sikusitiri haki yako moyoni mwangu; </q1>
<q2>Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako. </q2>
<q1>Sikuficha fadhili zako wala kweli yako </q1>
<q2>Katika kusanyiko kubwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>40:10</xo>
<xt>Mdo 20:20; Rum 1:16,17; Flp 3:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Nawe, 
<nd>Bwana</nd>, usinizuilie rehema zako, </q1>
<q2>Fadhili zako na kweli yako na zinihifadhi daima. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>40:11</xo>
<xt>Zab 43:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Kwa maana mabaya yasiyohesabika </q1>
<q2>Yamenizunguka mimi. </q2>
<q1>Maovu yangu yamenipata, </q1>
<q2>Wala siwezi kuona. </q2>
<q1>Yamezidi kuliko nywele za kichwa changu, </q1>
<q2>Na moyo wangu umeniacha. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>40:12</xo>
<xt>Zab 38:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uwe radhi kuniokoa, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unisaidie hima. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Waaibike, wafedheheke pamoja, </q1>
<q2>Wanaoitafuta nafsi yangu waiangamize. </q2>
<q1>Warudishwe nyuma, watahayarishwe, </q1>
<q2>Wapendezwao na shari yangu. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Wakae hali ya ukiwa, na iwe aibu yao, </q1>
<q2>Wanaoniambia, Ewe! Ewe! </q2>
<q1><vn>16 </vn>Washangilie, wakufurahie, </q1>
<q2>Wote wakutafutao. </q2>
<q1>Waupendao wokovu wako </q1>
<q2>Waseme daima, Atukuzwe 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Nami ni maskini na mhitaji, </q1>
<q2>Bwana atanitunza. </q2>
<q1>Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu, </q1>
<q2>Ee Mungu wangu, usikawie. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>40:17</xo>
<xt>Neh 5:19; Yon 1:6</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>41</cn>
<q1><vn>1 </vn>Heri amkumbukaye mnyonge; </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> atamwokoa siku ya taabu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>41:1</xo>
<xt>Mit 14:21; Mk 10:21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>
<nd>Bwana</nd> atamlinda na kumhifadhi hai, </q1>
<q1>Naye atafanikiwa katika nchi; </q1>
<q2>Wala usimtie katika hali wamtakiayo adui zake. </q2>
<q1><vn>3 </vn>
<nd>Bwana</nd> atamtegemeza alipo mgonjwa kitandani. </q1>
<q2>Katika ugonjwa wake umemtandikia. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Nami nalisema, 
<nd>Bwana</nd>, unifadhili, </q1>
<q2>Uniponye roho yangu maana nimekutenda dhambi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>41:4</xo>
<xt>Zab 6:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Adui zangu wananitaja kwa maneno mabaya, </q1>
<q2>Atakufa lini, jina lake likapotea? </q2>
<q1><vn>6 </vn>Na mmoja wao akija kunitazama asema uongo, </q1>
<q2>Moyo wake hujikusanyia maovu, </q2>
<q2>Naye atokapo nje huyanena. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>41:6</xo>
<xt>Zab 12:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Wote wanaonichukia wananinong'ona, </q1>
<q2>Wananiwazia mabaya. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Neno la kisirani limemgandama, </q1>
<q2>Na iwapo amelala hatasimama tena. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Msiri wangu tena niliyemtumaini, </q1>
<q2>Aliyekula chakula changu, </q2>
<q2>Ameniinulia kisigino chake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>41:9</xo>
<xt>Mt 26:23; Oba 1:7; Mk 14:18; Lk 22:21; Yn 13:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Lakini Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, unifadhili, </q1>
<q2>Uniinue nipate kuwalipa. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Kwa neno hili nimejua ya kuwa wapendezwa nami, </q1>
<q2>Kwa kuwa adui yangu hasimangi kwa kunishinda. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Nami katika ukamilifu wangu umenitegemeza, </q1>
<q2>Umeniweka mbele za uso wako milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>41:12</xo>
<xt>Zab 34:15; Mdo 2:28</xt></note></f> </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>13 </vn>Na atukuzwe 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wa Israeli, </q1>
<q2>Tangu milele hata milele. Amina na Amina. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>41:13</xo>
<xt>Zab 106:48</xt></note></f> </q2>
<d>KITABU CHA PILI </d>
<b></b></c>

<c><cn>42</cn>
<q1><vn>1 </vn>Kama ayala aioneavyo shauku mito ya maji. </q1>
<q2>Vivyo hivyo nafsi yangu inakuonea shauku, Ee Mungu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Nafsi yangu inamwonea kiu MUNGU, Mungu aliye hai, </q1>
<q2>Lini nitakapokuja nionekane mbele za Mungu? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>42:2</xo>
<xt>Yn 7:37; 1 The 1:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku, </q1>
<q2>Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Nayakumbuka hayo nikiweka wazi nafsi yangu ndani yangu, </q1>
<q2>Jinsi nilivyokuwa nikienda na mkutano, </q2>
<q1>Na kuwaongoza nyumbani kwa Mungu, </q1>
<q2>Kwa sauti ya furaha na kusifu, mkutano wa sikukuu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>42:4</xo>
<xt>Isa 30:29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Nafsi yangu, kwa nini kuinama, </q1>
<q1>Na kufadhaika ndani yangu? </q1>
<q2>Umtumaini Mungu; </q2>
<q1>Kwa maana nitakuja kumsifu, </q1>
<q1>Aliye afya ya uso wangu, </q1>
<q2>Na Mungu wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>42:5</xo>
<xt>Zab 56:3,11; Isa 50:10; Omb 3:24</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nafsi yangu imeinama ndani yangu, kwa hiyo nitakukumbuka, </q1>
<q1>Toka nchi ya Yordani, na Mahermoni, na toka kilima cha Mizari. </q1>
<q1><vn>7 </vn>Kilindi chapigia kelele kilindi kwa sauti ya maboromoko ya maji yako, </q1>
<q2>Gharika zako zote na mawimbi yako yote yamepita juu yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>42:7</xo>
<xt>Eze 7:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Mchana 
<nd>Bwana</nd> ataagiza fadhili zake, na usiku wimbo wake utakuwa nami, </q1>
<q1>Naam, maombi kwa Mungu aliye uhai wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>42:8</xo>
<xt>Kum 28:8</xt></note></f> </q1>
<q1><vn>9 </vn>Nitamwambia Mungu, mwamba wangu, Kwa nini umenisahau? </q1>
<q2>Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea? </q2>
<q1><vn>10 </vn>Watesi wangu hunitukana mithili ya kuniponda mifupa yangu, </q1>
<q2>Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako? </q2>
<q1><vn>11 </vn>Nafsi yangu, kwa nini kuinama, </q1>
<q1>Na kufadhaika ndani yangu? </q1>
<q2>Umtumaini Mungu; </q2>
<q1>Kwa maana nitakuja kumsifu, </q1>
<q1>Aliye afya ya uso wangu, </q1>
<q2>Na Mungu wangu. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>43</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Bwana, unihukumu, unitetee kwa taifa lisilo haki, </q1>
<q2>Uniokoe na mtu wa hila asiye haki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>43:1</xo>
<xt>Zab 7:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kwa kuwa Wewe ndiwe Mungu uliye nguvu zangu; kwa nini umenitupa? </q1>
<q2>Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>43:2</xo>
<xt>Zab 28:7; Isa 26:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Niletewe nuru yako na kweli yako ziniongoze, </q1>
<q2>Zinifikishe kwenye mlima wako mtakatifu na hata maskani yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>43:3</xo>
<xt>Zab 2:6; 3:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye </q1>
<q2>furaha yangu na shangwe yangu; </q2>
<q2>Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Nafsi yangu, kwa nini kuinama, </q1>
<q1>Na kufadhaika ndani yangu? </q1>
<q2>Umtumaini Mungu; </q2>
<q1>Kwa maana nitakuja kumsifu, </q1>
<q1>Aliye afya ya uso wangu, </q1>
<q1>Na Mungu wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>43:5</xo>
<xt>Zab 42:5,11</xt></note></f> </q1>
<b></b></c>

<c><cn>44</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu </q1>
<q2>Baba zetu wametuambia, </q2>
<q2>Matendo uliyoyatenda siku zao, siku za kale. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Wewe kwa mkono wako uliwafukuza mataifa, </q1>
<q2>Ukawakalisha wao. </q2>
<q1>Wewe uliwatesa watu wa nchi, </q1>
<q2>Ukawaeneza wao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>44:2</xo>
<xt>Kut 15:17; Kum 7:1; Yos 10:42</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Maana si kwa upanga wao walivyoimiliki nchi, </q1>
<q2>Wala si mkono wao uliowaokoa; </q2>
<q1>Bali mkono wako wa kuume, naam, mkono wako, </q1>
<q2>Na nuru ya uso wako, kwa kuwa uliwaridhia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>44:3</xo>
<xt>Yos 24:12; Kum 4:37</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Ee Mungu, Wewe ndiwe mfalme wangu, </q1>
<q2>Uagize mambo ya wokovu kwa Yakobo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>44:4</xo>
<xt>Zab 74:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Kwa nguvu zako tutawaangusha watesi wetu; </q1>
<q2>Kwa jina lako tutawakanyaga watupingao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>44:5</xo>
<xt>Dan 8:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Maana sitautumainia upinde wangu, </q1>
<q2>Wala upanga wangu hautaniokoa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>44:6</xo>
<xt>Zab 33:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Bali Wewe ndiwe uliyetuokoa na watesi wetu; </q1>
<q2>Na watuchukiao umewaaibisha. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Tumejisifia Mungu mchana kutwa, </q1>
<q2>Na jina lako tutalishukuru milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>44:8</xo>
<xt>Zab 34:2; Rum 2:17; 1 Kor 1:31</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Lakini umetutupa, umetufedhehesha, </q1>
<q2>Wala hutoki na majeshi yetu. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Waturudisha nyuma tukampa mtesi kisogo, </q1>
<q2>Na watuchukiao wanajipatia mateka. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>44:10</xo>
<xt>Law 26:17; Kum 28:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Umetutoa kama kondoo tuwe chakula, </q1>
<q2>Na kututawanya kati ya mataifa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>44:11</xo>
<xt>Kum 4:27; 2 Fal 17:6; Zab 60:1; Yer 32:37; Lk 21:24</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Wawauza watu wako bila kupata mali, </q1>
<q2>Wala hukupata faida kwa thamani yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>44:12</xo>
<xt>Isa 52:3,4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Umetufanya kuwa lawama kwa jirani zetu, </q1>
<q2>Mzaha na dhihaka kwao wanaotuzunguka. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Umetufanya kuwa mithali kwa mataifa, </q1>
<q2>Sababu ya kutikisa kichwa kwa watu wa nchi. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Mchana kutwa fedheha yangu i mbele yangu, </q1>
<q2>Na haya ya uso wangu imenifunika, </q2>
<q1><vn>16 </vn>Kwa sauti ya mwenye kulaumu na kukufuru, </q1>
<q2>Kwa sababu ya adui na mjilipiza kisasi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>44:16</xo>
<xt>Zab 8:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Haya yote yametupata, bali hatukukusahau, </q1>
<q2>Wala hatukulihalifu agano lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>44:17</xo>
<xt>Dan 9:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>Hatukuiacha mioyo yetu irudi nyuma, </q1>
<q2>Wala hatua zetu hazikuiacha njia yako. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Hata utuponde katika kao la mbwa-mwitu, </q1>
<q2>Na kutufunika kwa uvuli wa mauti. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>44:19</xo>
<xt>Isa 34:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu, </q1>
<q2>Au kumnyoshea mungu mgeni mikono yetu; </q2>
<q1><vn>21 </vn>Je! Mungu hatalichunguza neno hilo? </q1>
<q2>Maana ndiye azijuaye siri za moyo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>44:21</xo>
<xt>Ayu 31:14; Zab 139:1; 1 Sam 16:7; Mhu 12:14; Yn 2:25; Mdo 1:24; Rum 2:16; Ebr 4:12; Ufu 2:23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>22 </vn>Hasha! Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; </q1>
<q2>Tunafanywa kondoo waendao kuchinjwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>44:22</xo>
<xt>Rum 8:36</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>23 </vn>Amka, Bwana, mbona umelala? </q1>
<q2>Ondoka, usitutupe kabisa. </q2>
<q1><vn>24 </vn>Mbona unatuficha uso wako, </q1>
<q2>Na kusahau kuonewa na kudhulumiwa kwetu? </q2>
<q1><vn>25 </vn>Maana nafsi yetu imeinama mavumbini, </q1>
<q2>Tumbo letu limegandamana na nchi. </q2>
<q1><vn>26 </vn>Uondoke, uwe msaada wetu, </q1>
<q2>Utukomboe kwa ajili ya fadhili zako. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>45</cn>
<q1><vn>1 </vn>Moyo wangu umefurika kwa neno jema, </q1>
<q2>Mimi nasema niliyomfanyizia mfalme; </q2>
<q2>Ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mstadi. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Wewe u mzuri sana kuliko wanadamu; </q1>
<q2>Neema imemiminiwa midomoni mwako, </q2>
<q2>Kwa hiyo Mungu amekubariki hata milele. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari, </q1>
<q2>Utukufu ni wako na fahari ni yako. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Katika fahari yako usitawi uendelee </q1>
<q2>Kwa ajili ya kweli na upole na haki </q2>
<q1>Na mkono wako wa kuume </q1>
<q2>Utakufundisha mambo ya kutisha. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Mishale yako ni mikali, watu huanguka chini yako; </q1>
<q2>Imo mioyoni mwa adui za mfalme. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele, </q1>
<q2>Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>45:6-7</xo>
<xt>Ebr 1:8-9; Zab 93:2; Isa 9:6,7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Umeipenda haki; </q1>
<q2>Umeichukia dhuluma. </q2>
<q1>Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta, </q1>
<q2>Mafuta ya furaha kuliko wenzako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>45:7</xo>
<xt>Zab 33:5; Mt 3:15; Ebr 1:9; Isa 61:1; Yn 20:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Mavazi yako yote hunukia manemane </q1>
<q2>Na udi na mdalasini. </q2>
<q1>Katika majumba ya pembe </q1>
<q2>Vinubi vimekufurahisha. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Binti za wafalme wamo </q1>
<q2>Miongoni mwa akina bibi wako wastahiki. </q2>
<q1>Mkono wako wa kuume amesimama malkia </q1>
<q2>Amevaa dhahabu ya Ofiri. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Sikia, binti, utazame, utege sikio lako, </q1>
<q2>Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>45:10</xo>
<xt>Kum 21:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Naye mfalme atautamani uzuri wako, </q1>
<q2>Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>45:11</xo>
<xt>Zab 95:6; Isa 54:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Na binti Tiro analeta kipawa chake, </q1>
<q2>Nao matajiri wa watu watajipendekeza kwako. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Binti mfalme yumo ndani ana fahari tupu, </q1>
<q2>Mavazi yake ni ya nyuzi za dhahabu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>45:13</xo>
<xt>Ufu 19:7,8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Atapelekwa kwa mfalme </q1>
<q2>Na mavazi yaliyofumwa kwa uzuri. </q2>
<q1>Wanawali wenzake wanaomfuata, </q1>
<q2>Watapelekwa kwako. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Watapelekwa kwa furaha na shangwe, </q1>
<q2>Na kuingia katika nyumba ya mfalme. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Badala ya baba zako watakuwapo watoto wako, </q1>
<q2>Utawafanya kuwa wakuu katika nchi zote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>45:16</xo>
<xt>1 Pet 2:9; Ufu 1:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Jina lako nitalifanya kuwa kumbukumbu </q1>
<q2>Katika vizazi vyote. </q2>
<q1>Kwa hiyo mataifa watakushukuru </q1>
<q2>Milele na milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>45:17</xo>
<xt>Isa 11:10; Mal 1:11</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>46</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, </q1>
<q2>Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, </q1>
<q2>Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Maji yake yajapovuma na kuumuka, </q1>
<q2>Ijapopepesuka milima kwa kiburi chake. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Kuna mto, vijito vyake vyaufurahisha mji wa Mungu, </q1>
<q2>Patakatifu pa maskani zake Aliye juu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>46:4</xo>
<xt>Isa 8:7; Ufu 22:1; 2 Nya 6:6; Zab 48:1; Isa 60:14; Ebr 12:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Mungu yu katikati yake hautatetemeshwa; </q1>
<q2>Mungu atausaidia asubuhi na mapema. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>46:5</xo>
<xt>Kum 23:14; Isa 12:6; Eze 43:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Mataifa yalighadhibika, falme zikataharuki; </q1>
<q2>Alitoa sauti yake, nchi ikayeyuka. </q2>
<q2><vn>7 </vn>
<nd>Bwana</nd> wa majeshi yu pamoja nasi, </q2>
<q2>Mungu wa Yakobo ni ngome yetu. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Njoni myatazame matendo ya 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Avikomesha vita hata mwisho wa dunia; </q1>
<q2>Avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Acheni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, </q1>
<q2>Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi. </q2>
<q2><vn>11 </vn>
<nd>Bwana</nd> wa majeshi yu pamoja nasi, </q2>
<q2>Mungu wa Yakobo ni ngome yetu. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>47</cn>
<q1><vn>1 </vn>Enyi watu wote, pigeni makofi, </q1>
<q2>Mpigieni Mungu kelele kwa Sauti ya shangwe. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> Aliye juu, mwenye kuogofya, </q1>
<q2>Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>47:2</xo>
<xt>Kum 7:21; Neh 1:5; Mal 1:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Atawatiisha watu wa nchi chini yetu, </q1>
<q2>Na mataifa chini ya miguu yetu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>47:3</xo>
<xt>Zab 18:47</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Atatuchagulia urithi wetu, </q1>
<q2>Fahari ya Yakobo ambaye alimpenda. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>47:4</xo>
<xt>1 Pet 1:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Mungu amepaa kwa kelele za shangwe, </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> kwa sauti ya baragumu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>47:5</xo>
<xt>Zab 24:7-10; Mdo 1:9; Efe 4:8-10; 1 Tim 3:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Mwimbieni Mungu, naam, imbeni; </q1>
<q2>Mwimbieni mfalme wetu, naam, imbeni. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote, </q1>
<q2>Imbeni kwa akili. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>47:7</xo>
<xt>Zek 14:9; 1 Kor 14:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Mungu awamiliki mataifa, </q1>
<q2>Mungu ameketi katika kiti chake kitakatifu. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Wakuu wa watu wamekusanyika, </q1>
<q2>Wawe watu wa Mungu wa Ibrahimu. </q2>
<q1>Maana ngao za dunia zina Mungu, </q1>
<q2>Ametukuka sana. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>48</cn>
<q1><vn>1 </vn>Bwana ndiye aliye mkuu, </q1>
<q2>Na mwenye kusifiwa sana. </q2>
<q1>Katika mji wa Mungu wetu, </q1>
<q2>Katika mlima wake mtakatifu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>48:1</xo>
<xt>Isa 2:2; Oba 1:17; Mik 4:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kuinuka kwake ni mzuri sana, </q1>
<q2>Ni furaha ya dunia yote. </q2>
<q1>Mlima Sayuni pande za kaskazini, </q1>
<q2>Mji wa Mfalme mkuu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>48:2</xo>
<xt>Mt 5:35; Yer 3:19; Omb 2:15; Eze 20:6; Isa 14:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Mungu katika majumba yake </q1>
<q2>Amejijulisha kuwa ngome. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Maana, tazama, wafalme walikusanyika; </q1>
<q2>Walipita wote pamoja. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>48:4</xo>
<xt>2 Sam 10:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Waliona, mara wakashangaa; </q1>
<q2>Wakafadhaika na kukimbia. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Papo hapo tetemeko liliwashika, </q1>
<q2>Utungu kama wa mwanamke azaaye. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Kwa upepo wa mashariki </q1>
<q2>Wavunja jahazi za Tarshishi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>48:7</xo>
<xt>Eze 27:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Kama tulivyosikia, ndivyo tulivyoona, </q1>
<q2>Katika mji wa 
<nd>Bwana</nd> wa majeshi. </q2>
<q1>Mji wa Mungu wetu; </q1>
<q2>Mungu ataufanya imara hata milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>48:8</xo>
<xt>Isa 2:2; Mik 4:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Tumezitafakari fadhili zako, Ee Mungu, </q1>
<q2>Katikati ya hekalu lako. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Kama lilivyo jina lako, Ee Mungu, </q1>
<q2>Ndivyo na sifa yako hata miisho ya dunia. </q2>
<q2>Mkono wako wa kuume umejaa haki; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>48:10</xo>
<xt>Mal 1:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Na ufurahi mlima Sayuni. </q1>
<q2>Binti za Yuda na washangilie </q2>
<q2>Kwa sababu ya hukumu zako. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Tembeeni katika Sayuni, </q1>
<q2>Uzungukeni mji, </q2>
<q1>Ihesabuni minara yake, </q1>
<q2><vn>13 </vn>Tieni moyoni boma zake, </q2>
<q1>Yafikirini majumba yake, </q1>
<q2>Mpate kuwaambia kizazi kitakachokuja. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Kwa maana ndivyo alivyo </q1>
<q2>MUNGU, Mungu wetu. </q2>
<q1>Milele na milele </q1>
<q2>Yeye ndiye atakayetuongoza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>48:14</xo>
<xt>Isa 25:9</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>49</cn>
<q1><vn>1 </vn>Sikieni haya, enyi mataifa yote; </q1>
<q2>Sikilizeni, ninyi nyote mnaokaa duniani. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Watu wakuu na watu wadogo wote pia, </q1>
<q2>Tajiri na maskini wote pamoja. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Kinywa changu kitanena hekima, </q1>
<q2>Na fikira za moyo wangu zitakuwa za busara. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Nitatega sikio langu nisikie mithali, </q1>
<q2>Na kufumbua fumbo langu kwa kinubi <f> <fn>-</fn><note>
<xo>49:4</xo>
<xt>Zab 78:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Kwa nini niogope siku za uovu, </q1>
<q2>Ubaya ukinizunguka miguuni pangu? </q2>
<q1><vn>6 </vn>Wa hao wanaozitumainia mali zao, </q1>
<q2>Na kujisifia wingi wa utajiri wao; </q2>
<q1><vn>7 </vn>Hakuna mtu awezaye kumkomboa ndugu yake, </q1>
<q2>Wala kumpa Mungu fidia kwa ajili yake, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>49:7</xo>
<xt>Mt 16:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>(Maana fidia ya nafsi zao ina gharama, </q1>
<q2>Wala hana budi kuiacha hata milele;) <f> <fn>-</fn><note>
<xo>49:8</xo>
<xt>Ayu 36:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>ili aishi sikuzote asilione kaburi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>49:9</xo>
<xt>Ebr 9:27; Zab 89:48</xt></note></f> </q1>
<q1><vn>10 </vn>Naam, ataliona, hata wenye hekima hufa; </q1>
<q2>Mpumbavu na mjinga hupotea pamoja, </q2>
<q2>Na kuwaachia wengine mali zao. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Makaburi ni nyumba zao hata milele, </q1>
<q2>Maskani zao vizazi hata vizazi. </q2>
<q1>Hao waliotaja mashamba yao </q1>
<q2>Kwa majina yao wenyewe. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Lakini mwanadamu hadumu katika heshima, </q1>
<q2>Bali amefanana na wanyama wapoteao. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Hiyo ndiyo njia yao, ujinga wao, </q1>
<q2>Nao walioko baada yao huyaridhia maneno yao. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Kama kondoo wamewekwa kwenda kuzimu, </q1>
<q2>Na mauti itawachunga; </q2>
<q1>Watu wanyofu watawamiliki asubuhi; </q1>
<q2>Umbo lao litachakaa, kao lao ni kuzimu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>49:14</xo>
<xt>Dan 7:22; Mal 4:3; Lk 22:30; 1 Kor 6:2; 2 Tim 2:12; Ufu 2:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Bali Mungu atanikomboa nafsi yangu, </q1>
<q2>Atanitoa mkononi mwa kuzimu, maana atanikaribisha. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>49:15</xo>
<xt>Hos 13:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Usiogope mtu atakapopata utajiri, </q1>
<q2>Na fahari ya nyumba yake itakapozidi. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Maana atakapokufa hatachukua cho chote; </q1>
<q2>Utukufu wake hautashuka ukimfuata. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Ajapojibariki nafsi yake alipokuwa hai, </q1>
<q2>Na watu watakusifu ukijitendea mema, </q2>
<q1><vn>19 </vn>Atakwenda kwenye kizazi cha baba zake </q1>
<q2>Hawataona nuru hata milele. </q2>
<q1><vn>20 </vn>Mwanadamu mwenye heshima, iwapo hana akili, </q1>
<q2>Amefanana na wanyama wapoteao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>49:20</xo>
<xt>Mhu 3:19-21</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>50</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mungu, Mungu 
<nd>Bwana</nd>, amenena, ameiita nchi, </q1>
<q2>Toka maawio ya jua hata machweo yake. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Tokea Sayuni, ukamilifu wa uzuri, </q1>
<q2>Mungu amemulika. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Mungu wetu atakuja wala hatanyamaza, </q1>
<q2>Moto utakula mbele zake, </q2>
<q2>na tufani yavuma sana ikimzunguka pande zote. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Ataziita mbingu zilizo juu, </q1>
<q2>Na nchi pia awahukumu watu wake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>50:4</xo>
<xt>Mik 6:1,2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Nikusanyieni wacha Mungu wangu </q1>
<q2>Waliofanya agano nami kwa dhabihu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>50:5</xo>
<xt>Isa 13:3; 1 Kor 6:2; 1 The 3:13; Yud 1:14; Kut 24:7; Isa 59:20,21; Ebr 8:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Na mbingu zitatangaza haki yake, </q1>
<q2>Kwa maana Mungu ndiye aliye hakimu. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Sikieni, enyi watu wangu, nami nitanena, </q1>
<q1>Mimi nitakushuhudia, Israeli; </q1>
<q2>Mimi ndimi niliye MUNGU, Mungu wako. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Sitakukemea kwa ajili ya dhabihu zako, </q1>
<q2>Na kafara zako ziko mbele zangu daima. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Sitatwaa ng'ombe katika nyumba yako, </q1>
<q2>Wala beberu katika mazizi yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>50:9</xo>
<xt>Isa 43:23; Mik 6:6; Mdo 17:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Maana kila hayawani ni wangu, </q1>
<q2>Na makundi juu ya milima elfu. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Nawajua ndege wote wa milima, </q1>
<q2>Na wanyama wote wa mashamba ni wangu </q2>
<q1><vn>12 </vn>Kama ningekuwa na njaa singekuambia, </q1>
<q2>Maana ulimwengu ni wangu, navyo viujazavyo. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Je! Nile nyama ya mafahali! </q1>
<q2>Au ninywe damu ya mbuzi! </q2>
<q1><vn>14 </vn>Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; </q1>
<q2>Mtimizie Aliye juu nadhiri zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>50:14</xo>
<xt>Hes 14:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Ukaniite siku ya mateso; </q1>
<q2>Nitakuokoa, na wewe utanitukuza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>50:15</xo>
<xt>Ayu 22:27; Zab 22:23; Mt 5:16; Yn 15:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Bali mtu asiye haki, Mungu amwambia, </q1>
<q1>Una nini wewe kuitangaza sheria yangu, </q1>
<q2>Na kuliweka agano langu kinywani mwako? </q2>
<q1><vn>17 </vn>Maana wewe umechukia maonyo, </q1>
<q2>Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>50:17</xo>
<xt>Mit 1:7; 5:12,13; Rum 2:21; 2 The 2:10-12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>Ulipomwona mwivi ulikuwa radhi naye, </q1>
<q2>Ukashirikiana na wazinzi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>50:18</xo>
<xt>Rum 1:32</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Umekiachia kinywa chako kinene mabaya, </q1>
<q2>Na ulimi wako watunga hila. </q2>
<q1><vn>20 </vn>Umekaa na kumsengenya ndugu yako, </q1>
<q2>Na mwana wa mama yako umemsingizia. </q2>
<q1><vn>21 </vn>Ndivyo ulivyofanya, nami nikanyamaza; </q1>
<q2>Ukadhani ya kuwa Mimi ni kama wewe. </q2>
<q1>Walakini nitakukemea; </q1>
<q2>Nitayapanga hayo mbele ya macho yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>50:21</xo>
<xt>Mhu 8:11; Rum 2:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>22 </vn>Yafahamuni hayo, </q1>
<q2>Ninyi mnaomsahau Mungu, </q2>
<q1>Nisije nikawararueni, </q1>
<q2>Asipatikane mwenye kuwaponya. </q2>
<q1><vn>23 </vn>Atoaye dhabihu za kushukuru, </q1>
<q2>Ndiye anayenitukuza. </q2>
<q1>Naye autengenezaye mwenendo wake, </q1>
<q2>Nitamwonyesha wokovu wa Mungu. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>51</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu, unirehemu, </q1>
<q2>Sawasawa na fadhili zako. </q2>
<q1>Kiasi cha wingi wa rehema zako, </q1>
<q2>Uyafute makosa yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>51:1</xo>
<xt>Kol 2:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Unioshe kabisa na uovu wangu, </q1>
<q2>Unitakase dhambi zangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>51:2</xo>
<xt>Eze 36:25; Zek 13:1; 1 Kor 6:11; Ebr 9:14; 1 Yoh 1:7; Ufu 1:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Maana nimejua mimi makosa yangu </q1>
<q2>Na dhambi yangu i mbele yangu daima. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>51:3</xo>
<xt>Zab 32:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Nimekutenda dhambi Wewe peke yako, </q1>
<q2>Na kufanya maovu mbele za macho yako. </q2>
<q1>Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo, </q1>
<q2>Na kuwa safi utoapo hukumu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>51:4</xo>
<xt>Rum 3:4; Lk 15:21; Mwa 39:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; </q1>
<q2>Mama yangu alinichukua mimba hatiani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>51:5</xo>
<xt>Ayu 14:4; Yn 3:6; Rum 5:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Tazama, wapendezwa na kweli iliyo moyoni; </q1>
<q2>Nawe utanijulisha hekima kwa siri, </q2>
<q1><vn>7 </vn>Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi, </q1>
<q2>Unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji </q2>
<q1><vn>8 </vn>Unifanye kusikia furaha na shangwe, </q1>
<q2>Mifupa uliyoiponda ifurahi. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu; </q1>
<q2>Uzifute hatia zangu zote. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Ee Mungu, uniumbie moyo safi, </q1>
<q2>Uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu <f> <fn>-</fn><note>
<xo>51:10</xo>
<xt>Mit 20:9; Yer 13:27; Eze 11:19; Mdo 15:9; Efe 2:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Usinitenge na uso wako, </q1>
<q2>Wala roho yako mtakatifu usiniondolee. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>51:11</xo>
<xt>Mwa 4:14; Eze 36:27; Rum 8:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Unirudishie furaha ya wokovu wako; </q1>
<q2>Unitegemeze kwa roho ya wepesi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>51:12</xo>
<xt>Rum 8:15; 2 Kor 3:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Nitawafundisha wakosaji njia zako, </q1>
<q2>Na wenye dhambi watarejea kwako. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Ee MUNGU, Mungu wa wokovu wangu, </q1>
<q2>Uniponye na damu za watu, </q2>
<q2>Na ulimi wangu utaiimba haki yako. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Ee Bwana, uifumbue midomo yangu, </q1>
<q2>Na kinywa changu kitazinena sifa zako. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa, </q1>
<q2>Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika; </q1>
<q2>Moyo uliovunjika na kupondeka, </q2>
<q2>Ee Mungu, hutaudharau. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako, </q1>
<q2>Uzijenge kuta za Yerusalemu. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za haki, </q1>
<q2>Na sadaka za kuteketezwa, na kafara. </q2>
<q1>Ndipo watakapotoa ng'ombe </q1>
<q2>Juu ya madhabahu yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>51:19</xo>
<xt>Mal 3:3</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>52</cn>
<q1><vn>1 </vn>Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari? </q1>
<q2>Wema wa Mungu upo sikuzote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>52:1</xo>
<xt>1 Sam 22:9-10; 21:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ulimi wako watunga madhara, </q1>
<q2>Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila <f> <fn>-</fn><note>
<xo>52:2</xo>
<xt>Zab 50:19; Mit 12:18; Zab 59:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Umependa mabaya kuliko mema, </q1>
<q2>Na uongo kuliko kusema kweli. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>52:3</xo>
<xt>Yer 9:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Umependa maneno yote ya kupoteza watu, </q1>
<q2>Ewe ulimi wenye hila. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Lakini Mungu atakuharibu hata milele; </q1>
<q2>Atakuondolea mbali; </q2>
<q1>Atakunyakua hemani mwako; </q1>
<q2>Atakung'oa katika nchi ya walio hai. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>52:5</xo>
<xt>Mit 2:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nao wenye haki wataona; </q1>
<q2>Wataingiwa na hofu na kumcheka; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>52:6</xo>
<xt>Ayu 22:19; Zab 58:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Kumbe! Huyu ndiye mtu yule, </q1>
<q2>Asiyemfanya Mungu kuwa nguvu zake. </q2>
<q1>Aliutumainia wingi wa mali zake, </q1>
<q2>Na kujifanya hodari kwa madhara yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>52:7</xo>
<xt>Ayu 31:24,25; Zab 49:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Bali mimi ni kama mzeituni </q1>
<q2>Umeao katika nyumba ya Mungu. </q2>
<q1>Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>52:8</xo>
<xt>Zab 92:13</xt></note></f> </q1>
<q1><vn>9 </vn>Nitakushukuru milele kwa maana umetenda; </q1>
<q2>Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema; </q2>
<q2>Mbele ya wacha Mungu wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>52:9</xo>
<xt>Zab 54:6</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>53</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu; </q1>
<q2>Wametenda uovu wa ufisadi na kuchukiza, </q2>
<q2>Hakuna atendaye mema. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>53:1-3</xo>
<xt>Rum 3:10-12; Zab 10:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Toka mbinguni MUNGU aliwachungulia wanadamu, </q1>
<q2>Aone kama yuko mtu mwenye akili, </q2>
<q2>Amtafutaye Mungu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>53:2</xo>
<xt>Zab 33:13; 2 Nya 15:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Kila mtu amepotoka, wameoza wote pamoja, </q1>
<q2>Hakuna atendaye mema, </q2>
<q2>La! Hata mmoja. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>53:3</xo>
<xt>Mhu 7:29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Je! Wafanyao maovu hawajui? </q1>
<q2>Walao watu wangu kama walavyo mkate, </q2>
<q2>Hawakumwita MUNGU. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>53:4</xo>
<xt>Yer 4:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Hapo waliingiwa na hofu pasipokuwapo hofu, </q1>
<q2>Maana Mungu ameitawanya mifupa yake aliyekuhusuru. </q2>
<q1>Umewatia aibu, </q1>
<q2>Kwa sababu MUNGU amewadharau. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Laiti wokovu wa Israeli utoke katika Sayuni! </q1>
<q1>MUNGU awarudishapo wafungwa wa watu wake; </q1>
<q2>Yakobo atashangilia, </q2>
<q2>Israeli atafurahi. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>54</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu, kwa jina lako uniokoe, </q1>
<q2>Na kwa uweza wako unifanyie hukumu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ee Mungu, uyasikie maombi yangu, </q1>
<q2>Uyasikilize maneno ya kinywa changu. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Kwa maana wageni wamenishambulia; </q1>
<q2>Watu watishao wananitafuta nafsi yangu; </q2>
<q2>Hawakumweka Mungu mbele yao. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Tazama, Mungu ndiye anayenisaidia; </q1>
<q2>Bwana ndiye anayenitegemeza nafsi yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>54:4</xo>
<xt>Zab 118:7; Isa 41:10; Rum 8:31,32; Ebr 13:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Atawarudishia adui zangu ubaya wao; </q1>
<q2>Uwaangamize kwa uaminifu wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>54:5</xo>
<xt>Zab 89:49</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Kwa ukunjufu wa moyo nitakutolea dhabihu; </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, nitalishukuru jina lako, maana ni jema. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Kwa kuwa limeniokoa na kila taabu; </q1>
<q2>Na jicho langu limeridhika </q2>
<q2>Kwa kuwatazama adui zangu. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>55</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu, uisikilize sala yangu, </q1>
<q2>Wala usijifiche nikuombapo rehema. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Unisikilize na kunijibu, </q1>
<q2>Nimetanga-tanga nikilalama na kuugua. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Kwa sababu ya sauti ya adui, </q1>
<q2>Kwa sababu ya dhuluma yake yule mwovu. </q2>
<q1>Kwa maana wananitupia uovu, </q1>
<q2>Na kwa ghadhabu wananiudhi. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Moyo wangu unaumia ndani yangu, </q1>
<q2>Na hofu za mauti zimeniangukia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>55:4</xo>
<xt>Zab 102:3-5; Mt 26:37,38; Yn 12:27; 2 Kor 1:8-10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Hofu na tetemeko limenijia, </q1>
<q2>Na hofu kubwa imenifunikiza. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nikasema, Ningekuwa na mbawa kama njiwa, </q1>
<q2>Ningerukia mbali na kustarehe. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ningekwenda zangu mbali, </q1>
<q2>Ningetua jangwani. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ningefanya haraka kuzikimbia </q1>
<q2>Dhoruba na tufani. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Ee Bwana, uwaangamize, uzichafue ndimi zao, </q1>
<q2>Maana nimeona dhuluma na fitina katika mji. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Mchana na usiku huzunguka kutani mwake; </q1>
<q2>Uovu na taabu zimo ndani yake; </q2>
<q1><vn>11 </vn>Tamaa mbaya zimo ndani yake; </q1>
<q2>Dhuluma na hila haziondoki mitaani mwake. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Kwa maana aliyetukana si adui; </q1>
<q2>Kama ndivyo, ningevumilia. </q2>
<q1>Aliyejitukuza juu yangu siye anichukiaye; </q1>
<q2>Kama ndivyo, ningejificha asinione. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Bali ni wewe, mtu mwenzangu, </q1>
<q2>Rafiki yangu, niliyejuana nawe sana. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>55:13</xo>
<xt>2 Sam 15:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Tulipeana shauri tamu; na kutembea </q1>
<q2>Nyumbani mwa Mungu pamoja na mkutano. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Mauti na iwapate kwa ghafula, </q1>
<q2>Na washuke kuzimu wangali hai, </q2>
<q2>Maana uovu u makaoni mwao na katikati yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>55:15</xo>
<xt>Hes 16:30</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Nami nitamwita Mungu, </q1>
<q2>Na 
<nd>Bwana</nd> ataniokoa; </q2>
<q1><vn>17 </vn>Jioni, asubuhi, na adhuhuri nitalalama na kuugua, </q1>
<q2>Naye ataisikia sauti yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>55:17</xo>
<xt>Dan 6:10; Lk 18:1; Mdo 3:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>Ameiokoa nafsi yangu iwe salama, asinikaribie mtu, </q1>
<q2>Maana walioshindana nami walikuwa wengi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>55:18</xo>
<xt>2 Nya 32:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Mungu atasikia na kuwajibu; </q1>
<q2>Ndiye Yeye akaaye tangu milele. </q2>
<q1>Mageuzi ya mambo hayawapati hao, </q1>
<q2>Kwa hiyo hawamchi Mungu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>55:19</xo>
<xt>Kum 33:27</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Amenyosha mkono awadhuru waliopatana naye, </q1>
<q2>Amelihalifu agano lake. </q2>
<q1><vn>21 </vn>Kinywa chake ni laini kuliko siagi, </q1>
<q2>Bali moyo wake ni vita. </q2>
<q1>Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, </q1>
<q2>Bali hayo ni panga wazi. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Umtwike 
<nd>Bwana</nd> mzigo wako naye atakutegemeza, </q1>
<q2>Hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>55:22</xo>
<xt>Zab 37:24</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>23 </vn>Nawe, Ee Mungu, utawatelemsha, </q1>
<q2>Walifikilie shimo la uharibifu; </q2>
<q1>Watu wa damu na hila hawataishi nusu ya siku zao, </q1>
<q2>Bali mimi nitakutumaini Wewe. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>56</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mungu, unirehemu, maana yuko atakaye kunimeza, </q1>
<q2>Mchana kutwa ananionea akileta vita. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>56:1</xo>
<xt>Zab 31:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Adui zangu wanataka kunimeza mchana kutwa, </q1>
<q2>Maana waletao vita juu yangu kwa kiburi ni wengi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>56:2</xo>
<xt>Zab 57:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>56:3</xo>
<xt>1 Sam 30:6; 2 Nya 20:3</xt></note></f> </q1>
<q1><vn>4 </vn>Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. </q1>
<q2>Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; </q2>
<q2>Mwenye mwili atanitenda nini? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>56:4</xo>
<xt>Ebr 13:5,6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Mchana kutwa wanapotosha maneno yangu, </q1>
<q2>Mawazo yao yote ni juu yangu kunitakia mabaya. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Hukutanika, hujificha, huziangalia nyayo zangu, </q1>
<q2>Kwa kuwa wameniotea nafsi yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>56:6</xo>
<xt>Mdo 4:27,28</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Je! Wataokoka kwa uovu wao? </q1>
<q2>Ee Mungu, uwaangamize kwa hasira yako. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Umehesabu kutanga-tanga kwangu; </q1>
<q2>Uyatie machozi yangu katika chupa yako; </q2>
<q2>(Je! Hayamo katika kitabu chako?) <f> <fn>-</fn><note>
<xo>56:8</xo>
<xt>Mal 3:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Ndipo adui zangu watarudi nyuma siku ile niitapo. </q1>
<q2>Neno hili najua kuwa MUNGU yu upande wangu; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>56:9</xo>
<xt>Isa 8:9,10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. </q1>
<q2>Kwa msaada wa 
<nd>Bwana</nd> nitalisifu neno lake. </q2>
<q2><vn>11 </vn>Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; </q2>
<q2>Mwanadamu atanitenda nini? </q2>
<q1><vn>12 </vn>Ee Mungu, nadhiri zako zi juu yangu; </q1>
<q2>Nitakutolea dhabihu za kushukuru. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>56:12</xo>
<xt>Zab 116:14-16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Maana umeniponya nafsi yangu na mauti; </q1>
<q2>Je! Hukuizuia miguu yangu isianguke? </q2>
<q1>Ili nienende mbele za Mungu </q1>
<q2>Katika nuru ya walio hai. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>56:13</xo>
<xt>Ayu 33:30</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>57</cn>
<q1><vn>1 </vn>Unirehemu, Ee Mungu, unirehemu mimi, </q1>
<q2>Maana nafsi yangu imekukimbilia Wewe. </q2>
<q1>Nitaukimbilia uvuli wa mbawa zako, </q1>
<q2>Hata misiba hii itakapopita. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>57:1</xo>
<xt>Isa 26:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Nitamwita MUNGU Aliye juu, </q1>
<q2>Mungu anitimiziaye mambo yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>57:2</xo>
<xt>Zab 138:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Atapeleka toka mbinguni na kuniokoa, </q1>
<q2>Atukanapo yule atakaye kunimeza. </q2>
<q1>Mungu atazipeleka </q1>
<q2>Fadhili zake na kweli yake <f> <fn>-</fn><note>
<xo>57:3</xo>
<xt>Zab 144:5; 40:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Nafsi yangu i kati ya simba, </q1>
<q2>Nitastarehe kati yao waliowaka moto. </q2>
<q1>Wanadamu meno yao ni mikuki na mishale, </q1>
<q2>Na ndimi zao ni upanga mkali. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>57:4</xo>
<xt>Mit 30:14; Zab 64:3</xt></note></f> </q2>
<q2><vn>5 </vn>Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, </q2>
<q2>Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>57:5</xo>
<xt>Zab 108:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Wameweka wavu ili kuninasa miguu; </q1>
<q2>Nafsi yangu imeinama; </q2>
<q1>Wamechimba shimo mbele yangu; </q1>
<q2>Wametumbukia ndani yake! <f> <fn>-</fn><note>
<xo>57:6</xo>
<xt>Zab 9:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ee Mungu, moyo wangu u thabiti, </q1>
<q2>Moyo wangu u thabiti. </q2>
<q2>Nitaimba, nitaimba zaburi, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>57:7</xo>
<xt>Zab 108:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Amka, utukufu wangu. </q1>
<q2>Amka, kinanda na kinubi, </q2>
<q2>Nitaamka alfajiri. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>57:8</xo>
<xt>Amu 5:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Ee Bwana, nitakushukuru kati ya watu, </q1>
<q2>Nitakuimbia zaburi kati ya mataifa. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Maana fadhili zako ni kubwa hata mbinguni, </q1>
<q2>Na uaminifu wako hata mawinguni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>57:10</xo>
<xt>Zab 108:4</xt></note></f> </q2>
<q2><vn>11 </vn>Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, </q2>
<q2>Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>58</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ni kweli, enyi wakuu, mnanena haki? </q1>
<q2>Enyi wanadamu, mnahukumu kwa adili? </q2>
<q1><vn>2 </vn>Sivyo! Mioyoni mwenu mnatenda maovu; </q1>
<q2>Katika nchi mnapima udhalimu wa mikono yenu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>58:2</xo>
<xt>Zab 94:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Wasio haki wamejitenga tangu kuzaliwa kwao; </q1>
<q2>Tangu tumboni wamepotea, wakisema uongo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>58:3</xo>
<xt>Zab 51:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Sumu yao, mfano wake ni sumu ya nyoka; </q1>
<q2>Mfano wao ni fira kiziwi azibaye sikio lake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>58:4</xo>
<xt>Zab 140:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Asiyeisikiliza sauti ya waganga, </q1>
<q2>Ijapo wanafanya uganga kwa ustadi. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Ee Mungu, uyavunje meno yao vinywani mwao; </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uyavunje magego ya wana-simba. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>58:6</xo>
<xt>Ayu 4:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Na watoweke kama maji yapitayo kwa kasi; </q1>
<q2>Akiielekeza mishale yake, iwe imetiwa ubutu. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Kama konokono ayeyukaye na kutoweka, </q1>
<q2>Kama mimba iliyoharibika, isiyoliona jua, </q2>
<q1><vn>9 </vn>Kabla ya masufuria yenu kupata moto wa miiba, </q1>
<q2>Ataipeperusha kama chamchela, </q2>
<q2>Iliyo mibichi na iliyo moto. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>58:9</xo>
<xt>Mit 10:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Mwenye haki atafurahi akionapo kisasi; </q1>
<q2>Ataiosha miguu yake katika damu ya wasio haki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>58:10</xo>
<xt>Kum 32:42; Ayu 22:19; Zab 18:47; Mit 10:11; Ufu 18:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Na mwanadamu atasema, </q1>
<q2>Hakika iko thawabu yake mwenye haki. </q2>
<q1>Hakika yuko Mungu </q1>
<q2>Anayehukumu katika dunia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>58:11</xo>
<xt>Rum 2:6-11; Ayu 34:11; Mhu 5:8; Yer 32:19; Eze 7:27; Rum 14:12; Ufu 2:23</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>59</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu wangu, uniponye na adui zangu, </q1>
<q2>Uniinue juu yao wanaoshindana nami. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Uniponye nao wafanyao maovu, </q1>
<q2>Uniokoe na watu wa damu. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Kwa maana wanaiotea nafsi yangu; </q1>
<q2>Wenye nguvu wamenikusanyikia; </q2>
<q1>Ee 
<nd>Bwana</nd>, si kwa kosa langu, </q1>
<q2>Wala si kwa hatia yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>59:3</xo>
<xt>1 Sam 26:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Bila kosa langu huenda mbio, hujiweka tayari; </q1>
<q2>Uamke uonane nami, na kutazama. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Na Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wa majeshi, </q1>
<q2>Mungu wa Israeli, uamke. </q2>
<q1>Uwapatilize mataifa yote; </q1>
<q2>Usiwarehemu waovu wafanyao uovu hata mmoja. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>59:5</xo>
<xt>Dan 4:35</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Wakati wa jioni hurudi, hulia kama mbwa, </q1>
<q2>Na kuzunguka-zunguka mjini. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Tazama, kwa vinywa vyao huteuka, </q1>
<q1>Midomoni mwao mna panga, </q1>
<q2>Kwa maana ni nani asikiaye? </q2>
<q1><vn>8 </vn>Na Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, utawacheka, </q1>
<q2>Utawadhihaki mataifa yote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>59:8</xo>
<xt>Zab 2:4; Mit 1:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Ee nguvu zangu, nitakungoja Wewe, </q1>
<q2>Maana Mungu ndiye aliye ngome yangu </q2>
<q1><vn>10 </vn>Mungu wa fadhili zangu atanitangulia, </q1>
<q2>Mungu atanijalia kuwatazama adui zangu. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Usiwaue, watu wangu wasije wakasahau; </q1>
<q1>Uwatawanye kwa uweza wako, </q1>
<q1>Na kuwaangamiza, Ee Bwana, ngao yetu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>59:11</xo>
<xt>Mwa 4:12,13</xt></note></f> </q1>
<q1><vn>12 </vn>Kwa dhambi ya kinywa chao, </q1>
<q2>Na kwa neno la midomo yao, </q2>
<q1>Wanaswe kwa kiburi chao, </q1>
<q2>Kwa ajili ya kulaani na uongo wasemao. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Uwakomeshe kwa hasira, </q1>
<q2>Uwakomeshe watoweke, </q2>
<q1>Wajue ya kuwa Mungu atawala katika Yakobo, </q1>
<q2>Na hata miisho ya dunia. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Wakati wa jioni hurudi, hulia kama mbwa, </q1>
<q2>Na kuzunguka-zunguka mjini. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Watatanga-tanga hao wakitafuta chakula; </q1>
<q2>Wasiposhiba watakesha usiku kucha. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Nami nitaziimba nguvu zako asubuhi, </q1>
<q2>Nitaziimba fadhili zako kwa furaha. </q2>
<q1>Kwa kuwa ndiwe uliyekuwa ngome yangu, </q1>
<q2>Na makimbilio siku ya shida yangu. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Ee nguvu zangu, nitakuimbia kwa furaha, </q1>
<q2>Maana Mungu ndiye aliye ngome yangu, </q2>
<q2>Mungu wa fadhili zangu. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>60</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu, umetutupa na kututawanya, </q1>
<q2>Umekuwa na hasira, uturudishe tena. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Umeitetemesha nchi na kuipasua, </q1>
<q2>Upaponye palipobomoka, maana inatikisika. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Umewaonyesha watu wako mazito, </q1>
<q2>Na kutunywesha mvinyo ya kutuyumbisha. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Umewapa wakuogopao bendera, </q1>
<q2>Ili itwekwe kwa ajili ya kweli. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>60:4</xo>
<xt>Isa 11:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Ili wapenzi wako waopolewe, </q1>
<q2>Uokoe kwa mkono wako wa kuume, utuitikie. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>60:5</xo>
<xt>Zab 108:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Mungu amenena kwa utakatifu wake, </q1>
<q2>Nami nitashangilia. </q2>
<q1>Nitaigawanya Shekemu, </q1>
<q2>Nitalipima bonde la Sukothi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>60:6</xo>
<xt>Zab 89:35; Mwa 12:6; Yos 13:27</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Gileadi ni yangu, na Manase ni yangu, </q1>
<q2>Na Efraimu ni nguvu ya kichwa changu. </q2>
<q2>Yuda ni fimbo yangu ya kifalme, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>60:7</xo>
<xt>Kum 33:17; Mwa 49:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Moabu ni bakuli langu la kunawia. </q1>
<q2>Nitamtupia Edomu kiatu changu, </q2>
<q2>Na kumpigia Filisti kelele za vita. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Ni nani atakayenipeleka hata mji wenye boma? </q1>
<q2>Ni nani atakayeniongoza hata Edomu? </q2>
<q1><vn>10 </vn>Ee Mungu, si Wewe uliyetutupa? </q1>
<q2>Wala, Ee Mungu, hutoki na majeshi yetu? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>60:10</xo>
<xt>Zab 44:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Utuletee msaada juu ya mtesi, </q1>
<q2>Maana wokovu wa binadamu haufai. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Kwa msaada wa Mungu tutatenda makuu, </q1>
<q2>Maana Yeye atawakanyaga watesi wetu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>60:12</xo>
<xt>1 Nya 19:13</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>61</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu, ukisikie kilio changu, </q1>
<q2>Uyasikilize maombi yangu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Toka mwisho wa nchi nitakulilia nikizimia moyo, </q1>
<q2>Uniongoze juu ya mwamba nisioweza kuupanda. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>61:2</xo>
<xt>1 Tim 2:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Kwa maana ulikuwa kimbilio langu, </q1>
<q2>Ngome yenye nguvu adui asinipate. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>61:3</xo>
<xt>Mit 18:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Nitakaa katika hema yako milele, </q1>
<q2>Nitaikimbilia sitara ya mbawa zako <f> <fn>-</fn><note>
<xo>61:4</xo>
<xt>Zab 15:1; 23:6; Ufu 3:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Maana Wewe, Mungu, umezisikia nadhiri zangu. </q1>
<q2>Umewapa urithi wao waliogopao jina lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>61:5</xo>
<xt>1 Kor 3:21-23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Utaziongeza siku za mfalme, </q1>
<q2>Miaka yake itakuwa kama vizazi vingi. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Atakaa mbele za Mungu milele, </q1>
<q2>Ziagize fadhili na kweli zimhifadhi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>61:7</xo>
<xt>Zab 41:12; Lk 1:32</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ndivyo nitakavyoliimbia jina lako daima, </q1>
<q2>Ili niondoe nadhiri zangu kila siku. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>61:8</xo>
<xt>Zab 56:12</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>62</cn>
<q1><vn>1 </vn>Nafsi yangu yamngoja Mungu peke yake kwa kimya, </q1>
<q2>Wokovu wangu hutoka kwake. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Yeye tu ndiye mwamba wangu na wokovu wangu, </q1>
<q2>Ngome yangu, sitatikisika sana. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Hata lini mtamshambulia mtu, </q1>
<q2>Mpate kumwua ninyi nyote pamoja? </q2>
<q1>Kama ukuta unaoinama, </q1>
<q2>Kama kitalu kilicho tayari kuanguka, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>62:3</xo>
<xt>Isa 30:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Hufanya shauri kumwangusha tu katika cheo chake; </q1>
<q2>Huufurahia uongo. </q2>
<q1>Kwa kinywa chao hubariki; </q1>
<q2>Kwa moyo wao hulaani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>62:4</xo>
<xt>Zab 28:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Nafsi yangu, umngoje Mungu peke yake kwa kimya. </q1>
<q2>Tumaini langu hutoka kwake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>62:5</xo>
<xt>Mik 7:7,10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Yeye tu ndiye mwamba wangu na wokovu wangu, </q1>
<q2>Ngome yangu, sitatikisika sana. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Kwa Mungu wokovu wangu, </q1>
<q2>Na utukufu wangu; </q2>
<q1>Mwamba wa nguvu zangu, </q1>
<q2>Na kimbilio langu ni kwa Mungu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>62:7</xo>
<xt>Yer 3:23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Enyi watu, mtumainini sikuzote, </q1>
<q2>Ifunueni mioyo yenu mbele zake; </q2>
<q1>Mungu ndiye kimbilio letu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>62:8</xo>
<xt>1 Sam 1:15; Zab 42:4</xt></note></f> </q1>
<q1><vn>9 </vn>Hakika binadamu ni ubatili, </q1>
<q1>Na wenye cheo ni uongo, </q1>
<q2>Katika mizani huinuka; </q2>
<q2>Wote pamoja ni hafifu kuliko ubatili. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Msiitumainie dhuluma, </q1>
<q2>Wala msijivune kwa unyang'anyi; </q2>
<q2>Mali izidipo msiiangalie sana moyoni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>62:10</xo>
<xt>Isa 26:4; Mk 10:23; Lk 12:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Mara moja amenena Mungu; </q1>
<q2>Mara mbili nimeyasikia haya, </q2>
<q2>Ya kuwa nguvu zina Mungu, </q2>
<q1><vn>12 </vn>Na fadhili ziko kwako, Ee Bwana; </q1>
<q2>Maana ndiwe umlipaye kila mtu </q2>
<q2>Sawasawa na haki yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>62:12</xo>
<xt>Ayu 34:11; Yer 17:10; Mt 16:27; 1 Pet 1:17; Rum 2:6; Ufu 2:23</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>63</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee MUNGU, Mungu wangu, nitakutafuta mapema, </q1>
<q2>Nafsi yangu inakuonea kiu, </q2>
<q1>Mwili wangu wakuonea shauku, </q1>
<q2>Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>63:1</xo>
<xt>1 Sam 23:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ndivyo nilivyokutazama katika patakatifu, </q1>
<q2>Nizione nguvu zako na utukufu wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>63:2</xo>
<xt>1 Nya 16:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai; </q1>
<q2>Midomo yangu itakusifu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>63:3</xo>
<xt>Yn 3:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai; </q1>
<q2>Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Nafsi yangu itakinai kama kushiba mafuta na vinono; </q1>
<q2>Kinywa changu kitakusifu kwa midomo ya furaha. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>63:5</xo>
<xt>Zab 17:15; Isa 25:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Ninapokukumbuka kitandani mwangu, </q1>
<q2>Nakutafakari Wewe makesha yote ya usiku. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>63:6</xo>
<xt>Zab 149:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Maana Wewe umekuwa msaada wangu, </q1>
<q2>Na uvulini mwa mbawa zako nitashangilia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>63:7</xo>
<xt>2 Kor 1:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Nafsi yangu inakuandama sana; </q1>
<q2>Mkono wako wa kuume unanitegemeza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>63:8</xo>
<xt>Isa 26:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Bali waitafutao nafsi yangu, ili kuiharibu, </q1>
<q2>Wataingia pande za nchi zilizo chini. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Watatolewa wafe kwa nguvu za upanga, </q1>
<q2>Watakuwa riziki za mbwa-mwitu. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Bali mfalme atamfurahia Mungu, </q1>
<q2>Kila aapaye kwa Yeye atashangilia, </q2>
<q2>Kwa maana vinywa vya waongo vitafumbwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>63:11</xo>
<xt>Sef 1:5</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>64</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mungu, uisikie sauti yangu katika malalamiko yangu; </q1>
<q2>Unilinde uhai wangu na hofu ya adui. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Utanificha mbali na shauri la siri la watenda mabaya, </q1>
<q2>Mbali na ghasia ya watu wafanyao maovu; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>64:2</xo>
<xt>Zab 143:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Waliounoa ulimi wao kama upanga, </q1>
<q2>Wameielekeza mishale yao, maneno ya uchungu, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>64:3</xo>
<xt>Zab 57:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Wapate kumpiga mkamilifu faraghani, </q1>
<q2>Kwa ghafula humpiga wala hawaogopi. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Walijifanya hodari katika jambo baya; </q1>
<q2>Hushauriana juu ya kutega mitego; </q2>
<q2>Husema, Ni nani atakayeiona? </q2>
<q1><vn>6 </vn>Hutunga maovu; husema, Tumefanya shauri kamili; </q1>
<q2>Na mawazo ya ndani ya kila mmoja wao, </q2>
<q2>Na moyo wake, huwa siri kabisa. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Kwa hiyo Mungu atawapiga shabaha, </q1>
<q2>Kwa mshale mara watapigwa. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ndivyo watakavyokwazwa, </q1>
<q2>Ulimi wao wenyewe ukishindana nao. </q2>
<q2>Wote wawaonao watatikisa kichwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>64:8</xo>
<xt>Mit 12:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Na watu wote wataogopa, </q1>
<q2>Wataitangaza kazi ya Mungu, </q2>
<q2>Na kuyafahamu matendo yake. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Mwenye haki atamfurahia 
<nd>Bwana</nd> na kumkimbilia, </q1>
<q2>Na wote wenye moyo wa adili watajisifu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>64:10</xo>
<xt>Zab 32:11; Flp 4:4</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>65</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu, sifa zakulaiki katika Sayuni, </q1>
<q2>Na kwako Wewe itaondolewa nadhiri. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Wewe usikiaye kuomba, </q1>
<q2>Wote wenye mwili watakujia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>65:2</xo>
<xt>Lk 11:9,10; Isa 66:23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Ingawa maovu mengi yanamshinda, </q1>
<q2>Wewe utayafunika maasi yetu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>65:3</xo>
<xt>Ebr 9:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Heri mtu yule umchaguaye, </q1>
<q2>Na kumkaribisha akae nyuani mwako. </q2>
<q1>Na tushibe wema wa nyumba yako, </q1>
<q2>Patakatifu pa hekalu lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>65:4</xo>
<xt>Zab 33:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Kwa mambo ya kutisha utatujibu, </q1>
<q2>Katika haki, Ee Mungu wa wokovu wetu. </q2>
<q1>Wewe uliye tumaini la miisho yote ya dunia, </q1>
<q2>Na la bahari iliyo mbali sana, </q2>
<q1><vn>6 </vn>Milima waiweka imara kwa nguvu zako, </q1>
<q2>Huku ukijifunga uweza kama mshipi. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Wautuliza uvumi wa bahari, </q1>
<q2>Uvumi wa mawimbi yake, </q2>
<q2>Na ghasia ya mataifa; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>65:7</xo>
<xt>Mt 8:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Kwa hiyo wakaao mbali kabisa huogopa ishara zako; </q1>
<q2>Milango ya asubuhi na jioni waifurahisha. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>65:8</xo>
<xt>Ayu 37:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Umeijilia nchi na kuisitawisha, </q1>
<q2>Umeitajirisha sana; </q2>
<q1>Mto wa Mungu umejaa maji; </q1>
<q2>Wawaruzuku watu nafaka </q2>
<q2>Maana ndiwe uitengenezaye ardhi. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Matuta yake wayajaza maji; </q1>
<q2>Wapasawazisha palipoinuka, </q2>
<q1>Wailainisha nchi kwa manyunyu; </q1>
<q2>Waibariki mimea yake. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Umeuvika mwaka taji ya wema wako; </q1>
<q2>Mapito yako yadondoza unono. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>65:11</xo>
<xt>Zab 104:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Huyadondokea malisho ya nyikani, </q1>
<q2>Na vilima vyajifunga furaha. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Na malisho yamevikwa kondoo, </q1>
<q2>Na mabonde yamepambwa nafaka, </q2>
<q2>Yanashangilia, naam, yanaimba. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>66</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote, </q1>
<q1><vn>2 </vn>Imbeni utukufu wa jina lake, </q1>
<q2>Tukuzeni sifa zake. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Mwambieni Mungu, Matendo yako yatisha kama nini! </q1>
<q1>Kwa ajili ya wingi wa nguvu zako, </q1>
<q2>Adui zako watakuja kunyenyekea mbele zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>66:3</xo>
<xt>Zab 18:44</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Nchi yote itakusujudia na kukuimbia, </q1>
<q2>Naam, italiimbia jina lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>66:4</xo>
<xt>Zab 67:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Njoni yatazameni matendo ya Mungu; </q1>
<q2>Hutisha kwa mambo awatendayo wanadamu; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>66:5</xo>
<xt>Zab 46:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Aligeuza bahari ikawa nchi kavu; </q1>
<q2>Katika mto walivuka kwa miguu; </q2>
<q2>Huko ndiko mlikomfurahia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>66:6</xo>
<xt>Kut 14:21; Yos 3:14-17; Zab 78:13; Isa 63:13,14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Atawala kwa uweza wake milele; </q1>
<q2>Macho yake yanaangalia mataifa; </q2>
<q2>Waasio wasijitukuze nafsi zao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>66:7</xo>
<xt>Zab 11:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Enyi mataifa, mtukuzeni Mungu wetu, </q1>
<q2>Itangazeni sauti ya sifa zake; </q2>
<q1><vn>9 </vn>Aliyeiweka nafsi yetu katika uhai, </q1>
<q2>Wala hakuuacha mguu wetu usogezwe. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Kwa maana umetupima, Ee Mungu, </q1>
<q2>Umetujaribu inavyojaribiwa fedha. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>66:10</xo>
<xt>Zek 13:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Ulituingiza ndani ya wavu, </q1>
<q2>Na kuweka viunoni mwetu mzigo uliotulemea. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Uliwapandisha watu </q1>
<q2>Juu ya vichwa vyetu. </q2>
<q1>Tulipita motoni na majini; </q1>
<q2>Ukatutoa na kutuleta kunako wingi. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Nitaingia nyumbani mwako na kafara; </q1>
<q2>Nitaondoa kwako nadhiri zangu; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>66:13</xo>
<xt>Zab 116:14,18; Mhu 5:4; Yon 2:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Ambazo midomo yangu ilizinena; </q1>
<q2>Kinywa changu kikazisema nilipokuwa taabuni. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Kafara za vinono nitakutolea, </q1>
<q1>Pamoja na fukizo la kondoo waume, </q1>
<q2>Nitatoa ng'ombe pamoja na mbuzi. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Njoni, sikieni, ninyi nyote mnaomcha Mungu, </q1>
<q2>Nami nitayatangaza aliyonitendea roho yangu. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Nalimwita kwa kinywa changu, </q1>
<q2>Na sifa kuu zilikuwa chini ya ulimi wangu. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Kama ningaliwaza maovu moyoni mwangu, </q1>
<q2>Bwana asingesikia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>66:18</xo>
<xt>Ayu 11:14,15; Mit 15:29; Isa 1:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Hakika Mungu amesikia; </q1>
<q2>Ameisikiliza sauti ya maombi yangu. </q2>
<q1><vn>20 </vn>Na ahimidiwe Mungu asiyeyakataa maombi yangu, </q1>
<q2>Wala kuniondolea fadhili zake. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>67</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mungu na atufadhili na kutubariki, </q1>
<q2>Na kutuangazia uso wake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>67:1</xo>
<xt>Zab 4:6; 31:16; 119:135; Hes 6:25,26; 2 Kor 4:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Njia yake ijulike duniani, </q1>
<q2>Wokovu wake katikati ya mataifa yote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>67:2</xo>
<xt>Mdo 13:10; Tit 2:11; Lk 2:30-32</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Watu na wakushukuru, Ee Mungu, </q1>
<q2>Watu wote na wakushukuru. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>67:3</xo>
<xt>Isa 24:15,16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Mataifa na washangilie, </q1>
<q2>Naam, waimbe kwa furaha, </q2>
<q1>Maana kwa haki utawahukumu watu, </q1>
<q2>Na kuwaongoza mataifa walioko duniani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>67:4</xo>
<xt>Zab 96:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Watu na wakushukuru, Ee Mungu, </q1>
<q2>Watu wote na wakushukuru. </q2>
<b></b>
<q1><vn>6 </vn>Nchi imetoa mazao yake </q1>
<q2>MUNGU, Mungu wetu, ametubariki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>67:6</xo>
<xt>Law 26:4; Isa 1:19; Zab 85:9-12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Mungu atatubariki sisi; </q1>
<q2>Miisho yote ya dunia itamcha Yeye. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>67:7</xo>
<xt>Zab 22:27</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>68</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mungu huondoka, adui zake wakatawanyika, </q1>
<q2>Nao wamchukiao huukimbia uso wake. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kama moshi upeperushwavyo, </q1>
<q2>Ndivyo uwapeperushavyo wao; </q2>
<q1>Kama nta iyeyukavyo mbele ya moto, </q1>
<q2>Ndivyo waovu wapoteavyo usoni pa Mungu. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Bali wenye haki hufurahi, </q1>
<q1>Na kuushangilia uso wa Mungu, </q1>
<q2>Naam, hupiga kelele kwa furaha. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Mwimbieni Mungu, lisifuni jina lake, </q1>
<q2>Mtengenezeeni njia ya barabara, </q2>
<q1>Apitaye majangwani kama mpanda farasi; </q1>
<q2>Jina lake ni YAHU; shangilieni mbele zake. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Baba wa yatima na mwamuzi wa wajane, </q1>
<q2>Mungu katika kao lake takatifu. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Mungu huwakalisha wapweke nyumbani; </q1>
<q1>Huwatoa wafungwa wakae hali ya kufanikiwa; </q1>
<q2>Bali wakaidi hukaa katika nchi kavu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>68:6</xo>
<xt>1Sam 2:5.</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>7 </vn>Ee Mungu, ulipotoka mbele ya watu wako, </q1>
<q2>Ulipopita nyikani, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>68:7</xo>
<xt>Hab 3:13.</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Nchi ilitetemeka </q1>
<q1>Naam, mbingu zilidondoka usoni pa Mungu; </q1>
<q2>Hata Sinai usoni pa Mungu; Mungu wa Israeli. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>68:8</xo>
<xt>Kut 19:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Ee Mungu, ulinyesha mvua ya neema; </q1>
<q2>Urithi wako ulipochoka uliutia nguvu. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Kabila yako ilifanya kao lake huko; </q1>
<q2>Ee Mungu, kwa wema wako uliwaruzuku walioonewa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>68:10</xo>
<xt>Zab 74:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Bwana analitoa neno lake; </q1>
<q2>Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa; </q2>
<q1><vn>12 </vn>Wafalme wa majeshi wanakimbia, wanakimbia; </q1>
<q2>Na mwanamke akaaye nyumbani agawa nyara. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Kwa nini kulala mazizini arukapo hua, </q1>
<q2>Mbawa zake ziking'aa kama fedha </q2>
<q2>Na manyoya yake kama dhahabu? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>68:13</xo>
<xt>Zab 81:6; Efe 5:26,27.</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Mwenyezi Mungu alipotawanya wafalme huko, </q1>
<q2>Kulinyesha theluji katika Salmoni. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Ni mlima wa Mungu mlima Bashani, </q1>
<q2>Ni mlima mrefu mlima Bashani. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Enyi milima mirefu, kwani kuutazama kwa wivu </q1>
<q1>Mlima alioutamani Mungu akae juu yake? </q1>
<q2>Naam, 
<nd>Bwana</nd> atakaa juu yake milele. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Magari ya Mungu ni ishirini elfu, maelfu maelfu; </q1>
<q2>Bwana yumo kati yao kama katika Sinai, </q2>
<q2>Katika patakatifu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>68:17</xo>
<xt>Kum 33:2; 2Fal 6:17; Dan 7:10.</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>Wewe umepaa juu, umeteka mateka, </q1>
<q2>Umepewa vipawa katikati ya wanadamu; </q2>
<q2>Naam, hata na wakaidi, 
<nd>Bwana</nd> Mungu akae nao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>68:18</xo>
<xt>Amu 5:12; Zab 78:60; Mdo 1:9; 2:4; Efe 4:8; 1Tim 1:13.</xt></note></f> </q2>
<q2><vn>19 </vn>Na ahimidiwe Bwana, </q2>
<q1>Siku kwa siku hutuchukulia mzigo wetu; </q1>
<q2>Mungu ndiye wokovu wetu. </q2>
<q1><vn>20 </vn>Mungu kwetu sisi ni Mungu wa kuokoa; </q1>
<q2>Na njia za kutoka mautini zina YEHOVA Bwana. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>68:20</xo>
<xt>Kum 32:39</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Naam, Mungu atakipasua kichwa cha adui zake, </q1>
<q2>Utosi wenye nywele wa mtu afulizaye kukosa. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Bwana alisema, Kutoka Bashani nitawarudisha, </q1>
<q2>Nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari; </q2>
<q1><vn>23 </vn>Uuchovye mguu wako katika damu ya adui zako, </q1>
<q2>Na ulimi wa mbwa zako upate sehemu yake. </q2>
<q1><vn>24 </vn>Ee Mungu, wameiona miendo yako; </q1>
<q2>Miendo ya Mungu wangu, Mfalme wangu, katika patakatifu </q2>
<q1><vn>25 </vn>Waimbaji hutangulia, nyuma yao wapigao vinanda, </q1>
<q2>Kati ya wanawali wapiga matari. </q2>
<q1><vn>26 </vn>Mhimidini Mungu katika mikutano, </q1>
<q2>Bwana katika makusanyiko ya Israeli. </q2>
<q1><vn>27 </vn>Yuko Benyamini mdogo, mtawala wao; </q1>
<q2>Wakuu wa Yuda, kundi lao; </q2>
<q1>Wakuu wa Zabuloni; </q1>
<q2>Wakuu wa Naftali. </q2>
<b></b>
<q1><vn>28 </vn>Ee Mungu, uziamuru nguvu zako; </q1>
<q2>Ee Mungu, uwe hodari uliyetufanyia makuu. </q2>
<q1><vn>29 </vn>Kwa ajili ya hekalu lako Yerusalemu </q1>
<q2>Wafalme watakuletea hedaya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>68:29</xo>
<xt>2Nya 32:23; Isa 60:16.</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>30 </vn>Mkemee mnyama wa manyasini; </q1>
<q2>Kundi la mafahali, na ndama za watu; </q2>
<q1>Hata wanyenyekee na kuleta vipande vya fedha, </q1>
<q2>Uwatawanye watu wapendao vita. </q2>
<q1><vn>31 </vn>Masheki watakuja kutoka Misri, </q1>
<q2>Kushi itamnyoshea Mungu mikono yake mara. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>68:31</xo>
<xt>Isa 19:19; 45:14; Sef 3:10; Mdo 8:27,28.</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>32 </vn>Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu, </q1>
<q2>Msifuni Bwana kwa nyimbo. </q2>
<q1><vn>33 </vn>Apandaye mbingu za mbingu za tangu milele; </q1>
<q2>Aitoa sauti yake, sauti ya nguvu. </q2>
<q1><vn>34 </vn>Mhesabieni Mungu nguvu; </q1>
<q2>Enzi yake i juu ya Israeli; </q2>
<q2>Na nguvu zake zi mawinguni. </q2>
<q1><vn>35 </vn>Mungu ni mwenye kutisha </q1>
<q2>Kutoka patakatifu pako. </q2>
<q1>Ndiye Mungu wa Israeli; </q1>
<q2>Yeye huwapa watu wake nguvu na uwezo. </q2>
<q2>Na ahimidiwe Mungu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>68:35</xo>
<xt>Isa 41:10; Zek 10:12; Yn 15:5; Efe 6:10; Flp 4:13.</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>69</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu, uniokoe, </q1>
<q2>Maana maji yamefika mpaka nafsini mwangu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ninazama katika matope mengi, </q1>
<q2>Pasipowezekana kusimama. </q2>
<q1>Nimefika penye maji ya vilindi, </q1>
<q2>Mkondo wa maji unanigharikisha. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Nimechoka kwa kulia kwangu, </q1>
<q2>Koo yangu imekauka. </q2>
<q1>Macho yangu yamedhoofu </q1>
<q2>Kwa kumngoja Mungu wangu. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Wanaonichukia bure ni wengi </q1>
<q2>Kuliko nywele za kichwa changu. </q2>
<q1>Watakao kunikatilia mbali wamekuwa hodari, </q1>
<q2>Adui zangu kwa sababu isiyo kweli. </q2>
<q1>Hata mimi nalilipishwa kwa nguvu </q1>
<q2>Vitu nisivyovichukua. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>69:4</xo>
<xt>Zab 35:19; Yn 15:25</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>5 </vn>Ee Mungu, unajua upumbavu wangu, </q1>
<q2>Wala hukufichwa dhambi yangu. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Wanaokungoja Wewe wasiaibishwe, </q1>
<q2>Kwa ajili yangu, Bwana, MUNGU wa majeshi. </q2>
<q1>Wanaokutafuta Wewe wasifedheheshwe, </q1>
<q2>Kwa ajili yangu, Ee Mungu wa Israeli. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Maana kwa ajili yako nimestahimili laumu, </q1>
<q2>Fedheha imenifunika uso wangu. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, </q1>
<q2>Na msikwao kwa wana wa mama yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>69:8</xo>
<xt>Isa 53:3; Yn 1:11.</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Maana wivu wa nyumba yako umenila, </q1>
<q2>Na laumu zao wanaokulaumu zimenipata. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>69:9</xo>
<xt>1 Fal 19:10; Zab 119:139; Yn 2:17; Rum 15:3.</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Nilipolia na kuiadhibu roho yangu kwa kufunga, </q1>
<q2>Ikawa laumu juu yangu. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Nilipofanya gunia kuwa nguo zangu, </q1>
<q2>Nikawa mithali kwao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>69:11</xo>
<xt>1Fal 9:7; Yer 24:9; Zab 44:13,14.</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>12 </vn>Waketio langoni hunisema, </q1>
<q2>Na nyimbo za walevi hunidhihaki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>69:12</xo>
<xt>Ayu 17:6; Omb 3:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Nami maombi yangu nakuomba Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Wakati ukupendezao; Ee Mungu, </q2>
<q1>Kwa wingi wa fadhili zako unijibu, </q1>
<q2>Katika kweli ya wokovu wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>69:13</xo>
<xt>Isa 49:8; 2 Kor 6:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Uniponye kwa kunitoa matopeni, </q1>
<q2>Wala usiniache nikazama. </q2>
<q1>Na niponywe nao wanaonichukia, </q1>
<q2>Na katika vilindi vya maji. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Mkondo usinigharikishe, wala vilindi visinimeze, </q1>
<q2>Wala shimo lisifumbe kinywa chake juu yangu. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unijibu, maana fadhili zako ni njema, </q1>
<q2>Kwa kadiri ya rehema zako unielekee. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Wala usinifiche uso wako, mimi mtumishi wako, </q1>
<q2>Maana mimi nimo taabuni, unijibu upesi. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Uikaribie nafsi yangu, uikomboe, </q1>
<q2>Kwa sababu ya adui zangu unifidie. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Wewe umejua kulaumiwa kwangu, </q1>
<q1>Na kuaibika na kufedheheka kwangu, </q1>
<q2>Mbele zako Wewe wako watesi wangu wote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>69:19</xo>
<xt>Zab 22:6; Isa 53:3; Ebr 12:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Laumu imenivunja moyo, </q1>
<q2>Nami ninaugua sana. </q2>
<q1>Nikangoja aje wa kunihurumia, wala hakuna; </q1>
<q2>Na wa kunifariji, wala sikumwona mtu. </q2>
<b></b>
<q1><vn>21 </vn>Wakanipa uchungu kuwa chakula changu; </q1>
<q2>Nami nilipokuwa na kiu wakaninywesha siki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>69:21</xo>
<xt>Mat 27:34; Mat 27:48; Mk 15:36; Lk 23:36; Yn 19:28-29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>22 </vn>Meza yao mbele yao na iwe mtego; </q1>
<q2>Naam, wakiwa salama na iwe tanzi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>69:22-23</xo>
<xt>Rum 11:9-10; 2 Kor 3:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>23 </vn>Macho yao yatiwe giza wasione, </q1>
<q2>Na viuno vyao uvitetemeshe daima. </q2>
<q1><vn>24 </vn>Uimwage ghadhabu yako juu yao, </q1>
<q2>Na ukali wa hasira yako uwapate. </q2>
<q1><vn>25 </vn>Matuo yao na yawe ukiwa, </q1>
<q2>Pasiwe na mtu wa kukaa hemani mwao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>69:25</xo>
<xt>Mdo 1:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>26 </vn>Maana wanamwudhi mtu uliyempiga Wewe, </q1>
<q2>Wanasimulia maumivu ya hao uliowatia jeraha. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>69:26</xo>
<xt>Isa 53:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>27 </vn>Uwaongezee uovu juu ya uovu, </q1>
<q2>Wala wasiingie katika haki yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>69:27</xo>
<xt>Rum 9:31</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>28 </vn>Na wafutwe katika chuo cha uhai, </q1>
<q2>Wala pamoja na wenye haki wasiandikwe. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>69:28</xo>
<xt>Kut 32:32; Ez 13:9; Lk 10:20; Flp 4:3; Ebr 12:23; Ufu 3:5; 13:8; 17:8</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>29 </vn>Nami niliye maskini na mtu wa huzuni, </q1>
<q2>Mungu, wokovu wako utaniinua. </q2>
<q1><vn>30 </vn>Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo, </q1>
<q2>Nami nitamtukuza kwa shukrani. </q2>
<q1><vn>31 </vn>Nayo yatampendeza 
<nd>Bwana</nd> kuliko ng'ombe, </q1>
<q2>Au ndama mwenye pembe na kwato. </q2>
<q1><vn>32 </vn>Walioonewa watakapoona watafurahi; </q1>
<q2>Enyi mmtafutao Mungu, mioyo yenu ihuishwe. </q2>
<q1><vn>33 </vn>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> huwasikia wahitaji, </q1>
<q2>Wala hawadharau wafungwa wake. </q2>
<q1><vn>34 </vn>Mbingu na nchi zimsifu, </q1>
<q2>Bahari na vyote viendavyo ndani yake. </q2>
<q1><vn>35 </vn>Maana Mungu ataiokoa Sayuni, na kuijenga miji ya Yuda, </q1>
<q2>Na watu watakaa ndani yake na kuimiliki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>69:35</xo>
<xt>Zab 57:18; 102:13, 16; Isa 14:32; 44:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>36 </vn>Wazao wa watumishi wake watairithi, </q1>
<q2>Nao walipendao jina lake watakaa humo. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>70</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu, uniokoe, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unisaidie hima. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Waaibike, wafedheheke, </q1>
<q2>Wanaoitafuta nafsi yangu. </q2>
<q1>Warudishwe nyuma, watahayarishwe, </q1>
<q2>Wapendezwao na shari yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>70:2</xo>
<xt>Zab 109:29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Warudi nyuma, na iwe aibu yao, </q1>
<q2>Wanaosema, Ewe! Ewe! </q2>
<q1><vn>4 </vn>Washangilie, wakufurahie, </q1>
<q2>Wote wakutafutao. </q2>
<q1>Waupendao wokovu wako </q1>
<q2>Waseme daima, Atukuzwe Mungu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>70:4</xo>
<xt>Isa 61:10; Hab 3:17; Rum 5:2; Fil 3:1; 1Pet 1:2-9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Nami ni maskini na mhitaji, </q1>
<q2>Ee Mungu, unijilie kwa haraka. </q2>
<q1>Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, usikawie. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>70:5</xo>
<xt>Zab 40:17; Amu 5:28; Zab 141:1; Ebr 10:37; Ufu 22:20</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>71</cn>
<q1><vn>1 </vn>Nimekukimbilia Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Nisiaibike milele. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kwa haki yako uniponye, uniopoe, </q1>
<q2>Unitegee sikio lako, uniokoe. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Uwe kwangu mwamba wa makazi yangu, </q1>
<q2>Nitakakokwenda sikuzote. </q2>
<q1>Umeamuru niokolewe, </q1>
<q2>Ndiwe genge langu na ngome yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>71:3</xo>
<xt>Zab 44:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Ee Mungu wangu, uniopoe mkononi mwa mkorofi, </q1>
<q2>Katika mkono wake mwovu, mdhalimu, </q2>
<q1><vn>5 </vn>Maana ndiwe taraja langu, Ee Bwana MUNGU, </q1>
<q2>Tumaini langu tokea ujana wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>71:5</xo>
<xt>Yer 17:7; Rum 15:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nimekutegemea Wewe tangu kuzaliwa, </q1>
<q1>Ndiwe uliyenitoa tumboni mwa mama yangu, </q1>
<q2>Ninakusifu Wewe daima. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>71:6</xo>
<xt>Zab 22:9; Isa 46:3; Yer 3:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Nimekuwa kitu cha ajabu kwa watu wengi, </q1>
<q2>Na Wewe ndiwe kimbilio langu la nguvu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>71:7</xo>
<xt>Isa 8:18; Zek 3:8; 1 kor 4:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Kinywa changu kitajazwa sifa zako, </q1>
<q2>Na heshima yako mchana kutwa. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Usinitupe wakati wa uzee, </q1>
<q2>Nguvu zangu zipungukapo usiniache. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Kwa maana adui zangu wananiamba, </q1>
<q2>Nao wanaoniotea roho yangu hushauriana. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>71:10</xo>
<xt>2 Sam 17:1; Mt 27:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Wakisema, Mungu amemwacha, </q1>
<q2>Mfuatieni, mkamateni, hakuna wa kumponya. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Ee Mungu, usiwe mbali nami; </q1>
<q2>Ee Mungu wangu, fanya haraka kunisaidia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>71:12</xo>
<xt>Zab 22:11; 35:22; 70:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Waaibishwe, watoweshwe, adui za nafsi yangu. </q1>
<q2>Wavikwe laumu na aibu wanaonitakia mabaya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>71:13</xo>
<xt>Zab 35:4; 40:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Nami nitatumaini daima, </q1>
<q2>Nitazidi kuongeza sifa zake zote. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Kinywa changu kitasimulia haki na wokovu wako </q1>
<q2>Mchana kutwa; maana sijui hesabu yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>71:15</xo>
<xt>Zab 35:28; 40:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Nitakuja na mambo ya ajabu ya Bwana MUNGU; </q1>
<q2>Nitawakumbusha watu haki yako Wewe peke yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>71:16</xo>
<xt>Zek 10:12; Efe 3:16; Flp 4:13; 2 Tim 2:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Ee Mungu, umenifundisha tokea ujana wangu; </q1>
<q2>Nimekuwa nikitangaza miujiza yako hata leo. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Na hata nikiwa ni mzee mwenye mvi, </q1>
<q2>Ee Mungu, usiniache. </q2>
<q1>Hata niwaeleze watu wa kizazi hiki nguvu zako, </q1>
<q2>Na kila atakayekuja uweza wako. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Na haki yako, Ee Mungu, </q1>
<q2>Imefika juu sana. </q2>
<q1>Wewe uliyefanya mambo makuu; </q1>
<q2>Ee Mungu, ni nani aliye kama Wewe? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>71:19</xo>
<xt>Zab 57:10; Mit 24:7; Isa 5:16; Kut 15:11; Zab 35:10; Isa 40:18, 25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Wewe, uliyetuonyesha mateso mengi, mabaya, </q1>
<q2>Utatuhuisha tena. </q2>
<q1>Utatupandisha juu tena </q1>
<q2>Tokea pande za chini ya nchi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>71:20</xo>
<xt>Zab 60:3; Hos 6:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Laiti ungeniongezea ukuu! </q1>
<q2>Urejee tena na kunifariji moyo. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Nami nitakushukuru kwa kinanda, </q1>
<q2>Na kweli yako, Ee Mungu wangu. </q2>
<q1>Nitakuimbia Wewe kwa kinubi, </q1>
<q2>Ee Mtakatifu wa Israeli. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>71:22</xo>
<xt>2 Fal 19:22: Isa 60:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>23 </vn>Midomo yangu itafurahi sana nikuimbiapo, </q1>
<q2>Na nafsi yangu uliyoikomboa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>71:23</xo>
<xt>Zab 103:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>24 </vn>Ulimi wangu nao utasimulia </q1>
<q2>Haki yako mchana kutwa. </q2>
<q1>Kwa maana wameaibishwa, </q1>
<q2>Wametahayarika, wanaonitakia mabaya. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>72</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu, mpe mfalme hukumu zako, </q1>
<q2>Na mwana wa mfalme haki yako. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Atawaamua watu wako kwa haki, </q1>
<q2>Na watu wako walioonewa kwa hukumu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>72:2</xo>
<xt>Isa 11:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Milima itawazalia watu amani, </q1>
<q2>Na vilima navyo kwa haki. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Atawahukumu walioonewa wa watu, </q1>
<q2>Atawaokoa wahitaji, atamseta mwenye kuonea. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Watakuogopa wakati wote wa kudumu jua, </q1>
<q2>Na wakati wa kung'aa mwezi kizazi hata kizazi. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Atashuka kama mvua juu ya majani yaliyokatwa, </q1>
<q2>Kama manyunyu yainyweshayo nchi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>72:6</xo>
<xt>2 Sam 23:4; hos 6:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Siku zake yeye, mtu mwenye haki atasitawi, </q1>
<q2>Na wingi wa amani hata mwezi utakapokoma. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>72:7</xo>
<xt>Isa 2:4; Dan 2:44; Lk. 1:33</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Na awe na enzi toka bahari hata bahari, </q1>
<q2>Toka Mto hata miisho ya dunia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>72:8</xo>
<xt>Kut 23:31 1 Fal 4:21, 24; Zab 2:8; Zek 9:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Wakaao jangwani na wainame mbele zake; </q1>
<q2>Adui zake na warambe mavumbi. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Wafalme wa Tarshishi na visiwa na walete kodi; </q1>
<q2>Wafalme wa Sheba na Seba na watoe vipawa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>72:10</xo>
<xt>Isa 49:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Naam, wafalme wote na wamsujudie; </q1>
<q2>Na mataifa yote wamtumikie. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Kwa maana atamkomboa mhitaji aliapo, </q1>
<q2>Na mtu aliyeonewa iwapo hana msaidizi. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Atamhurumia aliye dhaifu na maskini, </q1>
<q2>Na nafsi za wahitaji ataziokoa. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Atawakomboa nafsi zao na kuonewa na udhalimu, </q1>
<q2>Na damu yao ina thamani machoni pake. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Basi na aishi; </q1>
<q2>Na wampe dhahabu ya Sheba; </q2>
<q1>Na wamwombee daima; </q1>
<q2>Na kumbariki mchana kutwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>72:15</xo>
<xt>Mt 6:10; 1 kor 1:2, 3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Na uwepo wingi wa nafaka </q1>
<q2>Katika ardhi juu ya milima; </q2>
<q1>Matunda yake na yawaye-waye kama Lebanoni, </q1>
<q2>Na watu wa mjini wasitawi kama majani ya nchi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>72:16</xo>
<xt>1 Fal 4:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Jina lake na lidumu milele, </q1>
<q2>Pindi ling'aapo jua jina lake liwe na wazao; </q2>
<q1>Mataifa yote na wajibariki katika yeye, </q1>
<q2>Na kumwita heri. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>72:17</xo>
<xt>Mwan 12:3; Yer 4:2; Isa 45:23, 24; Lk 1:48; Flp 2:9-11</xt></note></f> </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>18 </vn>Na ahimidiwe 
<nd>Bwana</nd>, Mungu, Mungu wa Israeli, </q1>
<q2>Atendaye miujiza Yeye peke yake; </q2>
<q1><vn>19 </vn>Jina lake tukufu na lihimidiwe milele; </q1>
<q2>Dunia yote na ijae utukufu wake. Amina na Amina. </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>20 </vn>Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamekwisha. </q1>
<d>KITABU CHA TATU </d>
<b></b></c>

<c><cn>73</cn>
<q1><vn>1 </vn>Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, </q1>
<q2>Kwa hao walio safi mioyo yao. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Nami miguu yangu ilikuwa karibu na kupotoka, </q1>
<q2>Hatua zangu zilikuwa karibu na kuteleza. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Maana naliwaonea wivu wenye kujivuna, </q1>
<q2>Nilipoiona hali ya amani ya wasio haki. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Maana hawana maumivu katika kufa kwao, </q1>
<q2>Na mwili wao una nguvu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Katika taabu ya watu hawamo, </q1>
<q2>Wala hawapati mapigo pamoja na wanadamu. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Hivyo kiburi kimekuwa mkufu shingoni mwao, </q1>
<q2>Jeuri huwavika kama nguo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>73:6</xo>
<xt>Mhu 8:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Macho yao hutokeza kwa kunenepa, </q1>
<q2>Wameipita kadiri ya mawazo ya mioyo yao. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Hudhihaki, husimulia mabaya, </q1>
<q2>Husimulia udhalimu kana kwamba wako juu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>73:8</xo>
<xt>2 Pet 2:18; Yud 1:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Wameweka kinywa chao mbinguni, </q1>
<q2>Na ulimi wao hutanga-tanga duniani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>73:9</xo>
<xt>Ufu 13:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Kwa hiyo watu wake hugeuka huko, </q1>
<q2>Na maji yaliyojaa humezwa nao. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Nao husema, Mungu ajuaje? </q1>
<q2>Yako maarifa kwake aliye juu? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>73:11</xo>
<xt>Ayu 22:13; Zab 94:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Fahamu, ndivyo walivyo wasio haki, </q1>
<q2>Na kwa kustarehe sikuzote wamepata mali nyingi. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Hakika nimejisafisha moyo wangu bure, </q1>
<q2>Nimenawa mikono yangu kwa kutokukosa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>73:13</xo>
<xt>Ayu 21:15; Zab 24:4; Mal 3:14; Ebr 10:19-22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Maana mchana kutwa nimepigwa, </q1>
<q2>Na kuadhibiwa kila asubuhi. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Kama ningalisema, Nitasimulia kama hayo; </q1>
<q2>Kumbe! Ningaliwadanganya kizazi cha wana wako. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Nami nalifikiri jinsi ya kufahamu hayo; </q1>
<q2>Ikawa taabu machoni pangu; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>73:16</xo>
<xt>Mhu 8:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Hata nilipoingia katika patakatifu pa Mungu, </q1>
<q2>Nikautafakari mwisho wao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>73:17</xo>
<xt>Zab 77:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>Hakika Wewe huwaweka penye utelezi, </q1>
<q2>Huwaangusha mpaka palipoharibika. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Namna gani wamekuwa ukiwa mara! </q1>
<q2>Wametokomea na kutoweshwa kwa utisho. </q2>
<q1><vn>20 </vn>Ee Bwana, kama ndoto wakati wa kuamka, </q1>
<q2>Uondokapo utaidharau sanamu yao. </q2>
<q1><vn>21 </vn>Moyo wangu ulipoona uchungu, </q1>
<q2>Viuno vyangu viliponichoma, </q2>
<q1><vn>22 </vn>Nalikuwa kama mjinga, sijui neno; </q1>
<q2>Nalikuwa kama mnyama tu mbele zako. </q2>
<q1><vn>23 </vn>Walakini mimi ni pamoja nawe daima, </q1>
<q2>Umenishika mkono wa kuume. </q2>
<q1><vn>24 </vn>Utaniongoza kwa shauri lako, </q1>
<q2>Na baadaye utanikaribisha kwa utukufu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>73:24</xo>
<xt>Isa 58:8; Yn 14:3; 2 Kor 5:1;</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>25 </vn>Ni nani niliye naye mbinguni, </q1>
<q2>Wala duniani sina cha kupendeza ila Wewe. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>73:25</xo>
<xt>Isa 26:8, 9; Hab 3:17, 18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>26 </vn>Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, </q1>
<q2>Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu </q2>
<q2>Na sehemu yangu milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>73:26</xo>
<xt>Zab 84:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>27 </vn>Maana wajitengao nawe watapotea; </q1>
<q2>Umewaangamiza wote waliokuacha Wewe. </q2>
<q1><vn>28 </vn>Nami kumkaribia Mungu ni kwema kwangu; </q1>
<q2>Nimefanya kimbilio kwa Bwana MUNGU, </q2>
<q2>Niyahubiri matendo yako yote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>73:28</xo>
<xt>Ebr 10:22</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>74</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu, mbona umetutupa milele? </q1>
<q2>Kwa nini hasira yako inatoka moshi </q2>
<q2>Juu ya kondoo wa malisho yako? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>74:1</xo>
<xt>Zab 95:7; Yer 23:1; Eze 34:8, 31; Lk 12:32</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ulikumbuke kusanyiko lako, </q1>
<q2>Ulilolinunua zamani. </q2>
<q1>Ulilolikomboa liwe kabila ya urithi wako, </q1>
<q2>Mlima Sayuni ulioufanya maskani yako. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Upainulie miguu yako palipoharibika milele; </q1>
<q2>Adui ameufanya kila ubaya katika patakatifu. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Watesi wako wamenguruma kati ya kusanyiko lako; </q1>
<q2>Wameweka bendera zao ziwe alama. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>74:4</xo>
<xt>Dan 6:27</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Wanaonekana kama watu wainuao mashoka, </q1>
<q2>Waikate miti ya msituni. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Na sasa nakishi yake yote pia </q1>
<q2>Wanaivunja-vunja kwa mashoka na nyundo. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Wamepatia moto patakatifu pako; </q1>
<q2>Wamelinajisi kao la jina lako hata chini. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Walisema mioyoni mwao, </q1>
<q2>Na tuwaangamize kabisa; </q2>
<q1>Mahali penye mikutano ya Mungu </q1>
<q2>Wamepachoma moto katika nchi pia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>74:8</xo>
<xt>Zab 83:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Hatuzioni ishara zetu, wala sasa hakuna nabii, </q1>
<q2>Wala kwetu hakuna ajuaye, hata lini? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>74:9</xo>
<xt>1 Sam 3:1; Mik 3:6; Mt 16:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Ee Mungu, mtesi atalaumu hata lini? </q1>
<q2>Adui alidharau jina lako hata milele? </q2>
<q1><vn>11 </vn>Mbona unaurudisha mkono wako, </q1>
<q2>Naam, mkono wako wa kuume, </q2>
<q1>Uutoe kifuani mwako, </q1>
<q2>Ukawaangamize kabisa. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Lakini Mungu ni mfalme wangu tokea zamani, </q1>
<q2>Afanyaye mambo ya wokovu katikati ya nchi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>74:12</xo>
<xt>Zab 44:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Wewe umeipasua bahari kwa nguvu zako, </q1>
<q2>Umevivunja vichwa vya nyangumi juu ya maji. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>74:13</xo>
<xt>Kut 14:21; Isa 51:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Wewe uliviseta vichwa vya lewiathani, </q1>
<q2>Awe chakula cha watu wa jangwani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>74:14</xo>
<xt>Kut 17:5,6; Hes 14:9; Hes 20:11; Ayu 41:1; Isa 11:16; Isa 27:1; Yos 3:13; Zab 72:9; Zab 104:26; Zab 105:41; Hab 3:9; Ufu 16:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Wewe ulitokeza chemchemi na kijito; </q1>
<q2>Wewe ulikausha mito yenye maji sikuzote. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Mchana ni wako, usiku nao ni wako, </q1>
<q2>Ndiwe uliyeufanya mwanga na jua. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Wewe uliiweka mipaka yote ya dunia, </q1>
<q2>Kaskazi na kusi Wewe ulizitengeneza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>74:17</xo>
<xt>Mdo 17:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uyakumbuke hayo, adui amelaumu, </q1>
<q2>Na watu wapumbavu wamelidharau jina lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>74:18</xo>
<xt>Ufu 16:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Usimpe mnyama mkali nafsi ya hua wako; </q1>
<q2>Usiusahau milele uhai wa watu wako walioonewa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>74:19</xo>
<xt>Wim 2:14; 4:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Ulitafakari agano; </q1>
<q2>Maana mahali penye giza katika nchi </q2>
<q2>Pamejaa makao ya ukatili. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>74:20</xo>
<xt>Mwa 17:7; Law 26:44; Yer 33:21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Aliyeonewa asirejee ametiwa haya, </q1>
<q2>Mnyonge na mhitaji na walisifu jina lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>74:21</xo>
<xt>Zab 9:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>22 </vn>Ee Mungu, usimame, ujitetee mwenyewe, </q1>
<q2>Ukumbuke unavyotukanwa na mpumbavu mchana kutwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>74:22</xo>
<xt>Isa 37:23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>23 </vn>Usiisahau sauti ya watesi wako, </q1>
<q2>Ghasia yao wanaokuondokea inapaa daima. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>75</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu, twakushukuru. </q1>
<q2>Twakushukuru kwa kuwa Jina lako li karibu; </q2>
<q2>Watu huyasimulia matendo yako ya ajabu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Nitakapoufikia wakati ulioamriwa, </q1>
<q2>Mimi nitahukumu hukumu za haki. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Ingawa dunia na wote wakaao humo wataharuki, </q1>
<q2>Mimi mwenyewe nimezisimamisha nguzo zake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>75:3</xo>
<xt>Ebr 1:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Naliwaambia waliojivuna, Msijivune; </q1>
<q2>Na wasio haki, Msiiinue pembe. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Msiiinue pembe yenu juu, </q1>
<q2>Wala msinene kwa shingo ya kiburi. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Maana siko mashariki wala magharibi, </q1>
<q2>Wala nyikani itokako heshima. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Bali Mungu ndiye ahukumuye; </q1>
<q2>Humdhili huyu na kumwinua huyu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>75:7</xo>
<xt>1 Sam 2:7; 2 Sam 5:2; Dan 2:21; Lk 1:52</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Maana mkononi mwa 
<nd>Bwana</nd> mna kikombe, </q1>
<q2>Na mvinyo yake inatoka povu; </q2>
<q2>Kumejaa machanganyiko; </q2>
<q2>Naye huyamimina. </q2>
<q1>Na sira zake wasio haki wa dunia </q1>
<q2>Watazifyonza na kuzinywa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>75:8</xo>
<xt>Ayu 21:20; Yer 25:15; Ufu 14:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Bali mimi nitatangaza matendo yako milele, </q1>
<q2>Nitamwimbia Mungu wa Yakobo. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Pembe zote za wasio haki nitazikata, </q1>
<q2>Na pembe za mwenye haki zitainuka. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>76</cn>
<q1><vn>1 </vn>Katika Yuda Mungu amejulikana, </q1>
<q2>Katika Israeli jina lake ni kuu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kibanda chake pia kiko Salemu, </q1>
<q2>Na maskani yake iko Sayuni. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Huko ndiko alikoivunja mishale ya uta, </q1>
<q2>Ngao, na upanga, na zana za vita. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>76:3</xo>
<xt>Zab 46:9; Eze 39:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Wewe U mwenye fahari na adhama, </q1>
<q2>Toka milima ya mateka. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>76:4</xo>
<xt>Eze 38:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Wametekwa wenye moyo thabiti; </q1>
<q2>Wamelala usingizi; </q2>
<q1>Wala hawakuiona mikono yao </q1>
<q2>Watu wote walio hodari. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>76:5</xo>
<xt>Isa 46:12; Zab 13:3; Yer 51:39</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, </q1>
<q2>Gari na farasi wameshikwa na usingizi mzito. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>76:6</xo>
<xt>Kut 15:1; Nah 2:13; Zek 12:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Wewe ndiwe utishaye, naam, Wewe; </q1>
<q2>Naye ni nani awezaye kusimama ufanyapo hasira? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>76:7</xo>
<xt>ayu 41:10; Nah 1:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Toka mbinguni ulitangaza hukumu; </q1>
<q2>Nchi iliogopa, ikakaa kimya. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Mungu aliposimama ili kuhukumu </q1>
<q2>Na kuwaokoa wapole wa dunia wote pia. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Maana hasira ya binadamu itakusifu, </q1>
<q2>Masalio ya hasira utajifunga kama mshipi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>76:10</xo>
<xt>Kut 9:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Wekeni nadhiri, mkaziondoe </q1>
<q2>Kwa 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wenu. </q2>
<q1>Wote wanaomzunguka wamletee hedaya, </q1>
<q2>Yeye astahiliye kuogopwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>76:11</xo>
<xt>Mhu 5:4; Zab 68:29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Yeye huzikata roho za wakuu; </q1>
<q2>Na kuwatisha wafalme wa dunia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>76:12</xo>
<xt>Zab 68:35</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>77</cn>
<q1><vn>1 </vn>Nimpazie Mungu sauti yangu, </q1>
<q2>Naam, nimpazie Mungu, naye atanisikia. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Siku ya taabu yangu nalimtafuta Bwana; </q1>
<q2>Mkono wangu ulinyoshwa usiku, haukulegea; </q2>
<q2>Nafsi yangu ilikataa kufarijika. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>77:2</xo>
<xt>Zab 50:15; Isa 26:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Nilipotaka kumkumbuka Mungu nalifadhaika; </q1>
<q2>Nilipotaka kutafakari roho yangu ilizimia. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Ulizishika kope za macho yangu zisifumbike; </q1>
<q2>Naliona mashaka nisiweze kunena. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Nalifikiri habari za siku za kale, </q1>
<q2>Miaka ya zamani zilizopita. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>77:5</xo>
<xt>Kum 32:7; Zab 14:5; Isa 51:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nakumbuka wimbo wangu usiku, </q1>
<q2>Nawaza moyoni mwangu, </q2>
<q2>Roho yangu ikatafuta. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Je! Bwana atatupa milele na milele? </q1>
<q2>Hatatenda fadhili tena kabisa? </q2>
<q1><vn>8 </vn>Rehema zake zimekoma hata milele? </q1>
<q2>Ahadi yake imekwisha hata vizazi vyote? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>77:8</xo>
<xt>Isa 27:11; Yon 2:4; Hes 23:19; Yer 15:18; Rum 9:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Mungu amesahau fadhili zake? </q1>
<q2>Amezuia kwa hasira rehema zake? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>77:9</xo>
<xt>Isa 49:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Nikasema, Ndio udhaifu wangu huo; </q1>
<q2>Lakini nitaikumbuka miaka ya mkono wa kuume wake Aliye juu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>77:10</xo>
<xt>Ayu 42:3; Zab 31:22; Yer 10:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Nitayakumbuka matendo ya 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Naam, nitayakumbuka maajabu yako ya kale. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>77:11</xo>
<xt>1 Nya 16:12; Zab 28:5; Isa 5:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Pia nitaitafakari kazi yako yote; </q1>
<q2>Nitaziwaza habari za matendo yako. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Ee Mungu, njia yako i katika utakatifu; </q1>
<q2>Ni nani aliye mungu mkuu kama Mungu? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>77:13</xo>
<xt>Zab 73:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Wewe ndiwe Mungu ufanyaye maajabu; </q1>
<q2>Uliudhihirisha uweza wako kati ya mataifa. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Kwa mkono wako umewakomboa watu wako, </q1>
<q2>Wana wa Yakobo na Yusufu. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Ee Mungu, yale maji yalikuona, </q1>
<q2>Yale maji yalikuona, yakaogopa. </q2>
<q2>Vilindi vya maji navyo vikatetemeka, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>77:16</xo>
<xt>Kut 14:21; Yos 3:15, 16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Mawingu yakamwaga maji. </q1>
<q2>Mbingu nazo zikatoa sauti, </q2>
<q2>Mishale yako nayo ikatapakaa. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Sauti ya radi yako ikawa katika kisulisuli; </q1>
<q2>Umeme uliuangaza ulimwengu. </q2>
<q2>Nchi ilitetemeka na kutikisika; </q2>
<q1><vn>19 </vn>Njia yako ilikuwa katika bahari. </q1>
<q2>Na mapito yako yalikuwa katika maji makuu; </q2>
<q2>Hatua zako hazikujulikana. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>77:19</xo>
<xt>Hab 3:15; Kut 14:28; Ayu 37:23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Uliwaongoza watu wako kama kundi, </q1>
<q2>Kwa mkono wa Musa na Haruni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>77:20</xo>
<xt>Isa 63:11</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>78</cn>
<q1><vn>1 </vn>Enyi watu wangu, sikilizeni sheria yangu, </q1>
<q2>Tegeni masikio kwa maneno ya kinywa changu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:1</xo>
<xt>Kut 19:5; Kum 32:29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Na nifunue kinywa changu kwa mithali, </q1>
<q2>Niyatamke mafumbo ya kale. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:2</xo>
<xt>Zab 49:4; Mat 13:35</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Mambo tuliyoyasikia na kuyafahamu, </q1>
<q2>Ambayo baba zetu walituambia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:3</xo>
<xt>Zab 44:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Hayo hatutawaficha wana wao, </q1>
<q2>Huku tukiwaambia kizazi kingine, </q2>
<q1>Sifa za 
<nd>Bwana</nd>, na nguvu zake, </q1>
<q2>Na mambo yake ya ajabu aliyoyafanya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:4</xo>
<xt>Kum 4:9; Kut 12:26; Yosh 4:6,7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Maana alikaza ushuhuda katika Yakobo, </q1>
<q2>Na sheria aliiweka katika Israeli. </q2>
<q1>Aliyowaamuru baba zetu </q1>
<q2>Wawajulishe wana wao, </q2>
<q1><vn>6 </vn>Ili kizazi kingine wawe na habari, </q1>
<q2>Ndio hao wana watakaozaliwa. </q2>
<q2>Wasimame na kuwaambia wana wao <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:6</xo>
<xt>Zab 102:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Wamwekee Mungu tumaini lao. </q1>
<q2>Wala wasiyasahau matendo ya Mungu, </q2>
<q2>Bali wazishike amri zake. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Naam, wasiwe kama baba zao, </q1>
<q2>Kizazi cha ukaidi na uasi. </q2>
<q1>Kizazi kisichojitengeneza moyo, </q1>
<q2>Wala roho yake haikuwa amini kwa Mungu. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Wale Waefraimu, wenye silaha, wapiga upinde, </q1>
<q2>Walirudi nyuma siku ya vita. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Hawakulishika agano la Mungu; </q1>
<q2>Wakakataa kuenenda katika sheria yake; </q2>
<q1><vn>11 </vn>Wakayasahau matendo yake, </q1>
<q2>Na mambo yake ya ajabu aliyowaonyesha. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:11</xo>
<xt>Isa 17:10; Yer 2:32</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Mbele ya baba zao alifanya mambo ya ajabu, </q1>
<q2>Katika nchi ya Misri, konde la Soani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:12</xo>
<xt>Mwa 32:3; Kut 7:8--12:32; Isa 19:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Aliipasua bahari akawavusha; </q1>
<q2>Aliyasimamisha maji mfano wa chungu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:13</xo>
<xt>Kut 14:21-22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Akawaongoza kwa wingu mchana, </q1>
<q2>Na usiku kucha kwa nuru ya moto. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:14</xo>
<xt>Kut 13:21-22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Akapasua miamba jangwani; </q1>
<q2>Akawanywesha maji mengi kama maji ya vilindi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:15-16</xo>
<xt>Kut 17:1-7; Hes 20:2-13; Zab 105:41; isa 41:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Akatokeza na vijito gengeni, </q1>
<q2>Akatelemsha maji kama mito. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:16</xo>
<xt>Kumb 9:21</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>17 </vn>Lakini wakazidi kumtenda dhambi, </q1>
<q2>Walipomwasi Aliye juu katika nchi ya kiu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:17</xo>
<xt>Ebr 3:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>Wakamjaribu Mungu mioyoni mwao </q1>
<q2>Kwa kutaka chakula kwa tamaa zao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:18-31</xo>
<xt>Kut 16:2-15; Hes 11:4-23,31-35</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Naam, walimwamba Mungu, wakasema, </q1>
<q2>Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:19</xo>
<xt>Hes 11:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Tazama, aliupiga mwamba; </q1>
<q2>Maji yakabubujika, ikafurika mito. </q2>
<q1>Pia aweza kutupa chakula? </q1>
<q2>Atawaandalia watu wake nyama? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:20</xo>
<xt>Kut 17:6; Hes 20:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Hivyo 
<nd>Bwana</nd> aliposikia akaghadhibika; </q1>
<q2>Moto ukawashwa juu ya Yakobo, </q2>
<q2>Hasira nayo ikapanda juu ya Israeli. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Kwa kuwa hawakumwamini Mungu, </q1>
<q2>Wala hawakuutumainia wokovu wake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:22</xo>
<xt>Ebr 3:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>23 </vn>Lakini aliyaamuru mawingu juu; </q1>
<q2>Akaifungua milango ya mbinguni; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:23</xo>
<xt>Mwa 7:11; Kum 28:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>24 </vn>Akawanyeshea mana ili wale; </q1>
<q2>Akawapa nafaka ya mbinguni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:24</xo>
<xt>Neh 9:15, 20; Yn 6:31; 1 Kor 10:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>25 </vn>Mwanadamu akala chakula cha mashujaa; </q1>
<q2>Aliwapelekea chakula cha kuwashibisha. </q2>
<q1><vn>26 </vn>Aliuelekeza upepo wa mashariki mbinguni; </q1>
<q2>Akaiongoza kusi kwa uweza wake. </q2>
<q1><vn>27 </vn>Akawanyeshea nyama kama mavumbi, </q1>
<q2>Na ndege wenye mbawa, </q2>
<q2>Kama mchanga wa bahari. </q2>
<q1><vn>28 </vn>Akawaangusha kati ya matuo yao, </q1>
<q2>Pande zote za maskani zao. </q2>
<q1><vn>29 </vn>Wakala wakashiba sana; </q1>
<q2>Maana aliwaletea walivyovitamani; </q2>
<q1><vn>30 </vn>Hawakuachana na matakwa yao. </q1>
<q2>Ila chakula chao kikali ki vinywani mwao </q2>
<q1><vn>31 </vn>Hasira ya Mungu ikapanda juu yao, </q1>
<q2>Akawaua waliokuwa wanono; </q2>
<q2>Akawaangusha chini vijana wa Israeli. </q2>
<q1><vn>32 </vn>Pamoja na hayo wakazidi kutenda dhambi, </q1>
<q2>Wala hawakuyaamini matendo yake ya ajabu. </q2>
<q1><vn>33 </vn>Kwa hiyo akazikomesha siku zao kama pumzi, </q1>
<q2>Na miaka yao kwa hofu ya kuwasitusha. </q2>
<q1><vn>34 </vn>Alipowaua ndipo walipokuwa wakimtafuta; </q1>
<q2>Wakarudi wakamtaka Mungu kwa bidii. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:34</xo>
<xt>Hes 5:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>35 </vn>Wakakumbuka kuwa Mungu ni mwamba wao, </q1>
<q2>Na Mungu Aliye juu ni mkombozi wao. </q2>
<q1><vn>36 </vn>Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, </q1>
<q2>Wakamwambia uongo kwa ndimi zao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:36</xo>
<xt>Eze 33:31</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>37 </vn>Kwa maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, </q1>
<q2>Wala hawakuwa waaminifu katika agano lake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:37</xo>
<xt>Ac 8:21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>38 </vn>Lakini Yeye, kwa kuwa anayo rehema, </q1>
<q2>Husamehe uovu wala haangamizi. </q2>
<q1>Mara nyingi huipishia mbali ghadhabu yake, </q1>
<q2>Wala haiwashi hasira yake yote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:38</xo>
<xt>Kut 34:6; Neh 9:17; Zab 86:15; 1 Fal 21:29; Isa 489; Mik 7:18; Rum 2:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>39 </vn>Akakumbuka ya kuwa wao ni kiwiliwili, </q1>
<q2>Upepo upitao wala haurudi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:39</xo>
<xt>Mwa 6:3; Yn 3:6; Yak 4:14; Ayu 7:7, 16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>40 </vn>Walimwasi jangwani mara ngapi? </q1>
<q2>Na kumhuzunisha nyikani! </q2>
<q1><vn>41 </vn>Wakarudi nyuma wakamjaribu Mungu; </q1>
<q2>Wakampa mpaka Mtakatifu wa Israeli. </q2>
<q1><vn>42 </vn>Hawakuukumbuka mkono wake, </q1>
<q2>Wala siku ile alipowakomboa na mtesi. </q2>
<q1><vn>43 </vn>Alivyoziweka ishara zake katika Misri, </q1>
<q2>Na miujiza yake katika konde la Soani. </q2>
<q1><vn>44 </vn>Aligeuza damu mito yao, </q1>
<q2>Na vijito wasipate kunywa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:44</xo>
<xt>Kut 7:17-21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>45 </vn>Aliwapelekea mainzi wakawala, </q1>
<q2>Na vyura wakawaharibu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:45</xo>
<xt>Kut 8:1-6, 20-24</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>46 </vn>Akawapa tunutu mazao yao, </q1>
<q2>Na nzige kazi yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:46</xo>
<xt>Kut 10:12-15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>47 </vn>Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe, </q1>
<q2>Na mikuyu yao kwa mawe ya barafu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:47-48</xo>
<xt>Kut 9:22-25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>48 </vn>Akaacha ng'ombe zao wapigwe kwa mvua ya mawe, </q1>
<q2>Na makundi yao kwa umeme. </q2>
<q1><vn>49 </vn>Akawapelekea ukali wa hasira yake, </q1>
<q2>Ghadhabu, na uchungu, na taabu, </q2>
<q2>Kundi la malaika waletao mabaya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:49</xo>
<xt>Rum 2:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>50 </vn>Akiifanyizia njia hasira yake; </q1>
<q2>Wala hakuziepusha roho zao na mauti, </q2>
<q2>Bali aliiachia tauni uhai wao; </q2>
<q1><vn>51 </vn>Akampiga kila mzaliwa wa kwanza wa Misri, </q1>
<q2>Malimbuko ya nguvu katika hema za Hamu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:51</xo>
<xt>Mwa 9:22; Kut 12:29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>52 </vn>Bali aliwaongoza watu wake kama kondoo, </q1>
<q2>Akawachunga kama kundi jangwani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:52</xo>
<xt>Kut 13:17-22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>53 </vn>Hao akawachukua salama wala hawakuogopa, </q1>
<q2>Bali bahari iliwafunikiza adui zao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:53</xo>
<xt>Kut 14:26-28</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>54 </vn>Akawapeleka hadi mpaka wake mtakatifu, </q1>
<q2>Mlima alioununua kwa mkono wake wa kuume. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:54</xo>
<xt>Kut 15:17; Yos 3:14-17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>55 </vn>Akawafukuza mataifa mbele yao, </q1>
<q2>Akawapimia urithi kwa kamba, </q2>
<q2>Na kuwakalisha kabila za Israeli katika hema zao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:55</xo>
<xt>Yos 11:16-23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>56 </vn>Lakini walimjaribu Mungu Aliye juu, wakamwasi, </q1>
<q2>Wala hawakuzishika shuhuda zake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:56</xo>
<xt>Amu 2:11-15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>57 </vn>Bali walirudi nyuma, wakahaini kama baba zao; </q1>
<q2>Wakaepea kama upinde usiofaa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:57</xo>
<xt>Eze 20:27; Hos 7:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>58 </vn>Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu, </q1>
<q2>Wakamtia wivu kwa sanamu zao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:58</xo>
<xt>Law 26:30; Hes 33:52; Kum 12:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>59 </vn>Mungu akasikia, akaghadhibika, </q1>
<q2>Akamkataa Israeli kabisa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:59</xo>
<xt>Ebr 4:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>60 </vn>Akaiacha maskani ya Shilo, </q1>
<q2>Hema aliyoiweka katikati ya wanadamu; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:60</xo>
<xt>1 Sam 4:11; Yer 7:12; Yos 18:1; Yer 7:12-14; 26:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>61 </vn>Akaziacha nguvu zake kutekwa, </q1>
<q2>Na fahari yake mkononi mwa mtesi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:61</xo>
<xt>1 Sam 4:4-22; Amu 4:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>62 </vn>Akawatoa watu wake wapigwe kwa upanga; </q1>
<q2>Akaughadhibikia urithi wake. </q2>
<q1><vn>63 </vn>Moto ukawala vijana wao, </q1>
<q2>Wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi, </q2>
<q1><vn>64 </vn>Makuhani wao walianguka kwa upanga, </q1>
<q2>Wala wajane wao hawakuomboleza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:64</xo>
<xt>Ayu 27:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>65 </vn>Ndipo Bwana alipoamka kama aliyelala usingizi, </q1>
<q2>Kama shujaa apigaye kelele sababu ya mvinyo; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:65</xo>
<xt>Isa 42:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>66 </vn>Akawapiga watesi wake akawarudisha nyuma, </q1>
<q2>Akawatia aibu ya milele. </q2>
<q1><vn>67 </vn>Ila akaikataa hema ya Yusufu; </q1>
<q2>Wala hakuichagua kabila ya Efraimu. </q2>
<q1><vn>68 </vn>Bali aliichagua kabila ya Yuda, </q1>
<q2>Mlima Sayuni alioupenda. </q2>
<q1><vn>69 </vn>Akajenga patakatifu pake kama vilele, </q1>
<q2>Kama dunia aliyoiweka imara milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:69</xo>
<xt>1 Fal 6:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>70 </vn>Akamchagua Daudi, mtumishi wake, </q1>
<q2>Akamwondoa katika mazizi ya kondoo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:70-71</xo>
<xt>1 Sam 16:11-12; 2 Sam 7:8; 1 Nya 17:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>71 </vn>Nyuma ya kondoo wanyonyeshao alimwondoa, </q1>
<q2>Awachunge Yakobo watu wake, na Israeli urithi wake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:71</xo>
<xt>2 Sam 5:2; 1 Nya 11:2; Mik 5:2-4; Zek 11:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>72 </vn>Akawalisha kwa ukamilifu wa moyo wake, </q1>
<q2>Na kuwaongoza kwa busara ya mikono yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>78:72</xo>
<xt>1 Fal 9:4</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>79</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu, mataifa wameingia katika urithi wako, </q1>
<q2>Wamelinajisi hekalu lako takatifu. </q2>
<q2>Wamefanya Yerusalemu chungu chungu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>79:1</xo>
<xt>2 Fal 25:8-10; 2 Nya 36:17-19; Yer 26:18; Yer 52:12-14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Wameziacha maiti za watumishi wako </q1>
<q2>Ziwe chakula cha ndege wa angani. </q2>
<q1>Na miili ya watauwa wako </q1>
<q2>Iwe chakula cha wanyama wa nchi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>79:2</xo>
<xt>Yer 7:33</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Wamemwaga damu yao kama maji </q1>
<q2>Pande zote za Yerusalemu, </q2>
<q2>Wala hapakuwa na mzishi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>79:3</xo>
<xt>Ufu 11:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Tumekuwa lawama kwa jirani zetu, </q1>
<q2>Mzaha na dhihaka kwao wanaotuzunguka. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, hata lini? Utaona hasira milele? </q1>
<q2>Wivu wako utawaka kama moto? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>79:5</xo>
<xt>Kum 29:20; Eze 36:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Ukali wako uwamwagie mataifa wasiokujua, </q1>
<q2>Na falme za hao wasioliitia jina lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>79:6</xo>
<xt>Isa 45:4; Zab 53:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Kwa maana wamemla Yakobo, </q1>
<q2>Na matuo yake wameyaharibu. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Usikumbuke juu yetu maovu ya baba zetu, </q1>
<q2>Rehema zako zije kutulaki hima, </q2>
<q2>Kwa maana tumedhilika sana. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>79:8</xo>
<xt>Isa 43:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Ee Mungu wa wokovu wetu, utusaidie, </q1>
<q2>Kwa ajili ya utukufu wa jina lako. </q2>
<q1>Utuokoe, utughofiri dhambi zetu, </q1>
<q2>Kwa ajili ya jina lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>79:9</xo>
<xt>Yos 7:0; Yer 14:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Kwa nini mataifa kusema, </q1>
<q2>Yuko wapi Mungu wao? </q2>
<q1>Kisasi cha damu ya watumishi wako iliyomwagika </q1>
<q2>Kijulike kati ya mataifa machoni petu. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Kuugua kwake aliyefungwa </q1>
<q2>Na kuingie mbele zako. </q2>
<q1>Kwa kadiri ya uweza wa mkono wako </q1>
<q2>Uwahifadhi wana wa mauti. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>79:11</xo>
<xt>Hes 14:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Uwalipe jirani zetu mara saba vifuani mwao </q1>
<q2>Laumu zao walizokulaumu, Ee Bwana. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Na sisi tulio watu wako, </q1>
<q2>Na kondoo za malisho yako, </q2>
<q1>Tutakushukuru milele; </q1>
<q2>Tutazisimulia sifa zako kizazi kwa kizazi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>79:13</xo>
<xt>Isa 43:21</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>80</cn>
<q1><vn>1 </vn>Wewe uchungaye Israeli, usikie, </q1>
<q2>Wewe umwongozaye Yusufu kama kundi; </q2>
<q2>Wewe uketiye juu ya makerubi, utoe nuru. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>80:1</xo>
<xt>Kut 25:22; Kum 33:2; Sam 4:4; Zab 89:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Mbele ya Efraimu, na Benyamini, na Manase, </q1>
<q2>Uziamshe nguvu zako, </q2>
<q2>Uje, utuokoe. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Ee Mungu, uturudishe, </q1>
<q2>Uangazishe uso wako nasi tutaokoka. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>80:3</xo>
<xt>1 Fal 18:37</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>4 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wa majeshi, hata lini </q1>
<q2>Utayaghadhibikia maombi ya watu wako? </q2>
<q1><vn>5 </vn>Umewalisha mkate wa machozi, </q1>
<q2>Umewanywesha machozi kwa kipimo kikuu. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Unatufanya sababu ya ugomvi kwa jirani zetu, </q1>
<q2>Na adui zetu wanacheka wao kwa wao. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ee Mungu wa majeshi, uturudishe, </q1>
<q2>Uangazishe uso wako nasi tutaokoka. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ulileta mzabibu kutoka Misri, </q1>
<q2>Ukawafukuza mataifa ukaupanda. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>80:8</xo>
<xt>Isa 5:1, 7; Yer 2:21; Eze 15:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Ulitengeneza nafasi mbele yake, </q1>
<q2>Nao ukatia mizizi sana ukaijaza nchi. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Milima ilifunikwa kwa uvuli wake, </q1>
<q2>Matawi yake ni kama mierezi ya Mungu. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Nao uliyaeneza matawi yake hata baharini, </q1>
<q2>Na vichipukizi vyake hata kunako Mto. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>80:11</xo>
<xt>Kut 23:31; Zab 72:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Kwa nini umezibomoa kuta zake, </q1>
<q2>Wakauchuma wote wapitao njiani? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>80:12</xo>
<xt>Isa 5:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Nguruwe wa msituni wanauharibu, </q1>
<q2>Na hayawani wa kondeni wanautafuna. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Ee Mungu wa majeshi, tunakusihi, urudi, </q1>
<q2>Utazame toka juu uone, uujilie mzabibu huu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>80:14</xo>
<xt>Zek 1:12, 16, 17; Isa 63:15</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>15 </vn>Na mche ule ulioupanda </q1>
<q2>Kwa mkono wako wa kuume; </q2>
<q1>Na tawi lile ulilolifanya </q1>
<q2>Kuwa imara kwa nafsi yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>80:15</xo>
<xt>Isa 49:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Umechomwa moto; umekatwa; </q1>
<q2>Kwa lawama ya uso wako wanapotea. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Mkono wako na uwe juu yake </q1>
<q2>Mtu wa mkono wako wa kuume; </q2>
<q1>Juu ya mwanadamu uliyemfanya </q1>
<q2>Kuwa imara kwa nafsi yako; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>80:17</xo>
<xt>Zab 89:21; Kut 4:22; Zab 110:1; Dan 7:13, 14; Yn 5:21-27</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>Basi hatutakuacha kwa kurudi nyuma; </q1>
<q2>Utuhuishe nasi tutaliitia jina lako. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wa majeshi, uturudishe, </q1>
<q2>Uangazishe uso wako nasi tutaokoka. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>80:19</xo>
<xt>Hes 6:25; Zab 27:4,9</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>81</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha, </q1>
<q2>Mshangilieni Mungu wa Yakobo. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Pazeni zaburi, pigeni matari, </q1>
<q2>Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Pigeni panda mwandamo wa mwezi, </q1>
<q2>Wakati wa mbalamwezi, sikukuu yetu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>81:3</xo>
<xt>Hes 10:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Kwa maana ni sheria kwa Israeli, </q1>
<q2>Ni hukumu ya Mungu wa Yakobo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>81:4</xo>
<xt>Law 23:24; Hes 10:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Aliamuru iwe ushuhuda katika Yusufu, </q1>
<q2>Alipoondoka juu ya nchi ya Misri; </q2>
<q1>Maneno yake nisiyemjua naliyasikia. </q1>
<q1><vn>6 </vn>Nimelitenga bega lake na mzigo, </q1>
<q2>Mikono yake ikaachana na kikapu. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Katika shida uliniita nikakuokoa; </q1>
<q2>Nalikuitikia katika sitara ya radi; </q2>
<q2>Nalikujaribu penye maji ya Meriba. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>81:7</xo>
<xt>Kut 17:7; Hes 20:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya, </q1>
<q2>Ee Israeli, kama ukitaka kunisikiliza; </q2>
<q1><vn>9 </vn>Usiwe na mungu mgeni ndani yako; </q1>
<q2>Wala usimsujudie mungu mwingine. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>81:9</xo>
<xt>Kut 20:2-3; Kum 5:6-7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Mimi ndimi 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wako, </q1>
<q2>Niliyekupandisha toka nchi ya Misri; </q2>
<q2>Fumbua sana kinywa chako nami nitakijaza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>81:10</xo>
<xt>Zab 37:3; Yn 15:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu, </q1>
<q2>Wala Israeli hawakunitaka. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao, </q1>
<q2>Waenende katika mashauri yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>81:12</xo>
<xt>Mdo 7:42; Rum 1:24</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Laiti watu wangu wangenisikiliza, </q1>
<q2>Na Israeli angeenenda katika njia zangu; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>81:13</xo>
<xt>Kum 5:29; Isa 48:18; yer 44:4,5; Mt 23:37</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Ningewadhili adui zao kwa upesi, </q1>
<q2>Na juu ya watesi wao ningegeuza mkono wangu; </q2>
<q1><vn>15 </vn>Wamchukiao 
<nd>Bwana</nd> wangenyenyekea mbele zake, </q1>
<q2>Bali wakati wao ungedumu milele. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Naam, ningewalisha kwa unono wa ngano, </q1>
<q2>Ningewashibisha kwa asali itokayo mwambani. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>82</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mungu asimama katika kusanyiko la Mungu; </q1>
<q2>Katikati ya miungu anahukumu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>82:1</xo>
<xt>Mhu 5:8; Kut 21:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Hata lini mtahukumu kwa dhuluma, </q1>
<q2>Na kuzikubali nyuso za wabaya? </q2>
<q1><vn>3 </vn>Mfanyieni hukumu maskini na yatima; </q1>
<q2>Mtendeeni haki aliyeonewa na fukara; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>82;2</xo>
<xt>Kum 1:17; Zab 58:1,2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Mwokoeni maskini na mhitaji; </q1>
<q2>Mwopoeni mikononi mwa wadhalimu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Hawajui wala hawafahamu, hutembea gizani; </q1>
<q2>Misingi yote ya nchi imetikisika. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>82:1</xo>
<xt>Zab 11:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Mimi nimesema, Ndinyi miungu, </q1>
<q2>Na wana wa Aliye juu, nyote pia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>82:6</xo>
<xt>Ayu 21:32; Eze 31:14; Yn 10:34</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Lakini mtakufa kama wanadamu, </q1>
<q2>Mtaanguka kama mmoja wa wakuu. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ee Mungu, usimame, uihukumu nchi, </q1>
<q2>Maana Wewe utawarithi mataifa yote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>82:8</xo>
<xt>Zab 2:8; Ufu 11:15</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>83</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu, usistarehe, </q1>
<q2>Ee Mungu, usinyamae, wala usitulie. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Maana adui zako wanafanya ghasia, </q1>
<q2>Nao wakuchukiao wameviinua vichwa vyao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>83:2</xo>
<xt>Zab 2:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Juu ya watu wako wanafanya hila, </q1>
<q2>Na kushauriana juu yao uliowaficha. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>83:3</xo>
<xt>Zab 27:5; Kol 3:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Wamesema, Njoni, tuwakatilie mbali wasiwe taifa, </q1>
<q2>Na jina la Israeli halitakumbukwa tena. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>83:4</xo>
<xt>2 Sam 10:6; 2 Nya 20:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Maana wanashauriana kwa moyo mmoja, </q1>
<q2>Juu yako wanafanyana agano. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Hema za Edomu, na Waishmaeli, </q1>
<q2>Na Moabu, na Wahagari, </q2>
<q1><vn>7 </vn>Gebali, na Amoni, na Amaleki, </q1>
<q2>Na Filisti, nao wanaokaa Tiro, </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ashuri naye amepatana nao, </q1>
<q2>Wamewasaidia wana wa Lutu. </q2>
<b></b>
<q1><vn>9 </vn>Uwatende kama Midiani, kama Sisera, </q1>
<q2>Kama Yabini, penye kijito Kishoni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>83:9</xo>
<xt>Hes 31:7, 8; Isa 9:4; Amu 4:6-22; 7:1-23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Ambao waliangamizwa Endori; </q1>
<q2>Wakawa samadi juu ya nchi. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Uwafanye wakuu wao kama Orebu na Zeebu, </q1>
<q2>Na masheki yao wote kama Zeba na Zalmuna. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>83:11</xo>
<xt>Amu 7:25; 8:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Ambao Walisema, </q1>
<q2>Na tutamalaki makao ya Mungu. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Ee Mungu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, </q1>
<q2>Mithili ya makapi mbele ya upepo, </q2>
<q1><vn>14 </vn>Kama moto uteketezao msitu, </q1>
<q2>Kama miali ya moto iiwashayo milima, </q2>
<q1><vn>15 </vn>Ndivyo utakavyowafuatia kwa tufani yako, </q1>
<q2>Na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Uwajaze nyuso zao fedheha; </q1>
<q2>Wakalitafute jina lako, 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Waaibike, wafadhaike milele, </q1>
<q2>Naam, watahayarike na kupotea. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, </q1>
<q2>Ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>84</cn>
<q1><vn>1 </vn>Maskani zako zapendeza kama nini, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd> wa majeshi! <f> <fn>-</fn><note>
<xo>84:1</xo>
<xt>Zab 26:8; 27:4; Ebr 9:23,24; Ufu 21:2,2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Nafsi yangu imezionea shauku nyua za 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Naam, na kuzikondea. </q2>
<q1>Moyo wangu na mwili wangu </q1>
<q2>Vinamlilia Mungu aliye hai. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Shomoro naye ameona nyumba, </q1>
<q1>Na mbayuwayu amejipatia kioto, </q1>
<q2>Alipoweka makinda yake, </q2>
<q1>Kwenye madhabahu zako, Ee 
<nd>Bwana</nd> wa majeshi, </q1>
<q2>Mfalme wangu na Mungu wangu. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Heri wakaao nyumbani mwako, </q1>
<q2>Wanakuhimidi daima. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Heri ambaye nguvu zake zatoka kwako, </q1>
<q2>Na njia ziendazo Sayuni zimo moyoni mwake. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Wakipita kati ya bonde la Vilio, </q1>
<q1>Hulifanya kuwa chemchemi, </q1>
<q2>Naam, mvua ya vuli hulivika baraka </q2>
<q1><vn>7 </vn>Huendelea toka nguvu hata nguvu, </q1>
<q2>Huonekana Sayuni kila mmoja mbele za Mungu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>84:7</xo>
<xt>Kum 16:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>
<nd>Bwana</nd>, Mungu wa majeshi, uyasikie maombi yangu, </q1>
<q2>Ee Mungu wa Yakobo, usikilize, </q2>
<q1><vn>9 </vn>Ee Mungu, ngao yetu, uangalie, </q1>
<q2>Umtazame uso masihi<f> <fn>f</fn><note>
<fr>84:9</fr>
<ft> Au, mtiwa mafuta.</ft></note></f> wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>84:9</xo>
<xt>Mwa 15:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Hakika siku moja katika nyua zako </q1>
<q2>Ni bora kuliko siku elfu. </q2>
<q1>Ningependa kuwa bawabu nyumbani mwa Mungu wangu, </q1>
<q2>Kuliko kukaa katika hema za uovu. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd>, Mungu, ni jua na ngao, </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> atatoa neema na utukufu. </q2>
<q1>Hatawanyima kitu chema </q1>
<q2>Hao waendao kwa ukamilifu. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd> wa majeshi, </q1>
<q2>Heri mwanadamu anayekutumaini Wewe. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>85</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd>, umeiridhia nchi yako, </q1>
<q2>Umewarejeza mateka wa Yakobo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>85:1</xo>
<xt>Yer 30:18; Eze 39:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Umeusamehe uovu wa watu wako, </q1>
<q2>Umezisitiri hatia zao zote. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Umeiondoa ghadhabu yako yote, </q1>
<q2>Umerudi na kuuacha ukali wa hasira yako. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Mungu wa wokovu wetu, uturudishe, </q1>
<q2>Uikomeshe hasira uliyo nayo juu yetu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Je! Utatufanyia hasira hata milele? </q1>
<q2>Utadumisha ghadhabu kizazi hata kizazi? </q2>
<q1><vn>6 </vn>Je! Hutaki kurudi na kutuhuisha, </q1>
<q2>Watu wako wakufurahie? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>85:6</xo>
<xt>Hab 3:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, utuonyeshe rehema zako, </q1>
<q2>Utupe wokovu wako. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Na nisikie atakavyosema Mungu 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Maana atawaambia watu wake amani, </q2>
<q1>Naam, na watauwa wake pia, </q1>
<q2>Bali wasiurudie upumbavu tena. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>85:8</xo>
<xt>Hab 2;1; Zek 9:10; 2 Pet 2:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Hakika wokovu wake u karibu na wamchao, </q1>
<q2>Utukufu ukae katika nchi yetu. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Fadhili na kweli zimekutana, </q1>
<q2>Haki na amani zimehusiana. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>85:10</xo>
<xt>Mik 7:20; Yn 1:17; Zab 72:2, 3: Isa 32;17; Lk 2:14; Yh 14:27;</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Kweli imechipuka katika nchi, </q1>
<q2>Haki imechungulia kutoka mbinguni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>85:11</xo>
<xt>Isa 45:8; 2 Kor 5:14-21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Naam, 
<nd>Bwana</nd> atatoa kilicho chema, </q1>
<q2>Na nchi yetu itatoa mazao yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>85:12</xo>
<xt>Yak 1:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Haki itakwenda mbele zake, </q1>
<q2>Nayo itazifanya hatua zake kuwa njia. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>86</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, utege sikio lako unijibu, </q1>
<q2>Maana mimi ni maskini na mhitaji </q2>
<q1><vn>2 </vn>Unihifadhi nafsi yangu, </q1>
<q2>Maana mimi ni mcha Mungu. </q2>
<q1>Wewe uliye Mungu wangu, </q1>
<q2>Umwokoe mtumishi wako anayekutumaini. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Wewe, Bwana, unifadhili, </q1>
<q2>Maana nakulilia Wewe mchana kutwa. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Uifurahishe nafsi ya mtumishi wako, </q1>
<q2>Maana nafsi yangu nakuinulia Wewe, Bwana. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Kwa maana Wewe, Bwana, U mwema, </q1>
<q2>Umekuwa tayari kusamehe, </q2>
<q1>Na mwingi wa fadhili, </q1>
<q2>Kwa watu wote wakuitao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>86:5</xo>
<xt>Zab 130:7-8; Yoe 2:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uyasikie maombi yangu; </q1>
<q2>Uisikilize sauti ya dua zangu. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Siku ya mateso yangu nitakuita, </q1>
<q2>Kwa maana utaniitikia. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Katikati ya miungu hakuna kama Wewe, Bwana, </q1>
<q2>Wala matendo mfano wa matendo yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>86:8</xo>
<xt>Kut 15:11; Kum 3:24; 1 Sam 2:2; 2 Sam 7:22; 1 Fal 8:23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Mataifa yote uliowafanya watakuja; </q1>
<q2>Watakusujudia Wewe, Bwana, </q2>
<q1>Watalitukuza jina lako; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>86:9</xo>
<xt>Zab 95:6-7; Isa 43:7; Ufu 15:4</xt></note></f> </q1>
<q1><vn>10 </vn>Kwa kuwa ndiwe uliye mkuu, </q1>
<q1>Wewe ndiwe mfanya miujiza, </q1>
<q2>Ndiwe Mungu peke yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>86:10</xo>
<xt>Kum 6:4; Isa 37:16; Mk 12:29; 1 Kor 8:4; Efe 4:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unifundishe njia yako; </q1>
<q2>Nitakwenda katika kweli yako; </q2>
<q1>Moyo wangu na ufurahi kulicha jina lako; </q1>
<q2><vn>12 </vn>Nitakusifu Wewe, Bwana, Mungu wangu, </q2>
<q1>Kwa moyo wangu wote, </q1>
<q2>Nitalitukuza jina lako milele. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Maana fadhili zako kwangu ni nyingi sana; </q1>
<q2>Umeiopoa nafsi yangu na kuzimu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>86:13</xo>
<xt>Zab 56:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Ee Mungu, wenye kiburi wamenishambulia; </q1>
<q2>Mkutano wa wakatili wamenitafuta roho. </q2>
<q1>Wala hawakukuweka Wewe </q1>
<q2>Mbele ya macho yao. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Lakini Wewe, Bwana, </q1>
<q2>U Mungu wa rehema na neema, </q2>
<q1>Mvumilivu, mwingi wa fadhili na kweli. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>86:15</xo>
<xt>Kut 34:6; Hes 14:18; Neh 9:17; Yoe 2:13; Zab 103:8; 111:4</xt></note></f> </q1>
<q2><vn>16 </vn>Unielekee na kunifadhili mimi; </q2>
<q1>Mpe mtumishi wako nguvu zako, </q1>
<q2>Umwokoe mwana wa mjakazi wako. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Unifanyie ishara ya wema, </q1>
<q2>Wanichukiao waione na kuaibishwa. </q2>
<q1>Kwa kuwa Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Umenisaidia na kunifariji. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>87</cn>
<q1><vn>1 </vn>Msingi wake upo </q1>
<q2>Juu ya milima mitakatifu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>
<nd>Bwana</nd> ayapenda malango ya Sayuni </q1>
<q2>Kuliko maskani zote za Yakobo. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Umetajwa kwa mambo matukufu, </q1>
<q2>Ee Mji wa Mungu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>87:3</xo>
<xt>Isa 60:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Nitataja Rahabu na Babeli </q1>
<q2>Miongoni mwao wanaonijua. </q2>
<q1>Tazama Filisti, na Tiro, na Kushi; </q1>
<q2>Huyu alizaliwa humo. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Naam, mintarafu Sayuni itasemwa, </q1>
<q2>Huyu na huyu alizaliwa humo. </q2>
<q1>Na Yeye Aliye juu </q1>
<q2>Ataufanya imara. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>87:5</xo>
<xt>Eze 48:35; Mt 16:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>
<nd>Bwana</nd> atahesabu, awaandikapo mataifa, </q1>
<q2>Huyu alizaliwa humo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>87:6</xo>
<xt>Zab 22:30; Isa 4:3; Yer 3:19; Eze 13:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Waimbao na wachezao na waseme, </q1>
<q2>Visima vyangu vyote vimo mwako. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>88</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wa wokovu wangu </q1>
<q2>Mchana na usiku nimelia mbele zako. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Maombi yangu yafike mbele zako, </q1>
<q2>Uutegee ukelele wangu sikio lako. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Maana nafsi yangu imeshiba taabu, </q1>
<q2>Na uhai wangu umekaribia kuzimu. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Nimehesabiwa pamoja nao washukao shimoni; </q1>
<q2>Nimekuwa kama mtu asiye na msaada. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Miongoni mwao waliokufa nimetupwa, </q1>
<q2>Kama waliouawa walalao makaburini. </q2>
<q1>Hao ambao Wewe huwakumbuki tena, </q1>
<q2>Wametengwa mbali na mkono wako. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Mimi umenilaza katika shimo la chini, </q1>
<q2>Katika mahali penye giza vilindini. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ghadhabu yako imenilemea, </q1>
<q2>Umenitesa kwa mawimbi yako yote. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Wanijuao umewatenga nami; </q1>
<q2>Umenifanya kuwa chukizo kwao; </q2>
<q1>Nimefungwa wala siwezi kutoka. </q1>
<q2><vn>9 </vn>Jicho langu limefifia kwa ajili ya mateso </q2>
<q1>
<nd>Bwana</nd>, nimekuita kila siku; </q1>
<q2>Nimekunyoshea Wewe mikono yangu. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Wafu je! Utawafanyia miujiza? </q1>
<q2>Au waliofariki watasimama na kukuhimidi? </q2>
<q1><vn>11 </vn>Fadhili zako zitasimuliwa kaburini? </q1>
<q2>Au uaminifu wako katika uharibifu? </q2>
<q1><vn>12 </vn>Miujiza yako itajulikana gizani? </q1>
<q2>Au haki yako katika nchi ya usahaulifu? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>88:12</xo>
<xt>Ayu 10:21; Zab 31:12; Mhu 8:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Lakini mimi nimekulilia Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Na asubuhi maombi yangu yatakuwasilia. </q2>
<q1><vn>14 </vn>
<nd>Bwana</nd>, kwa nini kuitupa nafsi yangu, </q1>
<q2>Na kunificha uso wako? </q2>
<q1><vn>15 </vn>Nateswa mimi hali ya kufa tangu ujana, </q1>
<q2>Nimevumilia vitisho vyako na kufadhaika. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>88:15</xo>
<xt>Ayu 6:4; Isa 53:8; Dan 9:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Hasira zako kali zimepita juu yangu, </q1>
<q2>Maogofyo yako yameniangamiza. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Yamenizunguka kama maji mchana kutwa, </q1>
<q2>Yamenisonga yote pamoja. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Mpenzi na rafiki umewatenga nami, </q1>
<q2>Nao wanijuao wamo gizani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>88:18</xo>
<xt>Ayu 19:13</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>89</cn>
<q1><vn>1 </vn>Fadhili za 
<nd>Bwana</nd> nitaziimba milele; </q1>
<q2>Kwa kinywa changu nitavijulisha vizazi vyote uaminifu wako. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Maana nimesema, Fadhili zitajengwa milele; </q1>
<q2>Katika mbingu utauthibitisha uaminifu wako. </q2>
<b></b>
<q1><vn>3 </vn>Nimefanya agano na mteule wangu, </q1>
<q2>Nimemuapia Daudi, mtumishi wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:3</xo>
<xt>Eze 34:23; hes 3:5; Mdo 2:30; Ebr 7:21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Wazao wako nitawafanya imara milele, </q1>
<q2>Nitakijenga kiti chako cha enzi hata milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:4</xo>
<xt>2 Sam 7:12-16; 1 Fal 9:5; 1 Nya 17:11-14; Zab Isa 9:6, 7; Lk 1:32; 132:11; Mdo 2:30; Rum 1:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, mbingu zitayasifu maajabu yako, </q1>
<q2>Uaminifu wako katika kusanyiko la watakatifu. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Maana ni nani katika mbingu awezaye kulinganishwa na 
<nd>Bwana</nd>? </q1>
<q2>Ni nani afananaye na 
<nd>Bwana</nd> miongoni mwa malaika? </q2>
<q1><vn>7 </vn>Mungu huogopwa sana barazani pa watakatifu, </q1>
<q2>Ni wa kuhofiwa kuliko wote wanaomzunguka. </q2>
<q1><vn>8 </vn>
<nd>Bwana</nd>, Mungu wa majeshi, </q1>
<q2>Ni nani aliye hodari kama Wewe, Ee YAHU? </q2>
<q2>Na uaminifu wako unakuzunguka. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Wewe ndiwe ukitawalaye kiburi cha bahari. </q1>
<q2>Mawimbi yake yainukapo wayatuliza Wewe. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:9</xo>
<xt>Ayu 38:11; Nah 1:4; Mt 8:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Ndiwe uliyemseta Rahabu akawa kama aliyeuawa, </q1>
<q2>Kwa mkono hodari umewatawanya wakuchukiao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:10</xo>
<xt>Isa 30:7</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>11 </vn>Mbingu ni mali yako, nchi nayo ni mali yako, </q1>
<q2>Ulimwengu na vyote viujazavyo </q2>
<q2>Ndiwe uliyeupiga msingi wake. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Kaskazini na kusini ndiwe uliyeziumba, </q1>
<q2>Tabori na Hermoni hulifurahia jina lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:12</xo>
<xt>Yos 19:22; 12;1; Amu 4:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Mkono wako ni mkono wenye uweza, </q1>
<q2>Mkono wako una nguvu, </q2>
<q2>Mkono wako wa kuume umetukuka. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako, </q1>
<q2>Fadhili na kweli zahudhuria mbele za uso wako. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Heri watu wale waijuao sauti ya shangwe, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, huenenda katika nuru ya uso wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:15</xo>
<xt>Hes 10;10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Kwa jina lako hufurahi mchana kutwa, </q1>
<q2>Na kwa haki yako hutukuzwa. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Maana fahari ya nguvu zao ni Wewe, </q1>
<q2>Na kwa radhi yako pembe yetu itatukuka. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Maana ngao yetu ina 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Na mfalme wetu ni wake Mtakatifu wa Israeli. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:18</xo>
<xt>Hos 13:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Ndipo ulipowaambia watakatifu wako kwa njozi, </q1>
<q2>Ukasema, nimempa aliye hodari msaada; </q2>
<q2>Nimemtukuza aliyechaguliwa miongoni mwa watu. </q2>
<q1><vn>20 </vn>Nimemwona Daudi, mtumishi wangu, </q1>
<q2>Nimempaka mafuta yangu matakatifu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:20</xo>
<xt>1 Sam 13:14; 16:12; Mdo 13:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Ambaye mkono wangu utakuwa thabiti kwake, </q1>
<q2>Na mkono wangu utamtia nguvu. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Adui hatamwonea, </q1>
<q2>Wala mwana wa uovu hatamtesa. </q2>
<q1><vn>23 </vn>Bali nitawaponda watesi wake mbele yake, </q1>
<q2>Nitawapiga wanaomchukia. </q2>
<q1><vn>24 </vn>Uaminifu wangu na fadhili zangu atakuwa nazo, </q1>
<q2>Na kwa jina langu pembe yake itatukuka. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:24</xo>
<xt>Zab 61:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>25 </vn>Nitaweka mkono wake juu ya bahari, </q1>
<q2>Na mkono wake wa kuume juu ya mito. </q2>
<q1><vn>26 </vn>Yeye ataniita, Wewe baba yangu, </q1>
<q2>Mungu wangu na mwamba wa wokovu wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:26</xo>
<xt>2 Sam 7:14; 1 Nya 22:10; Yn 5:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>27 </vn>Nami nitamjalia kuwa mzaliwa wangu wa kwanza, </q1>
<q2>Kuwa juu sana kuliko wafalme wa dunia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:27</xo>
<xt>Zab 2:7; Ufu 1:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>28 </vn>Hata milele nitamwekea fadhili zangu, </q1>
<q2>Na agano langu litafanyika amini kwake. </q2>
<q1><vn>29 </vn>Wazao wake nao nitawadumisha milele, </q1>
<q2>Na kiti chake cha enzi kama siku za mbingu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:29</xo>
<xt>Isa 9:7; Yer 33:17; Dan 7:14; Kum 11:21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>30 </vn>Wanawe wakiiacha sheria yangu, </q1>
<q2>Wasiende katika hukumu zangu, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:30</xo>
<xt>2 Sam 7:14; Yer 9:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>31 </vn>Wakizihalifu amri zangu, </q1>
<q2>Wasiyashike maagizo yangu, </q2>
<q1><vn>32 </vn>Basi, nitawarudi makosa yao kwa fimbo, </q1>
<q2>Na uovu wao kwa mapigo. </q2>
<q1><vn>33 </vn>Lakini fadhili zangu sitamwondolea yeye, </q1>
<q2>Wala sitafanya uaminifu wangu kuwa uongo. </q2>
<q1><vn>34 </vn>Mimi sitalihalifu agano langu, </q1>
<q2>Sitalibadili neno lililotoka midomoni mwangu. </q2>
<q1><vn>35 </vn>Neno moja nimeliapa kwa utakatifu wangu, </q1>
<q2>Hakika sitamwambia Daudi uongo, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:35</xo>
<xt>Zab 110:4; Ebr 6:13, 17; Amo 4:2, 8:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>36 </vn>Wazao wake watadumu milele, </q1>
<q2>Na kiti chake kitakuwa kama jua mbele zangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:36</xo>
<xt>2 Sam 7:16; Lk 1:33; Yn 12:34</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>37 </vn>Kitathibitika milele kama mwezi; </q1>
<q2>Shahidi aliye mbinguni mwaminifu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:37</xo>
<xt>Yer 31:35</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>38 </vn>Walakini Wewe umemtupa na kumkataa, </q1>
<q2>Umemghadhibikia masihi<f> <fn>g</fn><note>
<fr>89:38</fr>
<ft> Au, mtiwa mafuta.</ft></note></f> wako. </q2>
<q1><vn>39 </vn>Umechukizwa na agano la mtumishi wako, </q1>
<q2>Umeinajisi taji yake na kuitupa chini. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:39</xo>
<xt>Omb 5:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>40 </vn>Umeyabomoa maboma yake yote, </q1>
<q2>Umezifanya ngome zake kuwa magofu. </q2>
<q1><vn>41 </vn>Wote wapitao njiani wanateka mali zake; </q1>
<q2>Amekuwa laumu kwa jirani zake; </q2>
<q1><vn>42 </vn>Umeutukuza mkono wa kuume wa watesi wake; </q1>
<q2>Umewafurahisha wote wanaomchukia. </q2>
<q1><vn>43 </vn>Pia umeurudisha nyuma ukali wa upanga wake; </q1>
<q2>Wala hukumsimamisha vitani. </q2>
<q1><vn>44 </vn>Umeikomesha fahari yake; </q1>
<q2>Kiti chake cha enzi umekitupa chini. </q2>
<q1><vn>45 </vn>Umezipunguza siku za ujana wake; </q1>
<q2>Umemvika aibu. </q2>
<b></b>
<q1><vn>46 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, hata lini? Utajificha hata milele? </q1>
<q2>Ghadhabu yako itawaka kama moto? </q2>
<q1><vn>47 </vn>Ukumbuke jinsi mimi nisivyo wa kudumu; </q1>
<q2>Kwa ubatili gani umeiumba jamii ya wanadamu! <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:47</xo>
<xt>Ayu 7:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>48 </vn>Ni mwanamume gani atakayeishi asione mauti, </q1>
<q2>Atakayejiokoa nafsi yake na mkono wa kuzimu? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:48</xo>
<xt>Ebr 11;5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>49 </vn>Bwana, zi wapi fadhili zako za kwanza, </q1>
<q2>Ulizomwapia Daudi kwa uaminifu wako? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>89:49</xo>
<xt>2 Sam 7:15; Isa 55:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>50 </vn>Ee Bwana, ukumbuke, </q1>
<q2>Wanavyosimangwa watumishi wako; </q2>
<q1>Jinsi ninavyostahimili kifuani mwangu </q1>
<q2>Masimango ya watu wengi. </q2>
<q1><vn>51 </vn>Ambayo adui zako wamesimanga, Ee 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Naam, wamezisimanga hatua za masihi<f> <fn>h</fn><note>
<fr>89:51</fr>
<ft> Au, mtiwa mafuta.</ft></note></f> wako. </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>52 </vn>Na ahimidiwe 
<nd>Bwana</nd> milele. Amina na Amina. </q1>
<d>KITABU CHA NNE </d>
<b></b></c>

<c><cn>90</cn>
<q1><vn>1 </vn>Wewe, Bwana, umekuwa makao yetu, </q1>
<q2>Kizazi baada ya kizazi. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kabla haijazaliwa milima, wala hujaiumba dunia, </q1>
<q2>Na tangu milele hata milele ndiwe Mungu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>90:2</xo>
<xt>Ayu 38:4-6; Mit 8:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Wamrudisha mtu mavumbini, </q1>
<q2>usemapo, Rudini, enyi wanadamu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>90:3</xo>
<xt>Mwa 3:19; Mhu 12:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Maana miaka elfu machoni pako </q1>
<q2>Ni kama siku ya jana ikiisha kupita, </q2>
<q2>Na kama kesha la usiku. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>90:4</xo>
<xt>Ebr 13:8; 2 Pet 3:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Wawagharikisha, huwa kama usingizi, </q1>
<q2>Asubuhi huwa kama majani yameayo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>90:5</xo>
<xt>Isa 40:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Asubuhi yachipuka na kumea, </q1>
<q2>Jioni yakatika na kukauka. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>90:6</xo>
<xt>Ayu 14:2; Zab 92:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Maana tumetoweshwa kwa hasira yako, </q1>
<q2>Na kwa ghadhabu yako tumefadhaishwa. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Umeyaweka maovu yetu mbele zako, </q1>
<q2>Siri zetu katika mwanga wa uso wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>90:8</xo>
<xt>Zab 50:21; Yer 16:17; Zab 19:12; Mit 5:21; Mhu 12:14; Rum 2:16; 1 Kor 4:5; Ebr 4:12, 13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Maana siku zetu zote zimepita katika hasira yako, </q1>
<q2>Tumetowesha miaka yetu kama kite. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Siku za miaka yetu ni miaka sabini, </q1>
<q2>Na ikiwa tuna nguvu miaka themanini; </q2>
<q1>Na kiburi chake ni taabu na ubatili, </q1>
<q2>Maana chapita upesi tukatokomea mara. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Ni nani aujuaye uweza wa hasira yako? </q1>
<q2>Na ghadhabu yako kama ipasavyo kicho chako? </q2>
<q1><vn>12 </vn>Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, </q1>
<q2>Tujipatie moyo wa hekima. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>90:12</xo>
<xt>Zab 39:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd> urudi, hata lini? </q1>
<q2>Uwahurumie watumishi wako. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Utushibishe asubuhi kwa fadhili zako, </q1>
<q2>Nasi tutashangilia na kufurahi siku zetu zote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>90:13</xo>
<xt>Kum 32:36</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Utufurahishe kwa kadiri ya siku ulizotutesa, </q1>
<q2>Kama miaka ile tuliyoona mabaya. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Matendo yako na yaonekane kwa watumishi wako, </q1>
<q2>Na adhama yako kwa watoto wao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>90:16</xo>
<xt>Zab 44:1; Hab 3:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Na uzuri wa 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wetu, uwe juu yetu, </q1>
<q2>Na kazi ya mikono yetu utufanyie thabiti, </q2>
<q2>Naam, kazi ya mikono yetu uithibitishe. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>90:17</xo>
<xt>Isa 26:12; 2 The 2;16, 17</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>91</cn>
<q1><vn>1 </vn>Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu </q1>
<q2>Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Nitasema, 
<nd>Bwana</nd> ndiye kimbilio langu na ngome yangu, </q1>
<q2>Mungu wangu nitakayemtumaini. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Maana Yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji, </q1>
<q2>Na katika tauni iharibuyo. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Kwa manyoya yake atakufunika, </q1>
<q2>Chini ya mbawa zake utapata kimbilio; </q2>
<q2>Uaminifu wake ni ngao na kigao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>91:4</xo>
<xt>Zab 61:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Hutaogopa hofu ya usiku, </q1>
<q2>Wala mshale urukao mchana, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>91:5</xo>
<xt>Ayu 5:19; Mit 3:23; Isa 43:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Wala tauni ipitayo gizani, </q1>
<q2>Wala uele uharibuo adhuhuri, </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ijapo watu elfu waanguka ubavuni pako. </q1>
<q2>Naam, kumi elfu mkono wako wa kuume! </q2>
<q2>Hata hivyo hautakukaribia wewe. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ila kwa macho yako utatazama, </q1>
<q2>Na kuyaona malipo ya wasio haki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>91:8</xo>
<xt>Mal 1:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Kwa kuwa Wewe 
<nd>Bwana</nd> ndiwe kimbilio langu; </q1>
<q2>Umemfanya Aliye juu kuwa makao yako. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Mabaya hayatakupata wewe, </q1>
<q2>Wala tauni haitaikaribia hema yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>91:10</xo>
<xt>Mit 1:33; 2 The 3:3; 2 Pet 2:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Kwa kuwa atakuagizia malaika zake </q1>
<q2>Wakulinde katika njia zako zote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>91:11</xo>
<xt>Mat 4:6; Lk 4:10</xt></note></f> <f> <fn>-</fn><note>
<xo>91:11</xo>
<xt>Zab 34:7; Mt 4:6; Lk 4:10; Ebr 1:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Mikononi mwao watakuchukua, </q1>
<q2>Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>91:12</xo>
<xt>Ayu 5:23; Zab 37:24; Mat 4:6; Lk 4:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Utawakanyaga simba na nyoka, </q1>
<q2>Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>91:13</xo>
<xt>Lk 10:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Kwa kuwa amekaza kunipenda </q1>
<q2>Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, </q2>
<q2>Kwa kuwa amenijua Jina langu. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Ataniita nami nitamwitikia; </q1>
<q2>Nitakuwa pamoja naye taabuni, </q2>
<q2>Nitamwokoa na kumtukuza; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>91:15</xo>
<xt>Ayu 22:27; Zab 18:3; yer 33:3; Zek 13:9; Ebr 5:7; Zab 43:2; 1 Sam 2;30</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Kwa siku nyingi nitamshibisha, </q1>
<q2>Nami nitamwonyesha wokovu wangu. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>92</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ni neno jema kumshukuru 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Na kuliimbia jina lako, Ee Uliye juu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kuzitangaza rehema zako asubuhi, </q1>
<q2>Na uaminifu wako wakati wa usiku. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Kwa chombo chenye nyuzi kumi, </q1>
<q2>Na kwa kinanda, </q2>
<q2>Na kwa mlio wa kinubi. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Kwa kuwa umenifurahisha, 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Kwa kazi yako; nitashangilia </q2>
<q2>Kwa ajili ya matendo ya mikono yako. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, jinsi yalivyo makuu matendo yako! </q1>
<q2>Mawazo yako ni mafumbo makubwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>92:5</xo>
<xt>Isa 28:29; Rum 11:23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Mtu mjinga hayatambui hayo, </q1>
<q2>Wala mpumbavu hayafahamu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>92:6</xo>
<xt>Zab 73:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Wasio haki wakichipuka kama majani </q1>
<q2>Na wote watendao maovu wakistawi. </q2>
<q2>Ni kwa kusudi waangamizwe milele; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>92:7</xo>
<xt>Ayu 21:7; Yer 12:1; Mal 3:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Bali Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, U Mtukufu hata milele. </q1>
<q1><vn>9 </vn>Maana hao adui zako, Ee 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Hao adui zako watapotea, </q2>
<q2>Na watendao maovu watatawanyika wote pia. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Bali pembe yangu umeiinua kama pembe ya nyati, </q1>
<q2>Nimepakwa mafuta mabichi. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Na jicho langu limewatazama walioniotea, </q1>
<q2>Sikio langu limesikia habari za waovu walionishambulia. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Mwenye haki atasitawi kama mtende, </q1>
<q2>Atakua kama mwerezi wa Lebanoni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>92:12</xo>
<xt>Zab 52:8; Wim 7:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Waliopandwa katika nyumba ya 
<nd>Bwana</nd> </q1>
<q2>Watasitawi katika nyua za Mungu wetu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>92:13</xo>
<xt>Isa 60:21; Mt 15:13; Yn 15:2,5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Watazaa matunda hadi wakati wa uzee, </q1>
<q2>Watajaa utomvu, watakuwa na ubichi. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Watangaze ya kuwa 
<nd>Bwana</nd> ni mwenye adili, </q1>
<q2>Mwamba wangu, ndani yake hamna udhalimu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>92:15</xo>
<xt>Kum 32:4; Rum 9:14</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>93</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd> ametamalaki, amejivika adhama, </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> amejivika, na kujikaza nguvu. </q2>
<q2>Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>93:1</xo>
<xt>Isa 52:7; Ufu 19:6; Ayu 40:10; Zab 104:1; Isa59:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kiti chako kimekuwa thabiti tokea zamani; </q1>
<q2>Wewe ndiwe uliye tangu milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>93:2</xo>
<xt>Mit 8:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, mito imepaza, </q1>
<q2>Mito imepaza sauti zake, </q2>
<q2>Mito imepaza uvumi wake. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Kupita sauti ya maji mengi, maji makuu, </q1>
<q2>Kupita mawimbi ya bahari yaumkayo, </q2>
<q2>
<nd>Bwana</nd> Aliye juu ndiye mwenye ukuu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>93:4</xo>
<xt>Zab 29:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Shuhuda zako ni amini sana; </q1>
<q2>Utakatifu ndio uifaao nyumba yako, </q2>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, milele na milele. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>94</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wa kisasi, </q1>
<q2>Mungu wa kisasi, uangaze, </q2>
<q1><vn>2 </vn>Mwenye kuihukumu nchi, ujitukuze, </q1>
<q2>Uwape wenye kiburi stahili zao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>94:2</xo>
<xt>Mwa 18:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>
<nd>Bwana</nd>, hata lini wasio haki, </q1>
<q2>Hata lini wasio haki watashangilia? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>94:3</xo>
<xt>Ayu 20:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Je! Wote watendao uovu watatoa maneno, </q1>
<q2>Na kusema majivuno, na kufanya kiburi? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>94:4</xo>
<xt>Yud 1:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, wanawaseta watu wako; </q1>
<q2>Wanautesa urithi wako; </q2>
<q1><vn>6 </vn>Wanamwua mjane na mgeni; </q1>
<q2>Wanawafisha yatima. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Nao husema, 
<nd>Bwana</nd> haoni; </q1>
<q2>Mungu wa Yakobo hafikiri. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Enyi wajinga miongoni mwa watu, fikirini; </q1>
<q2>Enyi wapumbavu, lini mtakapopata akili? </q2>
<q1><vn>9 </vn>Aliyelitia sikio mahali pake asisikie? </q1>
<q2>Aliyelifanya jicho asione? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>94:9</xo>
<xt>Kut 4:11; Mit 20:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Awaadibuye mataifa asikemee? </q1>
<q2>Amfundishaye mwanadamu asijue? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>94:10</xo>
<xt>Ayu 35:11; Yn 6:45; Isa 2:3, 28:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>
<nd>Bwana</nd> anajua mawazo ya mwanadamu, </q1>
<q2>Ya kuwa ni ubatili. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>94:11</xo>
<xt>1 Kor 1:21, 1 Kor 3:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, heri mtu yule umwadibuye, </q1>
<q2>Na kumfundisha kwa sheria yako; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>94:12</xo>
<xt>Ayu 5:17; Mit 3:11; 1 Kor 11:32</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Upate kumstarehesha siku za mabaya, </q1>
<q2>Hata asiye haki atakapochimbiwa shimo. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> hatawatupa watu wake, </q1>
<q2>Wala hutauacha urithi wake, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>94:14</xo>
<xt>Kum 31:6; 1 Sam 12:22; 1 Fal 6:13; Yer 31:37</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Maana hukumu itairejea haki, </q1>
<q2>Na wote walio wanyofu wa moyo wataifuata. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Ni nani atakayesimama </q1>
<q2>Kwa ajili yangu juu ya wabaya? </q2>
<q1>Ni nani atakayenisaidia </q1>
<q2>Juu yao wafanyao maovu? </q2>
<q1><vn>17 </vn>Kama 
<nd>Bwana</nd> asingalikuwa msaada wangu, </q1>
<q2>Nafsi yangu kwa upesi ingalikaa penye kimya. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Niliposema, Mguu wangu unateleza; </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, fadhili zako zilinitegemeza. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Katika wingi wa mawazo ya moyoni mwangu, </q1>
<q2>Faraja zako zaifurahisha roho yangu. </q2>
<q1><vn>20 </vn>Je! Kiti cha udhalimu kishirikiane nawe, </q1>
<q2>Kitungacho madhara kwa njia ya sheria? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>94:20</xo>
<xt>Amo 6:3; 2 Kor 6:14; Zab 58:2; Isa 10:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Huishambulia nafsi yake mwenye haki, </q1>
<q2>Na kuihukumu damu isiyo na hatia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>94:21</xo>
<xt>Mt 27:1; Kut 23:7; Mit 17:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>22 </vn>Lakini 
<nd>Bwana</nd> amekuwa ngome kwangu, </q1>
<q2>Na Mungu wangu mwamba wangu wa kukimbilia. </q2>
<q1><vn>23 </vn>Naye atawarudishia uovu wao, </q1>
<q2>Atawaangamiza katika ubaya wao, </q2>
<q2>Naam, 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wetu, atawaangamiza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>94:23</xo>
<xt>Mit 2:22</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>95</cn>
<q1><vn>1 </vn>Njoni, tumwimbie 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Tuje mbele zake kwa shukrani, </q1>
<q2>Tumfanyie shangwe kwa zaburi. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> ni Mungu mkuu, </q1>
<q2>Na Mfalme mkuu juu ya miungu yote. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Mkononi mwake zimo bonde za dunia, </q1>
<q2>Hata vilele vya milima ni vyake. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya, </q1>
<q2>Na mikono yake iliumba nchi kavu. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Njoni, tuabudu, tusujudu, </q1>
<q2>Tupige magoti mbele za 
<nd>Bwana</nd> aliyetuumba. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>95:6</xo>
<xt>1 Fal 8:54; 1 Nya 6:13; Ezr 9:5; Dan 6:10; Lk 22:41; Mdo 7:60; 1 Kor 6:20; Efe 3:14; Ayu 35:10; Isa 54:5; Yn 1:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Kwa maana ndiye Mungu wetu, </q1>
<q2>Na sisi tu watu wa malisho yake, </q2>
<q1>Na kondoo za mkono wake. </q1>
<q2>Ingekuwa heri leo msikie sauti yake! <f> <fn>-</fn><note>
<xo>95:7-8</xo>
<xt>Ebr 3:15, 4:7, Ebr 95:7-11, Ebr 3:7-11; Hes 14:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Msifanye migumu mioyo yenu; </q1>
<q2>Kama vile huko Meriba </q2>
<q2>Kama siku ya Masa jangwani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>95:8-9</xo>
<xt>Kut 17:1-7; Hes 20:2-13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Hapo waliponijaribu baba zenu, </q1>
<q2>Wakanipima, wakayaona matendo yangu. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Miaka arobaini nalihuzunika na kizazi kile, </q1>
<q2>Nikasema, Hao ni watu waliopotoka mioyo, </q2>
<q2>Hawakuzijua njia zangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>95:10</xo>
<xt>Ebr 3:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Nikaapa kwa hasira yangu </q1>
<q2>Wasiingie rahani mwangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>95:11</xo>
<xt>Hes 14:20-23; Kum 1:34-36; 12:9-10; Ebr 4:3,5</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>96</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mwimbieni 
<nd>Bwana</nd> wimbo mpya, </q1>
<q2>Mwimbieni 
<nd>Bwana</nd>, nchi yote. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Mwimbieni 
<nd>Bwana</nd>, libarikini jina lake, </q1>
<q2>Tangazeni wokovu wake siku kwa siku. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Wahubirini mataifa habari za utukufu wake, </q1>
<q2>Na watu wote habari za maajabu yake. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> ni mkuu mwenye kusifiwa sana. </q1>
<q2>Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Maana miungu yote ya watu si kitu, </q1>
<q2>Lakini 
<nd>Bwana</nd> ndiye aliyezifanya mbingu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>96:5</xo>
<xt>Isa 41:24; Yer 10:11; Hab 2:18-20; Mdo 19:26; 1 Kor 8:4, 5; Mwa 1:1; Isa 42:5; Yer 10:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Heshima na adhama ziko mbele zake, </q1>
<q2>Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Mpeni 
<nd>Bwana</nd>, enyi jamaa za watu, </q1>
<q2>Mpeni 
<nd>Bwana</nd> utukufu na nguvu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>96:7-9</xo>
<xt>Zab 29:1-2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Mpeni 
<nd>Bwana</nd> utukufu wa jina lake, </q1>
<q2>Leteni sadaka mkaziingie nyua zake. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Mwabuduni 
<nd>Bwana</nd> kwa uzuri wa utakatifu, </q1>
<q2>Tetemekeni mbele zake, nchi yote. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Semeni katika mataifa, 
<nd>Bwana</nd> ametamalaki; </q1>
<q2>Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike, </q2>
<q2>Atawahukumu watu kwa adili. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>96:10</xo>
<xt>Ufu 11:15; Yn 5:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Mbingu na zifurahi, nchi na ishangilie, </q1>
<q2>Bahari na ivume na vyote viijazavyo, </q2>
<q1><vn>12 </vn>Mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo, </q1>
<q2>Ndipo miti yote ya mwituni iimbe kwa furaha; </q2>
<q1><vn>13 </vn>Mbele za 
<nd>Bwana</nd>, kwa maana anakuja, </q1>
<q2>Kwa maana anakuja aihukumu nchi. </q2>
<q1>Atauhukumu ulimwengu kwa haki, </q1>
<q2>Na mataifa kwa uaminifu wake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>96:13</xo>
<xt>Ufu 19:11</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>97</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd> ametamalaki, nchi na ishangilie, </q1>
<q2>Visiwa vingi na vifurahi. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Mawingu na giza vyamzunguka, </q1>
<q2>Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Moto hutangulia mbele zake, </q1>
<q2>Nao huwateketeza watesi wake pande zote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>97:3</xo>
<xt>Dan 7:10; Hab 3:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Umeme wake uliuangaza ulimwengu, </q1>
<q2>Nchi ikaona ikatetemeka. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Milima iliyeyuka kama nta mbele za 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Mbele za Bwana wa dunia yote. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Mbingu zimetangaza haki yake, </q1>
<q2>Na watu wote wameuona utukufu wake. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Na waaibishwe wote waabuduo sanamu, </q1>
<q2>Wajivunao kwa vitu visivyofaa; </q2>
<q2>Enyi miungu yote, msujuduni Yeye. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>97:7</xo>
<xt>Kut 20:4; Law 26:1; Isa 37:18, 19; Yer 10:14; Ebr 1:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Sayuni imesikia na kufurahi, </q1>
<q2>Binti za Yuda walishangilia, </q2>
<q2>Kwa sababu ya hukumu zako, Ee 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Maana Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, ndiwe Uliye juu, </q1>
<q2>Juu sana kuliko nchi yote; </q2>
<q2>Umetukuka sana juu ya miungu yote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>97:9</xo>
<xt>Efe 1:21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Enyi mmpendao 
<nd>Bwana</nd>, uchukieni uovu; </q1>
<q2>Huwalinda nafsi zao watauwa wake, </q2>
<q2>Na kuwaokoa na mkono wa wasio haki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>97:10</xo>
<xt>Zab 101:3; Amo 5:15; Rum 7:15; 1 Sam 2:9; Mit 2:8; Dan 3:28</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Nuru imemzukia mwenye haki, </q1>
<q2>Na furaha wanyofu wa moyo. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Enyi wenye haki, mmfurahieni 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Na kulishukuru jina lake takatifu. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>98</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mwimbieni 
<nd>Bwana</nd> wimbo mpya, </q1>
<q2>Kwa maana ametenda mambo ya ajabu. </q2>
<q1>Mkono wa kuume wake mwenyewe, </q1>
<q2>Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>98:1</xo>
<xt>Isa 59:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>
<nd>Bwana</nd> ameufunua wokovu wake, </q1>
<q2>Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>98:2</xo>
<xt>Isa 52:10; Lk 2:30; Isa 62:2; Rum 3:25; Law 28:52; Kum 4:31; Mik 7:20; Lk 1:54; Isa 49:6; Lk 3:6; Mdo13:47</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Amezikumbuka rehema zake, </q1>
<q2>Na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli. </q2>
<q1>Miisho yote ya dunia imeuona </q1>
<q2>Wokovu wa Mungu wetu. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Mshangilieni 
<nd>Bwana</nd>, nchi yote, </q1>
<q2>Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni zaburi. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Mwimbieni 
<nd>Bwana</nd> zaburi kwa kinubi, </q1>
<q2>Kwa kinubi na sauti ya zaburi. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Kwa panda na sauti ya baragumu. </q1>
<q2>Shangilieni mbele za Mfalme, 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>98:6</xo>
<xt>Hes 10:10; 1 Nya 15:28; 2 Nya 29:27</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Bahari na ivume na vyote viijazavyo, </q1>
<q2>Ulimwengu nao wanaokaa ndani yake. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Mito na ipige makofi, </q1>
<q2>Milima na iimbe pamoja kwa furaha. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Mbele za 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Kwa maana anakuja aihukumu nchi. </q2>
<q1>Atauhukumu ulimwengu kwa haki, </q1>
<q2>Na mataifa kwa adili. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>99</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd> ametamalaki, mataifa wanatetemeka; </q1>
<q2>Ameketi juu ya makerubi, nchi inatikisika. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>99:1</xo>
<xt>Kut 25:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>
<nd>Bwana</nd> katika Sayuni ni mkuu, </q1>
<q2>Naye ametukuka juu ya mataifa yote. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Na walishukuru jina lake kuu la kuhofiwa; </q1>
<q2>Ndiye mtakatifu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>99:3</xo>
<xt>Kum 28:58; Isa 6:3; Ufu 4:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Nguvu za mfalme nazo zapenda hukumu; </q1>
<q2>Wewe ndiwe uliyeithibitisha adili; </q2>
<q2>Ulifanya hukumu na haki katika Yakobo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>99:4</xo>
<xt>Kum 32:3, 4; Ayu 36:5; Isa 11:3-5; Yer 235; Mwa 18:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Mtukuzeni 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wetu; </q1>
<q2>Sujuduni penye kiti cha miguu yake; </q2>
<q2>Ndiye mtakatifu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>99:5</xo>
<xt>1 Nya 28:2; Zab 132:7; Isa 66:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Musa na Haruni miongoni mwa makuhani wake, </q1>
<q2>Na Samweli miongoni mwao waliitiao jina lake, </q2>
<q2>Walipomwita Bwana aliwaitikia; </q2>
<q1><vn>7 </vn>Katika nguzo ya wingu alikuwa akisema nao. </q1>
<q2>Walishika shuhuda zake na amri aliyowapa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>99:7</xo>
<xt>Kut 19:9, Kut 33:9; Hes 12:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wetu, ndiwe uliyewajibu; </q1>
<q2>Ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe </q2>
<q2>Ingawa uliwapatiliza matendo yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>99:8</xo>
<xt>Hes 14:20; Sef 3:7; Kum 9:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Mtukuzeni 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wetu; </q1>
<q2>Sujuduni mkiukabili mlima wake mtakatifu; </q2>
<q2>Maana 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wetu, ndiye mtakatifu. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>100</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mfanyieni 
<nd>Bwana</nd> shangwe, dunia yote; </q1>
<q1><vn>2 </vn>Mtumikieni 
<nd>Bwana</nd> kwa furaha; </q1>
<q2>Njoni mbele zake kwa kuimba; </q2>
<q1><vn>3 </vn>Jueni kwamba 
<nd>Bwana</nd> ndiye Mungu; </q1>
<q2>Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake; </q2>
<q2>Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>100:3</xo>
<xt>Ayu 10:8, 9; Mhu 12;1; Efe 2:10; Eze 34:30</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; </q1>
<q2>Nyuani mwake kwa kusifu; </q2>
<q2>Mshukuruni, lihimidini jina lake; </q2>
<q1><vn>5 </vn>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> ndiye mwema; </q1>
<q2>Rehema zake ni za milele; </q2>
<q2>Na uaminifu wake vizazi na vizazi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>100:5</xo>
<xt>1 Nya 16:34; 2 Nya 5:13; 7:3; Ezr 3:11; Zab 106:1; 107:1; 118:1; 136:1; Yer 33:11</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>101</cn>
<q1><vn>1 </vn>Rehema na hukumu nitaziimba, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, nitakuimbia zaburi. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Nitaiangalia njia ya unyofu; </q1>
<q2>Utakuja kwangu lini? </q2>
<q1>Nitakwenda kwa unyofu wa moyo </q1>
<q2>Ndani ya nyumba yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>101:2</xo>
<xt>1 Sam 18:14; Mwa 18:19; Kum 6:7; 1 Fal 9:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Sitaweka mbele ya macho yangu </q1>
<q2>Neno la uovu. </q2>
<q1>Kazi yao waliopotoka naichukia, </q1>
<q2>Haitaambatana nami. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>101:3</xo>
<xt>Yosh 23:6; 1 Sam 12:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Moyo wa ukaidi utaondoka kwangu, </q1>
<q2>Lililo ovu sitalijua. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>101:4</xo>
<xt>Mt 7:23; 1 Kor 5:11; 2 Tim 2:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Amsingiziaye jirani yake kwa siri, </q1>
<q2>Huyo nitamharibu. </q2>
<q1>Mwenye macho ya kiburi na moyo wa majivuno, </q1>
<q2>Huyo sitavumilia naye. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>101:5</xo>
<xt>Mit 6:17; Lk 18:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi, </q1>
<q2>Hao wakae nami. </q2>
<q1>Yeye aendaye katika njia kamilifu, </q1>
<q2>Ndiye atakayenitumikia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>101:6</xo>
<xt>Rum 13:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Hatakaa ndani ya nyumba yangu </q1>
<q2>Mtu atendaye hila. </q2>
<q1>Asemaye uongo hatathibitika </q1>
<q2>Mbele ya macho yangu. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Asubuhi hata asubuhi nitawaharibu </q1>
<q2>Wabaya wote wa nchi. </q2>
<q1>Niwatenge wote watendao uovu </q1>
<q2>Na mji wa 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>101:8</xo>
<xt>Yer 21:12; Hose 9:3</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>102</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, usikie kuomba kwangu, </q1>
<q2>Kilio changu kikufikie. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Usinifiche uso wako siku ya shida yangu, </q1>
<q2>Unitegee sikio lako, siku niitapo unijibu upesi. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Maana siku zangu zinatoweka kama moshi, </q1>
<q2>Na mifupa yangu inateketea kama kinga. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:3</xo>
<xt>Yak 4:14; Omb 1:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Moyo wangu umepigwa kama majani na kukauka, </q1>
<q2>Naam, ninasahau kula chakula changu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Kwa ajili ya sauti ya kuugua kwangu </q1>
<q2>Mifupa yangu imegandamana na nyama yangu. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani, </q1>
<q2>Na kufanana na bundi wa mahameni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:6</xo>
<xt>Isa 34:11; Sef 2:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Nakesha, tena nimekuwa kama shomoro </q1>
<q2>Aliye peke yake juu ya nyumba. </q2>
<b></b>
<q1><vn>8 </vn>Adui zangu wananilaumu mchana kutwa; </q1>
<q2>Wanaonichukia kana kwamba wana wazimu </q2>
<q2>Huapa kwa kunitaja mimi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:8</xo>
<xt>Mdo 23:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Maana nimekula majivu kama chakula, </q1>
<q2>Na kukichanganya kinywaji changu na machozi. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Kwa sababu ya ghadhabu yako na hasira yako; </q1>
<q2>Maana umeniinua na kunitupilia mbali. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:10</xo>
<xt>Zab 30:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Siku zangu zi kama kivuli kilichotandaa, </q1>
<q2>Nami ninanyauka kama majani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:11</xo>
<xt>Yako 1:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Bali Wewe, 
<nd>Bwana</nd> utaketi ukimiliki milele, </q1>
<q2>Na kumbukumbu lako kizazi hata kizazi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:12</xo>
<xt>1 Tim 6:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Wewe mwenyewe utasimama, </q1>
<q2>Na kuirehemu Sayuni, </q2>
<q1>Kwa maana ndio wakati wa kuihurumia, </q1>
<q2>Naam, majira yaliyoamriwa yamewadia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:13</xo>
<xt>Isa 40:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Maana watumishi wako wameyaridhia mawe yake, </q1>
<q2>Na kuyaonea huruma mavumbi yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:14</xo>
<xt>Dan 9:2</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>15 </vn>Kisha mataifa wataliogopa jina la 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Na wafalme wote wa dunia utukufu wako; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:15</xo>
<xt>1 Fal 8:43</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>
<nd>Bwana</nd> atakapokuwa ameijenga Sayuni, </q1>
<q2>Atakapoonekana katika utukufu wake, </q2>
<q1><vn>17 </vn>Atakapoyaelekea maombi yake aliye mkiwa, </q1>
<q2>Asiyadharau maombi yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:17</xo>
<xt>Neh 2:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>Kizazi kitakachokuja kitaandikiwa hayo, </q1>
<q2>Na watu watakaoumbwa watamsifu 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:18</xo>
<xt>Rum 15:4; 1 Kor 10:11; Zab 22;31; Isa 43:21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Maana ametazama toka patakatifu pake pa juu, </q1>
<q2>Toka mbinguni 
<nd>Bwana</nd> ameiangalia nchi, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:19</xo>
<xt>Kum 26:15; Zab 14:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Ili akusikie kuugua kwake aliyefungwa, </q1>
<q2>Na kuwafungua walioandikiwa kufa. </q2>
<q1><vn>21 </vn>Watu walitangaze jina la 
<nd>Bwana</nd> katika Sayuni, </q1>
<q2>Na sifa zake katika Yerusalemu, </q2>
<q1><vn>22 </vn>Pindi mataifa watapokusanyika pamoja, </q1>
<q2>Falme nazo ili kumtumikia 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:22</xo>
<xt>Hos 1:11</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>23 </vn>Amezipunguza nguvu zangu njiani; </q1>
<q2>Amezifupisha siku zangu. </q2>
<q1><vn>24 </vn>Nitasema, Ee Mungu wangu, usiniondoe katikati ya siku zangu; </q1>
<q2>Miaka yako ni tangu kizazi hata kizazi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:24</xo>
<xt>Zab 90:2; Hab 1:12; Ufu 1:4,8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>25 </vn>Hapo mwanzo uliutia msingi wa nchi, </q1>
<q2>Na mbingu ni kazi ya mikono yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:25-27</xo>
<xt>Mwa 1;1; Kut 20:11; Ayu 38:4-7; Ebr 1:10-12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>26 </vn>Hizi zitaharibika, bali Wewe utadumu </q1>
<q2>Naam, hizi zitachakaa kama nguo; </q2>
<q1>Na kama mavazi utazibadilisha, </q1>
<q2>Nazo zitabadilika. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:26</xo>
<xt>Isa 66:22; Rum 8:20; 2 Pet 3:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>27 </vn>Lakini Wewe U Yeye yule; </q1>
<q2>Na miaka yako haitakoma. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>102:27</xo>
<xt>Mal 3:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>28 </vn>Wana wa watumishi wako watakaa, </q1>
<q2>Na wazao wao wataimarishwa mbele zako. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>103</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee nafsi yangu, umhimidi 
<nd>Bwana</nd>. </q1>
<q2>Naam, vyote vilivyo ndani yangu </q2>
<q2>Vilihimidi jina lake takatifu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ee nafsi yangu, umhimidi 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Wala usizisahau fadhili zake zote. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Akusamehe maovu yako yote, </q1>
<q2>Akuponya magonjwa yako yote, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>103:3</xo>
<xt>Isa 33:34; Mt 9:2; Mk 2:5; Lk 7:47; Kut 15:26; Yer 17:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Aukomboa uhai wako na kaburi, </q1>
<q2>Akutia taji ya fadhili na rehema, </q2>
<q1><vn>5 </vn>Aushibisha mema uzee wako, </q1>
<q2>Ujana wako ukarejezwa kama tai; </q2>
<q1><vn>6 </vn>
<nd>Bwana</nd> ndiye afanyaye mambo ya haki, </q1>
<q2>Na hukumu kwa wote wanaoonewa. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Alimjulisha Musa njia zake, </q1>
<q2>Wana wa Israeli matendo yake. </q2>
<q1><vn>8 </vn>
<nd>Bwana</nd> amejaa huruma na neema, </q1>
<q2>Haoni hasira upesi, ni mwingi wa fadhili. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>103:8</xo>
<xt>Kut 34:6; Hes 14:18; Kum 5:10; Yak 5:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Yeye hatateta sikuzote, </q1>
<q2>Wala hatashika hasira yake milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>103:9</xo>
<xt>Isa 57:16; Yer 3:5; Mik 7:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Hakututenda sawasawa na hatia zetu, </q1>
<q2>Wala hakutulipa kwa kadiri ya maovu yetu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>103:10</xo>
<xt>Ezr 9:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Maana mbingu zilivyoinuka juu ya nchi, </q1>
<q2>Kadiri ile ile rehema zake ni kuu kwa wamchao. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, </q1>
<q2>Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>103:12</xo>
<xt>Isa 43;25; Efe 1:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, </q1>
<q2>Ndivyo 
<nd>Bwana</nd> anavyowahurumia wamchao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>103:13</xo>
<xt>Kum 8:5; Isa 63:15, 16; Mal 3:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, </q1>
<q2>Na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Mwanadamu siku zake zi kama majani; </q1>
<q2>Kama ua la kondeni ndivyo asitawivyo. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Maana upepo hupita juu yake, kumbe haliko! </q1>
<q2>Na mahali pake hapatalijua tena. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Bali fadhili za 
<nd>Bwana</nd> zina wamchao </q1>
<q2>Tangu milele hata milele, </q2>
<q2>Na haki yake ina wana wa wana; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>103:17</xo>
<xt>Kut 20:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>Maana, wale walishikao agano lake, </q1>
<q2>Na kuyakumbuka maagizo yake ili wayafanye. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>103:18</xo>
<xt>Kum 7:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>
<nd>Bwana</nd> ameweka kiti chake cha enzi mbinguni, </q1>
<q2>Na ufalme wake unavitawala vitu vyote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>103:19</xo>
<xt>Zab 47:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Mhimidini 
<nd>Bwana</nd>, enyi malaika zake, </q1>
<q2>Ninyi mlio hodari, mtendao neno lake, </q2>
<q2>Mkiisikiliza sauti ya neno lake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>103:20</xo>
<xt>Mt 6:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Mhimidini 
<nd>Bwana</nd>, enyi majeshi yake yote, </q1>
<q2>Ninyi watumishi wake mfanyao mapenzi yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>103:21</xo>
<xt>Mwa 32:2; Dan 7:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>22 </vn>Mhimidini 
<nd>Bwana</nd>, enyi matendo yake yote, </q1>
<q2>Mahali pote pa milki yake. </q2>
<q2>Ee nafsi yangu, umhimidi 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>104</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee nafsi yangu, umhimidi 
<nd>Bwana</nd>. </q1>
<q2>Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wangu, </q2>
<q1>Umejifanya mkuu sana; </q1>
<q2>Umejivika heshima na adhama. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Umejivika nuru kama vazi; </q1>
<q2>Umezitandika mbingu kama pazia; </q2>
<q1><vn>3 </vn>Na kuziweka nguzo za orofa zake majini. </q1>
<q2>Huyafanya mawingu kuwa gari lake, </q2>
<q2>Na kwenda juu ya mabawa ya upepo, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:3</xo>
<xt>Amo 9:6; Isa 19:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Huwafanya malaika zake kuwa pepo, </q1>
<q2>Na watumishi wake kuwa moto wa miali. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:4</xo>
<xt>Ebr 1:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Uliiweka nchi juu ya misingi yake, </q1>
<q2>Isitikisike milele. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Uliifunika kwa vilindi kama kwa vazi, </q1>
<q2>Maji yalikuwa yakisimama juu ya milima. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Kwa kukemea kwako yakakimbia, </q1>
<q2>Kwa sauti ya radi yako yakaenda zake kasi, </q2>
<q1><vn>8 </vn>Yakapanda milima, yakatelemka mabondeni, </q1>
<q2>Mpaka mahali ulipoyatengenezea. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:8</xo>
<xt>Ayu 38:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Umeweka mpaka yasiupite, </q1>
<q2>Wala yasirudi kuifunikiza nchi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:9</xo>
<xt>Ayu 26:10; Zab 33:7; Yer 5:22; Mwa 9:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Hupeleka chemchemi katika mabonde; </q1>
<q2>Zapita kati ya milima; </q2>
<q1><vn>11 </vn>Zamnywesha kila mnyama wa kondeni; </q1>
<q2>Punda mwitu huzima kiu yao. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Kandokando hukaa ndege wa angani; </q1>
<q2>Kati ya matawi hutoa sauti zao. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Huinywesha milima toka orofa zake; </q1>
<q2>Nchi imeshiba mazao ya kazi zako. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Huyameesha majani kwa makundi, </q1>
<q2>Na maboga kwa matumizi ya mwanadamu; </q2>
<q2>Ili atoe chakula katika nchi, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:14</xo>
<xt>Mwa 1:29, 30; Zab 147:8; 136:25; Ayu 28:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Na divai imfurahishe mtu moyo wake. </q1>
<q2>Aung'aze uso wake kwa mafuta, </q2>
<q2>Na mkate umburudishe mtu moyo wake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:15</xo>
<xt>Amu 9:13; Mit 31:6,7; Mhu 10:19; yer 31:12; Mik 14:23; Yn 2:9, 10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Miti ya 
<nd>Bwana</nd> nayo imeshiba, </q1>
<q2>Mierezi ya Lebanoni aliyoipanda. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:16</xo>
<xt>Hes 24:6; Zab 29:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Ndimo ndege wafanyamo vitundu vyao, </q1>
<q2>Na korongo, misunobari ni nyumba yake. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Milima mirefu ndiko waliko mbuzi wa mwitu, </q1>
<q2>Na magenge ni kimbilio la wibari. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:18</xo>
<xt>Mith 30:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Aliufanya mwezi kwa ajili ya nyakati, </q1>
<q2>Jua latambua kuchwa kwake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:19</xo>
<xt>Mwan 1:14; Ayu 38:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Wewe hufanya giza, kukawa usiku, </q1>
<q2>Ndipo atambaapo kila mnyama wa mwitu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:20</xo>
<xt>Isa 45:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Wana-simba hunguruma wakitaka mawindo, </q1>
<q2>Ili kutafuta chakula chao kwa Mungu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:21</xo>
<xt>Ayu 38:39</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>22 </vn>Jua lachomoza, wanakwenda zao, </q1>
<q2>Na kujilaza mapangoni mwao. </q2>
<q1><vn>23 </vn>Mwanadamu atoka kwenda zake kazini, </q1>
<q2>Na kwenye utumishi wake mpaka jioni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:23</xo>
<xt>Mwan 3:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>24 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, jinsi yalivyo mengi matendo yako! </q1>
<q2>Kwa hekima umevifanya vyote pia. </q2>
<q2>Dunia imejaa mali zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:24</xo>
<xt>Mwa 1:20-22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>25 </vn>Bahari iko kule, kubwa na upana, </q1>
<q2>Ndimo mlimo viendavyo visivyohesabika, </q2>
<q2>Viumbe hai vidogo kwa vikubwa. </q2>
<q1><vn>26 </vn>Ndimo zipitamo merikebu, </q1>
<q2>Ndimo alimo lewiathani uliyemwumba acheze humo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:26</xo>
<xt>Ayu 41:1; Zab 74:14; Isa 27:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>27 </vn>Hao wote wanakungoja Wewe, </q1>
<q2>Uwape chakula chao kwa wakati wake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:27</xo>
<xt>Rum 11:36</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>28 </vn>Wewe huwapa, </q1>
<q2>Wao wanakiokota; </q2>
<q1>Wewe waukunjua mkono wako, </q1>
<q2>Wao wanashiba mema; </q2>
<q1><vn>29 </vn>Wewe wauficha uso wako, </q1>
<q2>Wao wanafadhaika; </q2>
<q1>Waiondoa pumzi yao, wanakufa, </q1>
<q2>Na kuyarudia mavumbi yao, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:29</xo>
<xt>Mhu 12:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>30 </vn>Waipeleka roho yako, wanaumbwa, </q1>
<q2>Nawe waufanya upya uso wa nchi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:15</xo>
<xt>Isa 32:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>31 </vn>Utukufu wa 
<nd>Bwana</nd> na udumu milele; </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> na ayafurahie matendo yake. </q2>
<q1><vn>32 </vn>Aitazama nchi, inatetemeka; </q1>
<q2>Aigusa milima, inatoka moshi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:32</xo>
<xt>Hab 3:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>33 </vn>Nitamwimbia 
<nd>Bwana</nd> maadamu ninaishi; </q1>
<q2>Nitamshangilia Mungu wangu nikiwa hai; </q2>
<q1><vn>34 </vn>Kutafakari kwangu na kuwe kutamu kwake; </q1>
<q2>Mimi nitamfurahia 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<q1><vn>35 </vn>Wenye dhambi waangamizwe katika nchi, </q1>
<q2>Watendao ubaya wasiwepo tena. </q2>
<q2>Ee nafsi yangu, umhimidi 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>104:35</xo>
<xt>Mit 2:22</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>105</cn>
<q1><vn>1 </vn>Haleluya.<f> <fn>i</fn><note>
<fr>105:1</fr>
<fq>Haleluya </fq>
<ft> maana yake ni, Msifuni </ft>
<nd>Bwana</nd>.</note></f> </q1>
<q2>Mshukuruni 
<nd>Bwana</nd>, liitieni jina lake, </q2>
<q2>Wajulisheni watu matendo yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:1</xo>
<xt>Isa 12:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi, </q1>
<q2>Zitafakarini ajabu zake zote. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Jisifuni kwa jina lake takatifu, </q1>
<q2>Na ufurahi moyo wao wamtafutao 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Mtakeni 
<nd>Bwana</nd> na nguvu zake, </q1>
<q2>Utafuteni uso wake sikuzote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:4</xo>
<xt>Zab 27:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Zikumbukeni ajabu zake alizozifanya, </q1>
<q2>Miujiza yake na hukumu za kinywa chake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:5</xo>
<xt>Kum 8:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Enyi wazao wa Ibrahimu, mtumishi wake; </q1>
<q2>Enyi wana wa Yakobo, wateule wake. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Yeye, 
<nd>Bwana</nd>, ndiye Mungu wetu; </q1>
<q2>Duniani mwote mna hukumu zake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:7</xo>
<xt>Isa 26:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Analikumbuka agano lake milele; </q1>
<q2>Neno lile aliloviamuru vizazi elfu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:8</xo>
<xt>Lk 1:72</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Agano alilofanya na Ibrahimu, </q1>
<q2>Na uapo wake kwa Isaka. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:9</xo>
<xt>Mwa 12:7; 17:8; 26:3.</xt></note></f> <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:9</xo>
<xt>Mwa 17:2; 22; 16; 26:3; Zab 111:5, 9; Dan 9:4; Lk 1:73; Ebr 6:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Alilomthibitishia Yakobo liwe amri, </q1>
<q2>Na Israeli liwe agano la milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:10-11</xo>
<xt>Mwa 28:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Akisema, Nitakupa wewe nchi ya Kanaani, </q1>
<q2>Iwe urithi wenu mliopimiwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:11</xo>
<xt>Mwa 15:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Walipokuwa watu wawezao kuhesabiwa, </q1>
<q2>Naam, watu wachache na wageni ndani yake, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:12</xo>
<xt>Mwa 34:30; Kum 7:7; Mwa 17:8; Ebr 11:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Wakatanga-tanga toka taifa hata taifa, </q1>
<q2>Toka ufalme mmoja hata kwa watu wengine. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Hakumwacha mtu awaonee, </q1>
<q2>Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:14-15</xo>
<xt>Mwa 12:17, 20:3-7, 35:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Akisema, Msiwaguse masihi<f> <fn>j</fn><note>
<fr>105:15</fr>
<ft> Au, mtiwa mafuta.</ft></note></f> wangu, </q1>
<q2>Wala msiwadhuru nabii zangu. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Akaiita njaa iijilie nchi, </q1>
<q2>Akakiharibu chakula chote walichokitegemea. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:16</xo>
<xt>Mwa 41:53-57; 2 Fal 8:1; Law 26:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Alimpeleka mtu mbele yao, </q1>
<q2>Yusufu aliuzwa utumwani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:17</xo>
<xt>Mwa 37:28; 45:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>Walimwumiza miguu yake kwa pingu, </q1>
<q2>Akatiwa katika minyororo ya chuma. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:18-19</xo>
<xt>Mwa 39:20--40:15,23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Hata wakati wa kuwadia neno lake, </q1>
<q2>Ahadi ya 
<nd>Bwana</nd> ilimjaribu. </q2>
<q1><vn>20 </vn>Mfalme alituma watu akamfungua, </q1>
<q2>Mkuu wa watu akamwachia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:20</xo>
<xt>Mwa 41:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Akamweka kuwa bwana wa nyumba yake, </q1>
<q2>Na mwenye amri juu ya mali zake zote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:21</xo>
<xt>Mwa 41:39-41</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>22 </vn>Awafunge masheki wake kama apendavyo, </q1>
<q2>Na kuwafundisha wazee wake hekima. </q2>
<q1><vn>23 </vn>Israeli naye akaingia Misri, </q1>
<q2>Yakobo akawa mgeni katika nchi ya Hamu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:23</xo>
<xt>Mwa 46:6; 47:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>24 </vn>Akawajalia watu wake wazae sana, </q1>
<q2>Akawafanya kuwa hodari kuliko watesi wao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:24-25</xo>
<xt>Kut 1:7-14; Kum 26:5; Mdo 7:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>25 </vn>Akawageuza moyo wawachukie watu wake, </q1>
<q2>Wakawatendea hila watumishi wake. </q2>
<q1><vn>26 </vn>Akamtuma Musa, mtumishi wake, </q1>
<q2>Na Haruni ambaye amemchagua. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:26</xo>
<xt>Kut 3:10--4:17; hes 16:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>27 </vn>Akaweka mambo ya ishara zake kati yao, </q1>
<q2>Na miujiza katika nchi ya Hamu. </q2>
<q1><vn>28 </vn>Alituma giza, kukafunga giza, </q1>
<q2>Wala hawakuyaasi maneno yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:28</xo>
<xt>Kut 10:21-23; Zab 99:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>29 </vn>Aliyageuza maji yao yakawa damu, </q1>
<q2>Akawafisha samaki wao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:29</xo>
<xt>Kut 7:17-21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>30 </vn>Nchi yao ilijaa vyura, </q1>
<q2>Vyumbani mwa wafalme wao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:30</xo>
<xt>Kut 8:1-6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>31 </vn>Alisema, kukaja makundi ya mainzi, </q1>
<q2>Na chawa mipakani mwao mwote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:31</xo>
<xt>Kut 8:16-17; 20-24</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>32 </vn>Badala ya mvua aliwapa mvua ya mawe, </q1>
<q2>Na moto wa miali katika nchi yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:32-33</xo>
<xt>Kut 9:22-25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>33 </vn>Akaipiga mizabibu yao na mitini yao, </q1>
<q2>Akaivunja miti ya mipaka yao. </q2>
<q1><vn>34 </vn>Alisema, kukaja nzige, </q1>
<q2>Na tunutu wasiohesabika; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:34-35</xo>
<xt>Kut 10:12-15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>35 </vn>Wakaila miche yote ya nchi yao, </q1>
<q2>Wakayala matunda ya ardhi yao. </q2>
<q1><vn>36 </vn>Akawapiga wazaliwa wa kwanza katika nchi, </q1>
<q2>Malimbuko ya nguvu zao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:36</xo>
<xt>Mwa 49:3; Kut 12:29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>37 </vn>Akawatoa hali wana fedha na dhahabu, </q1>
<q2>Katika kabila zao asiwepo mwenye kukwaa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:37-38</xo>
<xt>Kut 12:33-36</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>38 </vn>Misri ilifurahi walipoondoka, </q1>
<q2>Maana kwa ajili yao hofu imewaangukia. </q2>
<q1><vn>39 </vn>Alitandaza wingu liwe funiko, </q1>
<q2>Na moto utoe nuru usiku. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:39</xo>
<xt>Kut 13:21-22; Neh 9:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>40 </vn>Walipotaka akaleta kware, </q1>
<q2>Akawashibisha chakula cha mbinguni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:40</xo>
<xt>Kut 16:2-15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>41 </vn>Akaufunua mwamba, kukabubujika maji, </q1>
<q2>Yakapita pakavuni kama mto. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:41</xo>
<xt>Kut 17:1-7; Hes 20:2-13; Neh 9:15; Isa 48:21; 1 Kor 10:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>42 </vn>Maana alilikumbuka neno lake takatifu, </q1>
<q2>Na Ibrahimu, mtumishi wake. </q2>
<q1><vn>43 </vn>Akawatoa watu wake kwa shangwe, </q1>
<q2>Na wateule wake kwa nyimbo za furaha. </q2>
<q1><vn>44 </vn>Akawapa nchi za mataifa, wakairithi kazi ya watu; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:44</xo>
<xt>Kum 6:10; Yos 11:16-23, 13:7;</xt></note></f> </q1>
<q1><vn>45 </vn>Ili wazishike amri zake, na kuzitii sheria zake. </q1>
<q2>Haleluya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>105:45</xo>
<xt>Kum 4:1</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>106</cn>
<q1><vn>1 </vn>Haleluya. </q1>
<q1>Mshukuruni 
<nd>Bwana</nd> kwa kuwa ni mwema, </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:1</xo>
<xt>1 Nya 16:34; 2 Nya 5:13,7:3; Ezr 3:11; Zab 100:5 107:1; 118:1; 136:1; Isa 63:7; Yer 33:11; Mt 19:17;</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Nani awezaye kuyanena matendo makuu ya 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Kuzihubiri sifa zake zote? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:2</xo>
<xt>Zab 40:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Heri washikao hukumu, </q1>
<q2>Na kutenda haki sikuzote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:3</xo>
<xt>Yer 22:15,16; Mt 22:37; Zab 15:2; Mdo 24:16; Gal 6:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unikumbuke mimi, </q1>
<q2>Kwa kibali uliyo nayo kwa watu wako. </q2>
<q2>Unijilie kwa wokovu wako, </q2>
<q1><vn>5 </vn>Ili niuone wema wa wateule wako. </q1>
<q2>Nipate kuifurahia furaha ya taifa lako, </q2>
<q2>Na kujisifu pamoja na watu wako. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Tumetenda dhambi pamoja na baba zetu, </q1>
<q1>Tumetenda maovu, tumefanya ubaya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:6</xo>
<xt>Law 26:40; 1 Fal 8:47; Dan 9:5</xt></note></f> </q1>
<q1><vn>7 </vn>Baba zetu katika Misri </q1>
<q2>Hawakufikiri matendo yako ya ajabu; </q2>
<q1>Hawakukumbuka wingi wa fadhili zako; </q1>
<q2>Wakaasi penye bahari, bahari ya Shamu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:7</xo>
<xt>Kut 14:10-12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Lakini akawaokoa kwa ajili ya jina lake, </q1>
<q2>Ayadhihirishe matendo yake makuu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:8</xo>
<xt>Yosh 7,9; Zab 143:11; Yer 14:7,21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Akaikemea bahari ya Shamu ikakauka, </q1>
<q2>Akawaongoza vilindini kana kwamba ni uwanda. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:9-12</xo>
<xt>Kut 14:21-31; Nah 1:4; Isa 63:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Akawaokoa na mkono wa mtu aliyewachukia, </q1>
<q2>Na kuwakomboa na mkono wa adui zao. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Maji yakawafunika watesi wao, </q1>
<q2>Hakusalia hata mmoja wao. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Ndipo walipoyaamini maneno yake, </q1>
<q2>Waliziimba sifa zake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:12</xo>
<xt>Kut 15:1-21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Wakayasahau matendo yake kwa haraka, </q1>
<q2>Hawakulingojea shauri lake. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Bali walitamani sana jangwani, </q1>
<q2>Wakamjaribu Mungu nyikani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:14-15</xo>
<xt>Hes 11:4-34</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Akawapa walichomtaka, </q1>
<q2>Akawakondesha roho zao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:15</xo>
<xt>Isa 10:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Wakamhusudu Musa matuoni, </q1>
<q2>Na Haruni, mtakatifu wa 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:16-18</xo>
<xt>Hes 16:1-35</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Nchi ikapasuka ikammeza Dathani, </q1>
<q2>Ikaufunika mkutano wa Abiramu. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Moto ukawaka katika mkutano wao, </q1>
<q2>Miali yake ikawateketeza wabaya. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Walifanya ndama huko Horebu, </q1>
<q2>Wakaisujudia sanamu ya kuyeyuka. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:19-23</xo>
<xt>Kut 32:1-14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Wakaubadili utukufu wao </q1>
<q2>Kuwa mfano wa ng'ombe mla majani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:20</xo>
<xt>Yer 2:11; Rum 1:23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Wakamsahau Mungu, mwokozi wao, </q1>
<q2>Aliyetenda makuu katika Misri. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu, </q1>
<q2>Mambo ya kutisha penye bahari ya Shamu. </q2>
<q1><vn>23 </vn>Akasema ya kuwa atawaangamiza </q1>
<q2>Kama Musa, mteule wake, asingalisimama, </q2>
<q1>Mbele zake kama mahali palipobomoka, </q1>
<q2>Ili aigeuze hasira yake asije akawaharibu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:23</xo>
<xt>Kut 32:10; Kum 9:19; Eze 20:13, 13:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>24 </vn>Wakaidharau nchi ile ya kupendeza, </q1>
<q2>Wala hawakuliamini neno lake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:24-26</xo>
<xt>Hes 14:1-35</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>25 </vn>Bali wakanung'unika hemani mwao, </q1>
<q2>Wala hawakuisikiliza sauti ya 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<q1><vn>26 </vn>Ndipo alipowainulia mkono wake, </q1>
<q2>Ya kuwa atawaangamiza jangwani, </q2>
<q1><vn>27 </vn>Na kuwatawanya wazao wao kati ya mataifa, </q1>
<q2>Na kuwatapanya katika nchi mbali. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:27</xo>
<xt>Law 26:33</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>28 </vn>Wakajiambatiza na Baal-Peori, </q1>
<q2>Wakazila dhabihu za wafu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:28-31</xo>
<xt>Hes 25:1-13; Kum 4:3; Hos 9:10; Ufa 2:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>29 </vn>Wakamkasirisha kwa matendo yao; </q1>
<q2>Tauni ikawashambulia. </q2>
<q1><vn>30 </vn>Ndipo Finehasi akasimama akafanya hukumu; </q1>
<q2>Tauni ikazuiliwa. </q2>
<q1><vn>31 </vn>Akahesabiwa kuwa ana haki </q1>
<q2>Kizazi baada ya kizazi hata milele. </q2>
<q1><vn>32 </vn>Wakamghadhibisha penye maji ya Meriba, </q1>
<q2>Hasara ikampata Musa kwa ajili yao, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:32-33</xo>
<xt>Hes 20:2-13; Yak 3:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>33 </vn>Kwa sababu waliiasi roho yake, </q1>
<q2>Akasema yasiyofaa kwa midomo yake. </q2>
<q1><vn>34 </vn>Hawakuwaharibu watu wa nchi </q1>
<q2>Kama 
<nd>Bwana</nd> alivyowaambia; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:34-36</xo>
<xt>Amu 1:21; 2:1-3; 3:5-6; Kum 7:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>35 </vn>Bali walijichanganya na mataifa, </q1>
<q2>Wakajifunza matendo yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:35</xo>
<xt>Amu 3:5; Isa 2:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>36 </vn>Wakazitumikia sanamu zao, </q1>
<q2>Nazo zikawa mtego kwao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:36</xo>
<xt>Kut 23:33; Kum 7:10; Amu 2:12; 2 Falm 17:8-11; 2 Nya 33:2-7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>37 </vn>Naam, walitoa wana wao na binti zao </q1>
<q2>Kuwa dhabihu kwa mashetani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:37</xo>
<xt>Kum 12;30,31; Isa 57:5; Eze 16:20; 2 Fal 17:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>38 </vn>Wakamwaga damu isiyo na hatia, </q1>
<q2>Damu ya wana wao na binti zao, </q2>
<q1>Waliowatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani; </q1>
<q2>Nchi ikatiwa unajisi kwa damu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:38</xo>
<xt>Hes 35:33</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>39 </vn>Ndivyo walivyotiwa uchafu kwa kazi zao, </q1>
<q2>Wakafanya uasherati kwa matendo yao. </q2>
<q1><vn>40 </vn>Hasira ya 
<nd>Bwana</nd> ikawaka juu ya watu wake, </q1>
<q2>Akauchukia urithi wake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:40-46</xo>
<xt>Amu 2:14-18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>41 </vn>Akawatia mikononi mwa mataifa, </q1>
<q2>Nao waliowachukia wakawatawala. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:41</xo>
<xt>Amu 2:14; Neh 9:27</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>42 </vn>Adui zao wakawaonea, </q1>
<q2>Wakatiishwa chini ya mkono wao. </q2>
<q1><vn>43 </vn>Mara nyingi aliwaponya, </q1>
<q1>Bali walikuwa wakimwasi kwa mashauri yao, </q1>
<q2>Wakadhilika katika uovu wao. </q2>
<q1><vn>44 </vn>Lakini aliyaangalia mateso yao, </q1>
<q2>Aliposikia kilio chao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:44</xo>
<xt>Amu 10:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>45 </vn>Akawakumbukia agano lake; </q1>
<q2>Akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:44</xo>
<xt>Law 26:41; Omb 3:32</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>46 </vn>Akawajalia kuhurumiwa </q1>
<q2>Na watu wote waliowateka. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:46</xo>
<xt>Ezr 9:9; yer 42:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>47 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wetu, utuokoe, </q1>
<q2>Utukusanye kwa kututoa katika mataifa, </q2>
<q1>Tulishukuru jina lako takatifu, </q1>
<q2>Tuzifanyie shangwe sifa zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>106:47-48</xo>
<xt>1 Nya 16:35-36; Lk 1:74; 1 Kor 5:15</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>48 </vn>Na ahimidiwe 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wa Israeli, </q1>
<q2>Tangu milele hata milele. </q2>
<q1>Watu wote na waseme, Amina. </q1>
<q2>Haleluya. </q2>
<d>KITABU CHA TANO </d>
<b></b></c>

<c><cn>107</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mshukuruni 
<nd>Bwana</nd> kwa kuwa ni mwema, </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:1</xo>
<xt>1 Nya 16:34; 2 Nya 5:13; 7:3; Ezr 3:11; Zab 100:5; 106:1; 118:1; 136:1; Yer 33:11; Mat 19:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Na waseme hivi waliokombolewa na 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Wale aliowakomboa na mkono wa mtesi. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Akawakusanya kutoka nchi zote, </q1>
<q2>Mashariki na magharibi, kaskazini na kusini. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107;3</xo>
<xt>Zab 106:47; isa 49:12; Yer 29:14; Eze 39:27</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika; </q1>
<q2>Hawakuona mji wa kukaa. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Waliona njaa, waliona na kiu, </q1>
<q2>Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Wakamlilia 
<nd>Bwana</nd> katika dhiki zao, </q1>
<q2>Akawaponya na shida zao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:6</xo>
<xt>Zab 50:15; Isa 41:17; Yer 29:12-14; Hose 5:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Akawaongoza kwa njia ya kunyoka, </q1>
<q2>Wapate kwenda mpaka mji wa kukaa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:7</xo>
<xt>Ezr 8;21; Isa 63:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Na wamshukuru 
<nd>Bwana</nd>, kwa fadhili zake, </q1>
<q2>Na maajabu yake kwa wanadamu. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Maana hushibisha nafsi yenye shauku, </q1>
<q2>Na nafsi yenye njaa huijaza mema. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:9</xo>
<xt>Zab 34:10; isa 55:1; Mt 5:6; Lk 1:53</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Waliokaa katika giza na uvuli wa mauti, </q1>
<q2>Wamefungwa katika taabu na chuma, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:10</xo>
<xt>Ayu 36:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Kwa sababu waliyaasi maneno ya Mungu, </q1>
<q2>Wakalidharau shauri lake Aliye juu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:11</xo>
<xt>Omb 3:42; Zab 73:24; Lk 7;30; Mdo 20:27</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Hata akawadhili moyo kwa taabu, </q1>
<q2>Wakajikwaa wala hakuna msaidizi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:12</xo>
<xt>Isa 63:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Wakamlilia 
<nd>Bwana</nd> katika dhiki zao, </q1>
<q2>Akawaponya na shida zao. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Aliwatoa katika giza na uvuli wa mauti, </q1>
<q2>Akayavunja mafungo yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:14</xo>
<xt>Zab 146:7; Mdo 12:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Na wamshukuru 
<nd>Bwana</nd> kwa fadhili zake, </q1>
<q2>Na maajabu yake kwa wanadamu. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Maana ameivunja milango ya shaba, </q1>
<q2>Ameyakata mapingo ya chuma. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:16</xo>
<xt>Isa 45:2</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>17 </vn>Wapumbavu, kwa sababu ya ukosaji wao, </q1>
<q2>Na kwa sababu ya maovu yao, hujitesa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:17</xo>
<xt>Zab 14:1; Mit 1:22; Omb 3:39</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>Nafsi zao zachukia kila namna ya chakula, </q1>
<q2>Wameyakaribia malango ya mauti. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Wakamlilia 
<nd>Bwana</nd> katika dhiki zao, </q1>
<q2>Akawaponya na shida zao. </q2>
<q1><vn>20 </vn>Hulituma neno lake, huwaponya, </q1>
<q2>Huwatoa katika maangamizo yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:20</xo>
<xt>Hes 21:8; 2 Fal 20:4; Mt 8:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Na wamshukuru 
<nd>Bwana</nd> kwa fadhili zake, </q1>
<q2>Na maajabu yake kwa wanadamu. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Na wamtolee dhabihu za kushukuru, </q1>
<q2>Na kuyasimulia matendo yake kwa kuimba. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:22</xo>
<xt>Law 7:12; Zab 50:14; Ebr 13:15</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>23 </vn>Washukao baharini katika merikebu, </q1>
<q2>Wafanyao kazi yao katika maji mengi, </q2>
<q1><vn>24 </vn>Hao huziona kazi za 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Na maajabu yake vilindini. </q2>
<q1><vn>25 </vn>Maana husema, akavumisha upepo wa dhoruba, </q1>
<q2>Ukayainua juu mawimbi yake. </q2>
<q1><vn>26 </vn>Wapanda mbinguni, watelemka vilindini, </q1>
<q2>Nafsi yao yayeyuka kwa hali mbaya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:26</xo>
<xt>Zab 22:14; Isa 13:7; Nah 2;10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>27 </vn>Wayumba-yumba, wapepesuka kama mlevi, </q1>
<q2>Akili zao zote zawapotea. </q2>
<q1><vn>28 </vn>Wakamlilia 
<nd>Bwana</nd> katika dhiki zao, </q1>
<q2>Akawaponya na shida zao. </q2>
<q1><vn>29 </vn>Huituliza dhoruba, ikawa shwari, </q1>
<q2>Mawimbi yake yakanyamaza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:29</xo>
<xt>Zab 65:7; Isa 50:2; Mt 8:26; Mk 4:39-41</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>30 </vn>Ndipo walipofurahi kwa kuwa yametulia </q1>
<q2>Naye huwaleta mpaka bandari waliyoitamani. </q2>
<q1><vn>31 </vn>Na wamshukuru 
<nd>Bwana</nd> kwa fadhili zake, </q1>
<q2>Na maajabu yake kwa wanadamu. </q2>
<q1><vn>32 </vn>Na wamtukuze katika kusanyiko la watu, </q1>
<q2>Na wamhimidi katika baraza ya wazee. </q2>
<b></b>
<q1><vn>33 </vn>Amegeuza mito ikawa jangwa, </q1>
<q2>Na chemchemi za maji zikawa nchi ya kiu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:33</xo>
<xt>1 Fal 17:1; isa 34:9,10; Eze 30:12; Yoe 1:20; Nah 1:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>34 </vn>Nchi ya matunda mengi ikawa uwanda wa chumvi, </q1>
<q2>Kwa sababu ya ubaya wao walioikaa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:34</xo>
<xt>Mwa 13;10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>35 </vn>Amegeuza jangwa ikawa ziwa la maji, </q1>
<q2>Na nchi kavu ikawa chemchemi za maji. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:35</xo>
<xt>Isa 41:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>36 </vn>Maana amewakalisha huko wenye njaa, </q1>
<q2>Nao wametengeneza mji wa kukaa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:36</xo>
<xt>Mdo 17:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>37 </vn>Wakapanda mbegu katika mashamba, </q1>
<q2>Na kutia mizabibu iliyotoa matunda yake. </q2>
<q1><vn>38 </vn>Naye huwabariki wakaongezeka sana, </q1>
<q2>Wala hayapunguzi makundi yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:38</xo>
<xt>Mwa 12;2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>39 </vn>Kisha wakapungua na kudhilika, </q1>
<q2>Kwa kuonewa na mabaya na huzuni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:39</xo>
<xt>2 Fal 10:32; Ayu 12;21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>40 </vn>Akawamwagia wakuu dharau, </q1>
<q2>Na kuwazungusha katika nyika isiyo na njia. </q2>
<q1><vn>41 </vn>Akamweka mhitaji juu mbali na mateso, </q1>
<q2>Akamfanyia jamaa kama kundi la kondoo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:41</xo>
<xt>1 Sam 2:8; 2 Sam 7:8; Ayu 8:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>42 </vn>Wanyofu wa moyo wataona na kufurahi, </q1>
<q2>Na uovu wa kila namna utajifumba kinywa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:42</xo>
<xt>Ayu 22:19, 5:16; Mit 10:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>43 </vn>Aliye na hekima na ayaangalie hayo; </q1>
<q2>Na wazitafakari fadhili za 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>107:43</xo>
<xt>Yer 9;12; Dan 12;10</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>108</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu, moyo wangu u thabiti, </q1>
<q1>Nitaimba, nitaimba zaburi, </q1>
<q2>Naam, kwa utukufu wangu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Amka, kinanda na kinubi, </q1>
<q2>Nitaamka alfajiri. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, nitakushukuru kati ya watu, </q1>
<q2>Nitakuimbia zaburi kati ya mataifa. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Maana fadhili zako ni kubwa hata mbinguni, </q1>
<q2>Na uaminifu wako hata mawinguni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>108:4</xo>
<xt>Mik 7:18-20; Hes 14:18; Kum 7:9; Zab 36:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, </q1>
<q2>Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>108:5</xo>
<xt>Zab 57:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Ili wapenzi wako waopolewe, </q1>
<q2>Uokoe kwa mkono wako wa kuume, uniitikie. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Mungu amenena kwa utakatifu wake, </q1>
<q2>Nami nitashangilia. </q2>
<q1>Nitaigawanya Shekemu, </q1>
<q2>Nitalipima bonde la Sukothi. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Gileadi ni yangu, na Manase ni yangu, </q1>
<q2>Na Efraimu ni nguvu ya kichwa changu. </q2>
<q2>Yuda ni fimbo yangu ya kifalme, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>108:8</xo>
<xt>Mwa 49:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Moabu ni bakuli langu la kunawia. </q1>
<q2>Nitamtupia Edomu kiatu changu, </q2>
<q2>Na kumpigia Filisti kelele za vita. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Ni nani atakayenipeleka hata mji wenye boma? </q1>
<q2>Ni nani atakayeniongoza hata Edomu? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>108:10</xo>
<xt>Zab 60:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Ee Mungu, si Wewe uliyetutupa? </q1>
<q2>Wala, Ee Mungu, hutoki na majeshi yetu? </q2>
<q1><vn>12 </vn>Utuletee msaada juu ya mtesi, </q1>
<q2>Maana wokovu wa binadamu haufai. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Kwa msaada wa Mungu tutatenda makuu, </q1>
<q2>Maana Yeye atawakanyaga watesi wetu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:8</xo>
<xt>Isa 25:10, 30:3; Om 1:15; Mal 4:3; Mdo 1:20; ufu 14:19-20</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>109</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu wa sifa zangu, usinyamaze, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:1</xo>
<xt>Zab 83:1</xt></note></f> </q1>
<q1><vn>2 </vn>Kwa maana wamenifumbulia kinywa; </q1>
<q2>Kinywa cha mtu asiye haki, cha hila, </q2>
<q2>Wamesema nami kwa ulimi wa uongo. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Naam, kwa maneno ya chuki wamenizunguka, </q1>
<q2>Wamepigana nami bure. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:3</xo>
<xt>1 Sam 19:4,5; Zab 35:7,20; Yn 15:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Badala ya upendo wangu wao hunishitaki, </q1>
<q2>Ijapokuwa naliwaombea. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Wamenichukuza mabaya badala ya mema, </q1>
<q2>Na chuki badala ya upendo wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:5</xo>
<xt>Zab 38:20</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>6 </vn>Uweke mtu mkorofi juu yake, </q1>
<q2>Mshitaki asimame mkono wake wa kuume. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Katika kuhukumiwa ataonekana hana haki, </q1>
<q2>Na sala yake itadhaniwa kuwa ni dhambi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:7</xo>
<xt>Mit 28:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Siku zake na ziwe chache, </q1>
<q2>Usimamizi wake na atwae mtu mwingine. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:8</xo>
<xt>Mdo 1:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Wanawe na wawe yatima, </q1>
<q2>Na mkewe na awe mjane. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:9</xo>
<xt>Kut 22:24; Yer 18:21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Kutanga na watange wanawe na kuomba, </q1>
<q2>Watafute chakula mbali na mahame yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:10</xo>
<xt>Mwa 4:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Mdai na anase vitu vyote alivyo navyo, </q1>
<q2>Wageni na wateke mapato ya kazi yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:11</xo>
<xt>Ayu 18:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Asiwe na mtu wa kumfanyia fadhili, </q1>
<q2>Wala mtu wa kuwahurumia yatima wake. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Wazao wake waangamizwe, </q1>
<q2>Jina lao likafutwe katika kizazi cha pili. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:13</xo>
<xt>Zab 37:28; Mit 10:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Uovu wa baba zake ukumbukwe mbele za 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Na dhambi ya mamaye isifutwe. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:14</xo>
<xt>Kut 20:5; Neh 4:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Ziwe mbele za 
<nd>Bwana</nd> daima, </q1>
<q2>Aliondoe kumbukumbu lao duniani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:15</xo>
<xt>Ayu 18:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Kwa kuwa hakukumbuka kutenda fadhili, </q1>
<q2>Bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, </q2>
<q2>Hata akamfisha mtu aliyevunjika moyo, </q2>
<q1><vn>17 </vn>Naye alipenda kulaani, nako kukampata. </q1>
<q2>Hakupendezwa na kubariki, kukawa mbali naye, </q2>
<q1><vn>18 </vn>Alijivika laana kana kwamba ni vazi lake. </q1>
<q2>Ikamwingilia moyoni kama maji, </q2>
<q2>Na kama mafuta mifupani mwake. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Na iwe kwake kama vazi ajivikalo, </q1>
<q2>Na kama mshipi ajifungao daima. </q2>
<q1><vn>20 </vn>Ndiyo malipo ya washitaki wangu toka kwa 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Na ya hao wanaoisingizia nafsi yangu mabaya. </q2>
<b></b>
<q1><vn>21 </vn>Na Wewe, MUNGU, Bwana, unitendee kwa ajili ya jina lako, </q1>
<q2>Kwa kuwa fadhili zako ni njema uniokoe. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Kwa maana mimi ni mnyonge na mhitaji, </q1>
<q2>Na moyo wangu umejeruhi ndani yangu. </q2>
<q1><vn>23 </vn>Ninapita kama kivuli kianzacho kutoweka, </q1>
<q2>Ninapeperushwa kama nzige. </q2>
<q1><vn>24 </vn>Magoti yangu yamedhoofu kwa kufunga, </q1>
<q2>Na mwili wangu umekonda kwa kukosa mafuta. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:24</xo>
<xt>Ebr 12:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>25 </vn>Nami nalikuwa laumu kwao, </q1>
<q2>Wanionapo hutikisa vichwa vyao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:25</xo>
<xt>Isa 37:22; Mat 27:39; Mk 15:29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>26 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wangu, unisaidie, </q1>
<q2>Uniokoe sawasawa na fadhili zako. </q2>
<q1><vn>27 </vn>Nao wakajue ya kuwa ndio mkono wako; </q1>
<q2>Wewe, 
<nd>Bwana</nd>, umeyafanya hayo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:27</xo>
<xt>Ayu 37:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>28 </vn>Wao walaani, bali Wewe utabariki, </q1>
<q2>Wameondoka wao wakaaibishwa, </q2>
<q2>Bali mtumishi wako atafurahi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>109:28</xo>
<xt>Hes 22:12; Isa 65:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>29 </vn>Washitaki wangu watavikwa fedheha, </q1>
<q2>Watajivika aibu yao kama joho. </q2>
<q1><vn>30 </vn>Nitamshukuru 
<nd>Bwana</nd> kwa kinywa changu, </q1>
<q2>Naam, nitamsifu katikati ya mkutano. </q2>
<q1><vn>31 </vn>Maana atasimama mkono wa kuume wa mhitaji </q1>
<q2>Amwokoe na wanaoihukumu nafsi yake. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>110</cn>
<q1><vn>1 </vn>Neno la 
<nd>Bwana</nd> kwa Bwana wangu, </q1>
<q2>Uketi mkono wangu wa kuume, </q2>
<q1>Hata niwafanyapo adui zako </q1>
<q2>Kuwa chini ya miguu yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>110:1</xo>
<xt>Zab 45:6; Mat 22:44; Mk 12:36; Lk 20:42-43; 1 Kor 15:25; Mdo 2:34-35; 1 Kor 15:25; Efe 1:20-22; Kol 3:1; Ebr 1:13; 8:1; 10:12-13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>
<nd>Bwana</nd> atainyosha toka Sayuni </q1>
<q2>Fimbo ya nguvu zako. </q2>
<q2>Uwe na enzi kati ya adui zako; </q2>
<q1><vn>3 </vn>Watu wako wanajitoa kwa hiari, </q1>
<q2>Siku ya uwezo wako; </q2>
<q1>Kwa uzuri wa utakatifu, </q1>
<q2>Tokea tumbo la asubuhi, </q2>
<q2>Unao umande wa ujana wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>110:3</xo>
<xt>Amu 5:2; Zab 96:9; Mdo 2:41</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>
<nd>Bwana</nd> ameapa, </q1>
<q2>Wala hataghairi, </q2>
<q1>Ndiwe kuhani hata milele, </q1>
<q2>Kwa mfano wa Melkizedeki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>110:4</xo>
<xt>Hes 23:19; Zek 6:13; -Ebr 5:6; 6:20; 7:17,21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Bwana yu mkono wako wa kuume; </q1>
<q2>Ataseta wafalme, </q2>
<q2>Siku ya ghadhabu yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>110:5</xo>
<xt>Zab 16:8; 2:5; Rum 2:5; Ufu 11:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Atahukumu kati ya mataifa, </q1>
<q2>Ataijaza nchi mizoga; </q2>
<q2>Ataseta kichwa katika nchi nyingi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>110:6</xo>
<xt>Hab 3:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Atakunywa maji ya mto njiani; </q1>
<q2>Kwa hiyo atakiinua kichwa chake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>110:7</xo>
<xt>Isa 61:1; Yn 3:34; Isa 53:12</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>111</cn>
<q1><vn>1 </vn>Haleluya<f> <fn>k</fn><note>
<fr>111:1</fr>
<fq>Haleluya </fq>
<ft> maana yake ni, Msifuni </ft>
<nd>Bwana</nd>.</note></f>. </q1>
<q2>Nitamshukuru 
<nd>Bwana</nd> kwa moyo wangu wote, </q2>
<q2>Barazani pa wanyofu wa moyo na katika mkutano. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Matendo ya 
<nd>Bwana</nd> ni makuu, </q1>
<q2>Yafikiriwa sana na wapendezwao nayo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>111:2</xo>
<xt>Ayu 38:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Kazi yake ni heshima na adhama, </q1>
<q2>Na haki yake yakaa milele. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Amefanya ukumbusho wa matendo yake ya ajabu; </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> ni mwenye fadhili na rehema. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Amewapa wamchao chakula; </q1>
<q2>Atalikumbuka agano lake milele. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Amewajulisha watu wake uwezo wa matendo yake, </q1>
<q2>Kwa kuwapa urithi wa mataifa. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Matendo ya mikono yake ni kweli na hukumu, </q1>
<q2>Maagizo yake yote ni amini, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>111:7</xo>
<xt>Zab 19:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Yamethibitika milele na milele, </q1>
<q2>Yamefanywa katika kweli na adili. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>111:8</xo>
<xt>Ufu 15:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Amewapelekea watu wake ukombozi, </q1>
<q2>Ameamuru agano lake liwe la milele, </q2>
<q2>Jina lake ni takatifu la kuogopwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>111:8</xo>
<xt>Ufu 15:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Kumcha 
<nd>Bwana</nd> ndio mwanzo wa hekima, </q1>
<q2>Wote wafanyao hayo wana akili njema, </q2>
<q2>Sifa zake zakaa milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>111:10</xo>
<xt>Kum 4:6; Ayu 28:28; Mit 1:7; 9:10; Mhu 12;3</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>112</cn>
<q1><vn>1 </vn>Haleluya. </q1>
<q1>Heri mtu yule amchaye 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Apendezwaye sana na maagizo yake. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Wazao wake watakuwa hodari duniani; </q1>
<q2>Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Nyumbani mwake mna utajiri na mali, </q1>
<q2>Na haki yake yakaa milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>112:3</xo>
<xt>Mit 3:16, 15:6; Isa 33:6; Mt 6:33; 2 Kor 6:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Nuru huwazukia wenye adili gizani; </q1>
<q2>Ana fadhili na huruma na haki. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Heri atendaye fadhili na kukopesha; </q1>
<q2>Atengenezaye mambo yake kwa haki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>112:5</xo>
<xt>Lk 6:35</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Kwa maana hataondoshwa kamwe; </q1>
<q2>Mwenye haki atakumbukwa milele. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Hataogopa habari mbaya; </q1>
<q2>Moyo wake u imara ukimtumaini 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Moyo wake umethibitika hataogopa, </q1>
<q2>Hata awaone watesi wake wameshindwa. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Amekirimu, na kuwapa maskini, </q1>
<q2>Haki yake yakaa milele, </q2>
<q2>Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>112:9</xo>
<xt>Lk 11:41; Rum 12:13; Mdo 4:35; 20:35; 2 Kor 8:9; 9:9; 1 Tim 6:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Asiye haki ataona na kusikitika, </q1>
<q2>Atasaga meno yake na kuyeyuka, </q2>
<q2>Tamaa ya wasio haki itapotea. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>112:10</xo>
<xt>Lk 13;28</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>113</cn>
<q1><vn>1 </vn>Haleluya. </q1>
<q1>Enyi watumishi wa 
<nd>Bwana</nd>, sifuni, </q1>
<q2>Lisifuni jina la 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Jina la 
<nd>Bwana</nd> lihimidiwe </q1>
<q2>Tangu leo na hata milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>113:2</xo>
<xt>Dan 2:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Toka maawio ya jua hata machweo yake </q1>
<q2>Jina la 
<nd>Bwana</nd> husifiwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>113:3</xo>
<xt>Isa 59:19; Hab 2:14; Mal 1:11; Ufu 11:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>
<nd>Bwana</nd> ni mkuu juu ya mataifa yote, </q1>
<q2>Na utukufu wake ni juu ya mbingu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Ni nani aliye mfano wa 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Mungu wetu aketiye juu; </q2>
<q1><vn>6 </vn>Anyenyekeaye kutazama, </q1>
<q2>Mbinguni na duniani? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>113:6</xo>
<xt>Isa 57:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, </q1>
<q2>Na kumpandisha maskini kutoka jaani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>113:7</xo>
<xt>1 Sam 2:8; Isa 26:19; Dan 12:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Amketishe pamoja na wakuu, </q1>
<q2>Pamoja na wakuu wa watu wake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>113:8</xo>
<xt>Ayu 36:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Huweka nyumbani mwanamke aliye tasa, </q1>
<q2>Awe mama ya watoto mwenye furaha. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>113:9</xo>
<xt>1 Sam 2:5; Gal 4:27</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>114</cn>
<q1><vn>1 </vn>Haleluya. </q1>
<q1>Israeli alipotoka Misri, </q1>
<q2>Na Yakobo katika watu wa lugha ya kigeni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>114:1</xo>
<xt>Kut 12:51</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Yuda ilikuwa patakatifu pake, </q1>
<q2>Israeli milki yake. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Bahari iliona ikakimbia, </q1>
<q2>Yordani ilirudishwa nyuma. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>114:3</xo>
<xt>Kut 14:21; Yos 3:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Milima iliruka kama kondoo waume, </q1>
<q2>Vilima kama wana-kondoo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>114:4</xo>
<xt>Zab 29:6; 68:16; Hab 3:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Ee bahari, una nini, ukimbie? </q1>
<q2>Yordani, urudi nyuma? </q2>
<q1><vn>6 </vn>Enyi milima, mruke kama kondoo waume? </q1>
<q2>Enyi vilima, kama wana-kondoo? </q2>
<q1><vn>7 </vn>Tetemeka, Ee nchi, mbele za uso wa Bwana, </q1>
<q2>Mbele za uso wa Mungu wa Yakobo. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Augeuza mwamba kuwa ziwa la maji, </q1>
<q2>Jiwe gumu kuwa chemchemi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>114:8</xo>
<xt>Kut 17:1-7; Hes 20:2-13; Zab 107:35</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>115</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, kutukuza usitutukuze sisi, </q1>
<q2>Bali ulitukuze jina lako, </q2>
<q1>Kwa ajili ya fadhili zako, </q1>
<q2>Kwa ajili ya uaminifu wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>115:1</xo>
<xt>Isa 48:11; Eze 36:32</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kwa nini mataifa kusema, </q1>
<q2>Yuko wapi Mungu wao? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>115:2</xo>
<xt>Zab 42:3, 10; 79:10; Yoe 2:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Lakini Mungu wetu yuko mbinguni, </q1>
<q2>Alitakalo lote amelitenda. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>115:3</xo>
<xt>1 Nya 16:26, Zab 135:6; Dan 4:35</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Sanamu zao ni fedha na dhahabu, </q1>
<q2>Kazi ya mikono ya wanadamu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>115:4-8</xo>
<xt>Kum 4:28; Zab 135:15-18; isa 40:19; yer 20:3; Hos 8:6; 1 Kor 10:19, 20 Ufu 9:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Zina vinywa lakini hazisemi, </q1>
<q2>Zina macho lakini hazioni, </q2>
<q1><vn>6 </vn>Zina masikio lakini hazisikii, </q1>
<q2>Zina pua lakini hazisikii harufu, </q2>
<q1><vn>7 </vn>Mikono lakini hazishiki, miguu lakini haziendi, </q1>
<q2>Wala hazitoi sauti kwa koo zake. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Wazifanyao watafanana nazo, </q1>
<q2>Kila mmoja anayezitumainia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>115:8</xo>
<xt>Zab 135:18; Isa 44:9, 10; Yon 2:8; Hab 2:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Enyi Israeli, mtumainini 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Yeye ni msaada wao na ngao yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>115:9</xo>
<xt>Zab 33:20; Mit 30:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Enyi mlango wa Haruni, mtumainini 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Yeye ni msaada wao na ngao yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>115:10</xo>
<xt>Mal 2:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Enyi mmchao 
<nd>Bwana</nd>, mtumainini 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Yeye ni msaada wao na ngao yao. </q2>
<q1><vn>12 </vn>
<nd>Bwana</nd> ametukumbuka, </q1>
<q2>Naye atatubariki sisi. </q2>
<q1>Ataubariki mlango wa Israeli, </q1>
<q2>Ataubariki mlango wa Haruni, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>115:12</xo>
<xt>Efe 1:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Atawabariki wamchao 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Wadogo kwa wakubwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>115:13</xo>
<xt>Law 26:3; Kum 11:27; Zab 24:4; Mit 10:6; Ufu 11:18; 19:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>
<nd>Bwana</nd> na awaongeze ninyi, </q1>
<q2>Ninyi na watoto wenu. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Na mbarikiwe ninyi na 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Aliyezifanya mbingu na nchi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>115:15</xo>
<xt>Mwa 14:19; 1:1; Zab 96:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Mbingu ni mbingu za 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Bali nchi amewapa wanadamu. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Sio wafu wamsifuo 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Wala wo wote washukao kwenye kimya; </q2>
<q1><vn>18 </vn>Bali sisi tutamhimidi 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Tangu leo na hata milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>115:18</xo>
<xt>Zab 145:2; Dan 2:20</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>116</cn>
<q1><vn>1 </vn>Haleluya. </q1>
<q1>Nampenda 
<nd>Bwana</nd> kwa kuwa anaisikiliza </q1>
<q2>Sauti yangu na dua zangu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kwa maana amenitegea sikio lake, </q1>
<q2>Kwa hiyo nitamwita siku zangu zote. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Kamba za mauti zilinizunguka, </q1>
<q2>Shida za kuzimu zilinipata. </q2>
<q2>Naliona taabu na huzuni; </q2>
<q1><vn>4 </vn>Nikaliitia jina la 
<nd>Bwana</nd>. </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, nakuomba sana, </q2>
<q2>Uniokoe nafsi yangu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>
<nd>Bwana</nd> ni mwenye neema na haki, </q1>
<q2>Naam, Mungu wetu ni mwenye rehema. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>116:5</xo>
<xt>Ezr 9:15; Neh 9:8; Zab 11:7; Yer 12:1; Omb 1:18; Ufu 16:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>
<nd>Bwana</nd> huwalinda wasio na hila; </q1>
<q2>Nalidhilika, akaniokoa. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ee nafsi yangu, urudi rahani mwako, </q1>
<q2>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> amekutendea ukarimu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>116:7</xo>
<xt>Yer 6:16; Mt 11:29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Maana umeniponya nafsi yangu na mauti, </q1>
<q2>Macho yangu na machozi, </q2>
<q2>Na miguu yangu na kuanguka. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Nitaenenda mbele za 
<nd>Bwana</nd> </q1>
<q2>Katika nchi za walio hai. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Naliamini, kwa maana nitasema, </q1>
<q2>Mimi naliteswa sana. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>116:10</xo>
<xt>2 Kor 4:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Mimi nalisema kwa haraka yangu, </q1>
<q2>Wanadamu wote ni waongo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>116:11</xo>
<xt>2 Fal 4:16; Yer 9:5; Rum 3:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Nimrudishie 
<nd>Bwana</nd> nini </q1>
<q2>Kwa ukarimu wake wote alionitendea? </q2>
<q1><vn>13 </vn>Nitakipokea kikombe cha wokovu; </q1>
<q2>Na kulitangaza jina la 
<nd>Bwana</nd>; </q2>
<q1><vn>14 </vn>Nitaziondoa nadhiri zangu kwa 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Naam, mbele ya watu wake wote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>116:14</xo>
<xt>Zab 22:25; Yon 2:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Ina thamani machoni pa 
<nd>Bwana</nd> </q1>
<q2>Mauti ya wacha Mungu wake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>116:15</xo>
<xt>Ayu 5:26; Zab 72:14; Lk 16:22; Ufu 14:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, hakika mimi ni mtumishi wako, </q1>
<q2>Mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako, </q2>
<q2>Umevifungua vifungo vyangu. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Nitakutolea dhabihu ya kushukuru; </q1>
<q2>Na kulitangaza jina la 
<nd>Bwana</nd>; </q2>
<q1><vn>18 </vn>Nitaziondoa nadhiri zangu kwa 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Naam, mbele ya watu wake wote. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Katika nyua za nyumba ya 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Ndani yako, Ee Yerusalemu. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>117</cn>
<q1><vn>1 </vn>Haleluya. </q1>
<q1>Enyi mataifa yote, msifuni 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Enyi watu wote, mhimidini. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>117:1</xo>
<xt>Rum 15:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Maana fadhili zake kwetu sisi ni kuu, </q1>
<q2>Na uaminifu wa 
<nd>Bwana</nd> ni wa milele. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>118</cn>
<q1><vn>1 </vn>Haleluya. </q1>
<q1>Mshukuruni 
<nd>Bwana</nd> kwa kuwa ni mwema, </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:1</xo>
<xt>1 Nya 16:18,34; 2 Nya 5:13; 7:3; Ezr 3:11; Zab 100:5;106:1; 107:1; 136:1; Yer 33:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Israeli na aseme sasa, </q1>
<q2>Ya kwamba fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:2</xo>
<xt>Zab 115:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Mlango wa Haruni na waseme sasa, </q1>
<q2>Ya kwamba fadhili zake ni za milele. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Wamchao 
<nd>Bwana</nd> na waseme sasa, </q1>
<q2>Ya kwamba fadhili zake ni za milele. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Katika shida yangu nalimwita 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> akanijibu akaniweka panapo nafasi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:5</xo>
<xt>Zab 18:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>
<nd>Bwana</nd> yuko upande wangu, sitaogopa; </q1>
<q2>Mwanadamu atanitenda nini? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:6</xo>
<xt>Ebr 13:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>
<nd>Bwana</nd> yuko upande wangu, msaidizi wangu, </q1>
<q2>Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118;7</xo>
<xt>Zab 54:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ni heri kumkimbilia 
<nd>Bwana</nd> </q1>
<q2>Kuliko kuwatumainia wanadamu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:8</xo>
<xt>Zab 62:8; Isa 2:22; Yer 17:5,7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Ni heri kumkimbilia 
<nd>Bwana</nd>. </q1>
<q2>Kuliko kuwatumainia wakuu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:9</xo>
<xt>Zab 146:3, Isa 30:2,3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Mataifa yote walinizunguka; </q1>
<q2>Kwa jina la 
<nd>Bwana</nd> naliwakatilia mbali. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Walinizunguka, naam, walinizunguka; </q1>
<q2>Kwa jina la 
<nd>Bwana</nd> naliwakatilia mbali. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:11</xo>
<xt>Zab 88:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Walinizunguka kama nyuki, </q1>
<q2>Walizimika kama moto wa miibani; </q2>
<q2>Kwa jina la 
<nd>Bwana</nd> naliwakatilia mbali. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:12</xo>
<xt>Kum 1:44; Mhu 7:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Ulinisukuma sana ili nianguke; </q1>
<q2>Lakini 
<nd>Bwana</nd> akanisaidia. </q2>
<q1><vn>14 </vn>
<nd>Bwana</nd> ni nguvu zangu na wimbo wangu, </q1>
<q2>Naye amekuwa wokovu wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:14</xo>
<xt>Kut 15:2; Isa 12:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Sauti ya furaha na wokovu </q1>
<q2>Imo hemani mwao wenye haki; </q2>
<q2>Mkono wa kuume wa 
<nd>Bwana</nd> hutenda makuu. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Mkono wa kuume wa 
<nd>Bwana</nd> umetukuzwa; </q1>
<q2>Mkono wa kuume wa 
<nd>Bwana</nd> hutenda makuu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:16</xo>
<xt>Kut 15:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Sitakufa bali nitaishi, </q1>
<q2>Nami nitayasimulia matendo ya 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:17</xo>
<xt>Zab 6:5; 73:28</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>
<nd>Bwana</nd> ameniadhibu sana, </q1>
<q2>Lakini hakuniacha nife. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:18</xo>
<xt>Mit 3:11, 12; 1 Kor 11:32</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Nifungulieni malango ya haki, </q1>
<q2>Nitaingia na kumshukuru 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:19</xo>
<xt>Isa 26:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Lango hili ni la 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Wenye haki ndio watakaoliingia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:20</xo>
<xt>Zab 24:7; Isa 35:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Nitakushukuru kwa maana umenijibu, </q1>
<q2>Nawe umekuwa wokovu wangu. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Jiwe walilolikataa waashi </q1>
<q2>Limekuwa jiwe kuu la pembeni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:22</xo>
<xt>Mt 21;42; Mk 12:10; Lk 20:17; Mdo 4:11; Efe 2;20; 1 Pet 2:4,7</xt></note></f> <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:22-23</xo>
<xt>Mat 21:42; Mk 12:10-11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>23 </vn>Neno hili limetoka kwa 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Nalo ni ajabu machoni petu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:23</xo>
<xt>Ayu 5:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>24 </vn>Siku hii ndiyo aliyoifanya 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Tutashangilia na kuifurahia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:24</xo>
<xt>2 Kor 6:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>25 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, utuokoe, twakusihi; </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, utufanikishe, twakusihi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:25</xo>
<xt>Mat 21:9; Mk 11:9; Yn 12:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>26 </vn>Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Tumewabarikia toka nyumbani mwa 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:26</xo>
<xt>Zek 4:7; Mat 21:9; 23:39; Mk 11:9; Lk 13:35; 19:38; Yn 12:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>27 </vn>
<nd>Bwana</nd> ndiye aliye Mungu, </q1>
<q2>Naye ndiye aliyetupa nuru. </q2>
<q1>Ifungeni dhabihu kwa kamba </q1>
<q2>Pembeni mwa madhabahu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:27</xo>
<xt>Est 8:16; Mik 7:9; Mal 4:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>28 </vn>Ndiwe Mungu wangu, nami nitakushukuru, </q1>
<q2>Ndiwe Mungu wangu, nami nitakutukuza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>118:28</xo>
<xt>Kut 15:2; Isa 25:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>29 </vn>Mshukuruni 
<nd>Bwana</nd> kwa kuwa ni mwema, </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>119</cn>
<q1><vn>1 </vn>Heri walio kamili njia zao, </q1>
<q2>Waendao katika sheria ya 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:1</xo>
<xt>Zab 128:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Heri wazitiio shuhuda zake, </q1>
<q2>Wamtafutao kwa moyo wote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:2</xo>
<xt>Kum 4:29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Naam, hawakutenda ubatili, </q1>
<q2>Wamekwenda katika njia zake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:3</xo>
<xt>Rum 7:16,17; 1 yoh 3:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Wewe umetuamuru mausia yako, </q1>
<q2>Ili sisi tuyatii sana. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Ningependa njia zangu ziwe thabiti, </q1>
<q2>Nizitii amri zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:5</xo>
<xt>Yer 31:33; Rum 7:22,23; 2 Kor 3:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Ndipo mimi sitaaibika, </q1>
<q2>Nikiyaangalia maagizo yako yote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:6</xo>
<xt>Ayu 22:26; 1 Yoh 2:28</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Nitakushukuru kwa unyofu wa moyo, </q1>
<q2>Nikiisha kujifunza hukumu za haki yako </q2>
<q1><vn>8 </vn>Nitazitii amri zako, </q1>
<q2>Usiniache kabisa </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>9 </vn>Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? </q1>
<q2>Kwa kutii, akilifuata neno lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:9</xo>
<xt>Mit 1:4,10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Kwa moyo wangu wote nimekutafuta, </q1>
<q2>Usiniache nipotee mbali na maagizo yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:10</xo>
<xt>2 Nya 15:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, </q1>
<q2>Nisije nikakutenda dhambi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:11</xo>
<xt>Lk 2:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, umehimidiwa, </q1>
<q2>Unifundishe amri zako. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Kwa midomo yangu nimezisimulia </q1>
<q2>Hukumu zote za kinywa chako. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Nimeifurahia njia ya shuhuda zako </q1>
<q2>Kana kwamba ni mali mengi. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Nitayatafakari mausia yako, </q1>
<q2>Nami nitaziangalia njia zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:15</xo>
<xt>Zab 1:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Nitajifurahisha sana kwa amri zako, </q1>
<q2>Sitalisahau neno lako. </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>17 </vn>Umtendee mtumishi wako ukarimu, </q1>
<q2>Nipate kuishi, nami nitalitii neno lako. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Unifumbue macho yangu niyatazame </q1>
<q2>Maajabu yatokayo katika sheria yako. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Mimi ni mgeni katika nchi, </q1>
<q2>Usinifiche maagizo yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:19</xo>
<xt>Mwa 47:9; Ebr 11:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Roho yangu imepondeka kwa kutamani </q1>
<q2>Hukumu zako kila wakati. </q2>
<q1><vn>21 </vn>Umewakemea wenye kiburi, </q1>
<q2>Wamelaaniwa waendao mbali na maagizo yako. </q2>
<q1><vn>22 </vn>Uniondolee laumu na dharau, </q1>
<q2>Kwa maana nimezishika shuhuda zako. </q2>
<q1><vn>23 </vn>Wakuu nao waliketi wakaninena, </q1>
<q2>Lakini mtumishi wako atazitafakari amri zako. </q2>
<q1><vn>24 </vn>Shuhuda zako nazo ndizo furaha yangu, </q1>
<q2>Na washauri wangu. </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>25 </vn>Nafsi yangu imeambatana na mavumbi, </q1>
<q2>Unihuishe sawasawa na neno lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:25</xo>
<xt>Zab 143:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>26 </vn>Nalizisimulia njia zangu ukanijibu, </q1>
<q2>Unifundishe amri zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:26</xo>
<xt>1 Fal 8:36; Zab 27:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>27 </vn>Unifahamishe njia ya mausia yako, </q1>
<q2>Nami nitayatafakari maajabu yako. </q2>
<q1><vn>28 </vn>Nafsi yangu imeyeyuka kwa uzito, </q1>
<q2>Unitie nguvu sawasawa na neno lako. </q2>
<q1><vn>29 </vn>Uniondolee njia ya uongo, </q1>
<q2>Unineemeshe kwa sheria yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:29</xo>
<xt>Mit 30:8; Ebr 8:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>30 </vn>Nimeichagua njia ya uaminifu, </q1>
<q2>Na kuziweka hukumu zako mbele yangu. </q2>
<q1><vn>31 </vn>Nimeambatana na shuhuda zako, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, usiniaibishe. </q2>
<q1><vn>32 </vn>Nitakwenda mbio katika njia ya maagizo yako, </q1>
<q2>Utakaponikunjua moyo wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:32</xo>
<xt>1 Fal 4:29; Isa 60:5; 2 Kor 6:11</xt></note></f> </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>33 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unifundishe njia ya amri zako, </q1>
<q2>Nami nitaishika hata mwisho. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:33</xo>
<xt>Mt 10:22; Ufu 2;26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>34 </vn>Unifahamishe nami nitaishika sheria yako, </q1>
<q2>Naam, nitaitii kwa moyo wangu wote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:34</xo>
<xt>Mit 2:6; Yak 1:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>35 </vn>Uniendeshe katika mapito ya maagizo yako, </q1>
<q2>Kwa maana nimependezwa nayo. </q2>
<q1><vn>36 </vn>Unielekeze moyo wangu na shuhuda zako, </q1>
<q2>Wala usiielekee tamaa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:36</xo>
<xt>Eze 33:31; Mk 7:21; Lk 12:15; 1 Tim 6:10; Ebr 13:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>37 </vn>Unigeuze macho yangu nisitazame visivyofaa, </q1>
<q2>Unihuishe katika njia yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:37</xo>
<xt>Ayu 31:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>38 </vn>Umthibitishie mtumishi wako ahadi yako, </q1>
<q2>Inayohusu kicho chako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:38</xo>
<xt>2 Sam 7:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>39 </vn>Uniondolee laumu niiogopayo, </q1>
<q2>Maana hukumu zako ni njema. </q2>
<q1><vn>40 </vn>Tazama, nimeyatamani mausia yako, </q1>
<q2>Unihuishe kwa haki yako. </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>41 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, fadhili zako zinifikie na mimi, </q1>
<q2>Naam, wokovu wako sawasawa na ahadi yako. </q2>
<q1><vn>42 </vn>Nami nitamjibu neno anilaumuye, </q1>
<q2>Kwa maana nalitumainia neno lako. </q2>
<q1><vn>43 </vn>Usiliondoe neno la kweli kinywani mwangu kamwe, </q1>
<q2>Maana nimezingojea hukumu zako. </q2>
<q1><vn>44 </vn>Nami nitaitii sheria yako daima, </q1>
<q2>Naam, milele na milele. </q2>
<q1><vn>45 </vn>Nami nitakwenda panapo nafasi, </q1>
<q2>Kwa kuwa nimejifunza mausia yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:45</xo>
<xt>Yn 8:32,36; Rum 8:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>46 </vn>Nitazinena shuhuda zako mbele ya wafalme, </q1>
<q2>Wala sitaona aibu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:46</xo>
<xt>Mt 10:18; Mdo 26:1,2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>47 </vn>Nami nitajifurahisha sana kwa maagizo yako, </q1>
<q2>Ambayo nimeyapenda. </q2>
<q1><vn>48 </vn>Na mikono yangu nitayainulia maagizo yako niliyoyapenda, </q1>
<q2>Nami nitazitafakari amri zako. </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>49 </vn>Likumbuke neno ulilomwambia mtumishi wako, </q1>
<q2>Kwa sababu umenitumainisha. </q2>
<q1><vn>50 </vn>Hii ndiyo faraja yangu katika taabu yangu, </q1>
<q2>Ya kwamba ahadi yako imenihuisha. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:50</xo>
<xt>Zab 27:13; Yer 15:16; Rum 5:3-5; Ebr 1:17-19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>51 </vn>Wenye kiburi wamenidharau mno, </q1>
<q2>Sikujiepusha na sheria zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:51</xo>
<xt>Yer 20:7; Ayu 23:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>52 </vn>Nimezikumbuka hukumu zako za kale, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, nikajifariji. </q2>
<q1><vn>53 </vn>Ghadhabu imenishika kwa sababu ya wasio haki, </q1>
<q2>Waiachao sheria yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:53</xo>
<xt>Ezr 9:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>54 </vn>Amri zako zimekuwa nyimbo zangu, </q1>
<q2>Katika nyumba ya ugeni wangu. </q2>
<q1><vn>55 </vn>Wakati wa usiku nimelikumbuka jina lako, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, nikaitii sheria yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:55</xo>
<xt>Zab 63:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>56 </vn>Hayo ndiyo niliyokuwa nayo, </q1>
<q2>Kwa sababu nimeyashika mausia yako. </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>57 </vn>
<nd>Bwana</nd> ndiye aliye fungu langu, </q1>
<q2>Nimesema kwamba nitayatii maneno yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:57</xo>
<xt>Zab 16:5; Yer 10:16; Omb 3:24</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>58 </vn>Nimekuomba radhi kwa moyo wangu wote, </q1>
<q2>Unifadhili sawasawa na ahadi yako. </q2>
<q1><vn>59 </vn>Nalizitafakari njia zangu, </q1>
<q2>Na miguu yangu nalizielekezea shuhuda zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:59</xo>
<xt>Omb 3:40; Yoe 2:13; Lk 15:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>60 </vn>Nalifanya haraka wala sikukawia, </q1>
<q2>Kuyatii maagizo yako. </q2>
<q1><vn>61 </vn>Kamba za wasio haki zimenifunga, </q1>
<q2>Sikuisahau sheria yako. </q2>
<q1><vn>62 </vn>Katikati ya usiku nitaamka nikushukuru, </q1>
<q2>Kwa sababu ya hukumu zako za haki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:62</xo>
<xt>Mdo 16:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>63 </vn>Mimi ni mwenzao watu wote wakuchao, </q1>
<q2>Na wale wayatiio mausia yako. </q2>
<q1><vn>64 </vn>
<nd>Bwana</nd>, dunia imejaa fadhili zako, </q1>
<q2>Unifundishe amri zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:64</xo>
<xt>Zab 33:5</xt></note></f> </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>65 </vn>Umemtendea mema mtumishi wako, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, sawasawa na neno lako. </q2>
<q1><vn>66 </vn>Unifundishe akili na maarifa, </q1>
<q2>Maana nimeyaamini maagizo yako. </q2>
<q1><vn>67 </vn>Kabla sijateswa mimi nalipotea, </q1>
<q2>Lakini sasa nimelitii neno lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:67</xo>
<xt>Kum 32:15; Yer 31:18; Hos 5:15; Ebr 12:11; Ufu 3:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>68 </vn>Wewe U mwema na mtenda mema, </q1>
<q2>Unifundishe amri zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:68</xo>
<xt>Kut 34:6; Zab 107:1; Mt 19:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>69 </vn>Wenye kiburi wamenizulia uongo, </q1>
<q2>Kwa moyo wangu wote nitayashika mausia yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:69</xo>
<xt>Ayu 13:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>70 </vn>Mioyo yao imenenepa kama shahamu, </q1>
<q2>Mimi nimeifurahia sheria yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:70</xo>
<xt>Mdo 28:27</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>71 </vn>Ilikuwa vema kwangu kuwa naliteswa, </q1>
<q2>Nipate kujifunza amri zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:71</xo>
<xt>Ebr 12:10; Mit 8:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>72 </vn>Sheria ya kinywa chako ni njema kwangu, </q1>
<q2>Kuliko maelfu ya dhahabu na fedha. </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>73 </vn>Mikono yako ilinifanya ikanitengeneza, </q1>
<q2>Unifahamishe nikajifunze maagizo yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:73</xo>
<xt>Ayu 10:8; Zab 100:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>74 </vn>Wakuchao na wanione na kufurahi, </q1>
<q2>Kwa sababu nimelingojea neno lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:74</xo>
<xt>Zab 34:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>75 </vn>Najua ya kuwa hukumu zako ni za haki, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, na kwa uaminifu umenitesa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:75</xo>
<xt>Zab 89:30-33; Ebr 12:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>76 </vn>Nakuomba, fadhili zako ziwe faraja kwangu, </q1>
<q2>Sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako. </q2>
<q1><vn>77 </vn>Rehema zako zinijie nipate kuishi, </q1>
<q2>Maana sheria yako ni furaha yangu. </q2>
<q1><vn>78 </vn>Wenye kiburi waaibike, maana wamenidhulumu kwa uongo, </q1>
<q2>Mimi nitayatafakari mausia yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:78</xo>
<xt>Zab 25:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>79 </vn>Wakuchao na wanirudie, </q1>
<q2>Nao watazijua shuhuda zako. </q2>
<q1><vn>80 </vn>Moyo wangu na uwe mkamilifu katika amri zako, </q1>
<q2>Nisije mimi nikaaibika. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:80</xo>
<xt>2 Nya 15:7; Mit 4:23; Yn 1:47</xt></note></f> </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>81 </vn>Nafsi yangu imefifia kwa kuutamani wokovu wako, </q1>
<q2>Nimelingojea neno lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:81</xo>
<xt>Zab 42:1,2; 73:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>82 </vn>Macho yangu yamefifia kwa kuitazamia ahadi yako, </q1>
<q2>Nisemapo, Lini utakaponifariji? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:82</xo>
<xt>Zab 69:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>83 </vn>Maana nimekuwa kama kiriba katika moshi, </q1>
<q2>Sikuzisahau amri zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:83</xo>
<xt>Ayu 30:30</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>84 </vn>Siku za mtumishi wako ni ngapi, </q1>
<q2>Lini utakapowahukumu wale wanaonifuatia? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:84</xo>
<xt>Zab 39:4; 7:6; ufu 6:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>85 </vn>Wenye kiburi wamenichimbia mashimo, </q1>
<q2>Ambao hawaifuati sheria yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:85</xo>
<xt>Zab 35:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>86 </vn>Maagizo yako yote ni amini, </q1>
<q2>Wananifuatia bure, unisaidie. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:86</xo>
<xt>Zab 7:1-5; 35:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>87 </vn>Walikuwa karibu na kunikomesha katika nchi, </q1>
<q2>Lakini sikuyaacha mausia yako. </q2>
<q1><vn>88 </vn>Unihuishe kwa fadhili zako, </q1>
<q2>Nami nitazishika shuhuda za kinywa chako. </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>89 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, neno lako lasimama </q1>
<q2>Imara mbinguni hata milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:89</xo>
<xt>Mt 5:18; 1 Pet 1:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>90 </vn>Uaminifu wako upo kizazi baada ya kizazi, </q1>
<q2>Umeiweka nchi, nayo inakaa. </q2>
<q1><vn>91 </vn>Kwa hukumu zako vimesimama imara hata leo, </q1>
<q2>Maana vitu vyote ni watumishi wako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:91</xo>
<xt>Mwa 8:22; Zab 148:6; yer 33:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>92 </vn>Kama sheria yako isingalikuwa furaha yangu, </q1>
<q2>Hapo ningalipotea katika taabu zangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:92</xo>
<xt>Rum 15:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>93 </vn>Hata milele sitayasahau maagizo yako, </q1>
<q2>Maana kwa hayo umenihuisha. </q2>
<q1><vn>94 </vn>Mimi ni wako, uniokoe, </q1>
<q2>Kwa maana nimejifunza mausia yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:94</xo>
<xt>Hos 2:7, 16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>95 </vn>Wasio haki wameniotea ili kunipoteza, </q1>
<q2>Nitazitafakari shuhuda zako. </q2>
<q1><vn>96 </vn>Nimeona ukamilifu wote kuwa na mwisho, </q1>
<q2>Bali agizo lako ni pana mno. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:96</xo>
<xt>Isa 40:8; Mt 5:18</xt></note></f> </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>97 </vn>Sheria yako naipenda mno ajabu, </q1>
<q2>Ndiyo kutafakari kwangu mchana kutwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:97</xo>
<xt>Zab 1:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>98 </vn>Maagizo yako hunitia hekima kuliko adui zangu, </q1>
<q2>Kwa maana ninayo sikuzote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:98</xo>
<xt>Kum 4:6,8; Isa 48:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>99 </vn>Ninazo akili kuliko wakufunzi wangu wote, </q1>
<q2>Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:99</xo>
<xt>2 Tim 3:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>100 </vn>Ninao ufahamu kuliko wazee, </q1>
<q2>Kwa kuwa nimeyashika mausia yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:100</xo>
<xt>Ayu 12:12; 32:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>101 </vn>Nimeiepusha miguu yangu na kila njia mbaya, </q1>
<q2>Ili nilitii neno lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:101</xo>
<xt>2 Kor 7:1; Mit 1:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>102 </vn>Sikujiepusha na hukumu zako, </q1>
<q2>Maana Wewe mwenyewe umenifundisha. </q2>
<q1><vn>103 </vn>Mausia yako ni matamu sana kwangu, </q1>
<q2>Kupita asali kinywani mwangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:103</xo>
<xt>Zab 19:10; Mit 8:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>104 </vn>Kwa mausia yako najipatia ufahamu, </q1>
<q2>Ndiyo maana naichukia kila njia ya uongo. </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>105 </vn>Neno lako ni taa ya miguu yangu, </q1>
<q2>Na mwanga wa njia yangu. </q2>
<q1><vn>106 </vn>Nimeapa nami nitaifikiliza, </q1>
<q2>Kuzishika hukumu za haki yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:106</xo>
<xt>Neh 10:29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>107 </vn>Nimeteswa mno; </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unihuishe sawasawa na neno lako. </q2>
<q1><vn>108 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uziridhie sadaka za kinywa changu, </q1>
<q2>Na kunifundisha hukumu zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:108</xo>
<xt>Hose 14:2; Ebr 13:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>109 </vn>Nafsi yangu imo mkononi mwangu daima, </q1>
<q2>Lakini sheria yako sikuisahau. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:10-9</xo>
<xt>Amu 12:3; Ayu 13:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>110 </vn>Watendao uovu wamenitegea mtego, </q1>
<q2>Lakini sikuikosa njia ya mausia yako. </q2>
<q1><vn>111 </vn>Shuhuda zako nimezifanya urithi wa milele, </q1>
<q2>Maana ndizo changamko la moyo wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:111</xo>
<xt>Kum 33:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>112 </vn>Nimeuelekeza moyo wangu nizitende amri zako, </q1>
<q2>Daima, naam, hata milele. </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>113 </vn>Watu wa kusita-sita nawachukia, </q1>
<q2>Lakini sheria yako naipenda. </q2>
<q1><vn>114 </vn>Ndiwe sitara yangu na ngao yangu, </q1>
<q2>Neno lako nimelingojea. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:114</xo>
<xt>Zab 32:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>115 </vn>Enyi watenda mabaya, ondokeni kwangu, </q1>
<q2>Niyashike maagizo ya Mungu wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:115</xo>
<xt>Zab 6:8; Mt 7:23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>116 </vn>Unitegemeze sawasawa na ahadi yako, nikaishi, </q1>
<q2>Wala usiniache niyaaibikie matumaini yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:116</xo>
<xt>Zab 25:2; Rum 5:5; 9:33</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>117 </vn>Unisaidie nami nitakuwa salama, </q1>
<q2>Nami nitaziangalia amri zako daima. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:117</xo>
<xt>Zab 71:6; Yn 10:28; Rum 14:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>118 </vn>Umewakataa wote wazikosao amri zako, </q1>
<q2>Kwa maana hila zao ni uongo. </q2>
<q1><vn>119 </vn>Wabaya wa nchi pia umewaondoa kama takataka, </q1>
<q2>Ndiyo maana nimezipenda shuhuda zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:119</xo>
<xt>Eze 22:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>120 </vn>Mwili wangu unatetemeka kwa kukucha Wewe, </q1>
<q2>Nami ninaziogopa hukumu zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:120</xo>
<xt>Hab 3:16</xt></note></f> </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>121 </vn>Nimefanya hukumu na haki, </q1>
<q2>Usiniache mikononi mwao wanaonionea. </q2>
<q1><vn>122 </vn>Uwe mdhamini wa mtumishi wako, apate mema, </q1>
<q2>Wenye kiburi wasinionee. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:122</xo>
<xt>Ebr 7:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>123 </vn>Macho yangu yamefifia kwa kuutamani wokovu wako, </q1>
<q2>Na ahadi ya haki yako. </q2>
<q1><vn>124 </vn>Kama zilivyo rehema zako umtendee mtumishi wako, </q1>
<q2>Na amri zako unifundishe. </q2>
<q1><vn>125 </vn>Mimi ni mtumishi wako, unifahamishe, </q1>
<q2>Nipate kuzijua shuhuda zako. </q2>
<q1><vn>126 </vn>Wakati umewadia 
<nd>Bwana</nd> atende kazi; </q1>
<q2>Kwa kuwa wameitangua sheria yako. </q2>
<q1><vn>127 </vn>Ndiyo maana nimeyapenda maagizo yako, </q1>
<q2>Kuliko dhahabu, naam, dhahabu iliyo safi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:127</xo>
<xt>Zab 19:10; Efe 3;8; Mit 3:13,18; 8:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>128 </vn>Maana nayaona mausia yako yote kuwa ya adili, </q1>
<q2>Kila njia ya uongo naichukia. </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>129 </vn>Shuhuda zako ni za ajabu, </q1>
<q2>Ndiyo maana roho yangu imezishika. </q2>
<q1><vn>130 </vn>Kufafanusha maneno yako kwatia nuru, </q1>
<q2>Na kumfahamisha mjinga. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:130</xo>
<xt>Zab 19:11; Mit 1:4; 2 Pet 1:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>131 </vn>Nalifunua kinywa changu nikatweta, </q1>
<q2>Maana naliyatamani maagizo yako. </q2>
<q1><vn>132 </vn>Unigeukie, unirehemu mimi, </q1>
<q2>Kama iwahusuvyo walipendao jina lako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:132</xo>
<xt>Kut 4:31; 1 Sam 1:11; Zab 106:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>133 </vn>Uzielekeze hatua zangu kwa neno lako, </q1>
<q2>Uovu usije ukanimiliki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:133</xo>
<xt>Rum 6:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>134 </vn>Unikomboe na dhuluma ya mwanadamu, </q1>
<q2>Nipate kuyashika mausia yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:134</xo>
<xt>Lk 1:74</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>135 </vn>Umwangazie mtumishi wako uso wako, </q1>
<q2>Na kunifundisha amri zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:135</xo>
<xt>Zab 4:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>136 </vn>Macho yangu yachuruzika mito ya maji, </q1>
<q2>Kwa sababu hawaitii sheria yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:136</xo>
<xt>Yer 9:1</xt></note></f> </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>137 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, Wewe ndiwe mwenye haki, </q1>
<q2>Na hukumu zako ni za adili. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:137</xo>
<xt>Neh 9:33; Yer 12:1; Dan 9:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>138 </vn>Umeziagiza shuhuda zako kwa haki, </q1>
<q2>Na kwa uaminifu mwingi. </q2>
<q1><vn>139 </vn>Juhudi yangu imeniangamiza, </q1>
<q2>Maana watesi wangu wameyasahau maneno yako. </q2>
<q1><vn>140 </vn>Neno lako limesafika sana, </q1>
<q2>Kwa hiyo mtumishi wako amelipenda. </q2>
<q1><vn>141 </vn>Mimi ni mdogo, nadharauliwa, </q1>
<q2>Lakini siyasahau mausia yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:141</xo>
<xt>Mith 15:16; Amo 7:2; Lk 6:20; 2 Kor 8:9; Yak 2;5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>142 </vn>Haki yako ni haki ya milele, </q1>
<q2>Na sheria yako ni kweli. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:142</xo>
<xt>Zab 19;9; Yn 17:17; Efe 1:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>143 </vn>Taabu na dhiki zimenipata, </q1>
<q2>Maagizo yako ni furaha yangu. </q2>
<q1><vn>144 </vn>Haki ya shuhuda zako ni ya milele, </q1>
<q2>Unifahamishe, nami nitaishi. </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>145 </vn>Nimeita kwa moyo wangu wote; Ee 
<nd>Bwana</nd>, uitike; </q1>
<q2>Nitazishika amri zako. </q2>
<q1><vn>146 </vn>Nimekuita Wewe, uniokoe, </q1>
<q2>Nami nitazishika shuhuda zako. </q2>
<q1><vn>147 </vn>Kutangulia mapambazuko naliomba msaada, </q1>
<q2>Naliyangojea maneno yako kwa tumaini. </q2>
<q1><vn>148 </vn>Macho yangu yalitangulia makesha ya usiku, </q1>
<q2>Ili kuitafakari ahadi yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:148</xo>
<xt>Zab 63:1,6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>149 </vn>Uisikie sauti yangu sawasawa na fadhili zako, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unihuishe sawasawa na hukumu yako. </q2>
<q1><vn>150 </vn>Wanakaribia wanaonifuatia kwa chuki, </q1>
<q2>Wamekwenda mbali na sheria yako. </q2>
<q1><vn>151 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, Wewe U karibu, </q1>
<q2>Na maagizo yako yote ni kweli. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:151</xo>
<xt>Zab 145:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>152 </vn>Tokea zamani nimejua kwa shuhuda zako, </q1>
<q2>Ya kuwa umeziweka zikae milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:152</xo>
<xt>Lk 21:33</xt></note></f> </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>153 </vn>Uyaangalie mateso yangu, uniokoe, </q1>
<q2>Maana sikuisahau sheria yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:153</xo>
<xt>Omb 5:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>154 </vn>Unitetee na kunikomboa, </q1>
<q2>Unihuishe sawasawa na ahadi yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:154</xo>
<xt>1 Sam 24:15; Zab 35;1; Mik 7:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>155 </vn>Wokovu u mbali na wasio haki, </q1>
<q2>Kwa maana hawajifunzi amri zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:155</xo>
<xt>Ayu 5:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>156 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, rehema zako ni nyingi, </q1>
<q2>Unihuishe sawasawa na hukumu zako. </q2>
<q1><vn>157 </vn>Wanaonifuatia na watesi wangu ni wengi, </q1>
<q2>Lakini sikujiepusha na shuhuda zako. </q2>
<q1><vn>158 </vn>Nimewaona watendao uhaini nikachukizwa, </q1>
<q2>Kwa sababu hawakulitii neno lako. </q2>
<q1><vn>159 </vn>Uangalie niyapendavyo mausia yako, </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unihuishe sawasawa na fadhili zako. </q2>
<q1><vn>160 </vn>Jumla ya neno lako ni kweli, </q1>
<q2>Na kila hukumu ya haki yako ni ya milele. </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>161 </vn>Wakuu wameniudhi bure, </q1>
<q2>Ila moyo wangu unayahofia maneno yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:161</xo>
<xt>1 Sam 24:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>162 </vn>Naifurahia ahadi yako, </q1>
<q2>Kama apataye mateka mengi. </q2>
<q1><vn>163 </vn>Nimeuchukia uongo, umenikirihi, </q1>
<q2>Sheria yako nimeipenda. </q2>
<q1><vn>164 </vn>Mara saba kila siku nakusifu, </q1>
<q2>Kwa sababu ya hukumu za haki yako. </q2>
<q1><vn>165 </vn>Wana amani nyingi waipendao sheria yako, </q1>
<q2>Wala hawana la kuwakwaza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119;165</xo>
<xt>Mit 3:2; Isa 32:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>166 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, nimeungojea wokovu wako, </q1>
<q2>Na maagizo yako nimeyatenda. </q2>
<q1><vn>167 </vn>Nafsi yangu imezishika shuhuda zako, </q1>
<q2>Nami nazipenda mno. </q2>
<q1><vn>168 </vn>Nimeyashika mausia yako na shuhuda zako, </q1>
<q2>Maana njia zangu zote zi mbele zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119;168</xo>
<xt>Ayu 34:21; Mit 5:21</xt></note></f> </q2>
<s>* * * </s>
<q1><vn>169 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, kilio changu na kikukaribie, </q1>
<q2>Unifahamishe sawasawa na neno lako. </q2>
<q1><vn>170 </vn>Dua yangu na ifike mbele zako, </q1>
<q2>Uniponye sawasawa na ahadi yako. </q2>
<q1><vn>171 </vn>Midomo yangu na itoe sifa, </q1>
<q2>Kwa kuwa unanifundisha mausia yako. </q2>
<q1><vn>172 </vn>Ulimi wangu na uiimbe ahadi yako, </q1>
<q2>Maana maagizo yako yote ni ya haki. </q2>
<q1><vn>173 </vn>Mkono wako na uwe tayari kunisaidia, </q1>
<q2>Maana nimeyachagua mausia yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:173</xo>
<xt>Yos 24:22; Mit 1:29; Lk 10:42</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>174 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, nimeutamani wokovu wako, </q1>
<q2>Na sheria yako ndiyo furaha yangu. </q2>
<q1><vn>175 </vn>Nafsi yangu na iishi, ipate kukusifu, </q1>
<q2>Na hukumu zako zinisaidie. </q2>
<q1><vn>176 </vn>Nimetanga-tanga kama kondoo aliyepotea; </q1>
<q2>Umtafute mtumishi wako; </q2>
<q2>Kwa maana sikuyasahau maagizo yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>119:176</xo>
<xt>Isa 53:6; Mt 10:6; Lk 15:4; 1 pet 2:25; Eze 34:6; Mt 18:11</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>120</cn>
<q1><vn>1 </vn>Katika shida yangu nalimlilia 
<nd>Bwana</nd> </q1>
<q2>Naye akaniitikia. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uiponye nafsi yangu </q1>
<q2>Na midomo ya uongo na ulimi wa hila. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Akupe nini, akuzidishie nini, </q1>
<q2>Ewe ulimi wenye hila? </q2>
<q1><vn>4 </vn>Mishale ya mtu hodari iliyochongoka, </q1>
<q2>Pamoja na makaa ya mretemu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Ole wangu mimi! </q1>
<q2>Kwa kuwa nimekaa katika Mesheki; </q2>
<q1>Na kufanya maskani yangu </q1>
<q2>Katikati ya hema za Kedari. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>120:5</xo>
<xt>Mwa 10:2; 1 Sam 25:1; yer 49:28</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nafsi yangu imekaa siku nyingi, </q1>
<q2>Pamoja naye aichukiaye amani. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Mimi ni wa amani; </q1>
<q2>Bali ninenapo, wao huelekea vita. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>121</cn>
<q1><vn>1 </vn>Nitayainua macho yangu niitazame milima, </q1>
<q2>Msaada wangu utatoka wapi? </q2>
<q1><vn>2 </vn>Msaada wangu u katika 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Aliyezifanya mbingu na nchi. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Asiuache mguu wako usogezwe; </q1>
<q2>Asisinzie akulindaye; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>121:3</xo>
<xt>1 Sam 2:9; Isa 27:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, </q1>
<q2>Yeye aliye mlinzi wa Israeli. </q2>
<q1><vn>5 </vn>
<nd>Bwana</nd> ndiye mlinzi wako; </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> ni uvuli mkono wako wa kuume. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Jua halitakupiga mchana, </q1>
<q2>Wala mwezi wakati wa usiku. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>121:6</xo>
<xt>Isa 49:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>
<nd>Bwana</nd> atakulinda na mabaya yote, </q1>
<q2>Atakulinda nafsi yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>121:7</xo>
<xt>Ayu 5:19; Zab 91:9, 10; Mit 12;21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>
<nd>Bwana</nd> atakulinda utokapo na uingiapo, </q1>
<q2>Tangu sasa na hata milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>121:8</xo>
<xt>Kum 28:6; Mit 2:8</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>122</cn>
<q1><vn>1 </vn>Nalifurahi waliponiambia, </q1>
<q2>Na twende nyumbani kwa 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>122:1</xo>
<xt>Isa 2:3; Yer 31:6; Zek 8:21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Miguu yetu imesimama </q1>
<q2>Ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Ee Yerusalemu uliyejengwa </q1>
<q2>Kama mji ulioshikamana, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>122:3</xo>
<xt>2 Sam 5:9; Efe 2:21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Huko ndiko walikopanda kabila, </q1>
<q2>Kabila za 
<nd>Bwana</nd>; </q2>
<q1>Ushuhuda kwa Israeli, </q1>
<q2>Walishukuru jina la 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>122:4</xo>
<xt>Kum 16:16; Kut 16:34</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Maana huko viliwekwa viti vya hukumu, </q1>
<q2>Viti vya enzi vya mbari ya Daudi. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Utakieni Yerusalemu amani; </q1>
<q2>Na wafanikiwe wakupendao; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>122:6</xo>
<xt>Isa 62:6; yer 51:50</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Amani na ikae ndani ya kuta zako, </q1>
<q2>Na kufanikiwa ndani ya majumba yako. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu </q1>
<q2>Niseme sasa, Amani ikae nawe. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Kwa ajili ya nyumba ya 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wetu, </q1>
<q2>Nikutafutie mema. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>123</cn>
<q1><vn>1 </vn>Nimekuinulia macho yangu, </q1>
<q2>Wewe uketiye mbinguni. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kama vile macho ya watumishi </q1>
<q2>Kwa mkono wa bwana zao </q2>
<q1>Kama macho ya mjakazi </q1>
<q2>Kwa mkono wa bibi yake; </q2>
<q1>Hivyo macho yetu humwelekea 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wetu, </q1>
<q2>Hata atakapoturehemu. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Uturehemu, Ee 
<nd>Bwana</nd>, uturehemu sisi, </q1>
<q2>Kwa maana tumeshiba dharau. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Nafsi zetu zimeshiba mzaha wa wenye raha, </q1>
<q2>Na dharau ya wenye kiburi. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>124</cn>
<q1><vn>1 </vn>Kama si 
<nd>Bwana</nd> aliyekuwa pamoja nasi, </q1>
<q2>Israeli na aseme sasa, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>124:1</xo>
<xt>Mwa 15:1; Hes 14:9; Yos 1:5; Ebr 13:5; Rum 8:31</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kama si 
<nd>Bwana</nd> aliyekuwa pamoja nasi, </q1>
<q2>Wanadamu walipotushambulia. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Papo hapo wangalitumeza hai, </q1>
<q2>Hasira yao ilipowaka juu yetu <f> <fn>-</fn><note>
<xo>123:3</xo>
<xt>Zab 35:25; Mit 1:12; Yer 51:34</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Papo hapo maji yangalitugharikisha, </q1>
<q2>Mto ungalipita juu ya roho zetu; </q2>
<q1><vn>5 </vn>Papo hapo yangalipita juu ya nafsi zetu </q1>
<q2>Maji yafurikayo. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Na ahimidiwe 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Asiyetutoa kuwa mawindo kwa meno yao. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Nafsi yetu imeokoka kama ndege </q1>
<q2>Katika mtego wa wawindaji, </q2>
<q2>Mtego umevunjika, nasi tumeokoka. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Msaada wetu u katika jina la 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Aliyezifanya mbingu na nchi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>124:8</xo>
<xt>Kut 18:4; Zab 12:2; Mit 18:10; Isa 50:10; Ebr 13:6</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>125</cn>
<q1><vn>1 </vn>Wamtumainio 
<nd>Bwana</nd> ni kama mlima Sayuni, </q1>
<q2>Ambao hautatikisika, wakaa milele. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, </q1>
<q2>Ndivyo 
<nd>Bwana</nd> anavyowazunguka watu wake, </q2>
<q2>Tangu sasa na hata milele. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Kwa maana fimbo ya udhalimu </q1>
<q2>Haitakaa juu ya fungu la wenye haki; </q2>
<q1>Wenye haki wasije wakainyosha </q1>
<q2>Mikono yao kwenye upotovu. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uwatendee mema walio wema, </q1>
<q2>Nao walio wanyofu wa moyo. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Bali wao wanaozigeukia njia zao zilizopotoka, </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> atawaondoa pamoja na watenda maovu. </q2>
<q2>Amani ikae na Israeli. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>125:5</xo>
<xt>Mit 2:15; Isa 59:8; Filp 2:15; Gal 6:16</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>126</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd> alipowarejeza mateka wa Sayuni, </q1>
<q2>Tulikuwa kama waotao ndoto. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>126:1</xo>
<xt>Mdo 12:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko, </q1>
<q2>Na ulimi wetu kelele za furaha. </q2>
<q1>Ndipo waliposema katika mataifa, </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> amewatendea mambo makuu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>126:2</xo>
<xt>Ayu 8:21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>
<nd>Bwana</nd> alitutendea mambo makuu, </q1>
<q2>Tulikuwa tukifurahi. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uwarejeze watu wetu waliofungwa, </q1>
<q2>Kama vijito vya Kusini. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Wapandao kwa machozi </q1>
<q2>Watavuna kwa kelele za furaha. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>126:5</xo>
<xt>Isa 12:1-3; Yer 31:9; Yoe 2:17; Mt 5:4; 2 Kor 7:8-11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Ingawa mtu anakwenda zake akilia, </q1>
<q2>Azichukuapo mbegu za kupanda. </q2>
<q1>Hakika atarudi kwa kelele za furaha, </q1>
<q2>Aichukuapo miganda yake. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>127</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd> asipoijenga nyumba </q1>
<q2>Waijengao wafanya kazi bure. </q2>
<q1>
<nd>Bwana</nd> asipoulinda mji </q1>
<q2>Yeye aulindaye akesha bure. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kazi yenu ni bure, mnaoamka mapema, </q1>
<q2>Na kukawia kwenda kulala, </q2>
<q1>Na kula chakula cha taabu; </q1>
<q2>Yeye humpa mpenzi wake usingizi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>127:2</xo>
<xt>Mwa 3:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Tazama, wana ndio urithi wa 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Uzao wa tumbo ni thawabu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>127:3</xo>
<xt>Mwa 33:5; Kum 28:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Kama mishale mkononi mwa shujaa, </q1>
<q2>Ndivyo walivyo wana wa ujanani. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Heri mtu yule </q1>
<q2>Aliyelijaza podo lake hivyo. </q2>
<q1>Naam, hawataona aibu </q1>
<q2>Wanaposema na adui langoni. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>128</cn>
<q1><vn>1 </vn>Heri kila mtu amchaye 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Aendaye katika njia yake. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Taabu ya mikono yako hakika utaila; </q1>
<q2>Utakuwa heri, na kwako kwema. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>128:2</xo>
<xt>Isa3:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao, </q1>
<q2>Vyumbani mwa nyumba yako. </q2>
<q1>Wanao kama miche ya mizeituni </q1>
<q2>Wakiizunguka meza yako. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye 
<nd>Bwana</nd>. </q1>
<q1><vn>5 </vn>
<nd>Bwana</nd> akubariki toka Sayuni; </q1>
<q2>Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>128:5</xo>
<xt>Zab 134:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Naam, ukawaone wana wa wanao. </q1>
<q2>Amani ikae na Israeli. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>128:6</xo>
<xt>Mwa 50:23</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>129</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mara nyingi wamenitesa tangu ujana wangu, </q1>
<q2>Israeli na aseme sasa, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>129:1</xo>
<xt>Eze 23:3; Hos 2:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Mara nyingi wamenitesa tangu ujana wangu, </q1>
<q2>Lakini hawakuniweza. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Wakulima wamelima mgongoni mwangu, </q1>
<q2>Wamefanya mirefu mifuo yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>129:3</xo>
<xt>Ebr 11:36</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>
<nd>Bwana</nd> ndiye mwenye haki, </q1>
<q2>Amezikata kamba zao wasio haki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>129:4</xo>
<xt>2 The 1:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Na waaibishwe, warudishwe nyuma, </q1>
<q2>Wote wanaoichukia Sayuni. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Na wawe kama majani ya darini </q1>
<q2>Yanyaukayo kabla hayajamea. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>129:6</xo>
<xt>Zab 37:2; yer 17:5-6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ambayo mvunaji haujazi mkono wake, </q1>
<q2>Wala mfunga miganda kifua chake. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Wala hawasemi wapitao, Amani ya 
<nd>Bwana</nd> ikae nanyi, </q1>
<q2>Twawabariki kwa jina la 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>129:8</xo>
<xt>Rut 2:4; Zab 118:26</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>130</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, toka vilindini nimekulilia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>130:1</xo>
<xt>Omb 3:55; Yon 2:2</xt></note></f> </q1>
<q2><vn>2 </vn>Bwana, uisikie sauti yangu. </q2>
<q1>Masikio yako na yaisikilize </q1>
<q2>Sauti ya dua zangu. </q2>
<q1><vn>3 </vn>
<nd>Bwana</nd>, kama Wewe ungehesabu maovu, </q1>
<q2>Ee Bwana, nani angesimama? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>130:3</xo>
<xt>Zab 143:2; Yn 8:7-9; Rum 3:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Lakini kwako kuna msamaha, </q1>
<q2>Ili Wewe uogopwe. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>130:4</xo>
<xt>2 The 1:6; Zab 37:2; Yer 17:6; Kut 3:4:7; Efe 1:7; 1 Fal 8:40; Yer 33:8,9; Ebr 12:28</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Nimemngoja 
<nd>Bwana</nd>, roho yangu imengoja, </q1>
<q2>Na neno lake nimelitumainia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>130:5</xo>
<xt>Isa 26:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nafsi yangu inamngoja Bwana, </q1>
<q2>Kuliko walinzi waingojavyo asubuhi, </q2>
<q2>Naam, walinzi waingojao asubuhi. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ee Israeli, umtarajie 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Maana kwa 
<nd>Bwana</nd> kuna fadhili, </q2>
<q1>Na kwake kuna ukombozi mwingi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>130:7</xo>
<xt>Isa 55:7</xt></note></f> </q1>
<q2><vn>8 </vn>Yeye atamkomboa Israeli na maovu yake yote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>130:8</xo>
<xt>Mat 1:21; Tit 2:14</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>131</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd>, moyo wangu hauna kiburi, </q1>
<q2>Wala macho yangu hayainuki. </q2>
<q1>Wala sijishughulishi na mambo makuu, </q1>
<q2>Wala na mambo yashindayo nguvu zangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>131:1</xo>
<xt>Rum 12:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Hakika nimeituliza nafsi yangu, </q1>
<q2>Na kuinyamazisha. </q2>
<q1>Kama mtoto aliyeachishwa </q1>
<q2>Kifuani mwa mama yake; </q2>
<q1>Kama mtoto aliyeachishwa, </q1>
<q2>Ndivyo roho yangu ilivyo kwangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>131:2</xo>
<xt>Mt 18:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Ee Israeli, umtarajie 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Tangu leo na hata milele. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>132</cn>
<q1><vn>1 </vn>
<nd>Bwana</nd>, umkumbukie Daudi </q1>
<q2>Taabu zake zote alizotaabika. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ndiye aliyemwapia 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Akaweka nadhiri kwa Shujaa wa Yakobo. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Sitaingia hemani mwa nyumba yangu, </q1>
<q2>Wala sitapanda matandiko ya kitanda changu; </q2>
<q1><vn>4 </vn>Sitaacha macho yangu kuwa na usingizi, </q1>
<q2>Wala kope zangu kusinzia; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>132:4</xo>
<xt>Rut 3:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Hata nitakapompatia 
<nd>Bwana</nd> mahali, </q1>
<q2>Na Shujaa wa Yakobo maskani. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Tazama, tulisikia habari zake katika Efrata, </q1>
<q2>Katika konde la Yearimu tuliiona. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>132:6-10</xo>
<xt>Yos 18:1; 1 Nya 13:5; 2 Nya 6:41-42; 1 Sam 17:12; 7:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Na tuingie katika maskani yake, </q1>
<q2>Tusujudu penye kiti cha kuwekea miguu yake. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uinuke, uende kwenye raha yako, </q1>
<q2>Wewe na sanduku la nguvu zako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>132:8</xo>
<xt>Hes 10:35</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Makuhani wako na wavikwe haki, </q1>
<q2>Watauwa wako na washangilie. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>132:9</xo>
<xt>Ayu 29:14; Isa 61:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Kwa ajili ya Daudi, mtumishi wako, </q1>
<q2>Usiurudishe nyuma uso wa masihi<f> <fn>l</fn><note>
<fr>132:10</fr>
<ft> Au, mtiwa mafuta.</ft></note></f> wako. </q2>
<q1><vn>11 </vn>
<nd>Bwana</nd> amemwapia Daudi neno la kweli, </q1>
<q2>Hatarudi nyuma akalihalifu, </q2>
<q1>Baadhi ya wazao wa mwili wako </q1>
<q2>Nitawaweka katika kiti chako cha enzi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>132:11</xo>
<xt>1 Fal 8:25; 2 Sam 7:12-16; 1 Nya 6:16; 1 Nya 17:11-14; Zab 89:4-5; Lk 1:69; Mdo 2:30</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Wanao wakiyashika maagano yangu, </q1>
<q2>Na shuhuda nitakazowafundisha; </q2>
<q1>Watoto wao nao wataketi </q1>
<q2>Katika kiti chako cha enzi milele. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> ameichagua Sayuni, </q1>
<q2>Ameitamani akae ndani yake. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Hapo ndipo mahali pangu pa raha milele, </q1>
<q2>Hapo nitakaa kwa maana nimepatamani. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Hakika nitavibariki vyakula vyake </q1>
<q2>Wahitaji wake nitawashibisha chakula. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Na makuhani wake nitawavika wokovu, </q1>
<q2>Na watauwa wake watashangilia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>132:16</xo>
<xt>2 Nya 6:41; Hos 11:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Hapo nitamchipushia Daudi pembe, </q1>
<q2>Na taa nimemtengenezea masihi<f> <fn>m</fn><note>
<fr>132:17</fr>
<ft> Au, mtiwa mafuta.</ft></note></f> wangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>132:17</xo>
<xt>1 Fal 11:36; Zab 92:10; Eze 29:21; Lk 1:69</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>18 </vn>Adui zake nitawavika aibu, </q1>
<q2>Bali juu yake taji yake itasitawi. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>133</cn>
<q1><vn>1 </vn>Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, </q1>
<q2>Ndugu wakae pamoja, kwa umoja. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>133:1</xo>
<xt>Mwa 13;8; 1 Kor 1:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ni kama mafuta mazuri kichwani, </q1>
<q2>Yashukayo ndevuni, ndevu za Haruni, </q2>
<q2>Yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>133:2</xo>
<xt>Kut 30:25</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Kama umande wa Hermoni ushukao milimani pa Sayuni. </q1>
<q2>Maana ndiko 
<nd>Bwana</nd> alikoamuru baraka, </q2>
<q2>Naam, uzima hata milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>133:3</xo>
<xt>Kum 4:48; 28:8; Law 25:11; Dan 12:2,3; Mt 25:34, 46; Yn 4:14; 17:3; Ebr 7:25; 1 Yoh 5:20</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>134</cn>
<q1><vn>1 </vn>Tazama, enyi watumishi wa 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Mhimidini 
<nd>Bwana</nd>, nyote pia. </q2>
<q1>Ninyi mnaosimama usiku </q1>
<q2>Katika nyumba ya 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>134:1</xo>
<xt>Law 8:35; 1 Nya 9:33; Zab 130:6; Lk 2:37</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Painulieni patakatifu mikono yenu, </q1>
<q2>Na kumhimidi 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>134:2</xo>
<xt>Zab 28:2; 1 Tim 2:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>
<nd>Bwana</nd> akubariki toka Sayuni, </q1>
<q2>Aliyezifanya mbingu na nchi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>134:3</xo>
<xt>Zab 124:8; 128:5</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>135</cn>
<q1><vn>1 </vn>Haleluya. </q1>
<q1>Lisifuni jina la 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Enyi watumishi wa 
<nd>Bwana</nd>, sifuni. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Ninyi msimamao nyumbani mwa 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Nyuani mwa nyumba ya Mungu wenu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>135:2</xo>
<xt>Lk 2:37</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Msifuni 
<nd>Bwana</nd> kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> ni mwema, </q1>
<q2>Liimbieni jina lake kwa maana lapendeza. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Kwa sababu 
<nd>Bwana</nd> amejichagulia Yakobo, </q1>
<q2>Na Israeli, wawe watu wake hasa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>135:4</xo>
<xt>Kut 19:5; Kum 7:6,7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Maana najua mimi ya kuwa 
<nd>Bwana</nd> ni mkuu, </q1>
<q2>Na Bwana wetu yu juu ya miungu yote. </q2>
<q1><vn>6 </vn>
<nd>Bwana</nd> amefanya kila lililompendeza, </q1>
<q2>Katika mbingu na katika nchi, </q2>
<q2>Katika bahari na katika vilindi vyote. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ndiye apandishaye mvuke toka miisho ya nchi; </q1>
<q2>Huifanyia mvua umeme; </q2>
<q2>Hutoa upepo katika hazina zake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>135:7</xo>
<xt>Mwa 2:6; Ayu 5:10; Yer 10:13; Zek 10:1 Ayu 28:25; 38:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Aliwapiga wazaliwa wa kwanza wa Misri, </q1>
<q2>Wa wanadamu na wa wanyama. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Alipeleka ishara na maajabu kati yako, Ee Misri, </q1>
<q2>Juu ya Farao na watumishi wake wote. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Aliwapiga mataifa mengi, </q1>
<q2>Akawaua wafalme wenye nguvu; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>135:10</xo>
<xt>Hes 21:24</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Sihoni, mfalme wa Waamori, </q1>
<q2>Na Ogu, mfalme wa Bashani, </q2>
<q2>Na falme zote za Kanaani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>135:11</xo>
<xt>Yosh 12:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Akaitoa nchi yao iwe urithi, </q1>
<q2>Urithi wa Israeli watu wake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>135:12</xo>
<xt>Mwa 17:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, jina lako ni la milele, </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd>, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>135:13</xo>
<xt>Kut 3:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> atawaamua watu wake, </q1>
<q2>Atawahurumia watumishi wake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>135:14</xo>
<xt>Kum 32:36</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, </q1>
<q2>Kazi ya mikono ya wanadamu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>135:15-18</xo>
<xt>Zab 115:4-8; Ufu 9:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Zina vinywa lakini hazisemi, </q1>
<q2>Zina macho lakini hazioni, </q2>
<q1><vn>17 </vn>Zina masikio lakini hazisikii, </q1>
<q2>Wala hamna pumzi vinywani mwake. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Wazifanyao watafanana nazo, </q1>
<q2>Na kila mmoja anayezitumainia. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Enyi mlango wa Israeli, mhimidini 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Enyi mlango wa Haruni, mhimidini 
<nd>Bwana</nd>; </q2>
<q1><vn>20 </vn>Enyi mlango wa Lawi, mhimidini 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Ninyi mnaomcha 
<nd>Bwana</nd>, mhimidini 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<q1><vn>21 </vn>Na ahimidiwe 
<nd>Bwana</nd> toka Sayuni, </q1>
<q2>Akaaye Yerusalemu. </q2>
<q2>Haleluya. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>136</cn>
<q1><vn>1 </vn>Mshukuruni 
<nd>Bwana</nd> kwa kuwa ni mwema; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:1</xo>
<xt>1 Nya 16:34; 2 Nya 5:13; 7:3; Ezr 3:11; Zab 100:5; 106:1; 107:1; 118:1; Yer 33:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Mshukuruni Mungu wa miungu; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:2</xo>
<xt>Kut 18:11; Kum 10:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Mshukuruni Bwana wa mabwana; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:3</xo>
<xt>1 Tim 6:15; Ufu 17:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Yeye peke yake afanya maajabu makuu; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Yeye aliyefanya mbingu kwa fahamu zake; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:5</xo>
<xt>Mwa 1:1; Mit 3:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:6</xo>
<xt>Mwa 1:2; Yer 10:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Yeye aliyefanya mianga mikubwa; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:7-9</xo>
<xt>Mwa 1:16; Kum 4:19</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Jua litawale mchana; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Mwezi na nyota zitawale usiku; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wa kwanza wao; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:10</xo>
<xt>Kut 12:29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Akawatoa Waisraeli katikati yao; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:11</xo>
<xt>Kut 12:51</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:13-15</xo>
<xt>Zab 78:13; Kut 14:21-29</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Akawavusha Israeli katikati yake; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Yeye aliyewaongoza watu wake jangwani; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:16</xo>
<xt>Kum 8:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>17 </vn>Yeye aliyewapiga wafalme wakuu; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. </q2>
<q1><vn>18 </vn>Akawaua wafalme mashuhuri; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:18</xo>
<xt>Kum 29:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Sihoni, mfalme wa Waamori; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:19</xo>
<xt>Hes 21:21-30</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Na Ogu, mfalme wa Bashani; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:20</xo>
<xt>Hes 21:31-35</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Akaitoa nchi yao iwe urithi; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:21</xo>
<xt>Yosh 12:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>22 </vn>Urithi wa Israeli mtumishi wake; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. </q2>
<q1><vn>23 </vn>Aliyetukumbuka katika unyonge wetu; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:23</xo>
<xt>Mwa 8:1; Kum 32:36; Zab 102:17; Isa 63:9; Lk 1:48</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>24 </vn>Akatuokoa na watesi wetu; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. </q2>
<q1><vn>25 </vn>Kila chenye mwili akipa chakula chake; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>136:25</xo>
<xt>Zab 104:27</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>26 </vn>Mshukuruni Mungu wa mbingu; </q1>
<q2>Kwa maana fadhili zake ni za milele. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>137</cn>
<q1><vn>1 </vn>Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi, </q1>
<q2>Tukalia tulipoikumbuka Sayuni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>137:1</xo>
<xt>Eze 1:1; Dan 8:2; Isa 24:8; Omb 5:15; Amo 8:10; Ufu 18:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Katika miti iliyo katikati yake </q1>
<q2>Tulivitundika vinubi vyetu. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Maana huko waliotuchukua mateka </q1>
<q2>Walitaka tuwaimbie; </q2>
<q1>Na waliotuonea walitaka furaha; </q1>
<q2>Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Tuuimbeje wimbo wa 
<nd>Bwana</nd> </q1>
<q2>Katika nchi ya ugeni? </q2>
<q1><vn>5 </vn>Ee Yerusalemu, nikikusahau wewe, </q1>
<q2>Mkono wangu wa kuume na usahau. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Ulimi wangu na ugandamane </q1>
<q2>Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka. </q2>
<q1>Nisipoikuza Yerusalemu </q1>
<q2>Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>137:6</xo>
<xt>Eze 3:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uwakumbuke wana wa Edomu, </q1>
<q2>Siku ya Yerusalemu. </q2>
<q1>Waliosema, Bomoeni! </q1>
<q2>Bomoeni hata misingini! <f> <fn>-</fn><note>
<xo>137:7</xo>
<xt>Omb 4:22; Oba 1:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia, </q1>
<q2>Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>137:8</xo>
<xt>Isa 13;1; Ufu 18:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Heri yeye atakayewakamata wadogo wako, </q1>
<q2>Na kuwaseta wao juu ya mwamba. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>138</cn>
<q1><vn>1 </vn>Nitakushukuru kwa moyo wangu wote, </q1>
<q2>Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>138:1</xo>
<xt>Zab 119:46</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu, </q1>
<q2>Nitalishukuru jina lako, </q2>
<q1>Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako, </q1>
<q2>Kwa maana umeikuza ahadi yako, </q2>
<q2>Kuliko jina lako lote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>138:2</xo>
<xt>1 Fal 8:29; Zab 5:7; Dan 6:10; Yon 2:7; Isa 42:21</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Siku ile niliyokuita uliniitikia, </q1>
<q2>Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>138:3</xo>
<xt>2 Kor 12:9; Zek 10:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, wafalme wote wa dunia watakushukuru, </q1>
<q2>Watakapoyasikia maneno ya kinywa chako. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Naam, wataziimba njia za 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Kwa maana utukufu wa 
<nd>Bwana</nd> ni mkuu. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Ingawa 
<nd>Bwana</nd> yuko juu, amwona mnyenyekevu, </q1>
<q2>Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>138:6</xo>
<xt>Mit 3:34; Yak 4:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Nijapokwenda kati ya shida utanihuisha, </q1>
<q2>Utanyosha mkono juu ya hasira ya adui zangu, </q2>
<q2>Na mkono wako wa kuume utaniokoa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>138:7</xo>
<xt>Zab 23:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>
<nd>Bwana</nd> atanitimilizia mambo yangu; </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, fadhili zako ni za milele; </q2>
<q2>Usiziache kazi za mikono yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>138:8</xo>
<xt>Zab 57:2; Filp</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>139</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, umenichunguza na kunijua. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>139:1</xo>
<xt>Yer 12:3; Ufu 2:23</xt></note></f> </q1>
<q1><vn>2 </vn>Wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu; </q1>
<q2>Umelifahamu wazo langu tokea mbali. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>139:2</xo>
<xt>2 Fal 19:27; Mt 9:4; Yn 2:24</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu, </q1>
<q2>Umeelewa na njia zangu zote. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Maana hamna neno ulimini mwangu </q1>
<q2>Usilolijua kabisa, 
<nd>Bwana</nd>. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>139:4</xo>
<xt>Ebr 4:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Umenizingira nyuma na mbele, </q1>
<q2>Ukaniwekea mkono wako. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Maarifa hayo ni ya ajabu, yanishinda mimi, </q1>
<q2>Hayadirikiki, siwezi kuyafikia. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Niende wapi nijiepushe na roho yako? </q1>
<q2>Niende wapi niukimbie uso wako? </q2>
<q1><vn>8 </vn>Kama ningepanda mbinguni, Wewe uko; </q1>
<q2>Ningefanya kuzimu kitanda changu, Wewe uko. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>139:8</xo>
<xt>Mit 15:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Ningezitwaa mbawa za asubuhi, </q1>
<q2>Na kukaa pande za mwisho za bahari; </q2>
<q1><vn>10 </vn>Huko nako mkono wako utaniongoza, </q1>
<q2>Na mkono wako wa kuume utanishika. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Kama nikisema, Hakika giza litanifunika, </q1>
<q2>Na nuru inizungukayo ingekuwa usiku; </q2>
<q1><vn>12 </vn>Giza nalo halikufichi kitu, </q1>
<q2>Bali usiku huangaza kama mchana; </q2>
<q2>Giza na mwanga kwako ni sawasawa. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu, </q1>
<q2>Uliniunga tumboni mwa mama yangu. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa </q1>
<q2>Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha. </q2>
<q1>Matendo yako ni ya ajabu, </q1>
<q2>Na nafsi yangu yajua sana, </q2>
<q1><vn>15 </vn>Mifupa yangu haikusitirika kwako, </q1>
<q2>Nilipoumbwa kwa siri, </q2>
<q1>Nilipoungwa kwa ustadi pande za chini za nchi; </q1>
<q1><vn>16 </vn>Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; </q1>
<q2>Chuoni mwako ziliandikwa zote pia, </q2>
<q2>Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado. </q2>
<q1><vn>17 </vn>Mungu, fikira zako zina thamani nyingi kwangu; </q1>
<q2>Jinsi ilivyo kubwa jumla yake! </q2>
<q1><vn>18 </vn>Kama ningezihesabu ni nyingi kuliko mchanga; </q1>
<q2>Niamkapo nikali pamoja nawe. </q2>
<q1><vn>19 </vn>Ee Mungu, laiti ungewafisha waovu! </q1>
<q2>Enyi watu wa damu, ondokeni kwangu; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>139:19</xo>
<xt>Isa 11:4</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Kwa maana wakuasi kwa ubaya, </q1>
<q2>Adui zako wakutaja jina lako bure. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>139:20</xo>
<xt>Ayu 21:14, 15; Yud 1:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Je! 
<nd>Bwana</nd> nisiwachukie wanaokuchukia? </q1>
<q2>Nisikirihike nao wakuasio? </q2>
<q1><vn>22 </vn>Nawachukia kwa ukomo wa chuki, </q1>
<q2>Wamekuwa adui kwangu. </q2>
<q1><vn>23 </vn>Ee Mungu, unichunguze, uujue moyo wangu, </q1>
<q2>Unijaribu, uyajue mawazo yangu; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>139:23</xo>
<xt>Ayu 31:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>24 </vn>Uone kama iko njia iletayo majuto ndani yangu, </q1>
<q2>Ukaniongoze katika njia ya milele. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>139:24</xo>
<xt>Mt 7:14; Yn 14:6</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>140</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uniokoe na mtu mbaya, </q1>
<q2>Unihifadhi na mtu wa jeuri. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Waliowaza mabaya mioyoni mwao, </q1>
<q2>Kila siku huondokesha vita. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Wamenoa ndimi zao kama nyoka, </q1>
<q2>Sumu ya fira i chini ya midomo yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>140:3</xo>
<xt>Rum 3:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unilinde na mikono ya mtu asiye haki; </q1>
<q2>Unihifadhi na mtu wa jeuri; </q2>
<q2>Waliowaza kuzipotosha hatua zangu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Wenye kiburi wamenifichia mtego na kamba; </q1>
<q2>Wametandika wavu kando ya njia; </q2>
<q2>Wameniwekea matanzi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>140:5</xo>
<xt>Zab 10:9; Yer 18:22; Lk 11:53-54</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nimemwambia 
<nd>Bwana</nd>, Ndiwe Mungu wangu; </q1>
<q2>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uisikie sauti ya dua zangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>140:6</xo>
<xt>Zab 16:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ee MUNGU Bwana, nguvu za wokovu wangu, </q1>
<q2>Umenifunika kichwa changu siku ya vita. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>140:7</xo>
<xt>Kum 33:27-29; Zab 18:32</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, usimpe asiye haki tamaa zake, </q1>
<q2>Usiifanikishe hila yake, wasije wakajiinua. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>140:8</xo>
<xt>Ayu 5:12, 13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Nao wainuapo vichwa watu wanaonizunguka, </q1>
<q2>Madhara ya midomo yao yawafunike. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>140:9</xo>
<xt>Zab 7:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Makaa ya moto yawaangukie, watupwe motoni, </q1>
<q2>Na katika mashimo, wasipate kusimama tena. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>140:10</xo>
<xt>Zab 11:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Msingiziaji hatawekwa imara katika nchi, </q1>
<q2>Mtu wa jeuri, uovu humwinda kumwangamiza. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Najua ya kuwa 
<nd>Bwana</nd> atamfanyia mnyonge hukumu, </q1>
<q2>Na wahitaji haki yao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>140:12</xo>
<xt>Zab 109:31</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>13 </vn>Hakika wenye haki watalishukuru jina lako, </q1>
<q2>Wenye adili watakaa mahali ulipo Wewe. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>141</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, nimekuita, unijie hima, </q1>
<q2>Uisikie sauti yangu nikuitapo. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba, </q1>
<q2>Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>141:2</xo>
<xt>Efe 5:2; 1 Tim 2:8; Ufu 5:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uweke mlinzi kinywani pangu, </q1>
<q2>Mngojezi mlangoni pa midomo yangu. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Usiuelekeze moyo wangu kunako jambo baya, </q1>
<q2>Nisiyazoelee matendo yasiyofaa, </q2>
<q1>Pamoja na watu watendao maovu; </q1>
<q2>Wala nisile vyakula vyao vya anasa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>141:4</xo>
<xt>Mt 6:14; 20:15; Mit 23;6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili; </q1>
<q2>Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani; </q2>
<q1>Kichwa changu kisikatae, </q1>
<q2>Maana siachi kusali kati ya mabaya yao. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Makadhi wao wakiangushwa kando ya genge, </q1>
<q2>Watayasikia maneno yangu, maana ni matamu. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Kama kupasua kuni na kuzichanja juu ya nchi, </q1>
<q2>Ndivyo ilivyo mifupa yetu mdomoni pa kuzimu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>141:7</xo>
<xt>2 Kor 1:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Macho yangu yanakuelekea Wewe, MUNGU Bwana, </q1>
<q2>Nimekukimbilia Wewe, usiniache nafsi yangu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>141:8</xo>
<xt>Zab 25:15</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Unilinde na mtego walionitegea, </q1>
<q2>Na matanzi yao watendao maovu. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Wabaya na waanguke katika nyavu zao wenyewe, </q1>
<q2>Pindi mimi ninapopita salama. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>141:10</xo>
<xt>Est 7:10; Zab 7:15</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>142</cn>
<q1><vn>1 </vn>Kwa sauti yangu nitamlilia 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Kwa sauti yangu nitamwomba 
<nd>Bwana</nd> dua. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>142:1</xo>
<xt>1 Sam 22:1; 24:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Nitafunua mbele zake malalamiko yangu, </q1>
<q2>Shida yangu nitaitangaza mbele zake. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Nilipozimia roho uliyajua mapito yangu; </q1>
<q2>Katika njia niendayo wamenifichia mtego. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Utazame mkono wa kuume ukaone, </q1>
<q2>Kwa maana sina mtu anijuaye. </q2>
<q1>Makimbilio yamenipotea, </q1>
<q2>Hakuna wa kunitunza roho. </q2>
<q1><vn>5 </vn>
<nd>Bwana</nd>, nimekuita nikasema, Ndiwe kimbilio langu, </q1>
<q2>Fungu langu katika nchi ya walio hai. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>142:5</xo>
<xt>Omb 3:24</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Ukisikilize kilio changu, </q1>
<q2>Kwa maana nimedhilika sana. </q2>
<q1>Uniponye nao wanaonifuatia, </q1>
<q2>Kwa maana wao ni hodari kuliko mimi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>142:6</xo>
<xt>Zab 116:6; 7:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Uitoe nafsi yangu kifungoni. </q1>
<q2>Nipate kulishukuru jina lako. </q2>
<q1>Wenye haki watanizunguka, </q1>
<q2>Kwa kuwa Wewe unanikirimu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>142:7</xo>
<xt>Zab 34:2; 119:17</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>143</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uisikie sala yangu, uzisikilize dua zangu, </q1>
<q2>Kwa uaminifu wako unijibu kwa haki yako. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Wala usimhukumu mtumishi wako, </q1>
<q2>Maana kwako hakuna aliye hai mwenye haki. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>143:2</xo>
<xt>Ayu 14:3; 4:17; Mhu 7:20; Rum 3:20; Gal 2:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Maana adui ameifuatia nafsi yangu, </q1>
<q2>Ameutupa chini uzima wangu. </q2>
<q1>Amenikalisha mahali penye giza, </q1>
<q2>Kama watu waliokufa zamani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>143:3</xo>
<xt>Zab 7:1-2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Na roho yangu imezimia ndani yangu, </q1>
<q2>Moyo wangu ndani yangu umesituka. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>143:4</xo>
<xt>Zab 61:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Nimezikumbuka siku za kale, </q1>
<q2>Nimeyatafakari matendo yako yote, </q2>
<q2>Naziwaza kazi za mikono yako. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>143:5</xo>
<xt>Zab 77:5, 11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Nakunyoshea mikono yangu; </q1>
<q2>Nafsi yangu inakuonea kiu kama nchi kame. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>143:6</xo>
<xt>Zab 28:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unijibu hima, roho yangu imelegea; </q1>
<q2>Usinifiche uso wako, </q2>
<q2>Nisifanane nao washukao shimoni </q2>
<q1><vn>8 </vn>Unifanye kusikia fadhili zako asubuhi, </q1>
<q2>Kwa maana nimekutumaini Wewe. </q2>
<q1>Unijulishe njia nitakayoiendea, </q1>
<q2>Kwa maana nakuinulia nafsi yangu. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, uniponye na adui zangu; </q1>
<q2>Nimekukimbilia Wewe, unifiche. </q2>
<q1><vn>10 </vn>Unifundishe kuyatenda mapenzi yako, </q1>
<q2>Kwa maana ndiwe Mungu wangu; </q2>
<q2>Roho yako mwema aniongoze kwenye nchi sawa, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>143:10</xo>
<xt>Zab 25:4; Yn 14:26; Rum 5:5; Efe 4:30; Gal 5:22-23</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, unihuishe kwa ajili ya jina lako, </q1>
<q2>Kwa haki yako unitoe roho yangu taabuni; </q2>
<q1><vn>12 </vn>Kwa fadhili zako utawakatilia mbali adui zangu; </q1>
<q2>Na kuwaangamiza wote wanitesao nafsi, </q2>
<q2>Kwa maana mimi ni mtumishi wako. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>144</cn>
<q1><vn>1 </vn>Na ahimidiwe 
<nd>Bwana</nd>, mwamba wangu, </q1>
<q2>Anifundishaye mikono yangu vita, </q2>
<q2>Vidole vyangu kupigana. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>144:1</xo>
<xt>2 Sam 22;35</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Mhisani wangu na boma langu, </q1>
<q2>Ngome yangu na mwokozi wangu, </q2>
<q1>Ngao yangu niliyemkimbilia, </q1>
<q2>Huwatiisha watu wangu chini yangu. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, mtu ni kitu gani hata umjue? </q1>
<q2>Na binadamu hata umwangalie? <f> <fn>-</fn><note>
<xo>144:3</xo>
<xt>Ayu 7:17-18; Zab 8:4; Ebr 2:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Binadamu amefanana na ubatili, </q1>
<q2>Siku zake ni kama kivuli kipitacho. </q2>
<q1><vn>5 </vn>
<nd>Bwana</nd>, uziinamishe mbingu zako, ushuke, </q1>
<q2>Uiguse milima nayo itatoka moshi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>144:5</xo>
<xt>Isa 64:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Utupe umeme, uwatawanye, </q1>
<q2>Uipige mishale yako, uwafadhaishe. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Uinyoshe mikono yako toka juu, uniponye, </q1>
<q2>Unitoe katika maji mengi, katika mkono wa wageni. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>144:7</xo>
<xt>Zab 69:1; Mal 2:11</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Vinywa vyao vyasema visivyofaa, </q1>
<q2>Na mkono wao wa kuume ni mkono wa uongo. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya, </q1>
<q2>Kwa kinanda chenye nyuzi kumi nitakuimbia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>144:9</xo>
<xt>Zab 33;2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Awapaye wafalme wokovu, </q1>
<q2>Amwokoa Daudi, mtumishi wake, na upanga wa uovu. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Uniponye, unitoe, </q1>
<q2>Katika mkono wa wageni. </q2>
<q1>Vinywa vyao vyasema visivyofaa, </q1>
<q2>Na mkono wao wa kuume ni mkono wa uongo. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Wana wetu na wawe kama miche </q1>
<q2>Waliokua ujanani. </q2>
<q1>Binti zetu kama nguzo za pembeni </q1>
<q2>Zilizonakishwa kwa kupamba hekalu. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Ghala zetu na zijae </q1>
<q2>Zenye akiba za jinsi zote. </q2>
<q1>Kondoo zetu na wazae </q1>
<q2>Elfu na makumi elfu mashambani mwetu. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Ng'ombe zetu na wachukue mizigo, </q1>
<q2>Kusiwe na kushambuliwa. </q2>
<q1>Wala kusiwe na kuhamishwa, </q1>
<q2>Wala malalamiko katika njia zetu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>144:14</xo>
<xt>Law 26:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>15 </vn>Heri watu wenye hali hiyo, </q1>
<q2>Heri watu wenye 
<nd>Bwana</nd> kuwa Mungu wao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>144:15</xo>
<xt>Kum 33:29</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>145</cn>
<q1><vn>1 </vn>Ee Mungu wangu, Mfalme, nitakutukuza, </q1>
<q2>Nitalihimidi jina lako milele na milele. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Kila siku nitakuhimidi, </q1>
<q2>Nitalisifu jina lako milele na milele. </q2>
<q1><vn>3 </vn>
<nd>Bwana</nd> ndiye mkuu mwenye kusifiwa sana, </q1>
<q2>Wala ukuu wake hautambulikani. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Kizazi kwa kizazi kitayasifu matendo yako, </q1>
<q2>Kitayatangaza matendo yako makuu. </q2>
<q1><vn>5 </vn>Nitaifikiri fahari ya utukufu wa adhama yako, </q1>
<q2>Na matendo yako yote ya ajabu. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Watu watayataja matendo yako ya kutisha, </q1>
<q2>Nami nitausimulia ukuu wako. </q2>
<q1><vn>7 </vn>Watalihubiri kumbukumbu la wema wako mkuu. </q1>
<q2>Wataiimba haki yako. </q2>
<q1><vn>8 </vn>
<nd>Bwana</nd> ana fadhili, ni mwingi wa huruma, </q1>
<q2>Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>145:8</xo>
<xt>Kut 34:6; Hes 14:18; Zab 86:5, 15; 57:10; Omb 3:22, 23; Yn 1:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>
<nd>Bwana</nd> ni mwema kwa watu wote, </q1>
<q2>Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>145:9</xo>
<xt>Zab 100:5; Nah 1:7; Mt 5:45; Mdo 14:17</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Ee 
<nd>Bwana</nd>, kazi zako zote zitakushukuru, </q1>
<q2>Na wacha Mungu wako watakuhimidi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>145:10</xo>
<xt>Zab 19:1</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>Wataunena utukufu wa ufalme wako, </q1>
<q2>Na kuuhadithia uweza wako. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Ili kuwajulisha watu matendo yake makuu, </q1>
<q2>Na utukufu wa fahari ya ufalme wake. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Ufalme wako ni ufalme wa zamani zote, </q1>
<q2>Na mamlaka yako ni ya vizazi vyote. </q2>
<q1><vn>14 </vn>
<nd>Bwana</nd> huwategemeza wote waangukao, </q1>
<q2>Huwainua wote walioinama chini. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Macho ya watu wote yakuelekea Wewe, </q1>
<q2>Nawe huwapa chakula chao wakati wake. </q2>
<q1><vn>16 </vn>Waufumbua mkono wako, </q1>
<q2>Wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake. </q2>
<q1><vn>17 </vn>
<nd>Bwana</nd> ni mwenye haki katika njia zake zote, </q1>
<q2>Na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote. </q2>
<q1><vn>18 </vn>
<nd>Bwana</nd> yu karibu na wote wamwitao, </q1>
<q2>Wote wamwitao kwa uaminifu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>145:18</xo>
<xt>Zab 91:1; Isa 61:10; Yn 14:23; Yak 4:8; 1 Yoh 2:24; Yud 1:23; Ufu 3:20; Yn 4:24</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>19 </vn>Atawafanyia wamchao matakwa yao, </q1>
<q2>Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>145:19</xo>
<xt>1 Yoh 5:14</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>
<nd>Bwana</nd> huwahifadhi wote wampendao, </q1>
<q2>Na wote wasio haki atawaangamiza. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>145:20</xo>
<xt>1 Pet 1:5</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>21 </vn>Kinywa changu kitazinena sifa za 
<nd>Bwana</nd>; </q1>
<q2>Wote wenye mwili na walihimidi jina lake takatifu </q2>
<q2>milele na milele. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>146</cn>
<q1><vn>1 </vn>Haleluya.<f> <fn>n</fn><note>
<fr>146:1</fr>
<fq>Haleluya </fq>
<ft> maana yake ni, Msifuni </ft>
<nd>Bwana</nd>.</note></f> </q1>
<q2>Ee nafsi yangu, umsifu 
<nd>Bwana</nd>. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Nitamsifu 
<nd>Bwana</nd> muda ninaoishi, </q1>
<q2>Nitamwimbia Mungu wangu ningali ni hai. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Msiwatumainie wakuu, </q1>
<q2>Wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>146:3</xo>
<xt>Isa 2:22</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake, </q1>
<q2>Siku hiyo mawazo yake yapotea. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>146:4</xo>
<xt>Mhu 12:7; 1 Kor 2:6</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Heri ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, </q1>
<q2>Na tumaini lake ni kwa 
<nd>Bwana</nd>, Mungu wake, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>146:5</xo>
<xt>Yer 17:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Aliyezifanya mbingu na nchi, </q1>
<q2>Bahari na vitu vyote vilivyomo. </q2>
<q2>Huishika kweli milele, <f> <fn>-</fn><note>
<xo>146:6</xo>
<xt>Mik 7:20; Mdo 4:24; 14:15; Ufu 14:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Huwafanyia hukumu walioonewa, </q1>
<q2>Huwapa wenye njaa chakula; </q2>
<q2>
<nd>Bwana</nd> hufungua waliofungwa; </q2>
<q1><vn>8 </vn>
<nd>Bwana</nd> huwafumbua macho waliopofuka; </q1>
<q2>
<nd>Bwana</nd> huwainua walioinama; </q2>
<q2>
<nd>Bwana</nd> huwapenda wenye haki; </q2>
<q1><vn>9 </vn>
<nd>Bwana</nd> huwahifadhi wageni; </q1>
<q2>Huwategemeza yatima na mjane; </q2>
<q2>Bali njia ya wasio haki huipotosha. </q2>
<q1><vn>10 </vn>
<nd>Bwana</nd> atamiliki milele, </q1>
<q2>Mungu wako, Ee Sayuni, kizazi hata kizazi. </q2>
<q2>Haleluya. </q2>
<b></b></c>

<c><cn>147</cn>
<q1><vn>1 </vn>Haleluya. </q1>
<q2>Msifuni Bwana; </q2>
<q1>Maana ni vema kumwimbia Mungu wetu, </q1>
<q2>Maana kwapendeza, kusifu ni kuzuri. </q2>
<q1><vn>2 </vn>
<nd>Bwana</nd> ndiye aijengaye Yerusalemu, </q1>
<q2>Huwakusanya waliotawanyika wa Israeli. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>147:2</xo>
<xt>Kum 30;3; Isa 27:13; Yer 32:37; Eze 36:24</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Huwaponya waliopondeka moyo, </q1>
<q2>Na kuziganga jeraha zao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>147:3</xo>
<xt>Isa 61:1; Lk 4:18</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>4 </vn>Huihesabu idadi ya nyota, </q1>
<q2>Huzipa zote majina. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>147:4</xo>
<xt>Mwa 15:5; Isa 40:26</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Bwana wetu ni mkuu na mwingi wa nguvu, </q1>
<q2>Akili zake hazina mpaka. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>147:5</xo>
<xt>1 Nya 16:25; Nah 1:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>
<nd>Bwana</nd> huwategemeza wenye upole, </q1>
<q2>Huwaangusha chini wenye jeuri. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>147:6</xo>
<xt>Zab 146:8</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Mwimbieni 
<nd>Bwana</nd> kwa kushukuru, </q1>
<q2>Mwimbieni Mungu wetu kwa kinubi. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>147:7</xo>
<xt>Efe 5:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Huzifunika mbingu kwa mawingu, </q1>
<q2>Huitengenezea nchi mvua, </q2>
<q2>Na kuyameesha majani milimani. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>147:8</xo>
<xt>Ayu 38:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>9 </vn>Humpa mnyama chakula chake, </q1>
<q2>Wana-kunguru waliao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>147:9</xo>
<xt>Ayu 38:41; Mt 6:26; Lk 12:24</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Hapendezwi na nguvu za farasi, </q1>
<q2>Wala hairidhii miguu ya mtu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>147:10</xo>
<xt>Hos 1:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>11 </vn>
<nd>Bwana</nd> huwaridhia wao wamchao, </q1>
<q2>Na kuzitarajia fadhili zake. </q2>
<q1><vn>12 </vn>Msifu 
<nd>Bwana</nd>, Ee Yerusalemu; </q1>
<q2>Msifu Mungu wako, Ee Sayuni. </q2>
<q1><vn>13 </vn>Maana ameyakaza mapingo ya malango yako, </q1>
<q2>Amewabariki wanao ndani yako. </q2>
<q1><vn>14 </vn>Ndiye afanyaye amani mipakani mwako, </q1>
<q2>Akushibishaye kwa unono wa ngano. </q2>
<q1><vn>15 </vn>Huipeleka amri yake juu ya nchi, </q1>
<q2>Neno lake lapiga mbio sana. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>147:15</xo>
<xt>Ayu 37:12</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>16 </vn>Ndiye atoaye theluji kama sufu, </q1>
<q2>Huimwaga barafu yake kama majivu, </q2>
<q1><vn>17 </vn>Hutupa mvua ya mawe kama makombo, </q1>
<q2>Mbele ya baridi yake ni nani awezaye kusimama? </q2>
<q1><vn>18 </vn>Hulituma neno lake na kuviyeyusha, </q1>
<q1>Huuvumisha upepo wake, maji yakatiririka. </q1>
<q1><vn>19 </vn>Humhubiri Yakobo neno lake, </q1>
<q2>Na Israeli amri zake na hukumu zake. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>147:19</xo>
<xt>Kum 33;4; Mal 4:4; Rum 3:2</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>20 </vn>Hakulitendea taifa lo lote mambo kama hayo, </q1>
<q2>Wala hukumu zake hawakuzijua. </q2>
<q2>Haleluya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>147:20</xo>
<xt>Kum 4:32; Mdo 14:16; Rum 3:1-2</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>148</cn>
<q1><vn>1 </vn>Haleluya. </q1>
<q1>Msifuni 
<nd>Bwana</nd> kutoka mbinguni; </q1>
<q2>Msifuni katika mahali palipo juu. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Msifuni, enyi malaika wake wote; </q1>
<q2>Msifuni, majeshi yake yote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>148:2</xo>
<xt>Dan 7:10; Ebr 1:7</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Msifuni, jua na mwezi; </q1>
<q2>Msifuni, nyota zote zenye mwanga. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Msifuni, enyi mbingu za mbingu, </q1>
<q2>Nanyi maji mlioko juu ya mbingu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>148:4</xo>
<xt>1 Fal 8:27</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Na vilisifu jina la 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Kwa maana aliamuru, vikaumbwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>148:5</xo>
<xt>Ebr 11:3</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>6 </vn>Amevithibitisha hata milele na milele, </q1>
<q2>Ametoa amri wala haitapita. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>148:6</xo>
<xt>Yer 33:25</xt></note></f> </q2>
<b></b>
<q1><vn>7 </vn>Msifuni 
<nd>Bwana</nd> kutoka nchi, </q1>
<q2>Enyi nyangumi na vilindi vyote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>148:7</xo>
<xt>Isa 43:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>8 </vn>Moto na mvua ya mawe, theluji na mvuke, </q1>
<q2>Upepo wa dhoruba ulitendao neno lake. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Milima na vilima vyote, </q1>
<q2>Miti yenye matunda na mierezi yote. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>148:9</xo>
<xt>Isa 49:13</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>10 </vn>Hayawani, na wanyama wafugwao, </q1>
<q2>Vitambaavyo, na ndege wenye mbawa. </q2>
<q1><vn>11 </vn>Wafalme wa dunia, na watu wote, </q1>
<q2>Wakuu, na makadhi wote wa dunia. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>148:11</xo>
<xt>Mdo 17:28</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>12 </vn>Vijana waume, na wanawali, </q1>
<q2>Wazee, na watoto; </q2>
<q1><vn>13 </vn>Na walisifu jina la 
<nd>Bwana</nd>, </q1>
<q2>Maana jina lake peke yake limetukuka; </q2>
<q2>Adhama yake i juu ya nchi na mbingu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>148:13</xo>
<xt>Isa 6:3; Fil 2:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>14 </vn>Naye amewainulia watu wake pembe, </q1>
<q2>Sifa za watauwa wake wote; </q2>
<q1>Wana wa Israeli, watu walio karibu naye. </q1>
<q2>Haleluya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>148:14</xo>
<xt>Efe 2:17; 1 Pet 2:9</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>149</cn>
<q1><vn>1 </vn>Haleluya. </q1>
<q1>Mwimbieni 
<nd>Bwana</nd> wimbo mpya, </q1>
<q2>Sifa zake katika kusanyiko la watauwa. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>149:1</xo>
<xt>Isa 42:10</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>2 </vn>Israeli na amfurahie Yeye aliyemfanya, </q1>
<q2>Wana wa Sayuni na wamshangilie mfalme wao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>149:2</xo>
<xt>Ayu 35:10; Zek 9:9</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>3 </vn>Na walisifu jina lake kwa kucheza, </q1>
<q2>Kwa matari na kinubi wamwimbie. </q2>
<q1><vn>4 </vn>Kwa kuwa 
<nd>Bwana</nd> awaridhia watu wake, </q1>
<q2>Huwapamba wenye upole kwa wokovu. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>149:4</xo>
<xt>Mit 11:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Watauwa na waushangilie utukufu, </q1>
<q2>Waimbe kwa sauti kuu vitandani mwao. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Sifa kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao, </q1>
<q2>Na upanga mkali kuwili mikononi mwao. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>149:6</xo>
<xt>Kum 7:1-2; Ebr 4:12; Ufu 1:16</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>7 </vn>Ili kufanya kisasi juu ya mataifa, </q1>
<q2>Na adhabu juu ya kabila za watu. </q2>
<q1><vn>8 </vn>Wawafunge wafalme wao kwa minyororo, </q1>
<q2>Na wakuu wao kwa pingu za chuma. </q2>
<q1><vn>9 </vn>Kuwafanyia hukumu iliyoandikwa; </q1>
<q2>Hiyo ndiyo heshima ya watauwa wake wote. </q2>
<q2>Haleluya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>149:9</xo>
<xt>Kumb 7:1-2; Ufu 5:21; Rum 16:20; 1 Yoh 5:4</xt></note></f> </q2>
<b></b></c>

<c><cn>150</cn>
<q1><vn>1 </vn>Haleluya. </q1>
<q1>Msifuni Mungu katika patakatifu pake; </q1>
<q2>Msifuni katika anga la uweza wake. </q2>
<q1><vn>2 </vn>Msifuni kwa matendo yake makuu; </q1>
<q2>Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake. </q2>
<q1><vn>3 </vn>Msifuni kwa mvumo wa baragumu; </q1>
<q2>Msifuni kwa kinanda na kinubi; </q2>
<q1><vn>4 </vn>Msifuni kwa matari na kucheza; </q1>
<q2>Msifuni kwa zeze na filimbi; <f> <fn>-</fn><note>
<xo>150:4</xo>
<xt>Kut 15:20; Isa 38:20</xt></note></f> </q2>
<q1><vn>5 </vn>Msifuni kwa matoazi yaliayo; </q1>
<q2>Msifuni kwa matoazi yavumayo sana. </q2>
<q1><vn>6 </vn>Kila mwenye pumzi na amsifu 
<nd>Bwana</nd>. </q1>
<q2>Haleluya. <f> <fn>-</fn><note>
<xo>150:6</xo>
<xt>Ufu 5:13</xt></note></f> </q2>
</c>
</book>
